DOKEZO Waziri Gwajima, hii anayofanya Lillian Mwasha kwa watoto siyo sawa

DOKEZO Waziri Gwajima, hii anayofanya Lillian Mwasha kwa watoto siyo sawa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kigezo cha kukataa mimba, kuweka condition love
Moja kwa moja ni kwamba hawapendiwi
Ulitaka athibitisheje?
Hakuna nguvu kubwa kama hiyo aliyowapa kumtumainia Mungu wao
Na bd kawambia anataka kukutana nao likizo
Unajua anataka kufanya nini
Sawa hawapendwi lakini alikuwa na njia nzuri zaidi ya na kuwapa kama ni ushauri au jambo jingine analoona ni sahihi kwa na si kuwaita mbele ya kadamnasi hii.
 
Mkuu, sisi tumeumbwa kuwaongoza wanawake, sisi wanaume ni viongozi wao. Mwanaume ni mtatuzi wa changamoto zote.

Huwezi kumuacha mtoto wako apate shida kwasababu ya visirani na tabia mbaya za mwanamke uliyezaa nae. Unaweza kukaa mbali na mwanamke uliyezaa nae ila hutakiwi kukaa mbali na mtoto wako, damu yako. Wapo wanaume wameenda hadi mahakamani ili wapate fursa ya kulea watoto wao pale ambapo mwanamke ameanza kuleta visirani.

Ukitafuta sababu za kutelekeza mtoto au kutotimiza wajibu wako kama mzazi hautozikosa mkuu. Lakini zote hazitokuwa na mashiko hata kidogo.
Ni kweli kabisa unayoyasema. Kama hujaoa mwombe sana Mungu akupe mke mwema vinginevyo ni hatari ya kifo. Tena wengine wanakuvuruga kwa kushirikiana na mama yake mzazi. Utaomba ardhi ipasuke ujifukie. Kina mama wengi wameharibu maisha ya watoto wao kipuuzi kabisa.
 
Kumbe kaliwa kichwa ...safi sana..hivi haoni aibu ,hata kaa Waziri hayupo sahihi( sio Kwa muktadha huu) Mpe hata heshima yake !
Hivi ni Mawaziri wangapi wamepita hiyo sekta ,walikuwa passive ...huyu anafanya vizuri! Tumpe Moyo ! Ninaongea haya Kwa uzoefu mkubwa!
Ndio wamemla kichwa, alianzia ubishani wake kwenye ule uzi wa watu wa Arusha waliojiwekea utaratibu wa kuwawajibisha vijana wasio na maadili.

Nadhani akaona haitoshi akaja kumvaa na kwenye huu uzi. Na ndio maana kama unafatilia huu uzi unakuta waziri kam-mention kumjibu huyo bibi, but ukirudi nyuma huoni alichoandika. Inamaana alivyoandika ujinga wake mods wakafuta halafu wakamsokomeza lupango.
 
Jana kwenye uzi mwingine nikaona anamparamia Dk. Gwajima analeta ubishani wa kijinga licha ya kupatiwa majibu sahihi. Nikataka nimwambie waziri kuwa huyo bibi kuna sababu nyingine inayofanya alete ubishani na sio hoja iliyo mezani, ila nikasita. Bahati nzuri mods wamepita naye, bibi yupo segerea ya JF anasoma kama guest muda huu.
Yaani anakuwa mjinga mjinga licha ya kuwa kwa umri anaweza kuwa amewapita 90% ya wanaJF.
Yani mtu unaweza kuwa na akili nzuri ya darasani ukajua mambo mengi ila ukishaingiza chuki za kidini basi akili zinapotea..hiyo bibi ni ana chuki mnoo..huyo hafai kwenye jamii iliostaarabika
 
Ushirikishaji jamii ni muhimu. Mm nitapita jamii itabaki, nao washike wajibu wao kwa uendelevu wao kwenye Ustawi na Maendeleo ya Jamii. Mm Niko mkutano Mumbai, India na bado nimeona nikainuka kusukuma ajenda. Nimepoa hapo kweli?[emoji9]

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Unafanya kazi nzuri Mh Waziri hata kuona jambo kwenye social media ukalitilia maanani inaonesha ni namna gani unajali.
 
Nadhani ku balance stori, wababa wenye hao watoto wangehojiwa pia kujua sababu za kutotoa matunzo kwa watoto wao. Sometimes wamama wanawalisha watoto matango pori na kupandikiza chuki kwa watoto wao ili wawachukie baba zao. Nasema hivyo kwa sababu
  1. Kuna wanaume wanalea watoto wasio wao kibiolojia (wamepakaziwa). Ni ngumu sana kwa wanaume wa namna hii kutoa matunzo kwa watoto ambao wanajua wamepakaziwa
  2. Kuna wanawake hawataki kukaa na wanaume na wanataka wajitegemee na watumie watoto kama kitega uchumi chake
  3. Kuna wanaume wako willing kulea watoto, lakini wanawekewa mazingira magumu (wanazuiwa) na wanawake waliozaa nao
 
This is not right kabisa. Hii sio njia kusolve tatizo amekosea sana hao watoto haujui ni kwa namna wamelishwa maneno na wazazi wao wa kike au yawezekana ni kweli. Lakini kuwaita mbele za watu na kutoa hukumu ya moja kwa moja kuwa kweli wanachukiwa na baba zao sio sahihi. Halafu unajiliza mbele yao huku ukisema unaomba. Sio kweli kabisa.

Huyu dada nilijua ni mtangazaji wa kawaida kumbe ni lifeminist la kwenda linafiki. Watoto hawajui kama wanadhalilishwa
 
Nani mwengine kasave namba ya wazir kama mim
Ahsante Sana ku save ndugu yangu, itakusaidia wewe na wengine wa karibu yako ambao, huwa naumia Sana kusikia mtu mmoja mwenye shida na jambo ambalo liko ofisini kwangu halafu bahati mbaya hajapata msaada katika mfumo rasmi halafu anaanza kulia peke yake hajui rufaa aifikishe vipi kwangu kwa haraka.

Huwa nikiona mtu mmoja kaamua ku save, huwa naamini nyuma yake wako kumi kama siyo 20. Umoja wetu ni nguvu yetu wala na ni msingi katika kusukuma mbele maendeleo na ustawi wa jamii na kupambana na kero kero za kutengenezwa na baadhi ya wasio na Nia njema[emoji1666][emoji1241]

Angalizo; Msipige Bali tumeni UJUMBE tafadhali. Na vema zaidi WhatsApp kwa kuwa naipata popote. Nikiwa nje ya nchi kama hivi sms za kawaida saa ingine mtihani. Ila Nina namba ingine pia ya 0734124191. Sms pia.

Ila call center yetu ni 0734986503 na 026 2160250. Saa za kazi siku za kazi. Kuna 116 kwa ajili ya taarifa za ukatili kwa watoto, siku zote saa 24.

Mkumbuke kuna namba ya IGP pia, 0699 998899.

Tukl vizuri kudhibiti wababaishaji na wanaoonea watu. 🇹🇿🤝

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Elimu kweli inahitajika kwa utaratibu mzuri na siyo kila mtu aonavyo yy. Mtu akiona anacho kipaji cha kutoa elimu, na aje tumjenge vzr ili asije kuharibu. Maana akiharibu hata yy hao hao anaojaribu kuwasaidia watamgeuka wakiona anaweza kuwa mtaji wao.

Hakika elimu kweli bado inahitajika kwa wingi na ndiyo maana sasa pamoja na huko kwenye jamii bado na redioni na mitandaoni humu tunafika mubashara kabisa. Mashuleni kuna miongozo ya madawati ya ulinzi pia, kuna namba za call center ikiwemo 116 kwa ajili ya watoto. Kifupi mifumo ipo sema Kila mmoja atimize wajibu tu. Ahsante kwa maoni juu ya umuhimu wa elimu.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Mweshimiwa waziri, makofi matatu kwako.🤓
Siyo kuongea sana ndo uwezo wa ufahamu na hekima,
Mara nyingi hawa wanaharati ndio chanzo cha migogoro kwenye familia,ndoa n.k
Pia na nyimbo za wasanii mkaziangalie zinatuharibia sana watoto.
Mfano mtoto wa chekechea ,anaimba wimbo "Nakupenda wewe na huyo Bwana wako"
Huyu ni mtoto wa kiume unategemea huyu mtoto akiwa mwalimu badaye awe mwalimu wa aina gani ?
 
Ahsante Sana ku save ndugu yangu, itakusaidia wewe na wengine wa karibu yako ambao, huwa naumia Sana kusikia mtu mmoja mwenye shida na jambo ambalo liko ofisini kwangu halafu bahati mbaya hajapata msaada katika mfumo rasmi halafu anaanza kulia peke yake hajui rufaa aifikishe vipi kwangu kwa haraka. Huwa nikiona mtu mmoja kaamua ku save, huwa naamini nyuma yake wako kumi kama siyo 20. Umoja wetu ni nguvu yetu wala na ni msingi katika kusukuma mbele maendeleo na ustawi wa jamii na kupambana na kero kero za kutengenezwa na baadhi ya wasio na Nia njema[emoji1666][emoji1241]

Angalizo; Msipige Bali tumeni UJUMBE tafadhali. Na vema zaidi WhatsApp kwa kuwa naipata popote. Nikiwa nje ya nchi kama hivi sms za kawaida saa ingine mtihani. Ila Nina namba ingine pia ya 0734124191. Sms pia.

Ila call center yetu ni 0734986503 na 026 2160250. Saa za kazi siku za kazi. Kuna 116 kwa ajili ya taarifa za ukatili kwa watoto, siku zote saa 24.

Mkumbuke kuna namba ya IGP pia, 0699 998899.

Tukl vizuri kudhibiti wababaishaji na wanaoonea watu. 🇹🇿🤝

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Asante sana mhe. Waziri kwa kuwa prompt kusikiliza hoja za wananchi. Laiti kila kiongozi wa umma angekuwa kama wewe, naamini shida zetu nyingi zingetatuliwa kwa haraka. Mungu akujaalie maisha yenye fanaka
 
Unafanya kazi nzuri Mh Waziri hata kuona jambo kwenye social media ukalitilia maanani inaonesha ni namna gani unajali.
Najitahidi Sana kuwa Karibu na saiti yangu ya Jamii Ili nipate mawazo ya kujenga Ili kwa nafasi yangu sasa niongezee tofali kadhaa kwenye nyumba yetu ya maendeleo na ustawi wa jamii, Ili muda wangu ukiisha wengine waje waendelee maana wala sitakaa milele nilipo.

Lakini Sasa mhhhh, wako watu wamebeba silaha za hasira na chuki wazi wazi sijui wanagombana na nani na kwa Sababu gani. [emoji848].

Mimi huyu, ambaye nimejiunganisha na uwepo wa Mungu wa mbinguni, hakika hakuna silaha iliyojengwa kwa msingi wa uovu na chuki itakayotumwa kubomoa ari yangu ya kuchati na jamii maana ndiyo saiti yangu na mm, haipo.

Wao wa brand tu jinsi gani hekima yao imejengwa na sisi tuta brand jinsi gani hekima yetu imejengwa. Mungu siku moja atabariki sawa na mizania yake. Tusonge mbele....

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Anawauliza watoto wanaochukiwa na baba zao. Je amewaandaa kisaikolojia? Mbona yaonekankama ni udhalilishaji kwa watoto na wazazi wao. Angalia clip hapa

very unreasonable, ni kama hukumu ya upande mmoja, na hajawauliza kama wao wanawapenda baba zao pia. feminism is poisonous. though historia yake yeye Lilian pia inaumiza.
 
Najitahidi Sana kuwa Karibu na saiti yangu ya Jamii Ili nipate mawazo ya kujenga Ili kwa nafasi yangu sasa niongezee tofali kadhaa kwenye nyumba yetu ya maendeleo na ustawi wa jamii, Ili muda wangu ukiisha wengine waje waendelee maana wala sitakaa milele nilipo.

Lakini Sasa mhhhh, wako watu wamebeba silaha za hasira na chuki wazi wazi sijui wanagombana na nani na kwa Sababu gani. [emoji848].

Mimi huyu, ambaye nimejiunganisha na uwepo wa Mungu wa mbinguni, hakika hakuna silaha iliyojengwa kwa msingi wa uovu na chuki itakayotumwa kubomoa ari yangu ya kuchati na jamii maana ndiyo saiti yangu na mm, haipo.

Wao wa brand tu jinsi gani hekima yao imejengwa na sisi tuta brand jinsi gani hekima yetu imejengwa. Mungu siku moja atabariki sawa na mizania yake. Tusonge mbele....

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Umejiunganisha na uwepo wa MUNGU kweli au ni hisia ndio zimekupelekea uongee hivyo mkuu?

Mana MUNGU hachelewi wala hawai kutupiga matukio sisi viumbe wake ili kutupima imani zetu..Haswa nyinyi Mama zetu anawapiga matukio sana ili kupima imani zenu.

MUNGU akuongoze kweli kweli na asikutoe kwenye reli yako.

Hapo sikunpangia MUNGU kazi ila nimemuomba akuongoze na kizazi chako.
 
Back
Top Bottom