Waziri Mkuu: Wanaolalama kupata ongezeko la 20,000 ni wale wenye mishahara mikubwa

Waziri Mkuu: Wanaolalama kupata ongezeko la 20,000 ni wale wenye mishahara mikubwa

Waziri Mkuu, Kasimu Majaliwa amesema wengi wanaolalamika kupata ongezeko dogo la mishahara ni wale ambao wana mishahara mikubwa. Ametolea mfano wa mawaziri kuwa wako baadhi ambao ongezeko lao ni 0.02%

Amewaomba watumishi kuwaamini viongozi wa vyama vya wafanyakazi. Amesema wengi waliopata ongezeko kubwa ni wale watumishi waliokuwa wanapata mishahara midogo.

Pia amesema wananchi wanapaswa kushukuru kwa ongezeko hilo ambalo miaka kadhaa iliyopita haikuwepo
Magufuli awamu yake yote hakuwa kuboresha maslai ya wafanyakazi, Samia anastahili pongezi sana
 
Kuna kitu sielewi, hii mishahara ya serikali ndio inayotumika sekta binafsi au? na vipi serikali inapanga mishahara ya sekta binafsi au uhusiano uko vipi kati ya serikali na mishahara ya sekta binafsi
 
Kwa hiyo akina sisi wenye mshahara wa 700k ni mkubwa kama wa mawaziri?
Kama una mshahara wa 700K maana yake, Nyongeza yako siyo pungufu ya Tsh 42,000 ( take home ) kwa mwezi ambayo Ni sawa na Tsh Laki 5+ kwa mwaka.
 
Tusiwafanye watumishi kuwa mazuzu na vyama vya wafanyakazi wasiburuzwe kizembe!

Binafsi mkewangu aliye mwalimu kaongezwa 3.7% ya mshahara wake sasa waeleze ukweli sio blah blah za kisiasa kutafuta masifa yasiyo stahili. Nchi za wenzetu walitangaziwa percentage ya nyongeza na ikatimizwa bila makelele sisi wanasiasa wanawazuga watumishi nakuleta janjajanja na maneno meeengi kisa nini!!! Kwanini nchi hii inaujinga mwiiingi? WHY?

Serikali iwe open na ifanye kazi kisomi na kistaarabu bila hila.
Swali, mishahara imeongezwa kwa asilimia ngapi?

Kama viongozi serikalini nao hawajui waseme waache kudanganya wafanyakazi kama watoto!!
Kama kipindi marehemu anaumwa mtu huyu alijitokeza na kudanganya wananchi kuwa haumwi yuko kazini mpaka kifo kilipowaumbua atashindwa nini kudanganya wafanyakazi kuhusu mishahara??? Sijawahi kumuamini huyu katelephone!! Aende akadanganye watoto wake, wafanyakazi ni wasomi na welewa kuliko yeye...SHAME!! asifanye tumwite MR. BIG LIER
Sasa aliekudanganya kuhusu mshahara humjui au unajitoa akili tu.

Fanya kazi acha kumtegemea mke apandishiwe mshahara ili ukakope kupitia mshahara wake.Ujanja ujanja tu
 
Magufuli awamu yake yote hakuwa kuboresha maslai ya wafanyakazi, Samia anastahili pongezi sana
Mama kajitahidi sana, japo hata Magufuli alijitahidi pia kwa maana mfumuko ulikua chini.

Mama tunaenda nae
 
Sasa aliekudanganya kuhusu mshahara humjui au unajitoa akili tu.

Fanya kazi acha kumtegemea mke apandishiwe mshahara ili ukakope kupitia mshahara wake.Ujanja ujanja tu
Tulia ww hujielewi utakuwa unaviela vyakikafara ndomana unabwabwaja ujinga
 
Kuna kitu sielewi, hii mishahara ya serikali ndio inayotumika sekta binafsi au? na vipi serikali inapanga mishahara ya sekta binafsi au uhusiano uko vipi kati ya serikali na mishahara ya sekta binafsi
Huelewi au akili huna? Serikali inapangaje mshahara sekta binafsi?
 
Kama una mshahara wa 700K maana yake, Nyongeza yako siyo pungufu ya Tsh 42,000 ( take home ) kwa mwezi ambayo Ni sawa na Tsh Laki 5+ kwa mwaka.
42 ni gross sio take home. Japo inatosha maana hakuna kazi wanafanya
 
Tatizo wameondoa increment...ambayo huwa inabusti sana salio mara dufu ya hilo ongezeko la elfu kumi na mbili..
Mbona hajazungumzia increments ambayo ipo kisheria na wameiondoa?
Kama serikali ambayo ndio mwajiri mkuu nchini inavunja Sheria wazi wazi na hawa waajiri wengine watafanyeje?
 
FY1mROKWQAQSpDs.jpg

Mhe. Waziri Mkuu amefafanua Vizuri Sana, Dhima ya Mhe Rais Samia Juu ya Sakata la nyongeza ya mshahara.

"78% YA WATUMISHI WAMEPOKEA NYONGEZA YA 23% YA MSHAHARA" Tukiwa bado katika kizungumkuti Juu ya Sakata la hivi karibuni kuhusu nyongeza ya mshahara kwa watumishi wa Umma, leo tarehe 29th mwezi July, Mhe Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania amefafanua wazi juu ya nyongeza hii ya asilimia 23%.

"Asilimia 75 - 78 ya watumishi wote wa Umma ndiyo wanaofaidika na hii asilimia 23 ya nyongeza ya mshahara, hata Mawaziri wetu na wao wanaongezewa asilimia 0.7" - Kassim Majaliwa - Waziri Mkuu

Waziri Mkuu ametoa ufafanuzi mzuri sana kuhusu mambo ya nyongeza ya 23.3% ya mishahara. Kama 78% ya wafanyakazi wote wamepata increment ya 23.3% then huyu anayelalamika ni nani?

"Ukiangalia mshahara kama wa Waziri wamepata 0.7%, sasa nani amepata hiyo ni yule mwenye kipato kikubwa, ujumbe wa msingi ni kwamba asilimia 23 iliyotamkwa haijalipa watu wote,"- Waziri Mkuu

"Hao wanaosema kwamba tumeongeza sh 20 ni wenye mishahara mikubwa, wako kwenye hii asilimia 22, huku ndiyo utawakuta Mawaziri, Makatibu Wakuu, Mameneja, Wakurugenzi na Wakuu wa mikoa ambao kidogo wana mshahara unaotosha,"- Waziri Mkuu

Hakika Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ana nia ya dhati, na wafanyakazi wote aliwaambia ataendelea kuboresha maslahi ya watumishi. Hivyo tuendelee kuumunga mkono.
 
Tatizo wameondoa increment...ambayo huwa inabusti sana salio mara dufu ya hilo ongezeko la elfu kumi na mbili..
Mbona hajazungumzia increments ambayo ipo kisheria na wameiondoa?
Kama serikali ambayo ndio mwajiri mkuu nchini inavunja Sheria wazi wazi na hawa waajiri wengine watafanyeje?
Increment kwa kiswahili ni ongezeko, au ulitaka kusemaje?
Uliajiriwa vipi ukiwa mweupe hivi?
 
Back
Top Bottom