Waziri Kabudi akanusha kuthibitisha kifo cha Mwanahabari, Azory Gwanda

Waziri Kabudi akanusha kuthibitisha kifo cha Mwanahabari, Azory Gwanda

Tuwape pole wana wa dodoma
Waziri amechemka on camera. Maelezo yake yaliacha mwanya kwa watu kuwa na tafsiri sahihi kuwa Aazory Gwanda amefariki.

Kakosea kwanza kwa kusema hivyo, halafu anaendelea kukosea kwa kushindwa kuomba radhi na kukubali kosa, analaumu tafsiri.
 
Unataka kutwambia kuwa watanzania woote 55m hawajui kiingereza?
Ujumbe tulioupata hapa ni kurudi darasani kujifunza lugha upya. Maana ni wengi tumemuelewa tofauti na alichokusudia kutueleza.
 
Huyo ndiye poropesa wetu nguri
Alipaswa kusema ‘waliopotea au kuuwawa’.

Siyo ‘waliopotea na kuuwawa’ maana hiyo inaacha mwanya wa tafsiri zingine.

Yeye kama mwanasheria nguli nilitegemea awe makini sana na uchaguzi wa maneno atumiayo.
 
Yeye ndiye anapaswa kurudi darasani kujifunza tofauti ya "disappeared and died" na "disappeared or died".

Kama hawa ndio watu wanaosimamia mikataba yetu, si ajabu tunapigwa changa la macho kila siku.

Ni kweli kabisa Mkuu,Neno moja hubadili maana ya Taarifa nzima katika tafsiri.Sisi tuna shika ile kauli ya Mwanzo.
 
Labda mimi ni mshauri tu professor Kabudi asiwe na pupa na papara anapongea na wanahabari kiukweli kauli yake haikua ina maanisha kupotea na kufa. But since he is on the side of the government any slip of a tongue in such issues is taken terribly serious! He should calibrate himself and adopt such communication skills that leaves no loopholes for misinterpretation of his verbal contents.
"Disappear and died" hapa alimaanisha kuwa kila mpoteaji hufa, therefor Gwanda kashakufa. Wewe ni nani kumsemea?
 
Utatetea hata visivyo stahili yaani anakana hata matamshi yake maana clip ipo
prof. hakukosea kabisa ila tumewazoea mkitengeneza tafsiri zenu mnapomchukia mtu na natambua Prof anachukiwa kwa nguvu na uwezo alionao katika kujenga hoja.

mlipokosea ni kudhani kwamba prof anaweza kuongea kama Sugu au Mbowe, lazima daima ujue kwamba yule mtu anapoongea anaongea mambo mazito na magumu kwa watanzania wengi kuyaelewa haraka
 
Nimesikiliza mara kadhaa yale mahojiano yaliyofanyika kwa lugha ya Kiingereza. Nikasikiliza pia alipohojiwa kwa lugha ya Kiswahili. Hakuna mahali prof Kabudi amesema Azory kafa. Sasa nimeamini kwamba ni kweli kuna watu wanatumia kila njia kuichafua serikali na viongozi wa nchi. Ni bahati mbaya sana.
"Disappear and die" tafsiri yake ni nini?
 
Aliyesema ni profesa na aliyefafanua ni daktari wa falsafa!
Hivi ukitoka kuwa Dk-PhD si ndio unakuwa profesa!? Tusaidiane maana wengine hatujui.
 
prof. hakukosea kabisa ila tumewazoea mkitengeneza tafsiri zenu mnapomchukia mtu na natambua Prof anachukiwa kwa nguvu na uwezo alionao katika kujenga hoja.

mlipokosea ni kudhani kwamba prof anaweza kuongea kama Sugu au Mbowe, lazima daima ujue kwamba yule mtu anapoongea anaongea mambo mazito na magumu kwa watanzania wengi kuyaelewa haraka
Mara ya kwanza niliamini sijamsikia akisema hivyo. Ikabidi nirudie kusikiliza mara 2 na bila shaka yeyote Prof. umpende usimpende aliyasema maneno hayo. Kitu cha kiungwana akubali tu kama amekosea na aombe radhi (ingawa sio kawaida yetu watanzania). Na kwa mwanasheria nilitegemea angekuwa makini zaidi. Hapa issue ya Mbowe na Sugu haingii kabisa Prof. ameharibu na Dr Abbasi angekaa mbali amuachie aliesema azungumze.
 
