Waziri Mkuu Kassim Majaliwa afika Kariakoo. Aagiza task force za TRA kusitisha shughuli zake haraka

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa afika Kariakoo. Aagiza task force za TRA kusitisha shughuli zake haraka

Sababu serikali badala ya kujiongeza Kariakoo iwe kimbilio la kanda hii nzima ya Africa, yenyewe ina ondoa mazingira hayo ya Kariakoo kuwa kitovu cha biashara.

Wakati viongozi wa Dubai n.k wao kila siku wanawaza Dubai izidi vipi kujitanua kama Centre ya kibiashara duniani, viongozi wa Tanzania hawana maono hayo, bali wanawaza kukamua kodi badala ya kuongeza wigo wa wingi wa wafanyabiasha ili ipelekee Kariakoo kuwa Dubai na kuchangia kodi.
Hatuna maono..watu waende kwa wenzetu wajifunze. Tatizo pia kuna mitandao ya rushwa..afisa anapewa laki mbili anahujumu kodi za mamilioni. We still have very long journey to go.
 
Wamekata umeme leo bungeni ili suala hilo lisijadiliwe kwa hofu ya baadhi ya wabunge kuliibua huko lijadiliwe kwa dharura.
 
Lipeni kodi , mnakwepa sana kodi
Baadhi ya mabango ni vigumu kuamini kwamba ni madai ya hawa watu.

Kwa mfano:
1. Kusajili 'Store' ni sheria kandamizi? Wanataka wao iweje?

2. EFD inaua biashara?

3. Wanataka "Uhuru" wa Biashara? wafanye watakavyo wao; bila kujali matakwa ya sheria zinazosimamia kazi zao?

Naona hapa kuna tatizo, na inawezekana wanakomaa kwa kujua alieko Ikulu ni mtu wa kusikia kila wanachotaka wao.
 
Baadhi ya mabango ni vigumu kuamini kwamba ni madai ya hawa watu.

Kwa mfano:
1. Kusajili 'Store' ni sheria kandamizi? Wanataka wao iweje?

2. EFD inaua biashara?

3. Wanataka "Uhuru" wa Biashara? wafanye watakavyo wao; bila kujali matakwa ya sheria zinazosimamia kazi zao?

Naona hapa kuna tatizo, na inawezekana wanakomaa kwa kujua alieko Ikulu ni mtu wa kusikia kila wanachotaka wao.
Eti bana, hawa wana janja janja nyingi
 
Ni haki yao kufunga au kufungua maduka na serikali haiwezi kuwalizimisha wafanyabishara kufanya kinyume na matakwa yao.

Tuliza akili.
 


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameamua kukutana na kuongea na Wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo leo ambapo tayari amefika Kariakoo muda huu badala ya Jumatano May 17,2023 ambayo ilitangazwa hapo wali hii ni kutokana na uzito wa suala hilo.

Awali mkutano kati ya Waziri Mkuu na Kamati ya Wafanyabiashara hao pamoja na TRA na Mawaziri wa Sekta husika ulitarajiwa kufanyika saa 8 Mchana kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu Magogoni-Ikulu Dar es salaam Jumatano May 17, 2023 kwa uratibu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makala, lakini Waziri Mkuu ameamua aende leoleo Kariakoo.
---
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa baada ya kusikiliza kero za Wafanyabiashara wa Kariakoo leo ameiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kufuta Vikosi Kazi (Task Forces) ambavyo amesema vinatumika kufanya kamatakamata na wakati mwingine kuchukua rushwa.

Waziri Mkuu Majaliwa akiwa Kariakoo jioni hii amesema “Tuna taarifa kuwa kuna kikosi kazi kimeundwa kinazunguka huko, Rais alikemea Vikosi Kazi (Task Forces) kwasababu vinatumika kuwasumbua Wafanyabishara na kuomba pia rushwa, naagiza hiyo Task Force isitishwe mara moja”.

“Task force hii ndio inaendesha kamatakamata kila siku, Kamishna wa Mapato ya Ndani TRA naagiza isitishwe, kanuni zipo sheria zipo zinatuelekeza namna ya kulipa kodi, kamatakamata hii inafukuza Wafanyabiashara Kariakoo na mbaya zaidi mnawakamata hadi Wageni kutoka nje”.

AWASHANGAA TRA kukaidi maagizo ya Rais
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameshangazwa na Watumishi wa ngazi za chini wakiwemo wa TRA kukaidi maagizo ya Rais wa Tanzania Dkt. Samia, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, wakisema ni maagizo ya kisiasa tu ambapo amesema wakimbaini anayetoa majibu hayo atachukuliwa hatua.

