Wenye GPA kubwa ndio muhimu tena wanatakiwa kuendelezwa kwa kutumia internship.Boss, sipo hata kwenye nafasi ya kushindana na yoyote kielimu katika kuchangia uchumi wa hii nchi.
Nilipata nafasi ya ajira nikafanya sehemu yangu na kumaliza na sasa nipo katika nafasi ya kuwezesha wengine wapate ajira. GPA sio suala langu tena maana wakati wangu ulishapita ila Natoa maoni kulingana na kile ninachokiona, kusema kuwa ni wivu hakutabadili uhalisia wa ninachokiona.
Vitendo unajifunza boss. Waziri aanzishe internship kwa watu wenye GPA kubwa ili waendelezwe wasaidie taifa letu.Huwezi jua labda na Tanzania tunao "Genius"" wengi tu.
Turudi kwenye mada. Unajua kwamba zamani usomi ulipimwa kwa uwezo binafsi wa mtu kujenga hoja na si vyeti!? na Vyuo walivyosoma hao unaowaita "Genius" vilikuwa havitumii mifumo kama hii inayotumika sasa?
Mimi naona mbali na GPA ni lazima usomi wa mtu upimwe kwa vitendo baada ya kufaulu nadharia/vitendo vya chuoni. Nchi zilizoendelea hutaka sana kujua baada ya kufaulu mitihani wewe binafsi unaweza kuongeza nini kwenye jamii na siyo kusema una GPA kubwa ama ndogo!!?
Wavumbuzi wengi hawakumbukwi kwa GPA bali kwa vumbuzi zao. Leo hii Mark Zuckerberg ama Bill Gates wanakumbukwa kwa uvumbuzi wao na si kwa GPA zao. Bado nasisitiza kwamba kigezo cha GPA kuwa kubwa ndiyo uajiriwe kuwa mhadhiri hakijatolewa na Profesa Mkenda.
Hii sasa ni hoja lakini haihusiani na ile ya usaili kindakindaki. Nchi yetu mfumo wa kuwalea wasomi wetu ni mbovu. Mazoezi kwa vitendo (internship) ndiyo humkomaza msomi. wanaofanya ni madaktari tu.Vitendo unajifunza boss. Waziri aanzishe internship kwa watu wenye GPA kubwa ili waendelezwe wasaidie taifa letu.
Unajiliwaza tu mkuu. Kigezo ndio hicho. Minimum GPA ni 3.8. Hapo ndio unqualify walau kuwa shortlisted kwa ajili ya interview. Na hizo ni guidelines za TCU. Hata kama unahisi una uwezo wa kufundisha, maadam hujakidhi hicho kigezo kimojawapo, sahau kuitwa kwny interview. Halafu tuache excuses za kufeli kwetu kwa kubeza waliofaulu kutuzidi. Mnatumia kigezo gani kuwa mwenye GPA kubwa kafake na mwenye GPA ndogo ni genuine? Nani aliyeingiza hii mentality kwa jamii?Ahahahahah kama umeniona vile, maana nishawahi kuitwa na. mkuu mmoja wa chuo alikuwa rafiki yangu huku Mkoani, akasema bora uje ufundishe, siuna-GPA ya 3.8 nikamwambia waapi mkuu, nina 3.7 ya SUA.
Ajira ikaishia hapo, na ninao uwezo mkubwa sana wa kufundisha lkn ndo hivyo tena ahahahah
Umemjibu vizuri sana. Ila hapo mwisho naomba nitakuchallange kidogo.Hivi mkuu umesoma kweli? Au wewe ndio miongoni mwa yale masifuri tuko nayo katika hii nchi?
Ni bahati mbaya sana na sijui kama unajua, uhusiano unaojaribu kuutengeneza kati ya matokeo ya mtu ya darasa la saba hadi kidato cha sita na GPA ya chuo ni uhusiano mfu na haupo.
Aya yako ya kwanza ndio kitu anacholia nacho Waziri, kuwa na GPA kubwa kutoka katika chuo chochote kile Tanzania isiwe kigezo pekee cha mtu kuajiriwa kuwa mkufunzi chuoni.
