Waziri Mkenda: Ajira ya Chuo Kikuu isiwe kuangalia GPA pekee lazima wapimwe, wafanye na usaili

Waziri Mkenda: Ajira ya Chuo Kikuu isiwe kuangalia GPA pekee lazima wapimwe, wafanye na usaili

Chuo kwa Tanzania ni elimu rahisi sana
Ukisoma Past paper tu umetoboa bila kuwa na haja ya kusoma mambo mengine yote, wanafunzi 90% hawajui sababu zao wao kusoma modules fulani zaidi ya kufaulu

80% ya watu wanaomaliza chuo huanza upya kutafuta kitu cha kufanya kwenye maisha, ukikutana na Mwalimu wa chuo ambaye hajawahi kufanya kazi kwenye kile alichosomea, ni weupe and very narrow minded
 
Tsh ametoa hoja yenye mantiki sana. inatakiwa idatishwe kule juu ya bandiko!!
Shukran sana mkuu kwa kuisapoti hoja. Tuna tatizo kubwa sana boss, mara ya mwisho nimepokea binti wa chuo hajui hata cheque ni kitu gani, hajui kujaza slip ya cheque, anatetemeka, ni kitu kipya kwake, hajawahi kukiona, ni jambo linalomtisha ila somo la Finance amefaulu na huenda katika mitiani yake ameshajibu swali la what is cheque, types of cheques kwa ufasaha.
 
Shukran sana mkuu kwa kuisapoti hoja.
Nahisi wengi hawajaelewa kilichoongelewa. Mkenda katoa maagizo baada ya matukio yanayoonesha kuna watu wana shahada za vyuo vikuu zisizoakisi uwezo wao wa kazi kuongezeka. Sasa si bora umsaili kabla ya kumuajiri? Tatizo liko wapi??

Inawezekanaje mtu kamaliza chuo kikuu lakini hawezi kuandika barua yenye mantiki ya kuomba kazi? Au inakuwaje mtu aliyesoma masomo yake kwa kiingereza kwa miaka zaidi ya saba awe hawezi kuongea ama kuandika kiingereza kwa ufasaha? Mtu kama huyu ili ujue uwezo wake njia rahisi si kumsaili?
 
Kweli nchi inaenda kubaya sana. Kwa hiyo wakifanyiwa usaili ndio elimu inakua bora. 😀😀😀😀😀.
Mtu mwenye GPA kubwa kwa vyuo kama SUA, MZUMBE na UDSM huyo anauwezo mkubwa, haina haja ya kujiuliza mara mbili.

Nenda uendako, kwenye usaili watu wanakalili na kufaulu baada ya hapo wanasahau. Ila mwenye GPA kubwa ni mtu mwenye uwezo.

Haiwezekani mtu kidato cha Nne abamize one ya saba, kidato cha sita one ya nne na chuo GPA ya 4.6. Useme hana uwezo badala yake utegemee kumpima kwenye usaili Ili kupima uwezo wake.

Tuwekeze kwenye practical zaidi

inategemea na wasaili uelewa wao na aina ya kazi inayoombwa... Kwenye usaili tunapima uelewa, atitude, commitment, behaviour nk..
kwenye uelewa itategemea aina ya kazi na uzoefu unaotakiwa... kama ni uzoefu wa zaidi ya 2yrs kwenye field fulani hapa unaweza kushangazwa na hata mwenye GPA ya 2.0....
 
Kweli nchi inaenda kubaya sana. Kwa hiyo wakifanyiwa usaili ndio elimu inakua bora. 😀😀😀😀😀.
Mtu mwenye GPA kubwa kwa vyuo kama SUA, MZUMBE na UDSM huyo anauwezo mkubwa, haina haja ya kujiuliza mara mbili.

Nenda uendako, kwenye usaili watu wanakalili na kufaulu baada ya hapo wanasahau. Ila mwenye GPA kubwa ni mtu mwenye uwezo.

Haiwezekani mtu kidato cha Nne abamize one ya saba, kidato cha sita one ya nne na chuo GPA ya 4.6. Useme hana uwezo badala yake utegemee kumpima kwenye usaili Ili kupima uwezo wake.

Tuwekeze kwenye practical zaidi
Bado huelewi mambo mengi. Watafute wenye GPA kubwa zaidi unaowafahamu, halafu angalia mafanikio yao ukilinganisha na wenye GPA za kawaida, halafu utatuambia.
 
Nahisi wengi hawajaelewa kilichoongelewa. Mkenda katoa maagizo baada ya matukio yanayoonesha kwamba watu wana shahada za vyuo vikuu zisizoakisi uwezo wao wa kazi kuongezeka. Sasa si bora umsaili kabla ya kumuajiri? Tatizo liko wapi??

