Waziri Mkuu: Wanaolalama kupata ongezeko la 20,000 ni wale wenye mishahara mikubwa

Waziri Mkuu: Wanaolalama kupata ongezeko la 20,000 ni wale wenye mishahara mikubwa

Waziri Mkuu, Kasimu Majaliwa amesema wengi wanaolalamika kupata ongezeko dogo la mishahara ni wale ambao wana mishahara mikubwa. Ametolea mfano wa mawaziri kuwa wako baadhi ambao ongezeko lao ni 0.02%

Amewaomba watumishi kuwaamini viongozi wa vyama vya wafanyakazi. Amesema wengi waliopata ongezeko kubwa ni wale watumishi waliokuwa wanapata mishahara midogo.

Pia amesema wananchi wanapaswa kushukuru kwa ongezeko hilo ambalo miaka kadhaa iliyopita haikuwepo
Safi sana Serikali,shikilieni hapo hapo..Majitu yana mavitambi ya wizi eti yaongezewe salary..

Nadhani sasa mjadala umefungwa.
 
Kwa majibu kama haya inatosha kusema 2025 wasalimie Ruangwa. Majibu hayana mashiko kabisa na mbaya zaidi Hangaya aliamua kuwapa matarajio makubwa wafanyakazi.
Ni lini na wabunge watalalamika posho ndogo? Ikitokea hii kweli nitaona uzalendo umemkuta mkutwa.
 
tena yule ni bora kuliko huyu, yule alipunguza PAYE ambayo iliongeza mshahara kiasi cha kutosha, huyu anashauriwa vibaya na walamba asali kina mwigulu, huku danganya toto nyongeza ya shahara huku unaongeza mitozo kila pahala ili mradi tu kumkera mwananchi, ee Mungu eee tumekuachia baba! amua na huu ugomvi
Wewe ni kajinga,umepunguziwa Paye kwa 1%,umeongezwa salary,umefutiwa uharamia wa loanboard na bado ukapandishwa daraja ila bado unaongea upumbavu wako...

Tote hayo yamefanyika kwa mwaka Mmja Bado inaongea upumbavu.
 
"Asilimia 75 - 78 ya watumishi wote wa Umma ndiyo wanaofaidika na hii asilimia 23 ya nyongeza ya mshahara, hata Mawaziri wetu na wao wanaongezewa asilimia 0.7" - Kassim Majaliwa - Waziri Mkuu""

mkuuu hapo umetishaaaaa
 
Kwa majibu kama haya inatosha kusema 2025 wasalimie Ruangwa. Majibu hayana mashiko kabisa na mbaya zaidi Hangaya aliamua kuwapa matarajio makubwa wafanyakazi.
Ni lini na wabunge watalalamika posho ndogo? Ikitokea hii kweli nitaona uzalendo umemkuta mkutwa.
Wewe ndio unachagua Rais? Nenda Kwa wananchi kawambie msichague ccm kwa sababu haijawaongezea watumishi salary uone utakachojibiwa.
 
Naona waziri mkuu ameamua kumwaga Petrol kwenye moto unaowaka!
Ngoja moto umlipukie vizuri.
 
Isije ikawa wamekwisha malizana na tucta kwa sababu kauli ya mara ya mwisho kutoka serikalini walisema tucta wameenda kujadiliana... Sasa tucta kabla hawajasema tena kitu leo waziri mkuu amezungumza
Sasa tucta ndio watafanya nini? Hoja ya tucta ni hiyo hiyo kwamba kima Cha juu hawajaongesewa salary hivyo waliowaombea 15% ambayo serikali imekataa.
 
Leo usiku au kesho kutatengenezwa bonge la tukio Kama uteuzi,utenguaji etc ili tukio hili lifunikwe.

Wataalam wako jikoni wakitengeneza movie la kihindi,'steringi' lazima afie kwny shamba la maua.
Hakuna chochote, serikali imeshaweka msimamo.
 
Leo usiku au kesho kutatengenezwa bonge la tukio Kama uteuzi,utenguaji etc ili tukio hili lifunikwe.

Wataalam wako jikoni wakitengeneza movie la kihindi,'steringi' lazima afie kwny shamba la maua.
Hakuna chochote, serikali imeshaweka msimamo.
 
Pishi la pilau limempata Majaliwa......lazima litiwe sukari!😂😂

Asilimia 73% !? Labda ukijumlisha na wale wa majeshi!

Asante Mama, hata kwa hiki, ukubwa wa chungu wakijua weye mpishi.
 
