Waziri wa Ardhi azuia mchakato wa kutaka kubomoa nyumba zaidi ya 100 zilizopo Mapinga

Waziri wa Ardhi azuia mchakato wa kutaka kubomoa nyumba zaidi ya 100 zilizopo Mapinga

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Baada ya Mdau kuelezea kuhusu mchakato wa kubomoa nyumba zaidi ya 100 zilizopo Mapinga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani, Serikali imechukua hatua ya kusitisha mchakato huo, malalamiko ya awali soma hapa ~ Nyumba zaidi ya 400 za Mapinga (Bagamoyo) kuwekewa X ili zivunjwe kuna harufu yenye shaka, Waziri Silaa fuatilia kinachoendelea

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa ameingilia kati mgogoro wa ardhi uliozua taharuki katika eneo la Mapinga wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani kati ya wananchi zaidi ya 100 na mtu mmoja ambaye aliyejulikana kwa majina ya Sevestine Mtunga ambaye anadai kumiliki eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 12 baada ya Mahakama kuwataka wananchi hao kuondoka eneo hilo.

Waziri Silaa ameelekeza zoezi hilo lisimame kwanza na kumuomba mwakilishi wa Sevestin Mtunga ampe muda ili Serikali iweze kulifanyia kazi swala hilo na kuondoa taharuki kwa wananchi kama maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kumwelekeza mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bi Halima Okash kukutana na pande zote kuanzia Jumanne 18 Juni 2024.
 
Kisheria hii imekaaje? Watu wamevamia, wamepelekwa mahakamani na wameshindwa, waziri anakuja kusitisha how?
Ni kituko cha karne amri ya mahakama inazuiliwa mahakamani huko huko. Sio kwa kauli ya waziri. Amri ya mahakama ni lazima itekelezwe na iheshimiwe hata kama ni chungu

Huyu waziri kwa kuingilia na kujaribu kuzuia amri ya mahakama apigwe cotempt of court. Anakuwa kama hajui utawala wa sheria
 
Ni kituko cha karne amri ya mahakama inazuiliwa mahakamani huko huko. Sio kwa kauli ya waziri. Amri ya mahakama ni lazima itekelezwe na iheshimiwe hata kama ni chungu
Unajuwa nazo Mahakama zetu chini ya Jaji Mkuu Prof Ibrahim Juma ziko CORRUPT.

Naamini ni nguvu ya fedha ndiyo imetembea hadi kufikia maamuzi hayo.

Mahakama palikuwa ni mahali pa haki enzi za Nyerere hadi Mkapa kwa kiasi kikubwa. Wakati wa JK kidogo tu ziliyumba.

Lakini alipokuja Mwendazake Mahakama ziligeuka kuwa "kangaroo courts"

Ngoja tutulie tusikie nini kitajiri
 
Ni kituko cha karne amri ya mahakama inazuiliwa mahakamani huko huko. Sio kwa kauli ya waziri. Amri ya mahakama ni lazima itekelezwe na iheshimiwe hata kama ni chungu

Huyu waziri kwa kuingilia na kujaribu kuzuia amri ya mahakama apigwe cotempt of court. Anakuwa kama hajui utawala wa sheria
Mahakama na Serikali hii ni mtu na Dada yake,ndio Maana Serikali ikitaka kuminya Haki za watu,wanapeleka vimemo mahakamani,umeteuliwa na RAIS,unawezaje kumpinga wakati chama kimoja kimeshika hatamu?
 
Watu tunaweza Ku comment kirahisi sana kwa kuwa hatuko kwenye position ya hao watu 100 ambao familia zao zitakosa makazi. Siamini kama hao watu kila mtu alijijia tu akajenga. Ni lazima waliuziwa. May be na matapeli kama ni kweli kiwanja cha huyo alieshinda kesi.
Kibinadamu tu, unawezaje kumbomolea mwenzio nyumba iliyomgharimu mamilioni tena usikute ya mkopo kisa ardhi mali yako. Nafikiri ni vyema serikali ingekaa na pande zote ili waone kila upande unanufaikaje.

Kiukweli Mimi sina hiyo nyumba ila nafeel maumivu wanayopitia hawa watu. Dunia tunapita. Imenikumbusha kipindi watu wanabomolewa kwa kuvamia eneo la yule mama mchungaji, aisee kuna baba anatoka job anakuta vyombo na familia wako nje, nyumba ishaanguka, alianguka na kupoteza fahamu, kuja kuzinduka ni machozi. Mwanaume kulia si jambo dogo. Leo hii mama mchungaji yuko ndani ya ardhi, ardhi na vilivyoko juu yake kaviacha. Kweli ilikuwa ni mali yake, ila asingepungukiwa kuwaachia wale maskini kisehemu tu katika eneo kubwa alilonalo, mbaya zaidi wao walitapeliwa na walikuwa tayari kumlipa vile viwanja.
 
Ni kituko cha karne amri ya mahakama inazuiliwa mahakamani huko huko. Sio kwa kauli ya waziri. Amri ya mahakama ni lazima itekelezwe na iheshimiwe hata kama ni chungu

Huyu waziri kwa kuingilia na kujaribu kuzuia amri ya mahakama apigwe cotempt of court. Anakuwa kama hajui utawala wa sheria
Na waziri mwenyewe ni mwanasheria wa mahakama!
 
