Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 21,470
- 40,593
Hii hoja yako mantiki yake ni nini??Hili swali lako haliendani na uhalisia. Shida ni kwamba huko makazini mnafanya kazi za kukusanya mafaili na kuweka kabatini. πππ
Hahaha
Kwani GPA inatokana na nini? Maana inawezekana tunazungumzia vitu visivyofanana.Yaani mtu ana GPA kubwa ya mathematics alafu azidiwe kwenye namba na mwenye GPA ndogo.
Ukitaka upate walimu wazuri vyuo vikuu, wenye GPA za juu wawe wanafanyiwa usaili wa kufundisha darasani kwa vitendo na si uasili wa mahojiano pekee. Ni vizuri kwamba GPA za juuu ziendelee kuwa ni kigezo kimojawapo, ila SECOND iwe usaili kwa njia ya vitendo, kufundisha darasaniKuanzia sasa Serikali itaanza kuzitazama ajira za vyuo vikuu badala ya kuangalia ubora wa ufaulu yaani GPA pekee sasa waajiriwe kwa kupimwa uwezo wao kwa kufanya usaili.
Kuangalia ufaulu pekee wa wanafunzi haitoshi kuboresha elimu badala yake ni muhimu kuongeza vigezo hivyo katika mapitio ya sera na mabadili ya mitaala jambo hilo litatazamwa kwa weledi mkubwa.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda ameyasema hayo leo tarehe 12 Disemba 2022 mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango wakati wa mahafali ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania iliyofanyika Kinondoni Jijini Dar es Salam.
Amesema wakati serikali inaongeza udahili wa wanafunzi haitakuwa tayari kuona ubora unapungua hivyo serikali inaendelea na mkakati wake wa kuhakikisha ubora wa elimu hususani katika vyuo vikuu unaimarika.
"Zamani ilikuwa rahisi kuwa Profesa ukiandika tu kwenye magazeti unakuwa Profesa lakini kwa sasa vigezo vya kuwa Profesa vimezidi kuwa vigumu kwa sababu tunataka maprofesa wetu wawe sawa na wale wa nchi zingine," amekaririwa Prof Mkenda.
Amesema katika mageuzi ya elimu yanayokuja ambapo wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ipo katika mapitio ya sera na mitaala miongoni mwa mambo yatakayofanyiwa kazi itakuwa ni pamoja na kuhakikisha wanaoajiriwa ni wanafunzi wenye sifa zinazotakiwa.
Pia, Waziri Mkenda amesema kuwa serikali kwa sasa inaendelea na Ujenzi wa Kampasi mpya za Vyuo Vikuu katika mikoa 14 Tanzania pamoja na upande wa Zanzibar (Unguja na Pemba) katika maeneo ambayo hayana vyuo vikuu ukiacha vyuo huria.
Mikoa hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na kampasi za vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini ni pamoja na Tabora, Katavi, Kigoma, Kagera, Singida, Manyara, Lindi, Rukwa, Mwanza, Simiyu, Tanga, Ruvuma, Shinyanga na Dodoma.
We ni km mtu aliyekata tamaa au una wivu wa kipuuzi. Kila kitu kukariri, kukariri maana yake nini. We usome PCM, mahesabu yote yale ya physics na Math ni kukariri? Kuakariri maana yake nini. Acha kupotosha watu.Katika mambo yanayoishusha elimu yetu ni hili suala la gpa.
1. Mtu anaishi Morogoro amesoma mzumbe sekondari Morogoro kakariri past paper kapata dv 1.
2. Ameenda Chuo Mzumbe morogoro kakariri wee kapata gpa ya juu. Anachukua na master kabisa ila hana exposure yoyote. Ulimwengu wake umejaa vitini, pastpapers na madesa.
Unampa ualimu afundishe, hana exposure, hana experience, anaijua morogoro tu. Matokeo yake anachokifanya ni kuambukiza wanafunzi kukariri kama alivyofanya yeye.
Kutunga mitihani migumu na kuwa na fixed marking scheme anayotumia kusahihisha, mwanafunzi akijiongeza kidogo nje ya marking scheme anapata sifuri. Mitoto ikija kazini watu wanaanza upya kuelekeza hata vitu vidogo vidogo.
Hivi haiwezekani vyuo vikatoa pesa nzuri kisha zikawa zinaenda kwenye mashirika makubwa na kuchukua wataalam waje kufundisha vijana wetu? Hawa malectures wawafundishe mwaka wa kwanza tu kwenye theory.
Yani mtu Uzi hasomi anawahi ku comment alafu apo naye anaponda elimu ya tzπππUmedandia treni kwa mbele, soma uelewe alichosema
Tumejaza vilaza kila sehemu. Wanakariri mambo halafu wanataka wao ndio watuongoze.Kwenda wapi?Kipindi cha nyuma nimebahatika kuchaguliwa kuwa kwenye kamati za ajira za baadhi ya taasisi hapa Tanganyika, hichi unachokisema labda nje ya nchi ila hapa nchini? Aisee hapana. Ukiajiri pima IQ achana na makaratasi ya GPA.
