Waziri Kigwangalla awacharukia wanaomsema hajui Kiingereza

Waziri Kigwangalla awacharukia wanaomsema hajui Kiingereza

Atakuwa Prof Karim Manji huyo?
Sky Eclat pitia hapa

Tulikuwa na tabia ya kupika wali kwenye ‘rice cooker’. Aliyekuwa Mrajis Msaidizi wakati huo alipiga marufuku, kwa sababu za kiusalama. Hatukuacha. Tulijificha zaidi.

Siku moja akafanya ukaguzi wa kushtukiza. Dogo alikuwa anapika. Mimi sipo. Watu wakakimbia wakaambizana. Dogo naye akapata taarifa. Akatorosha vyombo na misosi yote kwa dirishani, baada ya kufunga mlango kwa ndani na yeye akatoroka. Sijui alitorokaje. Ilikuwa floor ya kwanza!

Harufu ya wali iliyojaa chumbani ilisaliti. Profesa alikagua chumba hadi chumba huku akinusa harufu. Akabaini ni chumbani kwangu. Alikijua fika maana kilikuwa cha Rais mstaafu. Akafungua kwa ‘Master Key’ yake. Hakukuta mtu. Akaweka ‘lock’ ili nikirudi nikaripoti ndipo nifunguliwe.

Nikaarifiwa nikawahi maana la sivyo dogo angepata shida pa kulala. Mimi nilikuwa nishaoa na nimepanga Msasani. Kipindi hicho nilikuwa mwaka wa tano. Nililala chumbani pale mara chache tu nilipokuwa najisomea usiku wodini pamoja na wenzangu.

Nilipomfuata Prof., aling’aka kwa hasira, kwa kuwa hakuwa na ushahidi, na kwa kisirani, akanirudishia funguo zangu huku akiapa kunikomesha! Alianza kunitafuta darasani. ‘Akanikamata!’ #NjeYaBox #HK
 
naunga mkono hoja,kutojua lugha fulani hakuondoi usomi wa mtu,,ila kwa nchi yetu ukijua kiingereza tu basi utatazamwa kwa jicho tofauti,,,
humu ndani kuna "nyani" bingwa wa kiingereza hatari,ukibahatika kujua kiingereza kama cha yule kwa nchi yetu wewe ni msomi hata kama ni la saba
Elimu yote ya juu inafundishwa kwa Kiingereza sasa utakuwaje msomi Kama hujui Kiingereza? Na uliwezaje kufaulu Kama Kiingereza hujui?
 
Huku tunafika mbali.

Tusisujudie lugha ya utumwa na kudharau yetu ambayo Mwalimu Nyerere alipambana mno kuhakikisha Kila mtu anaizungumza...

Ufaransa, Ujerumani, Uchina, Urusi, Japan, South Korea, India na wengineo wote ambao wana nguvu wanatumia lugha yao....

Jifunzeni kuheshimu vya kwenu.

NYUMBANI NI NYUMBANI
Ngeli ya Nyerere ilikua ni usipime mzee baba,watu waliosoma masters za huko edenburg mwaka1958 huwezi kuwalinganishana na PH.d za hawa masela wa pale mabibo.
 
Tuna uwezo wa kuwa na wakalimani.

Mtu kutokujua Lugha ya malkia isiwe sababu ya yeye kutokupata nafasi.

Ukienda China Hadi mikataba na mataifa au makampuni ya uwekezaji ya nje wanaandika kichina, kwahiyo inakuwa juu yako kutafuta mtafsiri au mkalimani.

Haya mazungu haya tunayanyenyekea ila sio mazuri , angalia mfano mbichi tu wa Georgee Floyd. Hivyo haina haja ya kuyashobokea.
Sasa ulitaka wachina wajuaje kiingereza wkt wao from elementary schools to university wamesoma kwa kichina,huoni ajabu mtu from form 1 to university(degree,masters,PH.d) anatumia kiingereza lkn mpk leo hakijui?
 
Mliosoma English medium mtatujuza hapa.

