yaan una shauriwa jambo la maana na muhimu sana kwa mustakabali wa ustawi wa maisha yako kiuchumi, kisha una beza mawaidha hayo ya maana sana kwa kiburi namna hiyo gentleman? hiyo si sawa hata kidogo,

pale VETA unaweza kupata ujuzi katika fani za ufundi ujenzi, umeme, welding, useremala n.k hata ukiwa na masters ya makaratasi, kama unaona kilimo ni kigumu zaidi, maana huko ndiko zilipo ajira za uhakika na za kutosha kwa waTanzania wote 🐒
 
Mkuu mimi nina busara nyingi Sana kuliko kasimu.
Kasimu nilianze kumhofia tangu alipotuambia rais Magufuli Yuko timamu kiafya na anawasalimia.

Ukiniwekea kasimu mganga na kasimu majaliwa nachagua kasimu mganga.
Unaandika kwa trend. Yaani umeona watu wanahoji kwanini kasimu alisema magu mzima, wewe unaandika hivo hivo na unajiona timamu, yes wewe timamu i know. Lakini huwezi kumtoa mtu utimamu kwasababu ya taarifa ya kifo, ule ni msiba wa kitaifa kama sio Africa na Dunia, yule ni raisi. Huwezi tangaza kama unatangaza msiba wa juma msomali pale kiwalani, misiba yote iliyotikisa nchi ilidelay kutolewa taarifa makini kuepuka sintofahamu, maraisi wote. Na si Tanzania tu, hata duniani. Msiba wake unaangalia itifaki, whatever wewe unaona vibaya. Ila kwa wengi ni maumivu, kilio, na hata fursa. Hivo lazma serikali ijipange, kufannya taarifa kama ile.
Ndio majaliwa sio msomi wa masters au degree kubwa hizi, ila swala la veta liko sawa ila linapotoshwa na sisi wachache.
Ila pia hajalazimisha. Unaweza kusubiri ajira au kukaa nyumbani.
 
Hivi mlisikikiza vzr speech ama mnanukuu kama mnavyo fikilia tu coz sijaona tatizo la kauli ya wazir mkuu ama ni kutafuta trend tu, kuna degree gani zinaendesha bodaboda mtaani ? Ebu muacheni mzee wa watu
 
Kabla hatujakuonyesha mtoto wa mteule, na wewe tutajie mtoto wa mteule anayesoma kayumba, mbona tunapeleka watoto sisi watanzania. Au tuletee mtoto wa mteule anayesoma british council au kilimanjaro institute, maana wapo vijana wengi tu wamepita huko, wapo serene, wapo rungwe sinza, wapo tours huko arusha.
 
Kuambiwa mkasome VETA na degree zenu ndio povu liwatoke namna hii?
Hahhahahah hawa vijana na degree zao wanajikuta saana mtaa uko na formula zake, now days watu wenye ujuzi ndo kitu sio hizi papers mpka zifanyiwe internship ndo zianze kazi
 
Kulikuwa na ulazima gani wa kuwambia watu hali ya rais (Magufuli) kwani aliulizwa? Vitu vya kukurupuka ndivyo vinashusha hadhi ya mtu. Kuhusu kuwataka wahitimu kusoma veta sina shida naye lakini jamaa tangu alete kiherehere chake kipindi cha msiba wa Magufuli mi namwana kama zombi linaloendeshwa na Samia Hasani.
 
Kassim Majaliwa kiufupi umeshajipotezea heshima na heshima uliyobaki nayo ni ndogo Sana.