Kweli hii ni Serikali ya kipekee duniani,Prime Minister anaongea kauli nyepesi kwa mambo mazito huku akipigiwa makofi na watu walionuna mioyo.
Hilo ongezeko ni la ajabu kweli.Japokuwa mimi siyo mwanahisabati lakini kutoa na kujumlisha hakunishindi kihivyo.Nimebahatika kuona pay slip moja hapa,Basic 1,820,000/= mwezi June&July Basic salary 1,865,000 na kwa hesabu ya kichwa ongezeko ni =Tshs 45,000;ambayo ni sawa 2.5% na kwenye take home July imeongezeka Tsh 26,000 hivi ambayo ni sawa na 62.4% ya 45,000 aliyoongezewa ikiwa makato ni 23.6%,je huyo mtu naye aishukuru serikali kwa nyongeza aliyoisubiri kwa miaka 5?
Hapo bado hajakutana na tozo za miamala,VAT ya 18% kwa kila manunuzi,kupanda kwa bei za bidhaa na huduma kwa karibia 60% miaka 5 iliyopita.Funga kazi ni pensheni ya mkupuo ya 33.3%.Wafanyakazi wa Tanzania ya Tanganyika asipokufa kwa njaa atakufa kwa stress.
Mambo mazitk kama yapi? Kauli nyepesi kama ipi?

Badikishana salary wewe WA kima Cha juu na chini Ili ufairi 23%
 
Increment kwa kiswahili ni ongezeko, au ulitaka kusemaje?
Uliajiriwa vipi ukiwa mweupe hivi?
We jamaa ni mtumishi w umma au unaongea tu tubishane hapa.
Kwenye utumishi wa umma Kuna kitu kinaitwa increments ambayo hata rais asipoongeza mshahara wafanyakazi wote wanapata na ndio inavusha mfanyakazi kutoka scale moja kwenda nyingine...
Hiyo ndio inafanya mtu anayeanza kazi leo awe tofauti na aliyeanza miaka mitatu...
Waliacha kuitekeleza toka wakati wa Magu...
Na ni pesa nono sana kulingana na mshahara wako watu wanakunja mpk laki huko.
Kwa hiyo inngepaswa hili ongezeko ndani yake iwepo na increment yaani increment+ongezeko haingekuwa elfu 12 hata kidogo.
Increment kwa kiswahili ni ongezeko, au ulitaka kusemaje?
Uliajiriwa vipi ukiwa mweupe hivi?
Increment ni ongezeko la mwaka ambalo mtumishi anapaewa kupata hata kama rais hajaongeza mishahara..
Na huwa inakuwa inaandikwa kwenye offer letter right from the beginning unapopata cheo Fulani.
Hii ndio inamfanya mfanyakazi anayeanza kazi leo atofautiane mshahara na yule alieanza miaka mitatu iliyopita.
Kwa hiyo ongezeko hili lilipawa kuwa ni increment+ ongezeko isingekiwa elfu 12 hata kidogo.
Tatizo wee si mtumishi wa umma hatutaelewana
 
View attachment 2308131
Mhe. Waziri Mkuu amefafanua Vizuri Sana, Dhima ya Mhe Rais Samia Juu ya Sakata la nyongeza ya mshahara.

"78% YA WATUMISHI WAMEPOKEA NYONGEZA YA 23% YA MSHAHARA" Tukiwa bado katika kizungumkuti Juu ya Sakata la hivi karibuni kuhusu nyongeza ya mshahara kwa watumishi wa Umma, leo tarehe 29th mwezi July, Mhe Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania amefafanua wazi juu ya nyongeza hii ya asilimia 23%.

"Asilimia 75 - 78 ya watumishi wote wa Umma ndiyo wanaofaidika na hii asilimia 23 ya nyongeza ya mshahara, hata Mawaziri wetu na wao wanaongezewa asilimia 0.7" - Kassim Majaliwa - Waziri Mkuu

Waziri Mkuu ametoa ufafanuzi mzuri sana kuhusu mambo ya nyongeza ya 23.3% ya mishahara. Kama 78% ya wafanyakazi wote wamepata increment ya 23.3% then huyu anayelalamika ni nani?

"Ukiangalia mshahara kama wa Waziri wamepata 0.7%, sasa nani amepata hiyo ni yule mwenye kipato kikubwa, ujumbe wa msingi ni kwamba asilimia 23 iliyotamkwa haijalipa watu wote,"- Waziri Mkuu

"Hao wanaosema kwamba tumeongeza sh 20 ni wenye mishahara mikubwa, wako kwenye hii asilimia 22, huku ndiyo utawakuta Mawaziri, Makatibu Wakuu, Mameneja, Wakurugenzi na Wakuu wa mikoa ambao kidogo wana mshahara unaotosha,"- Waziri Mkuu

Hakika Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ana nia ya dhati, na wafanyakazi wote aliwaambia ataendelea kuboresha maslahi ya watumishi. Hivyo tuendelee kuumunga mkono.
Mambo yanazidi kuwa "zig zag" kwa hiyo 78% ya watumishi walikuwa wanakula 300000 ( kima cha chini) maana ndo waliopewa 23%
 
Back
Top Bottom