Waziri Mkuu Kassim Majaliwa afika Kariakoo. Aagiza task force za TRA kusitisha shughuli zake haraka

Oya hii habari mbona update yake inachelewa nini tatizo sie tuliombali na huko !?
 
Kulipa kodi halafu zinaenda kuchotwa (na CAG amelithibitisha hilo)ni sawasawa na kujaza maji kwenye Gunia Mgomo uendelee.

Na hizo zilizobakia zinaenda kulipiwa Mabango ya kusifiasifia.

Wizi umeongezeka.
Kweli kabisa tunabinywa kulipa kodi kisha kodi zetu wanajichotea na kuwekeza kwenye biashara zao binafsi na nyingine zinafijwa kwa kujaza mabango nchi nzima ya kusifia Samia kama vile ameshuka kutoka mbinguni
 
nimeishia hapo kwenye "mama sa100 oye"
yaani ushabadilika na kua mkutano wa kupiga kampeni baridi
 
Kumbe tatizo hakuwa Meko ila TRA kutumia mabavu kwenye kukusanya kodi ni kawaida yao.
 
Uamuzi wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, umekuja baada ya kusikiliza kero za Wafanyabiashara walioitisha Mgomo wa kutofungua Maduka leo Mei 15, 2023

Majaliwa amesema ‘Task Force’ hizo zimekuwa zikitumika kufanya kamatakamata ya Wafanyabiashara na wakati mwingine kujihusisha na Vitendo vya Rushwa

Ameongeza “Kamishna wa Mapato ya Ndani TRA,naagiza Task Force isitishwe, Kanuni zipo, Sheria zipo zinatuelekeza namna ya kulipa Kodi, kamatakamata hii inafukuza Wafanyabiashara Kariakoo na mbaya zaidi mnawakamata hadi Wageni kutoka nje”
 
Kuna jamaa alikuwa kwenye hiyo task force, bila kuficha alikuwa anajisifu kwa siku kulaza mpaka mil 4 ilikuwa ni kawaida kabisa.

Jina pia lilibadilika mtaani, alikuwa anaitwa 'kiongozi' au 'mkuu'.

Sasa kama imesitishwa hiyo task force jamaa sijui itakuwaje.
 
Ule mchezo wetu wa milioni milioni kwa siku 3 sijui utaendaje sasa..!
Shubamiti nyie wafanyabiashara!
 
Tanzania Ya Viwanda
Mkoa Wa Pwani Una Viwanda 700
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…