Akiongea na Wafanyabiashara wa Kariako leo Waziri Mkuu ameshangazwa na wanaodharau kauli za Viongozi Wakuu wa Kitaifa “Akitokea Mtu anasema lazima ulete barua ya agizo lililotolewa na Rais, Makamu wa Rais au Waziri Mkuu, mtuletee huyo Mtu, Rais,Makamu wa Rais na Waziri Mkuu hawaandiki barua, wataandika barua ngapi?”

“Rais na Makamu wa Rais wanapoagiza sisi wa chini tunatekeleza, leo TRA Rais amesema kodi za miaka mitano mziache, nyie mnadai barua kwa Watu wa Kariakoo hivi Mfanyabiashara wa Kariakoo atapata wapi barua ya Rais? halafu unamwambia Mfanyabiashara hilo ni agizo tu la kisiasa, yaani agizo lililotolewa na Rais unasema ni la kisiasa hiyo ni dharau na natamani ningemjua aliyesema hivyo tumchukulie hatua”.

Awaomba wafanyabiashara kufungua maduka yao
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaomba Wafanyabiashara wa Kariakoo kusitisha mgomo na kufungua maduka yao huku akiagiza TRA kuacha kuwaonea Wafanyabiashara.

Akiongea na Wafanyabiashara wa Kariakoo leo, PM Majaliwa amesema “Nimeacha Bunge nimewafuata kuja kujua kuna nini!? Soko la Kariakoo tunalitegemea kutuingizia mapato ni lazima tulitulinze , nimesoma mabango yenu moja baada ya moja, kuna linalosema “TRA mmefukuza Wageni’ , mmeongelea EFD n.k, hakuna jambo mtalifanya tutalichukulia rahisirahisi”

“Tabia ya kuonea Wafanyabiashara ikome mara moja, hii ya kukusanya tu mnakusanya tu mpaka damu itoke hii sio sawa, wengine mnawazidishia kodi ili mkae nao chini muwaombe rushwa na hii rushwa inafanya Wafanyabiashara watoe hadi pesa zao za mauzo”

“Wafanyabiashara sikieni ombi la Serikali fungueni maduka yenu na matatizo yote keshokutwa tunayajadili keshokutwa, ningeweza kusema kesho lakini Mh.Rais amenituma kumwakilisha kwenye maziko ya Mh. Membe acha niende kesho asubuhi, ilitakiwa niende leo nimeghairi naenda asubuhi kesho nazika narudi tutatue matatizo”.

Pia Soma:
- News Alert: - Mgomo mkubwa Soko la Kariakoo: Maduka yamefungwa, Mei 15, 2023

Nadhani PM amekosa ushawishi, kwenye hili.

Maneno matamu, lakini vitendo zero.

Ndio maana wameendelea kugoma.
Serikali ilifanyie hili kazi kwa upya na uwazi zaidi ili shughuli na maisha virejee Kariakoo.

"Usipoziba ufa utajenga ukuta"
 
Baadhi ya mabango ni vigumu kuamini kwamba ni madai ya hawa watu.

Kwa mfano:
1. Kusajili 'Store' ni sheria kandamizi? Wanataka wao iweje?

2. EFD inaua biashara?

3. Wanataka "Uhuru" wa Biashara? wafanye watakavyo wao; bila kujali matakwa ya sheria zinazosimamia kazi zao?

Naona hapa kuna tatizo, na inawezekana wanakomaa kwa kujua alieko Ikulu ni mtu wa kusikia kila wanachotaka wao.

Unajua mfanyabiashara wa Tanzania analipa kodi ngapi?? Ungekua unafanya biashara usingeandina huu ujinga. Tokeni huko maofisin mje kwenye biashara ndo mjue tunavyokutana navyo.
 
Unajua mfanyabiashara wa Tanzania analipa kodi ngapi?? Ungekua unafanya biashara usingeandina huu ujinga. Tokeni huko maofisin mje kwenye biashara ndo mjue tunavyokutana navyo.
Ni wazi kabisa hapa "mjinga" ni nani kati yangu na wewe.

Ujinga wako unatokana na kutoelewa kilichoandikwa hata kama unajua kusoma.

Usingekuwa mjinga ungetambua kwamba swala linaloongelewa siyo "kodi ngapi" anazolipa huyo mfanya biashara.
Ungejua swala la msingi ni kila mhusika atimize wajibu wake unapowekwa utaratibu kisheria.

Hizo "kodi ngapi" unazozungumzia wewe huko ndiko kunakotakiwa kushikia bango kabla ya sheria husika hazijatengenezwa kuhalalisha kodi hizo.

EFD unaikataa wewe kama mfanya bisahara, wewe kweli ni mfanya biashara au jambazi tu huko mitaani?
Sidhani kamwe kwamba wewe unao uelewa kweli wa kufanya biashara ni nini hasa!
 
Back
Top Bottom