Waziri yupo sahihi, watu wasipate ajira moja kwa moja baada ya kuwa na GPA kubwa, wapimwe kwanza. Kufundisha Chuo kikuu ni kazi inayohitaji mtu mwenye uelewa mpana sana na kudadavua mambo.
Wapo watu wenye GPA kubwa na walizipata kihalali kabisa kwa kukariri notes za darasani na kuyaotea maswali, hawa hawawezi kuwa wakufunzi kwasababu nje ya hiyo mitihani waliyofaulu hamna kitu kingine.
Lakini pia kuna waliopata hizo GPA kubwa kwa njia za kona kona kama kuwa karibu na wakufunzi, hawa pia kuwapa ajira moja kwa moja ni tatizo.
Vyuoni wapo wakufunzi ambao wanaingia kufundisha lakini anaishia kusoma notes, na hata akiulizwa swali na mwanafunzi anashindwa kujibu kwasababu alikariri na uwezo wake ni mdogo.
Andiko langu haliondoi ukweli kwamba wenye GPA ndogo ni VILAZA tu.
Weww jamaa una wivu na ujuaji mwingi Sana ,mbaya zaidi mmejaaa ofcin huko mnajiona Sana mnajua kuliko mtu yeyote ......Ninachokueleza ni kwamba graduates, matokeo yao ya makaratasi hayafanani na kilichomo kichwani, Nawapokea sana, nawapa nafasi sana, field wanaziomba sana, kujitolea na ajira wanaomba hivyo nakutana nao mara nyingi tu na wakati mwingine yule ambaye kwenye makaratasi wala haonekani mwenye elimu kubwa na diploma ya vyuo visivyo rasmi anafanya vizuri tu kuzidi vijana wa IAA, Mzumbe, UD, UDOM SAUT n.k.
Mfano wa swali jepesi katika field ya biashara ambalo mwanachuo yoyote esp mwenye GPA kubwa hakupaswa kushindwa kulijibu: Ni nyaraka zipi zinatumika kufanya miamala baina ya raia wawili walio nchi tofauti wakati wanafanya biashara?
Hii ni international trade, Mtu ana BBA na GPA fiirst class lakini anajibu mpaka unaona huruma, wakati mwingine unadhani ni panic unamwambia relax, kunywa maji unampigisha hadithi nyingine ili asiumie kisha ukishaona karudi normal unaruhusu panel iendelee ila still wengi wanashindwa na hapo swali limeulizwa kwa kiswahili.
BOSS NAKUELEZA, TUNA TATIZO LINALOPASWA KUFANYIWA KAZI. TUNAPOELEKEA IKITOKEA PAKAWA NA UHURU WA KUAJIRI BAINA YA EA VIJANA WETU WATAUMIA SANA.
Mkuu uwezo wa mtu wa kuhoji ,kujieleza na kuwa mbunifua utaujuje ? Kwenye interview ya masaa 3 au ?Huwezi jua labda na Tanzania tunao "Genius"" wengi tu.
Turudi kwenye mada. Unajua kwamba zamani usomi ulipimwa kwa uwezo binafsi wa mtu kujenga hoja na si vyeti!? na Vyuo walivyosoma hao unaowaita "Genius" vilikuwa havitumii mifumo kama hii inayotumika sasa?
Mimi naona mbali na GPA ni lazima usomi wa mtu upimwe kwa vitendo baada ya kufaulu nadharia/vitendo vya chuoni. Nchi zilizoendelea hutaka sana kujua baada ya kufaulu mitihani wewe binafsi unaweza kuongeza nini kwenye jamii na siyo kusema una GPA kubwa ama ndogo!!?
Wavumbuzi wengi hawakumbukwi kwa GPA bali kwa vumbuzi zao. Leo hii Mark Zuckerberg ama Bill Gates wanakumbukwa kwa uvumbuzi wao na si kwa GPA zao. Bado nasisitiza kwamba kigezo cha GPA kuwa kubwa ndiyo uajiriwe kuwa mhadhiri hakijatolewa na Profesa Mkenda.
