Waziri Mahiga: Serikali ya Uturuki imetuambia wamiliki wa shule za Feza ni magaidi

Hapo kunatengenezwa uzushi kuzichafua hizo shule hakuna lingine,tunajua upande flani hauna haki hapa tanzania basi tuachieni hata hivyo vichache jamani.
Udini ukikujaa ni shida. Waliosema ni waturuki ambao mwenye shule ni wao, kimasingi mwenye maslahi ya karibu zaidi ni mturuki(serikali ya uturuki), ww mtz kwa sababu ya agenda zako za udini unaona wao wanaonewa. Tuavhe chuki hizi ili kulinda Amani ya nchi yetu.
 
Wanayoyadai waturuki si ya kubezwa,watu wanaweza kujificha kwenye shughuli nzuri tu za kimaendeleo kumbe wana malengo mengine yaliyojificha.Mambo yanapotokea hufunua na mengine.
 
Ni vizuri pia tukang'oe bati za nyumba ya waziri mkuu na makamu wa raisi pale oysterbay tupeleke shule za kayumba pia ni za magaidi.......Udini na siasa ikitawala fikra yako huwezi tofautisha usiku wala mchana.
Mkuu hii haina Udini wala nini.
[emoji38] [emoji38] umekurupuka Bure. Huelewi msingi wa Tatizo.
 

Kwa Mara Ya Kwanza Ninawaona Wale Wanaoonekana Kuwa Na Maarifa Mengi Wakifichuo Hisia Zao Bila Ya Wenyewe Kujua!

Hivi Ni Kweli Nyinyi Hamujui Tofauti Ya TREASON (UHAINI) na TERRORISM (UGAIDI) ?

Kwasababu Yule Jamaa FETULLAH Anajuilikana Kimataifa Kuwa Ni Mtu Anaepigania Mageuzi Nchini Turkey, Na Ndiyo Maana Mataifa Ya Magharibi Yote Yanamuunga Mkono ikiwemo Marekani Ambayo Imempa Hifadhi Kwenye Nyumba Maalum Akilindwa Na Maafisa Wa Uslama wa CIA.

Na Mapinduzi Yaliyofanyika Uturuki Yaliungwa Mkono Na Marekani pamoja Na Mataifa Ya Ulaya Wakisema Kuwa Yangelifanikiwa Mapinduzi Hayo, Basi Wangelikuwa Wanaumaliza Ugaidi!! Kumbe Kwa Mtazamo Wa Wamagharibi Erdogan Ndiye Gaidi.

Serikali Ya Uturuki imeamua Kuwa Wale Wahaini Waliojaribu Kumpindua Rais Kuwaita MAGAIDI, Hivi Kumbe Maana Ya Gaidi Kwa Mtazamo Wako Na Mtazamo wa Waturuki Ni Yule Anaetaka Kumpindua Raisi??

Kwahiyo Wale Waliotaka Kumpindua NKURUNZIZA nao Ni Magaidi???

CCM waliopindua Zanzibar (1964) Nao Ni Magaidi??

Mkuu Si Kila Linapotumika Neno Ugaidi Unatakiwa Kuliunga Mkono eti tu Waliolengwa Ni Wafuasi Wa Dini Fulani.

Hayo Ni Maswala Ya Kisiasa si Ya Kidini.

Serikali Ya CCM zanzibar imeamua Kuvunja Maduka Ya Wapemba Pale Darajani Mjini Unguja wakiamini Kuwa Kuuwa Upinzani ni Lazima Uondoshe Zile Sehemu Zao Za Chanzo Cha Mapato.

Na Mfano Huo Ndiyo Anaotumia Erdogan Kutaka Kuuwa Upinzani Kwa Kuvunja Vyanzo Vyao Vya Mapato Kwa Ktumia Jina la Kuwabambikizia Ugaidi.

Tanzania Haiizidi Marekani Kwa Intelijensia, Mbona Marekani imekataa Kumlabel Fetullah Kuwa ni Gaidi?? Kwasababu inajua Kuwa Fetullah ni Mwanaharakati Anaepigania Demokrasia Na Wala si Ugaidi.
 

Kwani Mapinduzi Ni UGAIDI au UHAINI??

Naomba Majibu Mkuu.
 

