Waziri Mkenda: Ajira ya Chuo Kikuu isiwe kuangalia GPA pekee lazima wapimwe, wafanye na usaili

Waziri Mkenda: Ajira ya Chuo Kikuu isiwe kuangalia GPA pekee lazima wapimwe, wafanye na usaili

Boss, sipo hata kwenye nafasi ya kushindana na yoyote kielimu katika kuchangia uchumi wa hii nchi.

Nilipata nafasi ya ajira nikafanya sehemu yangu na kumaliza na sasa nipo katika nafasi ya kuwezesha wengine wapate ajira. GPA sio suala langu tena maana wakati wangu ulishapita ila Natoa maoni kulingana na kile ninachokiona, kusema kuwa ni wivu hakutabadili uhalisia wa ninachokiona.
Wenye GPA kubwa ndio muhimu tena wanatakiwa kuendelezwa kwa kutumia internship.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Huwezi jua labda na Tanzania tunao "Genius"" wengi tu.

Turudi kwenye mada. Unajua kwamba zamani usomi ulipimwa kwa uwezo binafsi wa mtu kujenga hoja na si vyeti!? na Vyuo walivyosoma hao unaowaita "Genius" vilikuwa havitumii mifumo kama hii inayotumika sasa?

Mimi naona mbali na GPA ni lazima usomi wa mtu upimwe kwa vitendo baada ya kufaulu nadharia/vitendo vya chuoni. Nchi zilizoendelea hutaka sana kujua baada ya kufaulu mitihani wewe binafsi unaweza kuongeza nini kwenye jamii na siyo kusema una GPA kubwa ama ndogo!!?

Wavumbuzi wengi hawakumbukwi kwa GPA bali kwa vumbuzi zao. Leo hii Mark Zuckerberg ama Bill Gates wanakumbukwa kwa uvumbuzi wao na si kwa GPA zao. Bado nasisitiza kwamba kigezo cha GPA kuwa kubwa ndiyo uajiriwe kuwa mhadhiri hakijatolewa na Profesa Mkenda.
Vitendo unajifunza boss. Waziri aanzishe internship kwa watu wenye GPA kubwa ili waendelezwe wasaidie taifa letu.
 
Vitendo unajifunza boss. Waziri aanzishe internship kwa watu wenye GPA kubwa ili waendelezwe wasaidie taifa letu.
Hii sasa ni hoja lakini haihusiani na ile ya usaili kindakindaki. Nchi yetu mfumo wa kuwalea wasomi wetu ni mbovu. Mazoezi kwa vitendo (internship) ndiyo humkomaza msomi. wanaofanya ni madaktari tu.
 
Wanataka kutupeleka sehemu fulani mbaya! Mwalimu hapaswi kuwa ni mtu ambaye hakufaulu kwa kiwango cha juu kabisa cha vitu alivovisoma.

Tukumbuke mwalimu wa shule aliyepata divisheni 4, ana ufahamu wa kiwango gani?? Je hivo ndivo mataifa mengine hufanya? Au ni jambo letu sisi ambalo litapelekea hata waalimu wetu kutokubalika kufundisha katika vyuo vya nje???
 
Ahahahahah kama umeniona vile, maana nishawahi kuitwa na. mkuu mmoja wa chuo alikuwa rafiki yangu huku Mkoani, akasema bora uje ufundishe, siuna-GPA ya 3.8 nikamwambia waapi mkuu, nina 3.7 ya SUA.

Ajira ikaishia hapo, na ninao uwezo mkubwa sana wa kufundisha lkn ndo hivyo tena ahahahah
Unajiliwaza tu mkuu. Kigezo ndio hicho. Minimum GPA ni 3.8. Hapo ndio unqualify walau kuwa shortlisted kwa ajili ya interview. Na hizo ni guidelines za TCU. Hata kama unahisi una uwezo wa kufundisha, maadam hujakidhi hicho kigezo kimojawapo, sahau kuitwa kwny interview. Halafu tuache excuses za kufeli kwetu kwa kubeza waliofaulu kutuzidi. Mnatumia kigezo gani kuwa mwenye GPA kubwa kafake na mwenye GPA ndogo ni genuine? Nani aliyeingiza hii mentality kwa jamii?
 