Inawezekanaje mtu kamaliza chuo kikuu lakini hawezi kuandika barua yenye mantiki ya kuomba kazi? Au inakuwaje mtu aliyesema kwa kiingereza kwa miaka zaidi ya saba awe hawezi kuongea ama kuandika kiingereza kwa ufasaha? Mtu kama huyu ili ujue uwezo wake njia rahisi si kumsaili>
Boss upo sahihi 100% kwenye hii comment uliyonijibu nimeedit na kuongeza mfano halisi kabisa. Halafu ni kama hawajui kuwa sekta binafsi ambayo inaajiri sana hawapendi kuajiri, wakulipe ili wakufundishe kazi wanataka wakulipe ili uzalishe na waone matokeo ndo maana hawajali vyeti siku hizi.
 
inategemea na wasaili uelewa wao na aina ya kazi inayoombwa... Kwenye usaili tunapima uelewa, atitude, commitment, behaviour nk..
kwenye uelewa itategemea aina ya kazi na uzoefu unaotakiwa... kama ni uzoefu wa zaidi ya 2yrs kwenye field fulani hapa unaweza kushangazwa na hata mwenye GPA ya 2.0....
Watu waelewe kuwa ukubwa wa GPA hauhusiani hata kidogo na uwezo wa mtu kufanya kazi tarajiwa. Hayo uliyoyataja ya uzowefu, tabia, hari ya kufanya hiyo kazi, mwenendo wa muombaji, utayari wa kuifanya hiyo kazi kwa mazingira tarajiwa, ndiyo huzingatiwa kwenye kuajiri mtu na siyo GPA yake.

Kuna usaili unafanyika wanaachwa wenye shahada wanachukuliwa watu wa kidato cha sita.
 
Malecturer wengi Tanzania ni Academician na sio watu wenye skills na exposure matokeo wanapump matheory.

Ni wakati wa Vyuo kujikita kwenye kuajili watu waliokaa kitaa kidogo na kupata life exosure + skills, mtu amemaliza say Electrical au Civil engineering then hajawahi kabisa kupractise alichosomea kwasababu ana GPA ya 4 unambakiza na kumfanya lecturer matokeo yake ni hasara kubwa kwa wanafunzi... Angalau muanze kuajili malecturer wenye experience ya kazi walizosomea nje uhadhiri.
 
Bado huelewi mambo mengi. Watafute wenye GPA kubwa zaidi unaowafahamu, halafu angalia mafanikio yao ukilinganisha na wenye GPA za kawaida, halafu utatuambia.
Acha uhuni tunazungumzia elimu. Mwenye GPA ndogo hana uwezo kielimu.
 
Kwanza isichukuliwe kwamba tunasema wachukuliwe wasio na sifa, hata Profesa Mkenda hakusema hivyo. Kinachosema ni kwamba zinawekwa sifa, wenye hizo sifa wanaomba kazi halafu wanasahiliwa ili kati yao wachukuliwe wale watakaothibitisha kwamba uwezo wao wa darasani haukuwa wa kukaririr bali ulitokana na wao kuelewa walichokuwa wanafundishwa.
 
Watu waelewe kuwa ukubwa wa GPA hauhusiani hata kidogo na uwezo wa mtu kufanya kazi tarajiwa. Hayo uliyoyataja ya uzowefu, tabia, hari ya kufanya hiyo kazi, mwenendo wa muombaji, utayari wa kuifanya hiyo kazi kwa mazingira tarajiwa, ndiyo huzingatiwa kwenye kuajiri mtu na siyo GPA yake.

Kuna usaili unafanyika wanaachwa wenye shahada wanachukuliwa watu wa kidato cha sita.
Huo ni mfumo uliotengenezwa, lkn GPA kubwa itabakia kuwa na uwezo. Yaani mtu ana GPA kubwa ya mathematics alafu azidiwe kwenye namba na mwenye GPA ndogo. 😀😀😀😀😀. Hizi ni chai.
Yaani mtu ana GPA kubwa ya coding alafu azidiwe coding na mtu mwenye GPA ya 3. 😀😀😀😀😀😀.
Nina GPA ya 3 lkn katika hilo siwezi amini.
 
Elimu ni nn? Maana hapa ndo tatizo linapoanza.

Mfano: Kujua Kusonga ugali ukaiva hiyo ni elimu.