Tuseme tu ukweli wenye GPA ndogo ni vilaza boss.Tumejaza vilaza kila sehemu. Wanakariri mambo halafu wanataka wao ndio watuongoze.Kwenda wapi?
Walimu Wawili Msaidizi wa walimu Mmoja darasa 350 wanafunzi ama zaidi, semester wiki 15, somo limepewa masaa manne na nusu kwa wiki. Vifaa vya practical vinafika sehemu husika kutoka kwa supplier wiki nne kabla semester Kwisha.... Mambo ni mengi muda mchache! Sijui nilikuwa naandika kitu gani ebu Meneja wa Makampuni fafanua mada ya bandiko lako.Tuwekeze kwenye practical zaidi
Kukariri hata njia za kufanya hisabati hukaririwa. Hiyo ni kawaida kwa mambo ya kusoma. Na hajasema kila mwenye GPA kubwa ameipata kwa kukariri lakini wapo pia waliopata GPA kubwa kwa kukariri.We ni km mtu aliyekata tamaa au una wivu wa kipuuzi. Kila kitu kukariri, kukariri maana yake nini. We usome PCM, mahesabu yote yale ya physics na Math ni kukariri? Kuakariri maana yake nini. Acha kupotosha watu.
Kasheshe inakuja pale Kuna Mwanafunzi ana jpei ya 4.3 kutoka Chuo Fulani na mwingine ana jpei 3.4 kutoka Chuo kingine na wote wamesoma programme hiyo hiyo ya uhandisi, Sayansi ama Sanaa lakini wakiwekwa kwenye mizania ya uelewa na kufanya kazi yule wa jpiei ya 3.4 unatamani huyu ndiye apewe kazi na inatakiwa jpei yake isome 4.6 kwenye transcript.... huo usaili one of the criteria lazima gpa at least 3.8 then mengine yanafuata.
I used to believe that...Ila kwenye haya maisha, tena baada ya kusoma degree moja, nimegundua kuwa wengi wa vipanga ndio vilaza wakutupwa.Tuseme tu ukweli wenye GPA ndogo ni vilaza boss.
Unaeleweka.Sijui naeleweka!!!!?
Kuwa na uwezo mkubwa wa kukariri na ku reproduce madesa, sio kuwa na IQ kubwa. Wale walio na uwezo wa kufikiri na kuona mambo ndio wanapaswa kukaa sehemu zote nyeti. Hata kama waqna GPA ndogo.Tumejaza vilaza kila sehemu. Wanakariri mambo halafu wanataka wao ndio watuongoze.Kwenda wapi?
Naam Sasa unaeleweka barabara.Unaeleweka.
Kenya mwezi jana kuna shirika lilitangaza kazi na sifa ikawa ni shahada ya uzamili (Masters' Degree) lakini kuna dada akaomba kwa kutumia Diploma na vyeti vingine ambatano. Baada ya mabishano ya muda kidogo, wasaili wakaamua kumweka kwenye orodha (shotlisted) ya watakaosailiwa.
Baada ya usaili huyo binti akawa wa pili kwa ubora kati ya waliosailiwa.. akapewa kazi.
Sijui nimeeleweka!!??
.... mchujo wa awali kabisa ni hiyo gpa; below 3.8 automatically havuki kwenda next stage. So, hakuna uwezekano wa 3.4 kukutana na wa 4.3 kwenye interview (face to face).Kasheshe inakuja pale Kuna Mwanafunzi ana jpei ya 4.3 kutoka Chuo Fulani na mwingine ana jpei 3.4 kutoka Chuo kingine na wote wamesoma programme hiyo hiyo ya uhandisi, Sayansi ama Sanaa lakini wakiwekwa kwenye mizania ya uelewa na kufanya kazi yule wa jpiei ya 3.4 unatamani huyu ndiye apewe kazi na inatakiwa jpei yake isome 4.6 kwenye transcript.
Sijui naeleweka!!!!?
Sijaelewa pia, nilitarajia iwe majarida ya kitaaluma. Je, yeye sio Professa kupitia kuandika magazetini au yeye sio wa zamani? Hiyo zamani ni kuanzia mwaka gani?Zamani Kuandika kwenye gazeti unakuwa profesa? Aliyeelewa tafadhali
Interview si zote za kuchuja wanaotakiwa kufanya kazi vyuo vikuu tu ndugu. Upo?.... mchujo wa awali kabisa ni hiyo gpa; below 3.8 automatically havuki kwenda next stage. So, hakuna uwezekano wa 3.4 kukutana na wa 4.3 kwenye interview (face to face).
Wale watu wanaofanya chaguzi (Shotlistings)za watu watakaosailiwa huwa hawafuati njia hiyo moja kwa moja.. Kwa uzowefu wao wanajua kwamba pamoja na kuweka vigezo fulani mahsusi, huwa wanatokea watu wengine wasio na vigezo hivyo kinadharia lakini kivitendo wakawa navyo..... mchujo wa awali kabisa ni hiyo gpa; below 3.8 automatically havuki kwenda next stage. So, hakuna uwezekano wa 3.4 kukutana na wa 4.3 kwenye interview (face to face).