Hivi mkuu umesoma kweli? Au wewe ndio miongoni mwa yale masifuri tuko nayo katika hii nchi?

Ni bahati mbaya sana na sijui kama unajua, uhusiano unaojaribu kuutengeneza kati ya matokeo ya mtu ya darasa la saba hadi kidato cha sita na GPA ya chuo ni uhusiano mfu na haupo.

Aya yako ya kwanza ndio kitu anacholia nacho Waziri, kuwa na GPA kubwa kutoka katika chuo chochote kile Tanzania isiwe kigezo pekee cha mtu kuajiriwa kuwa mkufunzi chuoni.

Waziri yupo sahihi, watu wasipate ajira moja kwa moja baada ya kuwa na GPA kubwa, wapimwe kwanza. Kufundisha Chuo kikuu ni kazi inayohitaji mtu mwenye uelewa mpana sana na kudadavua mambo.

Wapo watu wenye GPA kubwa na walizipata kihalali kabisa kwa kukariri notes za darasani na kuyaotea maswali, hawa hawawezi kuwa wakufunzi kwasababu nje ya hiyo mitihani waliyofaulu hamna kitu kingine.

Lakini pia kuna waliopata hizo GPA kubwa kwa njia za kona kona kama kuwa karibu na wakufunzi, hawa pia kuwapa ajira moja kwa moja ni tatizo.

Vyuoni wapo wakufunzi ambao wanaingia kufundisha lakini anaishia kusoma notes, na hata akiulizwa swali na mwanafunzi anashindwa kujibu kwasababu alikariri na uwezo wake ni mdogo.

Andiko langu haliondoi ukweli kwamba wenye GPA ndogo ni VILAZA tu.
Umemjibu vizuri sana. Ila hapo mwisho naomba nitakuchallange kidogo.

Tuna hili tatizo la kuhadaa wanafunzi kuwa ukifaulu umefanikiwa na ukifeli ww ni KILAZA, Vijana wanalenga kupata GPA nzuri mavyuoni bila kujali iwapo hiyo GPA kweli ipo kichwani na itamsaidia kutengeneza kipato wakati VILAZA wanatoka nje na kuipata elimu halisi ya hii dunia na matokeo yake tuna VILAZA wafanyabiashara, VILAZA mafundi, VILAZA wanasiasa wanaotoa ajira na wenye vipato wengi kuliko graduates wenye GPA KUBWA walio na kazi zenye msaada kwa jamii na kuwapatia vipato.

Sasa hivi kuna VILAZA BODABODA wanakipato cha uhakika kuliko wenye degree na tayari wapo wenye degree na GPA zao wanavizia kazi wanazoamini ni za VILAZA kama ya boda boda. Hichi ndicho kilichopo kwenye jamii.

Naamini tukijikita kwenye utendaji kuliko ufaulu wa makaratasi tu tutasaidia wengi.
 
Ninachokueleza ni kwamba graduates, matokeo yao ya makaratasi hayafanani na kilichomo kichwani, Nawapokea sana, nawapa nafasi sana, field wanaziomba sana, kujitolea na ajira wanaomba hivyo nakutana nao mara nyingi tu na wakati mwingine yule ambaye kwenye makaratasi wala haonekani mwenye elimu kubwa na diploma ya vyuo visivyo rasmi anafanya vizuri tu kuzidi vijana wa IAA, Mzumbe, UD, UDOM SAUT n.k.

Mfano wa swali jepesi katika field ya biashara ambalo mwanachuo yoyote esp mwenye GPA kubwa hakupaswa kushindwa kulijibu: Ni nyaraka zipi zinatumika kufanya miamala baina ya raia wawili walio nchi tofauti wakati wanafanya biashara?

