Wazee wa Tanga kusoma albadir kwa waliomuua Mzee Ali Mohamed Kibao

Wazee wa Tanga kusoma albadir kwa waliomuua Mzee Ali Mohamed Kibao

Hiyo haina masihara huwa haikosei kama atakayeisoma ni kweli ni mtaalamu achilia mbali na matapeli wa mjini wanaojifanya wanaijua kuisoma ili wapige hela.
Hiyo ni tofauti kabisa na mambo ya tunguri yenyewe inatenda haki kwa kumchagua kila aliyehusika na jambo ambalo limenuiwa na ikitumwa hairudi nyuma na haina tiba.
Hamas wangeshinda vita dhidi ya Israel hizo dua za Alibadili waislamu imani kali wakiiombea sana wayahudi washindwe kuwa wanadhulumu wapalestina haijafanya kazi .Hamas na wapalestina wanapukutika kila siku
 
Hamas wangeshinda vita dhidi ya Israel hizo dua za Alibadili waislamu imani kali wakiiombea sana wayahudi washindwe kuwa wanadhulumu wapalestina haijafanya kazi .Hamas na wapalestina wanapukutika kila siku
Hapa tunaongelea Bongo kwa huko hatujui mazingira yao yakoje na sheria zao zikoje
 
Hamas wangeshinda vita dhidi ya Israel hizo dua za Alibadili waislamu imani kali wakiiombea sana wayahudi washindwe kuwa wanadhulumu wapalestina haijafanya kazi .Hamas na wapalestina wanapukutika kila siku
Mbona unaenda mbali,nenda Tanga na Pemba kaulize,Watu wameokota sana makopo sababu ya albadili
 
Naweza kusema pasipo Shaka yoyote; wauaji wale walijua kama kuna Albadir, walijua ITASOMWA tu. Albadiri haina uhusiano wowote na Mungu, albadiri ni uchawi wa kidini; wauaji ni wachawi waliopitiliza; hakuna kitu kitawapata; wanajiamini cause wamebobea kwenye masuala ya kamati. Mungu pekee yake ndio anaweza kutoa ADHABU kwa wale wauaji.
 
Baadhi ya Wapemba hawataki muungano mbona hawajausomea albadili uvunjike ?
Hujaelewa maana ya Albadiri kumbe ndio maana unauliza maswali ya aina hiyo.
Albadir huwa haisomwi hovyo hovyo kama kununua Soda dukani huwa unamsomea mtu pale inapothibitika amekufanyia uovu uliokithiri na ukimsomea mtu kwa kumsingizia kosa inakurudia mwenyewe sasa kwenye ishu ya Muungano tulikubaliana wote tuungane hakuna mwenye kosa hapo utamsomea nani sasa
 
Ila kama inafanya kazi naona Albadiri isomwe tu ili waovu wapate haki yao. Hata kama kuna mshirikina mwenye uhakika na kazi yake tupo tayari kumlipa ili mradi waliofanya unyama wakione cha moto. Pata picha ni baba yako kashushwa kwenye basi ili kwenda kuuliwa? Ungejisikiaje? Binafsi kuna mama jirani alimlaza mama yangu selo kwa ugomvi wao hadi leo sijawahi samehe... Mama yangu na huyo mama washasameheana kitambo mno na ni marafiki ila mimi nimemtakia mama yangu mimi nitaendelea kumchukia huyo rafiki bila kujali kuwa wamepatana. Mzazi anauma mno.
Duh una hasira mbaya hufai kua kiongozi kma mama samia
 
Back
Top Bottom