Waziri Lukuvi: Kuanzia sasa ukiwa na kiwanja kinatakiwa kiitwe kwa jina lako na la mke wako

Waziri Lukuvi: Kuanzia sasa ukiwa na kiwanja kinatakiwa kiitwe kwa jina lako na la mke wako


Serikali imesema sheria inaruhusu hati ya kumiliki viwanja kuandikwa majina ya familia ikiwemo mume, mke pamoja na watoto hatua ambayo itasaidia kuondoa migogoro ya mirathi.

Akizungumza leo Jumamosi Desemba 19, mkoani Kilimanjaro. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wiliamu Lukuvi amesema kwa sasa wizara hiyo inasajili majina hayo na kwamba Watanzania watumie fursa hiyo vema kupunguza migogoro ya mirathi.

“Sisi katika wizara hii na serikalini humu tunapata shida sana ya kushughulikia mambo ya mirathi,wizara inakubali kusajili hati kwa majina zaidi ya mawili hata ukita baba,mama na watoto kusajili hati Moja inaruhusiwa hii inasaidia kuepusha matatizo ya miradhi hapo baadae,” amesema Lukuvi.

Aidha, Waziri Lukuvi ametoa wito kwa Watanzania wote kuona umuhimu wa kufanya hivyo kutokana na kwamba keai nyingi za miradhi huwa na changamoto nyingi”alisema

“Kesi nyingi za mirathi wanakuja wajomba ambao hawakujua jasho lenu ambalo mmelichuma wanaandika hati wao wanajimilikisha hiyo ni fursa kwa wananwake…washawishini waume zenu wakati wa kuandika hati mje na majina yenu wote…hata kama umeoa wanawake watatu, sheria ipo wazi,ukija na jina la mtoto chini ya miaka 18 tutasajili jina lake na msimamizi wake.

“Ndoa zote tutaandikisha, akifa mke mmoja inafahamika kwamba haki iliyobaki ni ya wake wawili waliobaki na kwa upande wa mtoto akifikisha miaka 18 kunauwezekano wa kufuta majina ya awali ya wazazi na kumuachi mtoto,” amesema Lukuvi.

Aidha amesema utaratibu huo ikifiatwa hakutakuwa na vikao vya familia vya miradhi na migogoro isiyo ya lazima.

“Sio lazima kwamba mtu alitaka hati aje na mme wake zao Ila ni jukumu langu kuwalemisha kwamba Hilo linawezek,” amesema.

Mtanzania
Huyu jamaa anazeeka vibaya..Spouse consent inatosha...awe mke au Mume. Kama mmeweza kuiba kura katika uchaguzi mkuu mnadhani yakiwekwa majina mawili kuchakachuka kutaisha?>
 
Heading na maelezo vinatofautiana.

Waziri ameshauri hajalazimisha. Mleta mada amepotosha.
 
Wana Habari mnadhalilisha taaluma yenu.

Lukuvi wote tumemsikia, hajasema hayo maneno. Of course sijasoma habari yako yote nimeona imejaa upuuzi tu.

Alichosema Lukuvi ni kwamba anatoa wito kwa wamama kushawishi waume zao pale wanapomilikishwa viwanja basi Hati za viwanja hivyo viwe pia na majina yao.

Hivyo ni suala la wito tu.
 
Kama nimeelewa ni kwamba kwa sasa upo huo uwezekano wa kuandikisha Mke, Mume n.k.....sidhani kama amesema ni lazima maana nasoma baadhi ya comment naona Watu wanatanguliza tu mihemuko.
Halafu hilo suala halijaanza sasa. Limekuwepo muda mrefu sana. Tuna viwanja vina majina mpaka ya watoto (minors) vinakuwa chini ya waangalizi (guardians).
 
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema sheria inaruhusu kuandikwa majina yote mawili ya wenza katika hati za umiliki ardhi na Wizara ya Ardhi imekuwa ikisajili Hati nyingi zenye majina yote mawili ya wenza na wengine husajili na majina ya watoto wao.
 
Kwani unafikiri hata sasa hivi Bank inachukua hati bila kibali cha mke au mme kama mali ni ya familia? Fanya utafiti kidogo kabla ya kuja na comment hapa mkuu!
Kwani unafikiri hata sasa hivi Bank inachukua hati bila kibali cha mke au mme kama mali ni ya familia? Fanya utafiti kidogo kabla ya kuja na comment hapa mkuu!
Hilo kila mtu analijua " spouse consent" hoja yangu iko kwenye utitiri wa beneficiaries wote kuandikwa kwenye title ina sense gani?! Ni upuuzi tu!
 
Hapo kwenye kuweka jina la watoto sawa....ila kuweka jina la hawa viumbe wengine kunawatengenezea picha kichwan mwao ambazo hatuzijui kabisa.
 
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema sheria inaruhusu kuandikwa majina yote mawili ya wenza katika hati za umiliki ardhi na Wizara ya Ardhi imekuwa ikisajili Hati nyingi zenye majina yote mawili ya wenza na wengine husajili na majina ya watoto wao.
Safi sana
 
Back
Top Bottom