Hii ni international trade, Mtu ana BBA na GPA fiirst class lakini anajibu mpaka unaona huruma, wakati mwingine unadhani ni panic unamwambia relax, kunywa maji unampigisha hadithi nyingine ili asiumie kisha ukishaona karudi normal unaruhusu panel iendelee ila still wengi wanashindwa na hapo swali limeulizwa kwa kiswahili.

BOSS NAKUELEZA, TUNA TATIZO LINALOPASWA KUFANYIWA KAZI. TUNAPOELEKEA IKITOKEA PAKAWA NA UHURU WA KUAJIRI BAINA YA EA VIJANA WETU WATAUMIA SANA.
Weww jamaa una wivu na ujuaji mwingi Sana ,mbaya zaidi mmejaaa ofcin huko mnajiona Sana mnajua kuliko mtu yeyote ......

Tanzania imejaa watu wa namna hii ,si ajabu ndio maana nchi ni ngumu Sana uchawi na rushwa vimekua Kwa Kasi kubwa sababu ya watu wa aina hii [emoji848][emoji848][emoji848]
 
Huwezi jua labda na Tanzania tunao "Genius"" wengi tu.

Turudi kwenye mada. Unajua kwamba zamani usomi ulipimwa kwa uwezo binafsi wa mtu kujenga hoja na si vyeti!? na Vyuo walivyosoma hao unaowaita "Genius" vilikuwa havitumii mifumo kama hii inayotumika sasa?

Mimi naona mbali na GPA ni lazima usomi wa mtu upimwe kwa vitendo baada ya kufaulu nadharia/vitendo vya chuoni. Nchi zilizoendelea hutaka sana kujua baada ya kufaulu mitihani wewe binafsi unaweza kuongeza nini kwenye jamii na siyo kusema una GPA kubwa ama ndogo!!?

Wavumbuzi wengi hawakumbukwi kwa GPA bali kwa vumbuzi zao. Leo hii Mark Zuckerberg ama Bill Gates wanakumbukwa kwa uvumbuzi wao na si kwa GPA zao. Bado nasisitiza kwamba kigezo cha GPA kuwa kubwa ndiyo uajiriwe kuwa mhadhiri hakijatolewa na Profesa Mkenda.
Mkuu uwezo wa mtu wa kuhoji ,kujieleza na kuwa mbunifua utaujuje ? Kwenye interview ya masaa 3 au ?

Mtu unakutana nae amekuwa mtu mzima ,miaka 30+ utajuaje uwezo wake haraka haraka kama sio kujua background yake (elimu toka primary, secondary,Hadi chuo )....

Ukiona hajapita kote huko ,huyo hana lolote na hana analolijua niamin Mimi ...


Na usipoteze muda kumwamin ,maana atakusumbua tu Bure ,hata kazi za kuelekezwa hata weza achana na swala la kuwa mbunifu...

Hao wote uliotaja hapo juu shule wameenda mzee[emoji2]
 
Weww jamaa una wivu na ujuaji mwingi Sana ,mbaya zaidi mmejaaa ofcin huko mnajiona Sana mnajua kuliko mtu yeyote ......

Tanzania imejaa watu wa namna hii ,si ajabu ndio maana nchi ni ngumu Sana uchawi na rushwa vimekua Kwa Kasi kubwa sababu ya watu wa aina hii [emoji848][emoji848][emoji848]
Haupo sahihi. Badili huu mtazamo.

Kama kila atakayekosoa ataitwa mchawi kisha kila mmoja akanyamaza sijui tutakuwa na jamii ya aina gani?

Uzuri Hapa tupo na fake ID, mtu unakuwa huru kusema lile unaloliona ni sawa bila kuwa na hofu ya kukosolewa utendaji wako katika jamii sababu hujulikani. HUU NDO UZURI WA MAX NA JF YAKE..
 