Haupo sahihi. Badili huu mtazamo.Weww jamaa una wivu na ujuaji mwingi Sana ,mbaya zaidi mmejaaa ofcin huko mnajiona Sana mnajua kuliko mtu yeyote ......
Tanzania imejaa watu wa namna hii ,si ajabu ndio maana nchi ni ngumu Sana uchawi na rushwa vimekua Kwa Kasi kubwa sababu ya watu wa aina hii [emoji848][emoji848][emoji848]
Mkuu Siku zote GPA ndo Hatua ya kwanza, waliofaulu ndo wanatazamwa kwanza na kutegemewa zaidi na ndio wanaopata nafasi kwanza,hata kipindi chetu ndivyo ilivyokuwa. Tatizo ya miaka hii kuanzia 2010 wenye GPA wanapoitwa ni kama wanawaambia watu mnachotegemea hamtakutana nacho, haya makaratasi yetu yasiwadanganye, jaribuni na wengine.Wenye GPA kubwa ndio muhimu tena wanatakiwa kuendelezwa kwa kutumia internship.
Umeongea kifalsafa sana. Sijui ni kwa nini wasomi wetu hii mantiki rahisi hawaielewi. GPA sawa, lakini kwenye usaili wenye hizo GPA wanashindwa kuthibitisha kwamba wanazo hizo GPA.Mkuu Siku zote GPA ndo Hatua ya kwanza, waliofaulu ndo wanatazamwa kwanza na kutegemewa zaidi na ndio wanaopata nafasi kwanza,hata kipindi chetu ndivyo ilivyokuwa. Tatizo ya miaka hii kuanzia 2010 wenye GPA wanapoitwa ni kama wanawaambia watu mnachotegemea hamtakutana nacho, haya makaratasi yetu yasiwadanganye, jaribuni na wengine.
Kweli mkuu, halafu nadhani tuna tatizo la kuuchukia ukweli. Yaani kama nina GPA kubwa na sina kazi basi akitokea anayesema GPA si kigezo pekee anachukiwa wakati ni suala jepesi tu, hakikisha kilichopo kwenye karatasi zako kipo kichwani basi.Umeongea kifalsafa sana. Sijui ni kwa nini wasomi wetu hii mantiki rahisi hawaielewi. GPA sawa, lakini kwenye usaili wenye hizo GPA wanashindwa kuthibitisha kwamba wanazo hizo GPA.
Huwezi kufanya usaili kwa watu wasio na sifa ya kusailiwa. Sasa wanaposhindwa kuthibitisha huo U- GPA wao, ndipo Waziri anapoona lazima marekebisho yafanyike kwenye hizo saili zao. Lakini linazuka jambo la kuonekana wenye GPA kubwa hawatakiwi kuajiriwa.
Hili neno sijui watu hawalijui maana yake!!??akitokea anayesema GPA si kigezo pekee anachukiwa wakati ni suala jepesi tu, hakikisha kilichopo kwenye karatasi zako kipo kichwani basi.
Wangewekeza kwenye kuboresha viwango vya elimu inayotolewa katika vyuo vilivyopo. Matokeo ya Law School yanatakiwa kuwaamsha.Kuanzia sasa Serikali itaanza kuzitazama ajira za vyuo vikuu badala ya kuangalia ubora wa ufaulu yaani GPA pekee sasa waajiriwe kwa kupimwa uwezo wao kwa kufanya usaili.
Kuangalia ufaulu pekee wa wanafunzi haitoshi kuboresha elimu badala yake ni muhimu kuongeza vigezo hivyo katika mapitio ya sera na mabadili ya mitaala jambo hilo litatazamwa kwa weledi mkubwa.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda ameyasema hayo leo tarehe 12 Disemba 2022 mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango wakati wa mahafali ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania iliyofanyika Kinondoni Jijini Dar es Salam.
Amesema wakati serikali inaongeza udahili wa wanafunzi haitakuwa tayari kuona ubora unapungua hivyo serikali inaendelea na mkakati wake wa kuhakikisha ubora wa elimu hususani katika vyuo vikuu unaimarika.