Sasa mwenye A+ ya kusonga ugali kwenye makaratasi na anayesonga ugali kwa exposure na uzoefu nani ana elimu yenye uzalishaji halisi?
Hili swali lako haliendani na uhalisia. Shida ni kwamba huko makazini mnafanya kazi za kukusanya mafaili na kuweka kabatini. 😀😀😀
 
Acha uhuni tunazungumzia elimu. Mwenye GPA ndogo hana uwezo kielimu.
Hii umekosea. Hebu nikupe mfano kwa kuuliza swali.

Mtoto aliyekariri akijibu swali la 2X2=4

Mtoto aliyeelewa akijibu swali la 2X2=4

Mtoto aliyechungulia kwa mwenzake 2X2=4

Mtoto aliyeuziwa mtihani naye akijibu 2X2=4

Hao wote si watakuwa wamefaulu, lakini je uwezo wao ni sawa? Ukiwasaili hautaona utofauti wao? GPA kubwa siyo kiashiria cha kweli kuoenesha ubora wa elimu aliyo nayo mtu.

Nikuibie siri. Vyuo vikuu vya Tanzania vinazingatia zaidi matokeo ya mwanafunzi kwenye mtihani wake wa Kidato cha nne.
 
Huo ni mfumo uliotengenezwa, lkn GPA kubwa itabakia kuwa na uwezo. Yaani mtu ana GPA kubwa ya mathematics alafu azidiwe kwenye namba na mwenye GPA ndogo. 😀😀😀😀😀. Hizi ni chai.
Yaani mtu ana GPA kubwa ya coding alafu azidiwe coding na mtu mwenye GPA ya 3. 😀😀😀😀😀😀
Kipindi cha nyuma nimebahatika kuchaguliwa kuwa kwenye kamati za ajira za baadhi ya taasisi hapa Tanganyika, hichi unachokisema labda nje ya nchi ila hapa nchini? Aisee hapana. Ukiajiri pima IQ achana na makaratasi ya GPA.
 
Hili swali lako haliendani na uhalisia. Shida ni kwamba huko makazini mnafanya kazi za kukusanya mafaili na kuweka kabatini. 😀😀😀
Sawa, wewe umesema na kuhitimisha. Basi ibaki kuwa hivi ulivyowaza.
 
Kuanzia sasa Serikali itaanza kuzitazama ajira za vyuo vikuu badala ya kuangalia ubora wa ufaulu yaani GPA pekee sasa waajiriwe kwa kupimwa uwezo wao kwa kufanya usaili.

Kuangalia ufaulu pekee wa wanafunzi haitoshi kuboresha elimu badala yake ni muhimu kuongeza vigezo hivyo katika mapitio ya sera na mabadili ya mitaala jambo hilo litatazamwa kwa weledi mkubwa.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda ameyasema hayo leo tarehe 12 Disemba 2022 mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango wakati wa mahafali ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania iliyofanyika Kinondoni Jijini Dar es Salam.

Amesema wakati serikali inaongeza udahili wa wanafunzi haitakuwa tayari kuona ubora unapungua hivyo serikali inaendelea na mkakati wake wa kuhakikisha ubora wa elimu hususani katika vyuo vikuu unaimarika.

"Zamani ilikuwa rahisi kuwa Profesa ukiandika tu kwenye magazeti unakuwa Profesa lakini kwa sasa vigezo vya kuwa Profesa vimezidi kuwa vigumu kwa sababu tunataka maprofesa wetu wawe sawa na wale wa nchi zingine," amekaririwa Prof Mkenda.

Amesema katika mageuzi ya elimu yanayokuja ambapo wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ipo katika mapitio ya sera na mitaala miongoni mwa mambo yatakayofanyiwa kazi itakuwa ni pamoja na kuhakikisha wanaoajiriwa ni wanafunzi wenye sifa zinazotakiwa.

Pia, Waziri Mkenda amesema kuwa serikali kwa sasa inaendelea na Ujenzi wa Kampasi mpya za Vyuo Vikuu katika mikoa 14 Tanzania pamoja na upande wa Zanzibar (Unguja na Pemba) katika maeneo ambayo hayana vyuo vikuu ukiacha vyuo huria.

Mikoa hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na kampasi za vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini ni pamoja na Tabora, Katavi, Kigoma, Kagera, Singida, Manyara, Lindi, Rukwa, Mwanza, Simiyu, Tanga, Ruvuma, Shinyanga na Dodoma.
A little too late...hii ya kulazimisha GPA kubwa wabaki vyuoni imetengeneza matatizo makubwa kuliko hata faida.
Tuna wasomi vilazi wametapakaa kila kona. Tunawaona wanavyoendesha mambo yao. Kama vile watu wasiosoma.
 
Back
Top Bottom