Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Kesho utasikia, Dodoma, Mbeya Arusha wagonjwa kibao

Tuombe huu ugonjwa usifike mikoa ya baridi kama Iringa, Rukwa, Mbeya, Arusha Knjaro na etc.

Watu watapukika hasa ndugu zetu wanaumwa tayari.
 
Kwa taarifa hii ya leo iliyotolewa na waziri wa afya na maelezo yake kwamba sasa tunaambukizana sisi kwa sisi, na pia kwa kuona Dar ndo ina wagonjwa wengi, naomba kutoa maoni kwamba, safari za mabasi kutoka Dar na kuingia Dar zisimamishwe.

Kwa wastani kuna mabasi 200 yanayotoka Dar na kuingia Dar kwa siku. Ni mabasi yenye safari za zaidi ya masaa siyo chini ya 3 na mengine huchukuwa masaa zaidi ya 16. Kwa tabia ya ugonjwa wa Corona na maabukizi yake, ni rahisi mgonjwa mmoja kuambukiza zaidi ya nusu ya abiria ndani ya basi moja. Vituo vya mabasi havina ukaguzi wa wagonjwa na mazingira ya ndani ya mabasi huwa ni magumu sana.

Tupeane maoni na tusikilizane kwamba pamoja na shughuli zetu kuendelea, serikali tusidieni kwa kuzuia safari za mabasi ya mikoni ili kuinusuru nchi.
Dar ni kitovu cha korona
 
Sasa wakizuia mabasi ina maana korona itabidi itumie bombadia kufika huko
 
Tunakuomba mungu tusaidie katika hili kwani
Bila wewe siye ni bure tu
Tukinge na tuponyeshe
AMEEN
 
Waziri wa afya Mh. Ummy muda huu anazungumza na viongozi mbalimbali wa dini juu ya mikakati ya kudhibiti Corona.

--
ALIYOZUNGUMZA WAZIRI UMMY MWALIMU (KWA UFUPI)

Viongozi wa dini mnayo nafasi ya kipekee kutoa taarifa sahihi, kwa weledi na uwazi, hivyo kupunguza uwepo wa taarifa zisizo za kweli zinazoweza kupelekea hofu, unyanyapaa na mashaka miongoni mwa wananchi.

Tunaomba pia ibada ifanyike muda mfupi, pia wekeni utaratibu wa kupunguza msongamano wa waumini wakati wa kuingia na kutoka katika nyumba za ibada.

Nimpongeza mkuu wa mkoa wa Pwani (Everist Ndikilo) kwa kuzuia kongamano la dini lililopangwa kufanywa na madhehebu ya kidini na kuhusishwa watu 3,000 wanaotoka nchi nzima.

Ugonjwa tumeletewa kutoka nje, hivi sasa takwimu za jana, juzi na wiki iliyopita tumeanza kuambukizana wenyewe kwa wenyewe. Ili viongozi wangu wa dini naomba niliweke wazi its no longer imported cases, tumeanza local transmission.

Ndani ya siku chache tutaingia katika community transmission. Maana yake tutapata mgonjwa ambaye hajui ugonjwa ameupata wapi? Sasa hivi amekuja mtu anamuambikiza fulani ndio maana tunafanya contact (muingiliano) kujua.

Lazima niwaambia ukweli nisiwafiche soon (karibuni), tutaingia kwenye community transmission. Bado tunatakiwa kuchukua tahadhari na kuongeza juhudi za kukabiliana na ugonjwa huu

Rais amesema hatuwezi kufunga kazi, kazi lazima tufanye lakini tuweze kudumisha kutokaribiana baina yetu. Hata Baba Askofu unaweza kufanya 'Video Conference' ukiwa na jambo na waumini

Tafiti zinaonesha virusi vya corona pia vinaambukizwa kwa njia ya hewa hivyo baada siku chache Serikali itatoa mwongozo ikiwa ni pamoja na kumtaka kila mtu anapotoka nyumbani awe amevaa barakoa ili kupunguza kasi ya mambukizi.

Mwanzoni kulikuwa na hisia kwamba Afrika hatuwezi kuumwa ugonjwa huu lakini leo kwa mujibu wa takwimu za Africa CDC, tuna wagonjwa takribani 10,000 na vifo vimefikia takribani 500

WHO ilitukadiria kufikia katikati ya Aprili tutakuwa na wagojwa 1000 nchini na katikati ya Mei tutakuwa na wagonjwa 10,000, kufikia sasa tumeruka kiunzi hicho kwa sababu hatuna wagonjwa wengi tunapaswa kumshukuru Mungu

Tunashauri wananchi tujiulize, je ni lazima tusafiri kutoka mijini kwenda vijijini wakati huu wa maambukizi ya corona? Tutafakari tusije tukawapelekea wazee wetu, wazazi wetu, na walezi wetu hivi virusi vya corona.
Wale wazungu kule waliosema Mwezi huu lile janga lao litahamia kwetu walikua na maana gani?
Na tusipolipata hilo Janga kama walivyotabiri, hawawezi kulazimisha hata kwa kutuletea wao kwa njia zao ili ionekane kua hawakukosea kqwenye utabiri wao??
 
