Waziri Mahiga: Serikali ya Uturuki imetuambia wamiliki wa shule za Feza ni magaidi

Waziri Mahiga: Serikali ya Uturuki imetuambia wamiliki wa shule za Feza ni magaidi

mimi ni mmoja wa wanafunzi nimesoma apo FEZA o-level na high-level. shule za FEZA hazina mtaala wowote unaofundisha ugaidi.

shule ina walimu mchanganyiko waturuki na watanzania. wanafunzi wengine niliosoma nao sasa hivi ni walimu apo FEZA. kwa mfano mkuu wa shule ya FEZA boys alisoma apo O-level baadae akafanya bachelor Uturuki na masters kafanya UDSM.

miaka yote iyo tumesoma mpaka sasa kila mtu anafanya maisha yake sijawahi kusikia ata siku moja mwanafunzi yeyote wa FEZA ambaye amefanya tukio la kigaidi. wengi wetu tumekua watu wema kutokana na mafunzo mazuri tuliyopata pale shuleni.

nimewahi kua moja wa kiongozi wa wanafunzi ila hakuna ata siku moja ambayo tumeelekezwa tufanye tukio la ovyo. shule ziko serious na elimu pekee. shule za FEZA zinajiendesha kutoakana na ada wanazolipa wazazi wa wanafunzi matajiri pia wanafunzi maskini wanasomeshwa kutokana na michango ya wazazi matajiri na baadhi ya wanafunzi waliosoma apo ambao asilimia kubwa wamefanikiwa kimaisha.

ivyo basi kwa mimi binafsi naweza kusema kuwa shule za FEZA hazina uhusiano wowote ule na ugaidi. Uturuki raisi Erdogan amevurugwa tu kutokana na sera zake za ovyo za kuminya demokrasia na ndio maana mpaka leo umoja wa ulaya (EU) wameshindwa kuiruhusu uturuki kujiunga na umoja huo kutokana na uvunjifu mkubwa wa demokrasia.

Waturuki ni watu wanapenda sana biashara na wamesambaa kila kona ya dunia na wamechangia kukua kwa uchumi kwa nchi mbalimbali duniani kwa kutoa ajira kwa wazawa wa mataifa ambayo wanawekeza. kwa mfano ukienda Poland, Germany na mataifa mengi tu ya ulaya jamaa wametoa ajira kwa mamilioni ya watu.

kwa mfano rafiki zangu wengi tu hapa bongo na ata nje ya nchi wanafanya kazi na waturuki na wako vizuri tu. Fethullah Gullen yeye sio mmiliki wa shule za FEZA ila yeye alitoa idea kwa waturuki kuanzisha mashule nje ya uturuki ili kutoa elimu bora kwa mataifa mbalimbali duniani.

Hachangii na wala hapewi ata senti kutoka kwenye shule. uwekezaji hapa bongo wote umefanywa kutokana na ada na michango ya watanzania wachache ambao wameshawishika kuchangia shule.

rafiki yangu mmoja baba yake mzazi ametoa tiles za shule nzima for free. mimi pamoja na wanafunzi wengine tumeshapiga rangi sana shule za FEZA kwa kujitolea. ivyo basi naweza sema shule za FEZA hazina uhusiano wowote ule ayo mambo yao ya ndani ya uturuki wajaribu kumalizana nayo wenyewe.

huo ubalozi kama unajua kuhusu iyo michango ya kigaidi basi wafungie hizo account ambazo zinapewa iyo misaada. Nigeria wamemgomea Erdogan na serikali yake kuhusu kufunga shule za aina ya FEZA ambazo zipo Uturuki ivyo serikali yetu isiyumbishwe kutokana na uyo Erdogan.

shule hizi zinazalisha wataalamu wakutosha ambao wana mchango mkubwa tu kwa taifa ili. rafiki zangu wengi tu sasa hivi ni madiktar katika hospitali za hapahapa nchini, wengine mainjia wazuri tu na wanasaidia mambo mbalimbali.
 
The bottom line of the entire story ni udini. Shule za FEZA ndio zilionekana kutoa upinzani mkalikwa shule za makanisa na hili lilikuwa halifurahiwi. Kama zilikuwa zinatumia mbinu za kigaidi kufundishia wanafunzi(sijui ndio maana wanafanya vizuri mitihani yao) Serikali ilikuwa wapi wakati wote huo " isiwashughulikie"? Wacheni unafiki wa kidini tena kweupe
Sasa n'jomba kwani hili sakata limeanzishwa na makanisa hapa bongo au limetoka Uturuki??!!
Watu wengine buana
 
Ujinga ni kubishana bila kuelewa mada, mapovu tu! Mimi nadhani haya mambo ya kidini tusiyatangulize kwa kila kitu. Dini bila kuwa wewe kwanza si dini hyo. Hata usipoelewa unachofundishwa na dini yako kwa tabia za kibishi utakwenda jahanam tu. Tusome mawazo ya wenzetu, tuyatafakari alafu tujibu hoja kwa hoja! Kwa kufanya hvo JF itakuwa sehemu nzuri sana kwa kujiongezea maarifa na kuelewa mambo yanayoendelea duniani kwa undani, vinginevyo ukiingia huku unaumua tu.

