Waziri Mkuu Kassim Majaliwa afika Kariakoo. Aagiza task force za TRA kusitisha shughuli zake haraka

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa afika Kariakoo. Aagiza task force za TRA kusitisha shughuli zake haraka



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameamua kukutana na kuongea na Wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo leo ambapo tayari amefika Kariakoo muda huu badala ya Jumatano May 17,2023 ambayo ilitangazwa hapo wali hii ni kutokana na uzito wa suala hilo.

Awali mkutano kati ya Waziri Mkuu na Kamati ya Wafanyabiashara hao pamoja na TRA na Mawaziri wa Sekta husika ulitarajiwa kufanyika saa 8 Mchana kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu Magogoni-Ikulu Dar es salaam Jumatano May 17, 2023 kwa uratibu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makala, lakini Waziri Mkuu ameamua aende leoleo Kariakoo.

Pia Soma:
- News Alert: - Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Oya hii habari mbona update yake inachelewa nini tatizo sie tuliombali na huko !?
 
Kulipa kodi halafu zinaenda kuchotwa (na CAG amelithibitisha hilo)ni sawasawa na kujaza maji kwenye Gunia Mgomo uendelee.

Na hizo zilizobakia zinaenda kulipiwa Mabango ya kusifiasifia.

Wizi umeongezeka.
Kweli kabisa tunabinywa kulipa kodi kisha kodi zetu wanajichotea na kuwekeza kwenye biashara zao binafsi na nyingine zinafijwa kwa kujaza mabango nchi nzima ya kusifia Samia kama vile ameshuka kutoka mbinguni
 


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameamua kukutana na kuongea na Wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo leo ambapo tayari amefika Kariakoo muda huu badala ya Jumatano May 17,2023 ambayo ilitangazwa hapo wali hii ni kutokana na uzito wa suala hilo.

Awali mkutano kati ya Waziri Mkuu na Kamati ya Wafanyabiashara hao pamoja na TRA na Mawaziri wa Sekta husika ulitarajiwa kufanyika saa 8 Mchana kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu Magogoni-Ikulu Dar es salaam Jumatano May 17, 2023 kwa uratibu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makala, lakini Waziri Mkuu ameamua aende leoleo Kariakoo.

Pia Soma:
- News Alert: - Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

nimeishia hapo kwenye "mama sa100 oye"
yaani ushabadilika na kua mkutano wa kupiga kampeni baridi
 
Kumbe tatizo hakuwa Meko ila TRA kutumia mabavu kwenye kukusanya kodi ni kawaida yao.
 
Uamuzi wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, umekuja baada ya kusikiliza kero za Wafanyabiashara walioitisha Mgomo wa kutofungua Maduka leo Mei 15, 2023

Majaliwa amesema ‘Task Force’ hizo zimekuwa zikitumika kufanya kamatakamata ya Wafanyabiashara na wakati mwingine kujihusisha na Vitendo vya Rushwa

Ameongeza “Kamishna wa Mapato ya Ndani TRA,naagiza Task Force isitishwe, Kanuni zipo, Sheria zipo zinatuelekeza namna ya kulipa Kodi, kamatakamata hii inafukuza Wafanyabiashara Kariakoo na mbaya zaidi mnawakamata hadi Wageni kutoka nje”
 
Kuna jamaa alikuwa kwenye hiyo task force, bila kuficha alikuwa anajisifu kwa siku kulaza mpaka mil 4 ilikuwa ni kawaida kabisa.

Jina pia lilibadilika mtaani, alikuwa anaitwa 'kiongozi' au 'mkuu'.

Sasa kama imesitishwa hiyo task force jamaa sijui itakuwaje.
 
Uamuzi wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, umekuja baada ya kusikiliza kero za Wafanyabiashara walioitisha Mgomo wa kutofungua Maduka leo Mei 15, 2023

Majaliwa amesema ‘Task Force’ hizo zimekuwa zikitumika kufanya kamatakamata ya Wafanyabiashara na wakati mwingine kujihusisha na Vitendo vya Rushwa

Ameongeza “Kamishna wa Mapato ya Ndani TRA,naagiza Task Force isitishwe, Kanuni zipo, Sheria zipo zinatuelekeza namna ya kulipa Kodi, kamatakamata hii inafukuza Wafanyabiashara Kariakoo na mbaya zaidi mnawakamata hadi Wageni kutoka nje”
Ule mchezo wetu wa milioni milioni kwa siku 3 sijui utaendaje sasa..!
Shubamiti nyie wafanyabiashara!
 
Tanzania Ya Viwanda
Mkoa Wa Pwani Una Viwanda 700
 
Back
Top Bottom