Waziri gani alimdhulumu Rais mstaafu Mwinyi vifaa vyake vya ujenzi?


..nahisi ni mifuko ya sementi iliganda mzee akadhani amefanyiwa fitina.🀣
 
Angekuwa mwendazake sasa, sijui angefanywa nini
 
..lakini kuna jedwali linaonyesha aliyempokea Mzee Mwinyi wizara ya mambo ya ndani ni Hassan Nasoro Moyo.

..Je, huko kwenye kitabu Mzee Mwinyi amemtaja kwa jina mhusika au ametuachia kitendawili tutegue wenyewe?
Soma bandiko Number 24.
 
..lakini kuna jedwali linaonyesha aliyempokea Mzee Mwinyi wizara ya mambo ya ndani ni Hassan Nasoro Moyo.

..Je, huko kwenye kitabu Mzee Mwinyi amemtaja kwa jina mhusika au ametuachia kitendawili tutegue wenyewe?
Mzee Moyo wakati Mzee Mwinyi anajiuzulu alikuwa ni Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa rais maana yake alikuwa ana nyumba tayari ya serikali.

Iko hivi ukiwa waziri ukahamishiwa wizara nyingine huhami nyumba unahama ofisi tu.
Kwa hiyo hakukuwa na sababu Mzee Moyo kuhama nyumba aliyokuwa akiishi wakati akiwa waziri wa Nchi na kuhamia alipokuwa anakaa Mzee Mwinyi eti kisa amemrithi wizarani.

Kilichofanyika ni kuwa Mzee Moyo alihama kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais na kwenda ofisi ya Mambo ya Ndani na sio kuhama nyumba.

Mzee Natepe(Major Geneal Mstaafu) aliteuliwa kuwa katika baraza la mawaziri na kulazimika kupewa nyumba na serikali na ndipo alipopewa ya anayetoka Mzee Mwinyi.
 
Anazungumziwa aliyerithi wizara baada ya Mwinyi kujiuzulu, au waziri kwenye serikali ya Mwinyi!
Kitabu kinasema "Baada ya Mzee Mwinyi kuchaguliwa Rais alimteua huyo bwana aliyemdhulumu vifaa vyake vya ujenzi na kumtoa kwenye nyumba.."

Msingi wa hoja yangu upo hapa
 
Huyu ni Mzanzibar tena ni muhasisi wa mapinduzi matukufu.
Kuasisi mapinduzi sio kuwa Mzanzibar, mzee Natepe kwao ni kusini. Kwani John Okelo aliyeongoza mapinduzi alikuwa Mzanzibar?
Kuna mzee Natepe na Kisasi, je unamfahamu mzee Kisasi?
 
Hiyo siyo sifa. Alilea mwizi, shame on him.
Kumsamehe na kumuonesha upendo mwizi au mtu aliekufanyia ubaya ni sifa nzuri ktk maisha... Hata Yesu aliwasamehe na kuwaombea msamaha kwa Mungu wale wote walimtesa mpk kufa pale msalabani, je kwa mtazamo wako unafikiri Yesu alikuwa mjinga?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…