UISLAMU NI MZURI ila kuna WAISLAMU WASIO WAZURI NA HUCHAFUA UISLAMU.
UKRISTO NI MZURI ILA KUNA WAKRISTO WASIO WAZURI WANAOHARIBU UKRISTO.​
Same kwa dini zote.
Upendo una maana sana kuliko dini zetu!
Madhara ya mambo ya kidini kwenye kila post au kila mahali ni hatari sana jamani, tusiyaombee tutalia.

Mwisho wa siku we are relatives, friends from and living in the same place, planet Earth.

Tuheshimu dini za wenzetu wawe na amani na furaha na hvyo kufanya dunia kuwa sehemu nzuri ya kuishi.
 

Attachments

  • WeareOne.jpg
    WeareOne.jpg
    15.4 KB · Views: 78
Unamaanisha shule za FEZA ni za upande flani na siyo za yule mturuki?
Taarifa zimepelekwa kwa hao jamaa kua huku tanzania kuna shule ya upande fulani imeanza kufaulisha sana tufanyeje ili tuiue tubaki na shule zetu?kwa vile nchi yetu ni ya upande fulani basi wakatoa ushirikiano haraka sana.
 
Kwa hiyo ao walimu wanaotumia mbinu za kigaidi kufundishia wameshakamatwa?
 
Hiyo kauli ya serikali ya Uturuki ni ya kipuuzi kabisa. Shule za FEZA zipo kwenye mataifa mbalimbali zaidi ya 50. Watoto wangu 3 wamesoma FEZA, Mmojawapo akiwa amejiunga mwaka huu. Wawili wa mwanzo waliwahi kutembelea Uturuki mara 2 wakiwa masomoni kwaajili ya mashindano mbalimbali. Wakiwa huko walitembelea majimbo na vyuo vikuu mbalimbali wakikaribishwa na viongozi wa majimbo wa serikali ya Uturuki. Ina maana sahizi ndiyo wamegundua kuwa shule hizo ni za kigaidi? Kwa nini haikusemwa miaka ya huko nyuma?

Huyu Waziri Mkuu alikwishawahi kufungwa alipokuwa mwanachama wa Islamic Party na anatajwa kuwa ni mdini, na wengi wanaomuunga mkono ni wale wenye siasa za mlengo wa kidini, sasa anawageuzia wapinzani wake. Huyu naona ameamua kuiga siasa za baadhi ya viongozi wa Kiafrika, usipokubaliana nao wanataka usifanikiwe katika shughuli zako nyingine ambazo una haki za kikatiba.
 
..wachangiaji wanakosea kulichukulia suala hili kirahisi-rahisi.

..wamiliki wa shule za Feza wanatuhumiwa kuhusika na UHAINI nchini kwao. Hizi ni tuhuma nzito.

..kama nchi tunatakiwa tuwe makini sana na watu hao.

..tuangalie maslahi mapana ya nchi yetu KIUCHUMI na KIUSALAMA.
Kanisa katoliki lilishiriki kwa kiasi kikubwa mauaji ya kimbari Rwanda,Tanzania tuwe makini na kanisa hilo na shule zake
 
Serikali ya Tanzania yasema haina ushahidi wa kutosha kuzitia hatiani shule za Feza zinazodaiwa kumilikiwa na raia wa Uturuki anayetuhumiwa kujihusisha na jaribio la kupindua Serikali ya Uturuki.

Serikali ya Uturuki inadai wamiliki wa shule hizo na baadhi ya wafanyabiashara wanafadhili ugaidi kwa kushirikiana na Imamu Fethullah Gulen anayeishi nchini Marekani ambaye ndio inadaiwa yuko nyuma ya jaribio la Mapinduzi.

= > Serikali ya Uturuki yatakiwa kuwasilisha taarifa zenye ushahidi wa kutosha juu ya hili.

= > Aidha, Ubalozi wa Uturuki Tanzania umedai kuwa baadhi ya walimu wa shule za FEZA ambao ni raia wa Uturuki wamekuwa wakitumia mbinu za kigaidi kufundisha wanafunzi.



Feza wakanusha kuhusika



Sio vizuri kupuuza mambo lakini ni vizuri serikali ya uturuki ithibitishe hayo kwa ushahidi
 
Waturuki wenyewe wanasema FEZA ni magaidi alafu nyie wabongo mnaleta ubishi..... Povu jingi..... Subirini muone
Umeona ee. Yaani Watanzania wanawajua zaidi waturuki kuliko waturuki wenzao!
 