Screenshot (3).png
 
Matatizo ya kuongea kiswahili kimoyo moyo na kubadilisha kwenda kingereza kumbe tunayo wengi. Siku prof ndalichako anamfokea mkandarasi wa kichina kwa kingereza nilitamani nizikwe kwa vichekoooo
 
Mimi kipindi kiingereza kipo sheki nilibahatika kukutana na Natives wenyewe,Americans. Waligundua kiingereza si lugha yangu hivyo wakawa wananiongelesha kwa spidi ndogo ili nielewe na mimi nikawa najibu kwa uwezo wangu na nikawa naeleweka.Ila kuna Mkenya fulani tulikuwa naye yeye alikifahamu sana tu na akawa anaona atapata ujiko zaidi kwa udhaifu wangu.Ila chakushangaza kazi nyingi zikawa zinakuja kwangu.
Siku moja nikawauliza mabosi wetu kulikoni,mbona mimi napata kazi nyingi kuliko yule jamaa.Wakasema wamependa jinsi ninavyofanya kazi zangu.Nikawauliza kuhusu lugha yangu sababu mwenzangu accent yake ilikuwa nearly American.Wakasema hilo nisijali,kwa spirit niliyonayo ntajua tu.Mwisho wakaniambia wanaenjoy kusikia Foreign Accent.
Baadaye kikakaa kichwani,japo si kivile.Sasa WaTz wenzangu huu ujasiri wa kuchekana kwenye lugha za kigeni sijui tunautoa wapi.
Umeongea kitu niliwahi kusikia sehemu, éti hawafurahii sana mtu kuongea lugha yao huku akijitahidi kufata accent yao. Wanasema wanafurahi kukusikia ukiongea kwa accent ya kwenu. Kweli kabisa
 
Bora asingewajibu[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Umeongea kitu niliwahi kusikia sehemu, éti hawafurahii sana mtu kuongea lugha yao huku akijitahidi kufata accent yao. Wanasema wanafurahi kukusikia ukiongea kwa accent ya kwenu. Kweli kabisa
Yeah boss ipo hivyo. Nawakubali sana hapo hawa watu.
 
People argue geography, others know English, dadeq!!
 
Haya ni matokeo ya "kujifunza lugha na kujifunza kuhusu lugha"
 
Kigwangalla awacharua wanaomsema hajui kingereza asema sio sifa kuijua

Waziri wa Maliasilia na Utalii, Dk. Hamis Kigwangalla amesema kuna watu huwa wanajaribu kumkosoa lugha yake ya kingereza.

“Huwa nina washangaa sana maana kwanza siyo sifa kujua lugha hiyo mimi naitumia kama njia ya kuwasiliana tu,” aliandika Kigwangalla katika ukurasa wake wa Twitter.

Aliongezea kuwa “Ningekuwa sijui kiswahili ama kikimbu na mtu akanicheka angekuwa na mantiki.

View attachment 1471687

Waziri anaihifadhi lugha ya Kiingereza kuwasiliana na watalii na katika masuala ya kikazi tu. Hapendi ujinga.
Akaazime kile Cha Mama wa Elimu,
"Put him inside"
 
.................................................................[snip]
Baadaye kikakaa kichwani,japo si kivile.Sasa WaTz wenzangu huu ujasiri wa kuchekana kwenye lugha za kigeni sijui tunautoa wapi.
Hiyo ni kawaida ya watu waliotawaliwa na kudhalauliwa. Huwa wakiachiwa uhuru bado wanapenda kuwa karibu na mtawala wao; kwa lugha, kwa kuvaa, kwa kutembea, n.k. TZ akina Kambona walikuwa bado wanachana nywele na kuzipasua kichwani kama mwingereza. Lugha ndo kabisaa! Hadi leo unaweza kupewa ajira kwa kuwakoga watu kwenye interview, hata kama taaluma ni sifuri.

Hapa JF utaona bado kuna watu wanazoza kwa kutamani sifa hiyo ingawa ukiwajaribu kwa thrd ya english, utaona wachangiaji wanapungua.
 
Back
Top Bottom