Sheria hiyo haijatoa Mamlaka uyasemayo.
Mtumishi wa Umma anawajibishwa kwa Mujibu wa Standing order.
Na hakuna Mahali standing order imeelekeza kwamba Mtumishi wa Umma akikosea atawekwa Mahabusu.
Cha Kukusaidia TAMISEMI = Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa hivyo Basi Maelekezo ya Waziri Ni Sahihi kwa Wahusika Halisi.
Nadhani hata hujui sheria inayo mpa mamlaka RCs na Dcs kumweka mtu ndani.
"Standing Order" nadhani unaitamka lakini hujui inahusika na nini kwa mtumishi wa Umma. Elewa katika utumishi wa Umma kuna sheria zinazoongoza utumishi wa Umma. Na kuna miongozo ya haki za kiutumishi. Hivyo tofautisha "Standing Order" na Sheria za utumishi wa Umma.
Standing order inatoa muongozo wa haki za kiutumishi. Lakini Sheria za utumishi wa Umma na kanuni zake za mwaka 2002, Inaeleza sheria nzima, na taratibu zote za kimaadili, utendaji na hata maelekezo ya kanuni za adhabu.
Hivyo usisome tu Standing order ukadhani kila kitu kimeelezwa humo. Elewa kwanza "Standing Order ni nini na inatumika wakati gani?
Kisha elewa Sheria za utumishi wa Umma na kanuni zake ni zipi na zinatumika kwenye nini?
Kuna katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo imewaelezea RCs ni nani? Na kisha Kuna sheria ya usalama, soma ujue Rcs na DCs wamepewa majukumu gani? Na utambue kuwa katika utumishi kuna utumishi wa kisiasa na utumishi wa kawaida. Je watumishi wa kisiasa wanaongozwa na sheria ipi katika uwajibishwaji wao!
Kuhusu kumwajibisha mtumishi wa umma umwajibishi kwa Standing Order bali unamwajibisha kwa Sheria za utumishi wa Umma na kanuni zake za mwaka 2002, ambayo inaeleza taratibu zote za uajibishwaji, na kutoa kanuni zake.
Unapongelea TAMISEMI naelewa kirefu chake. Ila ujue kuna miundo ya kiutumishi. Kimuundo katika utumishi maafisa wote wa Mkoani wanawajibika Wizara ya Utumishi. Nakupa mfano. Hospitali ya wilaya watumishi wake na Mganga Mkuu wa wilaya wanawajibika kwa Mkurugenzi wa halmashauri.
Lakini Mganga Mkuu wa mkoa, na manesi au wauguzi wanawajibika kwa RAS. Hata uhamisho wao wanapitishiwa kwa RAS na utumishi. Wakati Wilayani ni Mkurungezi kwa RAS na TAMISEMI.
Hiyvo Tawala za mikoa zipo ndani ya Tamisemi kwakua zinasimamia Serikali za mitaa. Lakini kimuundo wa Utumishi haziko Tamisemi moja kwa moja. Bali zinakuwa chini ya Wizara ya Utumishi. Hata wanapopandishwa vyeo inatoka moja kwa moja Utumishi. Tamisemi upokea tu nakala. RAS, ASS, Wataalamu wote mkoani, DAS, Afisa Tawala hawa wote wanakuwa chini ya Wizara ya Utumishi ndiko wanako wajibika kimuundo na si TAMISEMI.