Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa: Makamu wa Rais, Philip Mpango yuko nje kwa majukumu
Waziri Mkuu ( Premier ) Kassim Majaliwa nadhani GENTAMYCINE nilishakushauri hapa hapa JamiiForums kuwa kukiwa na Taharuki yoyote au Tukio lolote lile la Kihisia usipende kuwa na Kiherehere cha Kulisemea kwani Kirekodi una Gundu kwani kila ukijitokeza Kutetea Jambo fulani kwa dhana ya Kulificha huwa linakuumbua na hatimaye Kudharaulika, Kuchekwa na Kutoaminiwa tena.

Premier Kassim Majaliwa jana Umesikika na Kunukuliwa mahala ukisema kuwa Makamu wa Rais Dkt. Phillip Isidori Mpango yuko mzima na nje ya nchi anafanya Shughuli zake za Kiutendaji na Kiuwajibikaji.

Premier Kassim Majaliwa Mimi GENTAMYCINE sina tatizo na hii Taarifa yako ila Kinachonishtua zaidi ni kwamba hata kwa Hayati Dk. Magufuli Uvumi wa Kifo chake ulipoanza na Kuenea kwa Kasi ndani na nje ya Tanzania kama kawaida yako ya kuwa na Kiherehere ulijitokeza na Kutuambia kuwa yuko ni mzima wa Afya, ulizungumza nae, anakunywa Chai Ofisini huku akipitia Mafaili yake wakati kumbe tayari na zamani sana alishakuwa amelazwa katika Mochwari ya Hospitali mbili tofauti kabla ya kupelekwa katika Mochwari ya Wanamedani wa kati ya Kawe na Mwenge.

Binafsi sikuamini tena Premier KMK.
safari ambayo haijaratibiwa na nchi na hata kurugenzi ya ikulu isitoe taarifa ya safari yake? ukoo wa panya as usualy.
 
Mwaka fulani katika Dola ya Rumi alitokea Kiongozi mmoja akawaongopea wananchi kuhusu hali Kiongozi fulani lakini baadae ikaja kujulikana taarifa aliyotoa haikuwa sahihi.

Kiongozi huyo katika Dola ya Rumi mwaka huu 2023 amekuja na taarifa ambayo inatiliwa shaka kutokana na kuwepo na sintofahamu fulani

Je, wananchi katika Dola ya Rumi wamuamini au la?
 
Back
Top Bottom