Waziri Lukuvi: Kuanzia sasa ukiwa na kiwanja kinatakiwa kiitwe kwa jina lako na la mke wako

Waziri Lukuvi: Kuanzia sasa ukiwa na kiwanja kinatakiwa kiitwe kwa jina lako na la mke wako

Kwani unafikiri hata sasa hivi Bank inachukua hati bila kibali cha mke au mme kama mali ni ya familia? Fanya utafiti kidogo kabla ya kuja na comment hapa mkuu!
Na bank wakijaribu kuchukua hati bila consent ya mke, mdaiwa akishindwa kulipa mkopo bank hawawezi kuichukua mali ya familia km itathibitika mahakamani mke hakuwa na taarifa juu ya huo mkopo.
 
Binafsi kwenye maelezo yake sijaona tamko lolote. Naona ameleta awareness tu kwenye sheria iliyopo kuwa iko flexible.
 

Serikali imesema sheria inaruhusu hati ya kumiliki viwanja kuandikwa majina ya familia ikiwemo mume, mke pamoja na watoto hatua ambayo itasaidia kuondoa migogoro ya mirathi.

Akizungumza leo Jumamosi Desemba 19, mkoani Kilimanjaro. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wiliamu Lukuvi amesema kwa sasa wizara hiyo inasajili majina hayo na kwamba Watanzania watumie fursa hiyo vema kupunguza migogoro ya mirathi.

“Sisi katika wizara hii na serikalini humu tunapata shida sana ya kushughulikia mambo ya mirathi,wizara inakubali kusajili hati kwa majina zaidi ya mawili hata ukita baba,mama na watoto kusajili hati Moja inaruhusiwa hii inasaidia kuepusha matatizo ya miradhi hapo baadae,” amesema Lukuvi.

Aidha, Waziri Lukuvi ametoa wito kwa Watanzania wote kuona umuhimu wa kufanya hivyo kutokana na kwamba keai nyingi za miradhi huwa na changamoto nyingi”alisema

“Kesi nyingi za mirathi wanakuja wajomba ambao hawakujua jasho lenu ambalo mmelichuma wanaandika hati wao wanajimilikisha hiyo ni fursa kwa wananwake…washawishini waume zenu wakati wa kuandika hati mje na majina yenu wote…hata kama umeoa wanawake watatu, sheria ipo wazi,ukija na jina la mtoto chini ya miaka 18 tutasajili jina lake na msimamizi wake.

“Ndoa zote tutaandikisha, akifa mke mmoja inafahamika kwamba haki iliyobaki ni ya wake wawili waliobaki na kwa upande wa mtoto akifikisha miaka 18 kunauwezekano wa kufuta majina ya awali ya wazazi na kumuachi mtoto,” amesema Lukuvi.

Aidha amesema utaratibu huo ikifiatwa hakutakuwa na vikao vya familia vya miradhi na migogoro isiyo ya lazima.

“Sio lazima kwamba mtu alitaka hati aje na mme wake zao Ila ni jukumu langu kuwalemisha kwamba Hilo linawezek,” amesema.

Mtanzania
Mturuhusu na akina Joyce Mukya tuwaandikishe maana huku vyumbani ni balaa.
 

Serikali imesema sheria inaruhusu hati ya kumiliki viwanja kuandikwa majina ya familia ikiwemo mume, mke pamoja na watoto hatua ambayo itasaidia kuondoa migogoro ya mirathi.

Akizungumza leo Jumamosi Desemba 19, mkoani Kilimanjaro. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wiliamu Lukuvi amesema kwa sasa wizara hiyo inasajili majina hayo na kwamba Watanzania watumie fursa hiyo vema kupunguza migogoro ya mirathi.

“Sisi katika wizara hii na serikalini humu tunapata shida sana ya kushughulikia mambo ya mirathi,wizara inakubali kusajili hati kwa majina zaidi ya mawili hata ukita baba,mama na watoto kusajili hati Moja inaruhusiwa hii inasaidia kuepusha matatizo ya miradhi hapo baadae,” amesema Lukuvi.

Aidha, Waziri Lukuvi ametoa wito kwa Watanzania wote kuona umuhimu wa kufanya hivyo kutokana na kwamba keai nyingi za miradhi huwa na changamoto nyingi”alisema

“Kesi nyingi za mirathi wanakuja wajomba ambao hawakujua jasho lenu ambalo mmelichuma wanaandika hati wao wanajimilikisha hiyo ni fursa kwa wananwake…washawishini waume zenu wakati wa kuandika hati mje na majina yenu wote…hata kama umeoa wanawake watatu, sheria ipo wazi,ukija na jina la mtoto chini ya miaka 18 tutasajili jina lake na msimamizi wake.

“Ndoa zote tutaandikisha, akifa mke mmoja inafahamika kwamba haki iliyobaki ni ya wake wawili waliobaki na kwa upande wa mtoto akifikisha miaka 18 kunauwezekano wa kufuta majina ya awali ya wazazi na kumuachi mtoto,” amesema Lukuvi.

Aidha amesema utaratibu huo ikifiatwa hakutakuwa na vikao vya familia vya miradhi na migogoro isiyo ya lazima.

“Sio lazima kwamba mtu alitaka hati aje na mme wake zao Ila ni jukumu langu kuwalemisha kwamba Hilo linawezek,” amesema.

Mtanzania
Shida ni kuna wanawake nyoka mfano wa hua(Njiwa)
 
Lukuvi anasema 'hati inaruhusu' sasa wasoma vichwa vya habari mnaanza kumponda mzee wa watu bure. Yeye anasema inaruhusiwa katika hati kuandika majina ya mke watoto n.k ili kuelusha migogoro. Akashauri hasa wanawake watumie fursa 'kuwashawishi' waume zao kiwaandika. Msimshambulie mzee wa watu jamani hajawalazimisha na wala sheria hailazimishi.
 
Waziri angefanya kwanza consultation
Sheria ya ndoa ya 1971 inaruhusu kila mwana ndoa kumiliki mali separate
How under this juncture be applicable
 
Jamani waheshimiwa hii sio lazima 😊

Waziri katoa ushauri tu
 
Kama nimeelewa ni kwamba kwa sasa upo huo uwezekano wa kuandikisha Mke, Mume n.k.....sidhani kama amesema ni lazima maana nasoma baadhi ya comment naona Watu wanatanguliza tu mihemuko.
 
Nnaona mna comment kwa mhemko, mamlaka ya kufanya hivyo yapo wazi na ni suala la wake zetu kutushawishi, hata kwa ndumba tukawaweke kwenye hati ila siyo lazima
 
Waziri ameghafilika tu hakuna hitaji la kisheria kama hilo.
 
Back
Top Bottom