Fedha kweli kiboko yaani wanafundisha watoto wa baadhi ya mawaziri wetu kwa mbinu za kigaidi...!!! Nadhani kwa mbinu hizo lazima mtoto 'ameze' Multiplication table 1-12 ndani ya siku moja (Extremely, it is joke)
 
Mkuu hii haina Udini wala nini.
[emoji38] [emoji38] umekurupuka Bure. Huelewi msingi wa Tatizo.
Mkuu, Rais wake mteule wa Turkey, kamuhusisha na kashafungia taasisi zake mbalimbali mpaka sasa, sitegemei uje hapa useme unafahamu mienendo yake.
Ulielie mara hoo ni mtu mwema.

Angali hata itikadi yake ya siasa nchini kwake hauijui.
Network yaka na marafiki zake hauijui.
Hela yake anaitumiaje wewe hujui.

Tafiti zinaonyesha magaidi wakubwa duniani kuwahi kutokea, sio watu maskini na sio watu vichaa.
Hivyo hawakuingia huko kwasababu ya shida.

Siamini kama ni
Fair kuelewana na kamtu kamoja dhidi ya taifa zima la Turkey. Ni vyema tukijali usalama wa Taifa zima la turkey kwasababu hili taifa lina arab affiliates .turkey inaweza chafuka kukakosekana amani pale kama kule arabuni. Ukichukulia lime habour baadhi ya wakimbizi.

Mataifa kama haya yanafaa kuongoZwa na mkono wa chuma. Demokrasia kunjakunja kisha tupa kule.
 
Well said.
Lakini hata hao USA kwa kelele zao za Demokrasia wamepelekea kuleta matatizo kule arabuni.
Kwasababu hiyo
Wangemwacha huyo dikteta asimamie show. Ili Amani idumu.
 

Suluhisho Ni Moja tu, Kamtoe Huyo Mtoto Wako Hapo Shule Kama Unahisi Anapandikizwa Dangerous Doctrine.
 
Kwahiyo hizo fees wazazi wanalipa kwa njia moja au nyingine wanachangia pia ugaidi???
 
Aiseee Balozi wa Uturuki anasema shule zinamilikiwa na huyo aliyefadhili mapinduzi ,huku kwetu msemaji sijui mwalimu wa Feza anasema shule zinamilikiwa na Watanzania ,Mhhhh haya
 
Both
Haya mambo ni mapacha. Ina depend na situation.

Nimekusoma Mkuu!
Icheki Situation Hii..

Erdogan: Ni Mfuasi Wa Siasa Za Kiarabu, Almost ni Saudia Arabia.

Feitullah: (Mwanamapinduzi) Ni Mfuasi Wa Siasa Za Kimagharibi, Almost Marekani inayomfadhili.

Erdogan: Anawaita Wanamapinduzi Magaidi.

Wanamapinduzi: Wanamwita Erdogan Ni Gaidi anaewafadhili ISIS.

Marekani: Kasaport Kisiri Mapinduzi dhidi ya Erdogan.

Russia: Ndiye Aliyekwamisha Mapinduzi Kwa Kumtonya Erdogan Mchongo Wote Wa Maandalizi.

Jibu Hapo Unalo wewe Mimi Sikusaidii Kuwa Nani Ni Gaidi..

By The Way!!! Hapo Unaweza Jikuta Upo Middle of the War...

Et the End Hivyo ni Vita Kati Ya MAREKANI na URUSI wanavopambana Kidizaini.
 
Usibishe bishe hovyo kwa jambo usilolijua.
Toa ushahidi unaokinzana na wa serikali ya uturuki vinginevyo unapiga mboyoyo zisizo na maana

Kwani Wao Waturuki Kwanini Wasilete Ushahidi Wa Kuthibitisha Hilo??

Unataka Ushahidi Kutoka Kwangu Wa Kukanusha, Je Umeenda Huko Ubalozini Kwa Uturuki Ukadai Ushahidi Wa Kuthibitisha??

Wao si Wamesema Tu Kwa Kutuhumu bila ya Ushahidi wowote!! Sasa iweje Mimi Nishindwe Kusema Kwa Kukanusha.

Think Twice bro.
 
Kama njia za kigaidi zinafanya wawe juu haina budi mama Ndalichako aende pale kujifunza ili watoe seminar kwa walimu wa shule za kata kuwa magaidi, itasaidia wanafunzi kutocheza singeli na kuelewa masomo
 
Kwahiyo hayatuhusu kama ni kweli wachukuliwe msobe msobe wakachinjane huko kwao hatutaki damu sis
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…