TUJITEGEMEE
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 25,225
- 25,488
Nadhani hii haipishani saana na ile ya duka la dawa lisikae mita chache kutoka sehemu ya kuhudumia wagonjwa.Maswali ya kujiuliza...
Ni kweli kitengo hichi ndicho tatizo kwenye shirika?
CEO au Bodi wako likizo kuzitoa hizo sababu.
Vijana wanaonewa bure!
Taarifa ya kwa nini umeme unakatika hovyo haitasaidia chochote, watu wanataka umeme tu.Hapana ni kweli kwa nini umeme unakatika hovyo hakuna taarifa na hawasemi kuwaambia wananchi kuna nini umeme unakatika?
Lakini mkurugenzi mkuu anatakiwa kupewa onyo ,hawasimamii mameneja wa Mikoa.
HV Bado badra masoud Yuko pale siku hz azikiki kbsa
Anataka aingize propagandaUmeme ukatike alafu msemaji atetee VP shirika lake.
Waziri wa Nishati Mh Makamba amevunja kitengo cha habari na mawasiliano Tanesco akikituhumu kimeshindwa kulisemea shirika na kulitetea shirika kwenye nyakati ambazo kitengo na watu wake kimetakiwa kufanya hivyo!
Ikumbukwe kitengo cha habari na mawasiliano kinaongozwa na mwana dada Badra Masoud kwa misingi hiyo amekali kuti kavu ...
Maswali ya kujiuliza...
Ni kweli kitengo hichi ndicho tatizo kwenye shirika?
Ni kweli wameshindwa kuitetea tanesco?
View attachment 2095460
Hivi Haji Manara hawezi kazi ya usemaji tu pale wizarani?Waongeaji wa kwenye majukwaa mbona wapo wengi wawachukue hao hata wale wa zamani waliopo Bungeni sasa wapewe hii kazi
Sisi ni bla bla tu na siku zinakimbia hahaha
Ni mm hapa mkuu ndio niliuliza kumbe aliniingiza chaka mpumbavu kabisa hana AdabuAnaetumia hiyo ID hana majibu sahihi. Kuna member aliuliza kuhusu mita za vyumbani vya kupanga za kujitegemea, Kiuhalisia zipo na zinauzwa ila Kajibiwa hazipo/Hawana na hawaziuzi.
Kwa hili winchi ya Tani 26 natamani Mungu amfufue Nyerere ama jpm basi aongee tuone.Makamba anavyodai kitengo kimeshindwa kuitetea Tanesco ana maana gani? anataka kitengo kiwe kinazalisha propaganda au kifanyeje?
Navyojua hao watu wa idara ya habari wanatakiwa kupewa taarifa za majibu ya kero za wateja kutoka kwa wahusika (waziri, naibu wake, katibu mkuu nk) then wao ndio watangaze taarifa hizo kwa umma.
Sasa mfano wananchi wakiulizia ujio wa ile winchi ya tani 26 toka huko ilipoagizwa mbona mpaka leo kimya? Makamba anataka hao jamaa wa kitengo cha habari wajibu kitu gani kama hajawapa majibu?