Nakushauri Ujifunze kukaa Kimya hakuna faida utaipata baada ya kuwa mropokaji.
Mzee umeshiba makande unaongea ujinga sasa kuna shida gani ww mwenye degree uchwara kusoma veta ukawa na manufaa kwenye jamii kuliko kuzunguka na bahasha kuomba kazi ambayo hauwezi fanya
 
Huenda Majaliwa anaona mbali kuliko wanaopinga tuwaze nje ya box.Fikiria miaka kumi mbele itakuwaje.Kuna ubaya gani mtu akiwa na degree sociology,law,engineering kujua utengenezaji au usindikaji wa matunda?
Huyo mtu angesoma SUA toka mwanzo mambo ya agrobusiness ingekua poa sana kuliko engineering
 
Kauli mbovu, ya kijinga, kipumbavu,
Unajiuliza, ni, Sera, tafiti,ilani ya chama au, kitu gani, lini ilijadiliwa kwenye baraza LA mawaziri! Ma ccm wanavyokuja na matamko, utafikiri wameingia ikulu Jana!
Tatizo la ajira halijawahi kufanyiwa kazi, wameona vijana wanalalamika, wakaja na upuuzi wa tu me eti Kuta futa suruhisho la vijana wasio na ajira, hiki wanschokifanya ni upuuzi, wa ku buy time uchaguzi upite,
Nchi imefilisika haiwezi, hata kuajiri walimu wake wote,
 
Mtu mwenye
Cheti
Diploma
Degree/ bachelor

Mtu huyu si inaamaana tayar yuko na ujuzi (professionalism) kwahyo veta Tena kufanyaje ?
 
hizi ndizo moja ya akili tulizonazo kama taifa. Kwakweli inasikitisha sana. Embu tujitahidi kuwa tunafikiri kwa kina kabla ya kuropoka.
Shida yenu mnamawazo hasi kila wakati, yalichanganywa na chuki za kisiasa, ndio maana kila kauli ya kiongozi mnaona ni sumu na haifai, badala ya kupinga hiyo kauli, mngeleta hoja za maana kuonyesha kuwa hiyo kauli haifai.

Na juha wote kazi yao ni moja, kujiona yeye bora na anachoongea kina maana kuliko mwengine, kisha akaanza kukebehi kauli ya mwengine, kama ulivyoona wewe kuwa mimi naropoka... Jenga hoja na sio kukebehi
 
Alimaanisha mfumo wetu wa elimu umeshafeli.
 
Aliulizwa, alihojiwa na akajibu. Ni kawaida, Sijui kama unafatilia historia, ila raisi wa Malawi Bingu wa mutharika alipofariki 2012 tu hapo, alikaa siku 48, watu wakihoji, ndio akatangazwa kufariki.
Felix houphet nae, Ilitokea hivo hivo. Hii yote hufanywa ili kuhakikisha mchakato wa kisiasa wa kumpata mrithi wake unakua na utulivu. Na nimekupa sababu.
Mwingine ilikua gamal abdel nasser wa misri kama ulisoma history vizuri.
 
Kuambiwa mkasome VETA na degree zenu ndio povu liwatoke namna hii?
Hawana akili hawa vijana. Dunia ya leo unathaminiwa ukiwa na skills na sio certificates zenu mnazotembeza kutwa kucha barabarani!
 
Tumepigwa pale
 
Hizi si Sheria ambazo tumeziweka wenyewe na zinawwza zikaondolewa wakati wowote?
Au hi Sheria imetoka ktk Quran?
 
Ninafuatilia vyema. Haya nipe mfano kutoka katika nchi za ulaya maana hizi nchi za kiafrika zinafanana.
 
Usichokijua Kasimu kapeleka Chuo Kikuu Lindi. Endelea kuota
 
Aidha alikuwa amefuturu futari lililo chacha au alivimbiwa. Haiwezekani atamke hivi bila nafsi yake kumsuta kwamba ninaowaambia haya ni watoto wa Watanzania wenzangu ambao watoto wao hawana nafasi setikalini ama kwenye siasa. Inaonekana ukiwa kwenye siasa unaweza kuongea lolote lile. Watoto wake wako masomoni Ulaya na Marekani kwenye elimu bora sisi shule zetu ni hizi alizoanzisha Hayati Edward Lowassa, Mungu amlaze pema maana angalau watoto wanafika secondary school. Kama isingekuwa Lowassa nadhani tungeamriwa baada ya degree turudi kusomea elimu ya Chekechea ili tuweze kujiajiri. Hii aibu na fedhea kwa mfumo wa elimu Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…