Wenye GPA kubwa ndio muhimu tena wanatakiwa kuendelezwa kwa kutumia internship.
Mkuu Siku zote GPA ndo Hatua ya kwanza, waliofaulu ndo wanatazamwa kwanza na kutegemewa zaidi na ndio wanaopata nafasi kwanza,hata kipindi chetu ndivyo ilivyokuwa. Tatizo ya miaka hii kuanzia 2010 wenye GPA wanapoitwa ni kama wanawaambia watu mnachotegemea hamtakutana nacho, haya makaratasi yetu yasiwadanganye, jaribuni na wengine.
 
Mkuu Siku zote GPA ndo Hatua ya kwanza, waliofaulu ndo wanatazamwa kwanza na kutegemewa zaidi na ndio wanaopata nafasi kwanza,hata kipindi chetu ndivyo ilivyokuwa. Tatizo ya miaka hii kuanzia 2010 wenye GPA wanapoitwa ni kama wanawaambia watu mnachotegemea hamtakutana nacho, haya makaratasi yetu yasiwadanganye, jaribuni na wengine.
Umeongea kifalsafa sana. Sijui ni kwa nini wasomi wetu hii mantiki rahisi hawaielewi. GPA sawa, lakini kwenye usaili wenye hizo GPA wanashindwa kuthibitisha kwamba wanazo hizo GPA.

Huwezi kufanya usaili kwa watu wasio na sifa ya kusailiwa. Sasa wanaposhindwa kuthibitisha huo U- GPA wao, ndipo Waziri anapoona lazima marekebisho yafanyike kwenye hizo saili zao. Lakini linazuka jambo la kuonekana wenye GPA kubwa hawatakiwi kuajiriwa.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Umeongea kifalsafa sana. Sijui ni kwa nini wasomi wetu hii mantiki rahisi hawaielewi. GPA sawa, lakini kwenye usaili wenye hizo GPA wanashindwa kuthibitisha kwamba wanazo hizo GPA.

Huwezi kufanya usaili kwa watu wasio na sifa ya kusailiwa. Sasa wanaposhindwa kuthibitisha huo U- GPA wao, ndipo Waziri anapoona lazima marekebisho yafanyike kwenye hizo saili zao. Lakini linazuka jambo la kuonekana wenye GPA kubwa hawatakiwi kuajiriwa.
Kweli mkuu, halafu nadhani tuna tatizo la kuuchukia ukweli. Yaani kama nina GPA kubwa na sina kazi basi akitokea anayesema GPA si kigezo pekee anachukiwa wakati ni suala jepesi tu, hakikisha kilichopo kwenye karatasi zako kipo kichwani basi.
 
Kuanzia sasa Serikali itaanza kuzitazama ajira za vyuo vikuu badala ya kuangalia ubora wa ufaulu yaani GPA pekee sasa waajiriwe kwa kupimwa uwezo wao kwa kufanya usaili.

Kuangalia ufaulu pekee wa wanafunzi haitoshi kuboresha elimu badala yake ni muhimu kuongeza vigezo hivyo katika mapitio ya sera na mabadili ya mitaala jambo hilo litatazamwa kwa weledi mkubwa.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda ameyasema hayo leo tarehe 12 Disemba 2022 mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango wakati wa mahafali ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania iliyofanyika Kinondoni Jijini Dar es Salam.

Amesema wakati serikali inaongeza udahili wa wanafunzi haitakuwa tayari kuona ubora unapungua hivyo serikali inaendelea na mkakati wake wa kuhakikisha ubora wa elimu hususani katika vyuo vikuu unaimarika.

"Zamani ilikuwa rahisi kuwa Profesa ukiandika tu kwenye magazeti unakuwa Profesa lakini kwa sasa vigezo vya kuwa Profesa vimezidi kuwa vigumu kwa sababu tunataka maprofesa wetu wawe sawa na wale wa nchi zingine," amekaririwa Prof Mkenda.

