Waziri Katambi: Vijana ambao hawajapata mikopo ya Halmashauri pengine ni Wakenya

Waziri Katambi: Vijana ambao hawajapata mikopo ya Halmashauri pengine ni Wakenya

Miaka yote naamini mimi ni Mtanzania. Nina Kitambulisho cha Nida, Napiga Kura, nina Passport. Kumbe si Mtanzania.

Kwa kauli ya Katambi nmevuliwa nguo kabisa. Wazazi hawakuwahi kunambia mpaka Waziri leo ndo kasema. Sielewi hata huko Kenya ndugu zetu ni Kabila gani. Nmechanganyikiwa sana...
Usiume sana kijana,piga mahesabu tu,nchini hapa tupo jumla ya watu milioni 60!kama vijana ni milioni 30,hizo bilioni 150,ukizigawa kwa vijana kila mmoja anapata buku Tano tu!!!hata kilo ya nyama hainunui!!
 
Serikali ya Tanzania imedai bungeni leo kwamba imekwisha mwaga kitita cha Tsh Bilioni 150 kwa Halmashauri zote nchini , kwa lengo la kutoa Mikopo kwa Vijana ( MAMA ANAUPIGA MWINGI ) , Na kwamba Vijana wote wa Kitanzania waliohitaji Mikopo hiyo wamekwisha pata na wanaendelea na shughuli zao za ujasiria mali kama kawaida , na KWAMBA KAMA KUNA KIJANA ALIYEHITAJI PESA HIZO NA HAJAPATA BASI LABDA NI MKENYA .

Taarifa hiyo Nzuri , kabambe na ya kutia moyo imetolewa na Naibu Waziri Mh Katambi kwenye vikao vya bunge vinavyoendelea Dodoma .

Mungu ibariki Tanzania .
 

Si kweli kwamba vijana wa nchi hii hupata mikopo bali mikopo yote ihusuyo vijana hugawanwa na Viongozi wa chama tawala na vijana wao nao ni wale tu walio na connection.

Katambi acha dharau na hilo litakukosesha jimbo.

===
Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 18, 2022, bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalum Sophia Mwakagenda, alilohoji kuhusu vijana kutopata ajira kwa zaidi ya miaka 6 sasa pamoja na kwamba mfumo wa utoaji wa mikopo katika Halmashauri kwa vijana mfumo umewatupa nje.

"Sisi kama serikali tunazotakwimu za vijana hawa, na wale wote wanaofanya application za ajira, vyuo vikuu vyote tumekuwa tukipata taarifa, tunao vijana zaidi ya laki mbili wanaoingia kwenye soko la ajira kutoka vyuo mbalimbali, pia tuna mifumo na programu tunazoziandaa ikiwa ni pamoja na internship, kuangaliziwa ajira ndani na nje ya nchi,"amesema Katambia

Aidha Katambi ameongeza kuwa, "Tumekuwa tukiendelea kutoa mikopo na zaidi ya bilioni 150 zimekwishakutolewa kwa vijana mbalimbali, kama kuna vijana ambao wapo labda pengine sio Watanzania ni Wakenya utanisaidia niweze kuwaingiza hapa tuone namna gani tunawasaidia,"
Nchi hii ngumu sana wasukuma wanalewa madaraka mapema sana
 
Hiyo mikopo inaishiaga mifukoni mwao. Procedure zenyewe za kuipata ni shughuli pevu.
 
Serikali ya Tanzania imedai bungeni leo kwamba imekwisha mwaga kitita cha Tsh Bilioni 150 kwa Halmashauri zote nchini , kwa lengo la kutoa Mikopo kwa Vijana ( MAMA ANAUPIGA MWINGI ) , Na kwamba Vijana wote wa Kitanzania waliohitaji Mikopo hiyo wamekwisha pata na wanaendelea na shughuli zao za ujasiria mali kama kawaida , na KWAMBA KAMA KUNA KIJANA ALIYEHITAJI PESA HIZO NA HAJAPATA BASI LABDA NI MKENYA .

Taarifa hiyo Nzuri , kabambe na ya kutia moyo imetolewa na Naibu Waziri Mh Katambi kwenye vikao vya bunge vinavyoendelea Dodoma .

Mungu ibariki Tanzania .
Wapiga makofi/wagonga meza nao hawakuwa nyuma kama kawaida yao.
 
Nchi hii basi imejaa wakenya, watanzania wajitokeze tuwajue!
Aaaagh nimechokaaah! Seriously mwenye njaa hawezi tambuliwa na mwenye shibe!
 

Si kweli kwamba vijana wa nchi hii hupata mikopo bali mikopo yote ihusuyo vijana hugawanwa na Viongozi wa chama tawala na vijana wao nao ni wale tu walio na connection.

Katambi acha dharau na hilo litakukosesha jimbo.

===
Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 18, 2022, bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalum Sophia Mwakagenda, alilohoji kuhusu vijana kutopata ajira kwa zaidi ya miaka 6 sasa pamoja na kwamba mfumo wa utoaji wa mikopo katika Halmashauri kwa vijana mfumo umewatupa nje.

"Sisi kama serikali tunazotakwimu za vijana hawa, na wale wote wanaofanya application za ajira, vyuo vikuu vyote tumekuwa tukipata taarifa, tunao vijana zaidi ya laki mbili wanaoingia kwenye soko la ajira kutoka vyuo mbalimbali, pia tuna mifumo na programu tunazoziandaa ikiwa ni pamoja na internship, kuangaliziwa ajira ndani na nje ya nchi,"amesema Katambia

Aidha Katambi ameongeza kuwa, "Tumekuwa tukiendelea kutoa mikopo na zaidi ya bilioni 150 zimekwishakutolewa kwa vijana mbalimbali, kama kuna vijana ambao wapo labda pengine sio Watanzania ni Wakenya utanisaidia niweze kuwaingiza hapa tuone namna gani tunawasaidia,"
Huyu inabidi akamatwe na kutiwa ndani au hata kupigwa vidole tu ili ashike adabu
 
Back
Top Bottom