Waziri Jerry Silaa ana kitu, atafika mbali, abarikiwe

Waziri Jerry Silaa ana kitu, atafika mbali, abarikiwe

Kiongozi anajenga mifumo, hakuna mfumo aliojenga mpaka sasa, angekuwa na mfumo, asingekuwa na haja ya kutembea mpaka vyumbani mwa watu.

and land justice, kama ilivyo haki yoyote ile, huwezi kuifanya kwa mfumo wa mob justice, unakusanya vijitu mtaani, unasikiliza unaamua, hakuna due process halali ya kisheria ambayo itafanya haki ionekane inatendeka. Kuna mahala atakutana na jambo, yeye binafsi atadhalilika, na serikali itadhalilika.
Hio mifumo yote msingi si ni katiba ambayo mnaikataa? Kungekuwa na serious punishment kwa wanaokiuka katiba usingekuwepo ujinga ujinga tunaoshuhudia leo.
 
Ana uthubutu mkubwa wa kufanya maamuzi..Ni trait na attribute muhimu Kwa kiongozi..

Yamkini anayo mapungufu lakini anaonyesha njia ktk kuwapa haki Wasio na uwezo wa kupambana na wenye bila Za ukwasi..

KATIBA MPYA YAWEZA KUJENGA TAASISI IMARA ZA UTOAJI HAKI..Mfumo imara wa upatikanaji wa Mahakimu,Majaji,Waendesha mashitaka na Wanasheria waadirifu.
 
Kwa hiyo kwako wewe migogoro ya ardhi isipelekwe mahakama za ardhi ipelekwe kwa Slaa atatue yeye kwa sheria zake binafsi?
We jamaa usichoelewa ni nini? Mfano Sheria inasema penye Zebra usimame wewe umepitiliza umegonga mtu ukakimbia, baada ya kushikwa unajifanya hukugonga mtu unamvuta traffic pembeni na kumuhonga pesa ili asawazishe, aliedhurika akienda mahakamani anakuta jaji kahongwa tayari anazungushwa tena ili kunyimwa haki. Ikitokea kiongozi mwenye dhamana ya juu bila kutegemea mahakama akilisimamia hili kwa sheria kabisa unafikiria aliedhulumu haki atapona?
 
Ana uthubutu mkubwa wa kufanya maamuzi..Ni trait na attribute muhimu Kwa kiongozi..

Yamkini anayo mapungufu lakini anaonyesha njia ktk kuwapa haki Wasio na uwezo wa kupambana na wenye bila Za ukwasi..

KATIBA MPYA YAWEZA KUJENGA TAASISI IMARA ZA UTOAJI HAKI..Mfumo imara wa upatikanaji wa Mahakimu,Majaji,Waendesha mashitaka na Wanasheria waadirifu.
Ni ngumu sana kupata haki kwenye nchi corrupt kama yetu hii, alijisemea mzee Rostam kuwa huwezi kutegemea mahakama ambayo kiongozi akipiga simu na kutoa amri tu hukumu inabadilishwa.
 
Ana

Anafanya vizuri ila anachangamoto pia ya namna ya kushughulikia hiyo migororo Kwa baadhi ya maeneo apunguze mihemko atulize jazba awe mtulivu wakati anapotatua hiyo migororo...
Apunguze Kweli munkari, lakini sometimes hata ingekuwa wewe lazima ukasirike,

Imagine mtu amepora nyumba ya mtu kimabavu Kisha anakwambia, waziri ningependa nikuone kidogo pembeni tuzungumze tuyamalize, mbele ya umma, ungefeel aje?
 
Apunguze Kweli munkari, lakini sometimes hata ingekuwa wewe lazima ukasirike,

Imagine mtu amepora nyumba ya mtu kimabavu Kisha anakwambia, waziri ningependa nikuone kidogo pembeni tuzungumze tuyamalize, mbele ya umma, ungefeel aje?
Huwezi jisikia vizuri ila kama kiongozi lazima kutumia hekima na Busara hasa kwenye umati mkubwa wakati mwingine unapimwa tuu namna unavyoweza kutongoza.
 
Huwezi jisikia vizuri ila kama kiongozi lazima kutumia hekima na Busara hasa kwenye umati mkubwa wakati mwingine unapimwa tuu namna unavyoweza kutongoza.
Leo tena alikuwa kariakoo,

Mtoto amemtimua manake na nduguze kwenye ghorofa la URITHI,

Waziri, Ametoa maelekezo ya BUSARA sana, hapakuwa na mihemko,

Nadhani anajirekebisha.
 
Huwezi jisikia vizuri ila kama kiongozi lazima kutumia hekima na Busara hasa kwenye umati mkubwa wakati mwingine unapimwa tuu namna unavyoweza kutongoza.
Hekima na busara zinatakiwa pande zote mbili, kama Mzee Mmasi alishindwa kuonesha heshima na busara kwa Waziri, ulitegemea Waziri ndiyo amnyenyekee Mmasi kisa tu yeye ni kiongozi!?? Mmasi ni muhalifu kumbuka hilo!!
 
Salaam, Shalom!!

Nimefuatilia Kwa ukaribu jinsi waziri Jerry Slaa anavyofanya katika utatuzi wa migogoro ya ardhi, japo Bado ni mapema sana kusema kuwa anafanya vizuri, lakini Kwa sasa itoshe kusema ana kitu kinachoonekana, na atafika mbali, tuendelee kumwombea.

Nimesikiliza Kwa Umakini jinsi alovyotatua case ya Tajiri aitwaye Mzee Mmassy aliyenunua nyumba Kwa marehemu aliyeko kaburini, yaani document zinaonyesha marehemu akiwa kaburini alisaini mauziano na kumuuzia nyumba tajiri Mmassy,na jinsi alivyotatua case Ile Kwa uwazi Kwa kutumia nyaraka halali katika ofisi ya ardhi, na jinsi alivyoweza kuwarudishia nyumba watoto na mke wa marehemu nyumba Yao, kiukweli Mungu aendelee kumjalia uhai na AFYA na baraka kiongozi huyu.