Kwa taarifa hii ya leo iliyotolewa na waziri wa afya na maelezo yake kwamba sasa tunaambukizana sisi kwa sisi, na pia kwa kuona Dar ndo ina wagonjwa wengi, naomba kutoa maoni kwamba, safari za mabasi kutoka Dar na kuingia Dar zisimamishwe.

Kwa wastani kuna mabasi 200 yanayotoka Dar na kuingia Dar kwa siku. Ni mabasi yenye safari za zaidi ya masaa siyo chini ya 3 na mengine huchukuwa masaa zaidi ya 16. Kwa tabia ya ugonjwa wa Corona na maabukizi yake, ni rahisi mgonjwa mmoja kuambukiza zaidi ya nusu ya abiria ndani ya basi moja. Vituo vya mabasi havina ukaguzi wa wagonjwa na mazingira ya ndani ya mabasi huwa ni magumu sana.

Tupeane maoni na tusikilizane kwamba pamoja na shughuli zetu kuendelea, serikali tusidieni kwa kuzuia safari za mabasi ya mikoni ili kuinusuru nchi.

Subirini kwanza ufike mikoani ndiyo serikali itazuia watu kusafiri, tumemuachia Mungu kila kitu kitakaa sawa!
 
Vyovyote itakavyokua ila mm najua sikujiumba! Yupo alieniumba na ananijali. Atanipigania kwa kila hali mbaya itakayonikumba

Usisahau wakati mwingine anaweza kukutumia kama Mfano na akakuacha ukateketea Mkuu ,hakikisha una zingatia Ushauri wa Wataalam wa Afya kuhusu Ugonjwa huu mmbaya.
 
Piga kazi broo ulipe kod tujenge SGR na stiglers
Other ways hakuna wakukujali nchi hii
 
Tuchukue tahadhari kama wataalam wanavyoelekeza lakini Mungu ibaraki Tanzania
 
Tatizo kubwa la kwanza hakuna uwezo wa kuwa na test kits za kupima angalau watu 20,000 kwa siku.
Ukiweza kupima watu wengi kwa muda mfupi na kupata majibu sahihi inakuwa rahisi kuchagua mfumo wa lockdown au partial lockdown au vinginevyo.
Sijui ni unyonge wetu unaochangia sana kutoa maamuzi magumu ya kuruhusu watu waendelee na shughuli zao kana kwamba tumegeuka Sweden na Korea kusini.Sweden na Korea wanapima,wana mitambo,matajiri,na wamekubuu kwenye tekinologia.
Njia nyepesi ni lockdown ikiambatana na social distancing.
Nawashangaa Magufuli na Makonda wanapofanya maamuzi magumu bila kupima watu wengi kama 20000 kwa siku.
Tuache Bahati na sibu,ni wakati wa ukweli na uwazi katika sayansi na tekinologia ili kuokoa watu wengi.
 
Mipaka haijafungwa ndo Safari za ndani zisitishwe? Tupige kazi huku tukinawa mikono mara kwa mara, kwanza korona ni kaugonjwa kadogo tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni bora hata mipaka kutofungwa. Mabasi ya safari ndefu ni kama chumba cha hewa chafu.
Ukisafiri kwa basi toka Dar kwenda Arusha, mfano, ni kama una masaa 10 ya kuvuta hewa za watu 50 ndani ya basi. Huyu anakoroma kwa uchovu, yule anapiga chafya, yule anakohoa na kurusha basi zima, mwingine analazimisha mazungumzo nawe, yule anapiga kelele kwa mazungumzo na simu, nk. Ni kama uko msitu wa kubadilishana hewa chafu tu!

Leo nimeona taarifa ambayo sijaiamini, kwamba Waziri mkuu anasema shule mikoani zifunguliwe tar. 17. Kama ni kweli basi tuna tatizo la kimsingi. Kwa nini ufungue mikoani na kuzuia Dar, wakati mabasi yanakwenda mikoani kila siku kwa wingi kiasi hicho? Ni aibu tu!
 
Kuna haja ya kuimarisha usalama mikoa ya mipakani yaani hasa wilaya za mipakani kunauingiliano mkubwa sana wa watu. Kule kyela mto songwe watu wanavuka tuu free sawa na tunduma . Kuna haja ya kujifunza toka nchi tajiri kwann ugonjwa huu unawatesa pamoja na utajiri wao wameshindwa kudhibiti.
 
Tunaiomba serikali tu isiruhusu mfumo wa 5G nchini na vipimo feki vya COVID-19 vibavyotoa majibu fake na kupaisha maambukizi na hivyo kuongeza hofu kwa wananchi.Mfumo wa 5G unaotumia mm waves unashusha kinga sana na kuzuia damu kubeba hewa safi ya kutosha na hivyo kusababisha vifo vingi!Lakini tukumbuke pia kwamba hofu nayo inaua.

Tunaiomba pia serikali iwe makini na test kits zinazotumika kupimia COVID-19,are they really up to the job?Isije ikawa na zenyewe ni sehemu ya tatizo in one way or the other.Zipo test kits ambazo zimekuwa proved kuwa na corona,how can that be?Simuamini Bill Gates kabisa,he can do anything ili ahalalishe vaccine zake,he is so evil.
 
Back
Top Bottom