Baada ya Mdau kuelezea kuhusu mchakato wa kubomoa nyumba zaidi ya 100 zilizopo Mapinga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani, Serikali imechukua hatua ya kusitisha mchakato huo, malalamiko ya awali soma hapa ~ Nyumba zaidi ya 400 za Mapinga (Bagamoyo) kuwekewa X ili zivunjwe kuna harufu yenye shaka, Waziri Silaa fuatilia kinachoendelea

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa ameingilia kati mgogoro wa ardhi uliozua taharuki katika eneo la Mapinga wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani kati ya wananchi zaidi ya 100 na mtu mmoja ambaye aliyejulikana kwa majina ya Sevestine Mtunga ambaye anadai kumiliki eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 12 baada ya Mahakama kuwataka wananchi hao kuondoka eneo hilo.

Waziri Silaa ameelekeza zoezi hilo lisimame kwanza na kumuomba mwakilishi wa Sevestin Mtunga ampe muda ili Serikali iweze kulifanyia kazi swala hilo na kuondoa taharuki kwa wananchi kama maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kumwelekeza mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bi Halima Okash kukutana na pande zote kuanzia Jumanne 18 Juni 2024.
Mahakama naona kama imepinduliwa vile.
 
Swali zuri sana. Wataalam wa sheria watujuze.
Allen Kilewella
Tatizo hakuna mwenye miliki ya Ardhi Tanzania/Tanganyika. Ardhi ni mali ya watanzania wote na Rais ndiye mtunzaji (Custodian) wake.

Maana yake ni kwamba sisi wote ni wapangaji. Mwenye Ardhi humteua Waziri afanye kazi kwa niaba yake.

Chini ya waziri kuna kamishina wa Ardhi ambaye kwa niaba ya Rais ana uwezo wa kutengua upangaji wa mtu.

Kwa ivo kushinda kwako kesi mahakamani hakuzuii Waziri mwenye dhamana ya Ardhi kumpangisha mtu mwingine kwenye Ardhi unayoitumia.

Mahakama haizuii mamlaka ya waziri kupangisha (allocate) Ardhi yoyote ile toka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
 
Tatizo hakuna mwenye miliki ya Ardhi Tanzania/Tanganyika. Ardhi ni mali ya watanzania wote na Rais ndiye mtunzaji (Custodian) wake.

Maana yake ni kwamba sisi wote ni wapangaji. Mwenye Ardhi humteua Waziri afanye kazi kwa niaba yake.

Chini ya waziri kuna kamishina wa Ardhi ambaye kwa niaba ya Rais ana uwezo wa kutengua upangaji wa mtu.

Kwa ivo kushinda kwako kesi mahakamani hakuzuii Waziri mwenye dhamana ya Ardhi kumpangisha mtu mwingine kwenye Ardhi unayoitumia.

Mahakama haizuii mamlaka ya waziri kupangisha (allocate) Ardhi yoyote ile toka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Asante kwa ufafanuzi mzuri.
 
Watu tunaweza Ku comment kirahisi sana kwa kuwa hatuko kwenye position ya hao watu 100 ambao familia zao zitakosa makazi. Siamini kama hao watu kila mtu alijijia tu akajenga. Ni lazima waliuziwa. May be na matapeli kama ni kweli kiwanja cha huyo alieshinda kesi.
Kibinadamu tu, unawezaje kumbomolea mwenzio nyumba iliyomgharimu mamilioni tena usikute ya mkopo kisa ardhi mali yako. Nafikiri ni vyema serikali ingekaa na pande zote ili waone kila upande unanufaikaje.

Kiukweli Mimi sina hiyo nyumba ila nafeel maumivu wanayopitia hawa watu. Dunia tunapita. Imenikumbusha kipindi watu wanabomolewa kwa kuvamia eneo la yule mama mchungaji, aisee kuna baba anatoka job anakuta vyombo na familia wako nje, nyumba ishaanguka, alianguka na kupoteza fahamu, kuja kuzinduka ni machozi. Mwanaume kulia si jambo dogo. Leo hii mama mchungaji yuko ndani ya ardhi, ardhi na vilivyoko juu yake kaviacha. Kweli ilikuwa ni mali yake, ila asingepungukiwa kuwaachia wale maskini kisehemu tu katika eneo kubwa alilonalo, mbaya zaidi wao walitapeliwa na walikuwa tayari kumlipa vile viwanja.
Mkuu mara nyingi hao unaowahurumia ndo hodari wa kujibu hovyo na vitisho. Watu wengi hawapendi kufuata utaratibu wakati wa kununua ardhi. Wengi hupenda shortcut. Nina baba yangu mdogo alivamia eneo langu na kutaka kunipora eka 2 LIVE. Ilikuwa hatari. Sema kwa upande mwingine serikali ikaze uzi kwa watu wenye maeneo makubwa ila hawayaendelezi.
 
Katiba inasema ardhi ni mali ya serikali, mwananchi ni mpangaji tu, waziri ndiye mwenye dhamana ya ardhi, hapo unaonaje? Ahakikishe kuwa hapakuwa na hata chembe ya rushwa.
It's not true.

The Correct Provision is:

"All land in Tanzania is a public land and vested to the President as the Trustee on behalf of all citizens."

Kwa hiyo, SIYO KWELI kwamba ardhi yote ya Tanzania ni Mali ya Rais au Mali ya Serikali.
Ardhi ya Tanzania ni Mali ya Raia wote wa nchi hii ( Mali ya umma), Rais ni kama Mdhamini tu kwa niaba ya Wananchi wote.
 
Back
Top Bottom