Nilifanikiwa pia kufuatilia jinsi alivyosaidia kutatua mgogoro ulioletwa na Msama, Kwa kutomtendea HAKI yake mama yule aliyedai kiwanja chake, pia nimeona ufuatiliaji, uthubutu na uchapakazi wa Waziri huyu kijana Jerry Slaa.

Ni maombi yangu, akae chini na viongozi wenzie katika wizara yake na kuja na mpango MIKAKATI wa kutatua migogoro ya ardhi Nchi nzima bila kuwepo haja ya kusafiri huku na huko, uwepo mfumo mzuri na WA haraka zaidi kuwafikia wananchi na kutatua migogoro hiyo ya ardhi.

So far, KAZI imeonekana inafanyika,

Mungu Mbariki Waziri huyu Jerry Slaa,

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Ameeen.

Source: Milard Ayo tv.

Karibuni🙏
Hivi kuna jimbo Dsm ambalo halina maendeleo kuzidi Ukonga? Sasa Jerry ndio mbunge wa Ukonga na hana lolote analofanya mbali na kutafuta kiki
 
Mahakamani zinafanywa analysis nyingi kabla ya hukumu, huyo Silaa anayekaa vichochoroni usiku ana muda wa kutoshaha kufanya hivyo, kama jamaa aliingia kwa nguvu ya mahakama, huyo mama hatamaliza mwezi ndani ya nyumba hiyo, mahakama itamtoa, na Jerry akikoroma ataitwa mahakamani ajieleze kwa nini asifungwe kwa kudharau mahakama.

Mambo ya alikufa lini, kama hakuyasema mahakamani, ni kazi bure kwa sasa

Nvhimbi na Makala wamesema mambo ya Mahakamani yasiingiliwe, yeye anajitoa akili

Ivi tuteendelea kuwa wajinga na wapinga haki mpaka lin kwan wewe hujui mahakama zetu hazina haki kaka kumejaa rushwa na ukilitimba
 
Waziri yupo vizuri kichwani kabla hajakupiga nyundo anakupa ufafanuzi wa kisheria jamaa anabusara sana. Yaani mtu anapokonywa kiwanja alichodhulumu kimya kimya anaishia kutoa macho na kukuna upara, halafu wengi walio dhulumu watu viwanja ni wanene warefu na wana upara.
 
Ni maombi yangu, akae chini na viongozi wenzie katika wizara yake na kuja na mpango MIKAKATI wa kutatua migogoro ya ardhi Nchi nzima bila kuwepo haja ya kusafiri huku na huko, uwepo mfumo mzuri na WA haraka zaidi kuwafikia wananchi na kutatua migogoro hiyo ya ardhi.
Hao unaoomba akae nao chini na kuongea ndio wanaosababisha migogoro ya ardhi, by all means watamkwamisha tu. Hao watu wa ardhi ulaji, rushwa na ufisadi ni muhimu zaidi kuliko kitu kingine chochote. Solution nzuri ni kuwaamuru tu, wala siyo kujadiliana nao.
 
Una kichwa kizito sana kuelewa kitu kidogo sana kama hicho! Nakupa mfano mdogo sana, kama umeenda kupima DNA kwa Mkemia,na majibu ya katoka kua mtoto siyo wako, je utaenda mahakamani ili kupinga matokeo ya DNA!? Je Mahakama ikisema mtoto ni wako kwa sababu tu wwe ndiyo ulilea mimba utakubali!?
Unataka kusema wizara ya ardhi ndio ina mamlaka ya kutatua kesi za ardhi?
 
We jamaa usichoelewa ni nini? Mfano Sheria inasema penye Zebra usimame wewe umepitiliza umegonga mtu ukakimbia, baada ya kushikwa unajifanya hukugonga mtu unamvuta traffic pembeni na kumuhonga pesa ili asawazishe, aliedhurika akienda mahakamani anakuta jaji kahongwa tayari anazungushwa tena ili kunyimwa haki. Ikitokea kiongozi mwenye dhamana ya juu bila kutegemea mahakama akilisimamia hili kwa sheria kabisa unafikiria aliedhulumu haki atapona?
Wenye mamlaka ya kutatua malumbano na migogoro ya ardhi kati ya wahusika wawili ni Mahakama peke yake, sio waziri wa ardhi!
 
Kiongozi anajenga mifumo, hakuna mfumo aliojenga mpaka sasa, angekuwa na mfumo, asingekuwa na haja ya kutembea mpaka vyumbani mwa watu.

and land justice, kama ilivyo haki yoyote ile, huwezi kuifanya kwa mfumo wa mob justice, unakusanya vijitu mtaani, unasikiliza unaamua, hakuna due process halali ya kisheria ambayo itafanya haki ionekane inatendeka. Kuna mahala atakutana na jambo, yeye binafsi atadhalilika, na serikali itadhalilika.
Utapeli wanaofanyaa hao wanaotapeli watu Viwanja sio kwamba hakuna sheriaa.. Rushwaa imetawalaa sanaa sasa hakuna namna hata sheria iwe Ngumu vipi itaweza kufanya kaziii lazimaa Mtu aingie Field na kupambana na huu upuuzi direct... Hakuna rais alishawahi kufanya ziara nyingi za ndani ya nchi kama magu nadhani tuliona kazi aliyoifanyaa.. mtu mweusi bila kumfata nyuma nyuma kama mbuzii tegemea Madudu tu
 
Back
Top Bottom