Waziri Abdallah Ulega: Madai ya Samaki kuhifadhiwa kwa maji ya maiti ni hisia tu

Waziri Abdallah Ulega: Madai ya Samaki kuhifadhiwa kwa maji ya maiti ni hisia tu

Huyu Waziri naye ana upungufu mkubwa. Atawezaje kusema kuwa watanzania wapo salama wakati tunaambiwa kuwa 60% ya wagonjwa wote wa saratani wanatoka kanda ya Ziwa?

Yawezekana maji ya kuoshea maiti siyo chanzo cha hali hiyo, lakini kusema wakazi wa kanda ya ziwa wapo salama, ni uwongo. Linatakiwa lipatikane jibu, kwa nini wagonjwa wa saratani ni wengi sana kanda ya Ziwa kuliko maeneo mengine yote ya Tanzania?

Kwa sasa kila mwanachi achukue tahadhari kwa kuzingatia all hypotheses:

1) uhifadhi wa samaki kwa kutumia chemicals hatari (ulaji samaki wa ziwa Victoria ni hatari)

2) mercury poisoning (maji na vyakula vinavyopatikana maeneo ya machimbo ya wachimbaji madini wadogo ni hatari)

3) heavy metal contamination (maji na vyakula kutoka maeneo yaliyopo mazingira ya uchimbaji madini ni hatari)

4) madawa yanayotumika kwenye kilimo.cha pamba (ardhi inayotumika kwenye kilimo cha pamba ni hatari inapotumika katika kilimo cha mazao ya chakula).

5) utiririshaji wa maji ya sumu ndani ya ziwa kutoka viwandani (maji ya Ziwa Victoria ni hatari)

Chukua tahadhari mpaka sababu ya uhakika itakapopatikana. Utafiti wa jambo hili unaweza kuchukua miaka kadhaa mpaka kupata jibu la uhakika.
Point taken.
 
Haya ndio maswali tunayopaswa kujiuliza kwa sasa , kwamba Je kuna ukweli wa haya nambo au ndio tusubiri kanusho la Kuku au tusubiri kuambiwa Ng'ombe nao wanamekula majani yenye sumu ?

Je Kuna njama za kuwafanya Watanzania wote Vegetarians ?
HAKUNA aliyekushikia kisu kwamba usile samaki, umepewa tahadhari uamuzi ni wako. Tuliopo hosp ndio tunajua jinsi kansa inavyoua watu wengi
 
HAKUNA aliyekushikia kisu kwamba usile samaki, umepewa tahadhari uamuzi ni wako. Tuliopo hosp ndio tunajua jinsi kansa inavyoua watu wengi
Kansa ni ugonjwa tu unaoweza kumpata mtu yoyote ndo maana hadi watoto wadogo wanaweza kuumwa haijalishi wamekula kitu gani.na ulikuwepo miaka na miaka.Na kufa bado kuko pale pale sio lazima iwe kansa.
 
Kwa Hapa dar,
Hakuna pa kuponea,labda mboga ulime kwako

Mchicha wa ubungo
unalimwa msewe kando kando ya mfereji unaotililisha maji taka toka mlimani campus na chuo Cha maji

Ule wa mabibo sokoni,
Mwingi unamwagiliwa na majitaka tiririka kutoka hostel za wanachuo

Ule wa temeke,
Unamwagiliwa na majitaka tiririka toka msd na kiwanda Cha madawa keko.

Ukienda tandale,tandika manzese,mbagala,g/mboto,mtoni mtongani, magomeni,m/chai,muhimbili huko Ndo balaaa na nusu.
 
Huyu naye hakupaswa kusema kauli ile mbele za watu bila ushahidi wa kisayansi. Huyu ndiye alikuwa Waziri wa fedha. Kweli mtu kama huyo anafaa nafasi aliyo nayo? Hivi mama alimchagua kwa vigezo vipi? Nadhani wanajuana toka utotoni...
Kwani huyo mama naye alifika hapo kwa kigezo kipi? Acha vipofu waongozane wenyewe.
 
Sangara ndio basi tena
Hata mm sinunui tena Sangara na Sato.

Kati ya waziri na makamu wa rais nani mkubwa na mwenye taarifa nyingi zaidi kuliko mwingine?

Unanata nimuamini waziri halafu nimpuuze makqmu wa rais?
 
tutakapokubali siku shida ni INCOMPETENCE tunaweza kutibu mengi sana.
 
Hata mimi.VP yupo sahihi kabisa kuna siku nilinunua samaki sato mkoa fulani kanda ya kati wakati wa kuosha bombani povu kama sabuni omo vile.Ngoma kwenye kula hatufu ya formalin kama upo mochwari vile.Hiyo ilikuwa mwezi Juni kuanzia hapo niliapa sitakula tena samaki wa masafa ya mbali
Uhalifu huu unafanyika pia kwenye maduka ya nyama! Ukiona nyama inzi hawaisogelei jua ilishatiwa dawa ya kuhifadhia maiti.
 
kali ya VP kwenye nchi za wenzetu leo masoko ya hisa na mitaji yangeyumba sana.lkn kwa tanzania ni jambo la kawaida,naibu waziri anasema ni hisia tu!!!kwa hiyo makamu wa rais kaongea hisia,mungo,hajui...!lakini ni wa pili kwa mamlaka katika jamuhuri ya muungano wa tanzania.
 
NACHUKUA FULSA KUBWA KUSEMA HIVI SILI CHAMAKI TENA MTEE HAKUNA HIVYO AU JUZI TU TUMELISHWA MBOGA ZA MAJI YA MAITI NA SASA TUNAWEKEWA TENA HAPANA SILI LABDA ZA BWA LA MANYARA
 
Kauli za viongozi wetu kwa sasa nyingi zimekuwa za kuzua taharuki tu.
Nilidhani hilo ni suala laingia moja kwa moja kwenye kufanyiwa uchunguzi wa kisayansi na polisi wanakuwa washirikishwa.

Si kusema kufanywe utafiti.
 
Hivi anajua kuwa hata mapenzi ni hisia mwisho watu wananyanduana
 
Back
Top Bottom