Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Ukizingatia Ijumaa ya leo kuna ibada mbili zikusanyazo idadi kubwa ya waumini...

Ibada ya Ijumaa kuu...

Ibada ya kila Ijumaa kwa waumini wa kiislaam...



Cc: mahondaw
 
Hii nchi hii?unazuia msongamano kwa kufunga shule then makanisa yanaendelea tu,umy mbona mnacheza na afya za watanzania?
 
Enewei bado tuna muda kidogo, kama lockdown ya nchi nzima itasababisha tatizo kubwa kuliko tatizo la ugonjwa wenyewe, basi ifanyike lockdown ya mkoa kwa mkoa, kusiwe na muingiliano wa watu kutoka mko mmoja kwenda mwingine ili wananchi waendelee shughuli zao za kila siku huku wakichukua tahadhari zilizotolewa na mamlaka husika. Tuwena huruma ya kibinadamu angalau kwa wale wenye matatizo mengine ya afya pamoja na wazee wetu. Be humble, don't be the source of harm and don't harm your fellow human being 🙏🏽
 
Hawa kuna kitu wanatuficha hasa kwenye takwimu za walioambukizwa huu ugonjwa nchini. Ngoja ngoma isambae watafichua wenyewe.
Waziri ameeleza kile anachokijua.....
ww kama kuna jambo unaona limefichwa fichua
 
Waziri wa afya Mh. Ummy muda huu anazungumza na viongozi mbalimbali wa dini juu ya mikakati ya kudhibiti Corona.

--
ALIYOZUNGUMZA WAZIRI UMMY MWALIMU (KWA UFUPI)

Viongozi wa dini mnayo nafasi ya kipekee kutoa taarifa sahihi, kwa weledi na uwazi, hivyo kupunguza uwepo wa taarifa zisizo za kweli zinazoweza kupelekea hofu, unyanyapaa na mashaka miongoni mwa wananchi.

Tunaomba pia ibada ifanyike muda mfupi, pia wekeni utaratibu wa kupunguza msongamano wa waumini wakati wa kuingia na kutoka katika nyumba za ibada.

Nimpongeza mkuu wa mkoa wa Pwani (Everist Ndikilo) kwa kuzuia kongamano la dini lililopangwa kufanywa na madhehebu ya kidini na kuhusishwa watu 3,000 wanaotoka nchi nzima.

Ugonjwa tumeletewa kutoka nje, hivi sasa takwimu za jana, juzi na wiki iliyopita tumeanza kuambukizana wenyewe kwa wenyewe. Ili viongozi wangu wa dini naomba niliweke wazi its no longer imported cases, tumeanza local transmission.

Ndani ya siku chache tutaingia katika community transmission. Maana yake tutapata mgonjwa ambaye hajui ugonjwa ameupata wapi? Sasa hivi amekuja mtu anamuambikiza fulani ndio maana tunafanya contact (muingiliano) kujua.

Lazima niwaambia ukweli nisiwafiche soon (karibuni), tutaingia kwenye community transmission. Bado tunatakiwa kuchukua tahadhari na kuongeza juhudi za kukabiliana na ugonjwa huu

Rais amesema hatuwezi kufunga kazi, kazi lazima tufanye lakini tuweze kudumisha kutokaribiana baina yetu. Hata Baba Askofu unaweza kufanya 'Video Conference' ukiwa na jambo na waumini

Tafiti zinaonesha virusi vya corona pia vinaambukizwa kwa njia ya hewa hivyo baada siku chache Serikali itatoa mwongozo ikiwa ni pamoja na kumtaka kila mtu anapotoka nyumbani awe amevaa barakoa ili kupunguza kasi ya mambukizi.

Mwanzoni kulikuwa na hisia kwamba Afrika hatuwezi kuumwa ugonjwa huu lakini leo kwa mujibu wa takwimu za Africa CDC, tuna wagonjwa takribani 10,000 na vifo vimefikia takribani 500

WHO ilitukadiria kufikia katikati ya Aprili tutakuwa na wagojwa 1000 nchini na katikati ya Mei tutakuwa na wagonjwa 10,000, kufikia sasa tumeruka kiunzi hicho kwa sababu hatuna wagonjwa wengi tunapaswa kumshukuru Mungu

Tunashauri wananchi tujiulize, je ni lazima tusafiri kutoka mijini kwenda vijijini wakati huu wa maambukizi ya corona? Tutafakari tusije tukawapelekea wazee wetu, wazazi wetu, na walezi wetu hivi virusi vya corona.

Kwamba rais kasema hakuna kufunga kazi na Ummy kakubali. Sasa wanalia lia nini?

Nini hawakuambiwa?

Kwa nini Ummy hakumwachia rais uwaziri wake kama ni shinikizo lake kuwa kazi zisisimame hata kama sote tufe?

Nani anayeongoza hii vita ambaye:

1. Kashindwa kuwa wa msaada ugonjwa usiingie.
2. Kashindwa pia kuudhibiti ugonjwa isisambae.

Anayo mawazo ya kuuzuia usisambae au yupo yupo tu kamwachia Mungu?

Muda wa kupata majibu ni sasa.
 
Kwa kauli hizi watanzania tujiandae kisaikolojia chochote chaweza tokea, na tusubiri hizo siku chache zijazo tamko gani laja sanjari na uvaaji wa barakoa pindi watu watokapo majumbani
 
Kadri hizi habari zinavotoka naanza kuziona dalili mbaya najiona kabisa muda mfupi ujao nabeba kila kilicho cha muhimu narudi zangu kijijini hadi pale hill janga litakapokuwa limepita. Allah tuepushe
Unataka kuwapelekea korona kijijini acha hizo
 
Ukitaka kujua kama wanaficha au wanasema ukweli, ebu fanya kautafiti kadogo mtaani kwako. Wameugua wangapi hapo? Wamekufa wangapi hapo? Kama hawapo mtaani kwako wa mtaa wa nani? Ufipa?
Huu ujinga ndio mnaoutegemea kuwalaza akili watu.

Hebu eleza kama Tanzania nzima wakifa watu mia mbili kwa siku, kutokana na sababu yoyote ile, kama utajua hapo ulipo kuwa hao watu wamefariki siku hiyo?

Hata serikali yenyewe haina takwimu hizo!

Na huo ndio usingizi wa pono unaokulaza wewe.
 
Kwa tangazo la waziri jana.. kuna ulazima wa dar kufungwa.

Watu wasitoke na wala mtu asiingie kama wachina walivyo fanya wuhan.


Pia viongizi wote wanatakiwa kupimwa corona mapema wabunge, mawaziri, etc.


Madaktari wote na wahudumu wa afya wanatakiwa kupimwa kila siku.


Wengi wanaona dalili sio nzuri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom