Waziri Innocent Bashungwa awakabidhi Wakuu wa Majeshi Wastaafu Land Cruiser LC300 mpya

Waziri Innocent Bashungwa awakabidhi Wakuu wa Majeshi Wastaafu Land Cruiser LC300 mpya

Huyu anaogopa kuoindukiwa Urais na wenzake 2025, kwahiyo anaanza kutoa rushwa kwa watu wenye mizizi mirefu JWTZ, aache uoga

Hapana bana hajaanza kugawa haya huyu mama ni utaratibu wa miaka mingi tu.

Tofauti ni kwamba mwaka huu yamefanywa mbele ya camera,walianza na general mabeyo siku anastaafu akapewa ufunguo picha,akaja sirro nayeye akapewa prado na camera.

Si kwamba yameanza mwaka huu.
 
Vijana tuendelee kusubiri taifa la kesho!
Mara uzee huo..., bila hodi unaibukia taifa la tasaf!
Tuendelee kusoma namba
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Halafu kesho Mama anatuma mawaziri Ulaya kwa wafadhili kuomba hela za bajeti ya taifa....haibu sana.
 
Ni jambo zuri, lakini waangaliwe namna ya kujengewa na nyumba maana wastaafu wengi wanaishi nyumba zisizoendana na nafasi walizokuwa nazo ukuzingatia walihusika na ulinzi wa taifa hili
 
Mzee Ruksa alivyopewa zawadi ya gari kwenye birthday yake tulichonga sana, wakati yeye alikuwa Commander in Chief ambaye kiprotokali ni bosi wa wakuu wa majeshi😀
 
wanufaika wa magari hayo kwa mujibu wa sheria ni jaji mkuu, spika wastaafu, mawaziri wakuu wastaafu, wakurugenzi wa tiss, na kadhalika
mujibu wa sheria ipi

Waziri kasema ni agizo la Mama Samia

au kutaja hadharani sheria ya migawanyo ya ulaji wa viongozi ni kuvunja wa sheria ?
 
nyie gawaneni tu keki ya taifa.sie wengine tumesharidhika kula amani ya taifa.maana ukihoji tu unaambiwa unahatarisha amani ya nchi unataka tuwe kama sudan.
 

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Innocent Bashungwa @innocentbash amewakabidhi magari mapya Wakuu wa Majeshi Wastaafu kwa maelekezo ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wakuu wa Majeshi Wastaafu waliokabidhiwa magari ni CDF Mstaafu George Waitara na Robert Mboma na makabidhiano hayo yamefanyika katika Ofisi za Wizara ya Ulinzi Mtumba Jijini Dodoma

Akikabidhi Magari hayo, Waziri Bashungwa amesema kuwapatia Wastaafu hao magari ni sehemu ya maelekezo ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba wapatiwe magari mapya ambayo yanatengenezeka na spea zake zinapatikana kwa urahisi.

“Wakuu hawa wa Majeshi Wastaafu walifanya kazi kubwa na iliyotukuka kipindi cha utumishi wao kwa Nchi yetu, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan imewapatia magari na kuwatakia kheri na maisha marefu Majenerali Wastaafu hawa”

AYO TV
Nice
 
mbona huyu wa juzi kazi mwamunyange yeye hajakabidhiwa? ama yeye utaratibu wake uko tofauti? ila kwa nchi masikini kama bomgo kuendelea kukumbatia haya mashangingi ambayo ulaya yanamilikiwa na matajiri wakubwa tu ni kuendelea kuwa masikini tena masikini hohehahe.
Wao wanayo bado mazuri hayajachakaa
 
Napendekeza Hali ikiwanzuri kiuchumi wapewe helicopter na wake zao wapewe meli Kisha watoto zao treni Halafu wajukuu wapewe mabasi ya mwendo Kasi , vitukuu Range Rover!?? Poor country
 

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Innocent Bashungwa @innocentbash amewakabidhi magari mapya Wakuu wa Majeshi Wastaafu kwa maelekezo ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wakuu wa Majeshi Wastaafu waliokabidhiwa magari ni CDF Mstaafu George Waitara na Robert Mboma na makabidhiano hayo yamefanyika katika Ofisi za Wizara ya Ulinzi Mtumba Jijini Dodoma

Akikabidhi Magari hayo, Waziri Bashungwa amesema kuwapatia Wastaafu hao magari ni sehemu ya maelekezo ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba wapatiwe magari mapya ambayo yanatengenezeka na spea zake zinapatikana kwa urahisi.

“Wakuu hawa wa Majeshi Wastaafu walifanya kazi kubwa na iliyotukuka kipindi cha utumishi wao kwa Nchi yetu, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan imewapatia magari na kuwatakia kheri na maisha marefu Majenerali Wastaafu hawa”

AYO TV
Sisi wastaafu pia lakini hatujaongezwa pension kwa miaka zaidi ya 20! Nchi hii ni ngumu sana!
 
Sirro wamemuonea sana kumpa prado ambacho hata raia tu anaweza kununua.wanatakiwa wote wapewe gari sawa
 
Back
Top Bottom