Ameonyesha umbilimbi wake
Alipohojiwa wakati ule wa Lissu ndipo nilipoamini kuwa uprofressor alinunua
Amelikoroga aandae vikombe kunywa uji mbichi
Karma is a bitch karibu mtasema ukweli
Sidhani kama alinunua uprofessor. Shida inakuja pale wanapoingia kwenye siasa wengi hawana experience na ndio yanapowakuta hasa wanapojaribu kutetea visiyo kuwa na utetezi. Asinge unganisha ya Azory na yaliyowakuta wengine labda asinge likoroga. Wote wakina Bashiru, Mwakyembe, Kitila haya yanawahusu. Na majaji wasiokuwa waangalifu pia wameingia mkenge wa kutumika na wanasiasa (Kaijage na Mutungi ni mifano mizuri). Ni vizuri hili limemkuta kama ni mahiri kama tunavyo ambiwa atajitafakari sana, kwa wastarabu leo angeachia ngazi.
 
Mara ya kwanza niliamini sijamsikia akisema hivyo. Ikabidi nirudie kusikiliza mara 2 na bila shaka yeyote Prof. umpende usimpende aliyasema maneno hayo. Kitu cha kiungwana akubali tu kama amekosea na aombe radhi (ingawa sio kawaida yetu watanzania). Na kwa mwanasheria nilitegemea angekuwa makini zaidi. Hapa issue ya Mbowe na Sugu haingii kabisa Prof. ameharibu na Dr Abbasi angekaa mbali amuachie aliesema azungumze.
Mkubwa huwa hakosei hasa kwa hadhi yake ya uwaziri na uprofesa wake. Tujifunze tu kumuelewa hata kama anachotueleza hatukielewi tumuelewe tu hivyo hivyo.
 
Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amekanusha kuwa amethibitisha 'kifo' cha mwanahabari Azory Gwanda.

Msemaji mkuu wa serikali ya Tanzania, Dkt Hassan Abbas amemnukuu Profesa Kabudi kwa kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twitter akisema: "Nimepokea kwa masikitiko taarifa potofu zinazoendelea kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii ikinukuu kimakosa mahojiano yangu kwenye kipindi cha BBC FOCUS ON AFRICA zikidai kuwa nimethibitisha kwamba mwanahabari Azory Gwanda amefariki dunia."

Lakini Prof Kabudi pia amesema bado haijulikani kama Bw Gwanda yungali hai: "Mpaka sasa hakuna uthibitisho kuwa Azory yuko hai au amefariki. Vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kuchunguza tukio hilo na matukio mengine yaliyotokea katika machafuko ya Kibiti, Pwani yaliyosababisha ama watu kadhaa kupoteza maisha au kupotea."

Kabudi amesema kuwa, kilichotokea ni tafsiri potofu ya kile alishokisema: "Hii sio tafsiri sahihi kuhusu kile nilichokisema. Katika mahojiano hayo nilieleza kuwa tukio lililotokea Kibiti lilikuwa ni la kuhuzunisha na wapo watanzania waliouawa na wengine kupotea. SIKUTHIBITISHA kuwa Azory Gwanda amefariki."
Sasa Kabudi kawa mwanasiasa kwelikweli. Hata anatakiwa kuchunga kauli zake.
 
Huyo jamaa anaonekana ni mbabaishaji flani hivi!

Nguli gani wa sheria hajui matumizi ya ‘na’ na ‘au’ na implications zake?

Hapo kwenye maelezo yake alipaswa tu kusema kuwa aliteleza kidogo na hakumaanisha kama ilivyopokelewa na watu.

Instead, he’s doubling down on it and blaming others!

Ndo maana baadhi yetu tuliguna na kukuna vichwa vyetu tuliposikia kateuliwa kuwa waziri wa mambo ya nje.
....who disappeared and died/....who disappeared and who died/....who disappeared OR died....Kidhungu kigumu!
 
Back
Top Bottom