"Zamani ilikuwa rahisi kuwa Profesa ukiandika tu kwenye magazeti unakuwa Profesa lakini kwa sasa vigezo vya kuwa Profesa vimezidi kuwa vigumu kwa sababu tunataka maprofesa wetu wawe sawa na wale wa nchi zingine," amekaririwa Prof Mkenda.
Amesema katika mageuzi ya elimu yanayokuja ambapo wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ipo katika mapitio ya sera na mitaala miongoni mwa mambo yatakayofanyiwa kazi itakuwa ni pamoja na kuhakikisha wanaoajiriwa ni wanafunzi wenye sifa zinazotakiwa.
Pia, Waziri Mkenda amesema kuwa serikali kwa sasa inaendelea na Ujenzi wa Kampasi mpya za Vyuo Vikuu katika mikoa 14 Tanzania pamoja na upande wa Zanzibar (Unguja na Pemba) katika maeneo ambayo hayana vyuo vikuu ukiacha vyuo huria.
Mikoa hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na kampasi za vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini ni pamoja na Tabora, Katavi, Kigoma, Kagera, Singida, Manyara, Lindi, Rukwa, Mwanza, Simiyu, Tanga, Ruvuma, Shinyanga na Dodoma.
Hapo kwenye pisi kali nakubaliana Na ww kabisa, hizo pisi ukijenga nao mahusiano Mazur unatoboa kirahis mnoSiku hizi binti akiwa pisi kali anaruka na lecturers tu analamba GPA kali, kijana akiwa yupo kwenye circle ya huyo binti (wanafanya discussion pamoja ya mapepa anayovujishiwa) nae anakula GPA kali. Wakienda kwenye practical makazini wanaanza upya. Ufanisi hauendani na GPA.
Wale wenzangu na mie shule za kuunga unga msuli tembo marks sisimizi, wakikaza zaidi wanakula 4.0 kushuka chini.
Nimekumbuka mwaka wa pili chuoni kuna lecturer pisi kali haswa tuliletewa kala GPA 4.7 aje atufundishe parasitology, cha ajabu hata kudadavua lifecycle za Plasmodium na Wuchereria bancrofti ilikua changamoto.
Kwahiyo naunga mkono hoja, suala la kuangalia GPA katika kuajili hawa T.A na Lecturers vyuoni lisipewe mkazo sana bali wawe strict na usaili ili wapate cream iliyo bora kuwafundisha vijana wetu huko vyuoni.
Hahahaha. Wanalijua ila nadhani wapo ambao wakiwaza chuo alijifunza nn anaishia kukumbuka title ya kozi tu iliyoandikwa kwenye cheti sababu kilichopo kwenye printed results hakipo kichwani sasa huyu lazima aichukie hiyo sentensi GPA SI KIGEZO PEKEE.Hili neno sijui watu hawalijui maana yake!!??
Naunga mkono hoja. Unajua sana.Siku hizi binti akiwa pisi kali anaruka na lecturers tu analamba GPA kali, kijana akiwa yupo kwenye circle ya huyo binti (wanafanya discussion pamoja ya mapepa anayovujishiwa) nae anakula GPA kali. Wakienda kwenye practical makazini wanaanza upya. Ufanisi hauendani na GPA.
Wale wenzangu na mie shule za kuunga unga msuli tembo marks sisimizi, wakikaza zaidi wanakula 4.0 kushuka chini.
Nimekumbuka mwaka wa pili chuoni kuna lecturer pisi kali haswa tuliletewa kala GPA 4.7 aje atufundishe parasitology, cha ajabu hata kudadavua lifecycle za Plasmodium na Wuchereria bancrofti ilikua changamoto.
Kwahiyo naunga mkono hoja, suala la kuangalia GPA katika kuajili hawa T.A na Lecturers vyuoni lisipewe mkazo sana bali wawe strict na usaili ili wapate cream iliyo bora kuwafundisha vijana wetu huko vyuoni.
Si lazima kwanza ubadilishe mfumo wa kuwapata watoa elimu ndipo upate matokeo bora!!??Wangewekeza kwenye kuboresha viwango vya elimu inayotolewa katika vyuo vilivyopo. Matokeo ya Law School yanatakiwa kuwaamsha.
Amandla...