Mi nadhan kuna haja ya kulifuatilia hili kwa undani lisemwalo lipo kama halipo laja waturuki wanaofantlya biashara wapo weng dunian kwanin FEZA itajwe TISS inapaswa kufuatilia hili kwa kushirikiana na wenzao wa turkey vinginevyo baadae ikibainika ni kweli bas tutaonekana hatuna vyombo vya usalama vyenye weledi na ni fedheha kubwa sana kama taifa.
 
Waturuki wenyewe wanasema FEZA ni magaidi alafu nyie wabongo mnaleta ubishi..... Povu jingi..... Subirini muone

Nimelipenda andiko lako...watu 'wakifumuliwa' hapa tusianze kutafutana na kushutumiana humu....
 
mimi ni mmoja wa wanafunzi nimesoma apo FEZA o-level na high-level. shule za FEZA hazina mtaala wowote unaofundisha ugaidi. shule ina walimu mchanganyiko waturuki na watanzania. wanafunzi wengine niliosoma nao sasa hivi ni walimu apo FEZA. kwa mfano mkuu wa shule ya FEZA boys alisoma apo O-level baadae akafanya bachelor Uturuki na masters kafanya UDSM. miaka yote iyo tumesoma mpaka sasa kila mtu anafanya maisha yake sijawahi kusikia ata siku moja mwanafunzi yeyote wa FEZA ambaye amefanya tukio la kigaidi. wengi wetu tumekua watu wema kutokana na mafunzo mazuri tuliyopata pale shuleni. nimewahi kua moja wa kiongozi wa wanafunzi ila hakuna ata siku moja ambayo tumeelekezwa tufanye tukio la ovyo. shule ziko serious na elimu pekee. shule za FEZA zinajiendesha kutoakana na ada wanazolipa wazazi wa wanafunzi matajiri pia wanafunzi maskini wanasomeshwa kutokana na michango ya wazazi matajiri na baadhi ya wanafunzi waliosoma apo ambao asilimia kubwa wamefanikiwa kimaisha. ivyo basi kwa mimi binafsi naweza kusema kuwa shule za FEZA hazina uhusiano wowote ule na ugaidi. Uturuki raisi Erdogan amevurugwa tu kutokana na sera zake za ovyo za kuminya demokrasia na ndio maana mpaka leo umoja wa ulaya (EU) wameshindwa kuiruhusu uturuki kujiunga na umoja huo kutokana na uvunjifu mkubwa wa demokrasia. Waturuki ni watu wanapenda sana biashara na wamesambaa kila kona ya dunia na wamechangia kukua kwa uchumi kwa nchi mbalimbali duniani kwa kutoa ajira kwa wazawa wa mataifa ambayo wanawekeza. kwa mfano ukienda Poland, Germany na mataifa mengi tu ya ulaya jamaa wametoa ajira kwa mamilioni ya watu. kwa mfano rafiki zangu wengi tu hapa bongo na ata nje ya nchi wanafanya kazi na waturuki na wako vizuri tu. Fethullah Gullen yeye sio mmiliki wa shule za FEZA ila yeye alitoa idea kwa waturuki kuanzisha mashule nje ya uturuki ili kutoa elimu bora kwa mataifa mbalimbali duniani. Hachangii na wala hapewi ata senti kutoka kwenye shule. uwekezaji hapa bongo wote umefanywa kutokana na ada na michango ya watanzania wachache ambao wameshawishika kuchangia shule. rafiki yangu mmoja baba yake mzazi ametoa tiles za shule nzima for free. mimi pamoja na wanafunzi wengine tumeshapiga rangi sana shule za FEZA kwa kujitolea. ivyo basi naweza sema shule za FEZA hazina uhusiano wowote ule ayo mambo yao ya ndani ya uturuki wajaribu kumalizana nayo wenyewe. huo ubalozi kama unajua kuhusu iyo michango ya kigaidi basi wafungie hizo account ambazo zinapewa iyo misaada. Nigeria wamemgomea Erdogan na serikali yake kuhusu kufunga shule za aina ya FEZA ambazo zipo Uturuki ivyo serikali yetu isiyumbishwe kutokana na uyo Erdogan. shule hizi zinazalisha wataalamu wakutosha ambao wana mchango mkubwa tu kwa taifa ili. rafiki zangu wengi tu sasa hivi ni madiktar katika hospitali za hapahapa nchini, wengine mainjia wazuri tu na wanasaidia mambo mbalimbali.

Shule zinamilikiwa na nani? Watanzania au Waturuki under Ishik Foundation
 
Kanisa katoliki lilishiriki kwa kiasi kikubwa mauaji ya kimbari Rwanda,Tanzania tuwe makini na kanisa hilo na shule zake

..kuna taasisi za kidini hapa Tz zimetuhumiwa kuhusika na ugaidi na zimefungiwa.

..mimi sisemi shule hizo zifungiwe au zisifungiwe. Ninachotahadharisha mimi ni kwamba tuangalie maslahi mapana ya nchi yetu.
 
Back
Top Bottom