Amesema katika mageuzi ya elimu yanayokuja ambapo wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ipo katika mapitio ya sera na mitaala miongoni mwa mambo yatakayofanyiwa kazi itakuwa ni pamoja na kuhakikisha wanaoajiriwa ni wanafunzi wenye sifa zinazotakiwa.

Pia, Waziri Mkenda amesema kuwa serikali kwa sasa inaendelea na Ujenzi wa Kampasi mpya za Vyuo Vikuu katika mikoa 14 Tanzania pamoja na upande wa Zanzibar (Unguja na Pemba) katika maeneo ambayo hayana vyuo vikuu ukiacha vyuo huria.

Mikoa hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na kampasi za vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini ni pamoja na Tabora, Katavi, Kigoma, Kagera, Singida, Manyara, Lindi, Rukwa, Mwanza, Simiyu, Tanga, Ruvuma, Shinyanga na Dodoma.
Wangewekeza kwenye kuboresha viwango vya elimu inayotolewa katika vyuo vilivyopo. Matokeo ya Law School yanatakiwa kuwaamsha.

Amandla...
 
Siku hizi binti akiwa pisi kali anaruka na lecturers tu analamba GPA kali, kijana akiwa yupo kwenye circle ya huyo binti (wanafanya discussion pamoja ya mapepa anayovujishiwa) nae anakula GPA kali. Wakienda kwenye practical makazini wanaanza upya. Ufanisi hauendani na GPA.

Wale wenzangu na mie shule za kuunga unga msuli tembo marks sisimizi, wakikaza zaidi wanakula 4.0 kushuka chini.

Nimekumbuka mwaka wa pili chuoni kuna lecturer pisi kali haswa tuliletewa kala GPA 4.7 aje atufundishe parasitology, cha ajabu hata kudadavua lifecycle za Plasmodium na Wuchereria bancrofti ilikua changamoto.

Kwahiyo naunga mkono hoja, suala la kuangalia GPA katika kuajili hawa T.A na Lecturers vyuoni lisipewe mkazo sana bali wawe strict na usaili ili wapate cream iliyo bora kuwafundisha vijana wetu huko vyuoni.
Hapo kwenye pisi kali nakubaliana Na ww kabisa, hizo pisi ukijenga nao mahusiano Mazur unatoboa kirahis mno
 
Hili neno sijui watu hawalijui maana yake!!??
Hahahaha. Wanalijua ila nadhani wapo ambao wakiwaza chuo alijifunza nn anaishia kukumbuka title ya kozi tu iliyoandikwa kwenye cheti sababu kilichopo kwenye printed results hakipo kichwani sasa huyu lazima aichukie hiyo sentensi GPA SI KIGEZO PEKEE.
 
Usaili wa nini? Mtu hapati ajira mpaka baada ya muda wa matazamio kupita. Muda huo ndio unatakiwa kutumika kuamua kama mtu anastahili hiyo ajira au la.

Amandla...
 
Siku hizi binti akiwa pisi kali anaruka na lecturers tu analamba GPA kali, kijana akiwa yupo kwenye circle ya huyo binti (wanafanya discussion pamoja ya mapepa anayovujishiwa) nae anakula GPA kali. Wakienda kwenye practical makazini wanaanza upya. Ufanisi hauendani na GPA.

Wale wenzangu na mie shule za kuunga unga msuli tembo marks sisimizi, wakikaza zaidi wanakula 4.0 kushuka chini.

Nimekumbuka mwaka wa pili chuoni kuna lecturer pisi kali haswa tuliletewa kala GPA 4.7 aje atufundishe parasitology, cha ajabu hata kudadavua lifecycle za Plasmodium na Wuchereria bancrofti ilikua changamoto.

Kwahiyo naunga mkono hoja, suala la kuangalia GPA katika kuajili hawa T.A na Lecturers vyuoni lisipewe mkazo sana bali wawe strict na usaili ili wapate cream iliyo bora kuwafundisha vijana wetu huko vyuoni.
Naunga mkono hoja. Unajua sana.
 
Back
Top Bottom