Waziri wa Ardhi azuia mchakato wa kutaka kubomoa nyumba zaidi ya 100 zilizopo Mapinga

Waziri wa Ardhi azuia mchakato wa kutaka kubomoa nyumba zaidi ya 100 zilizopo Mapinga

Unajuwa nazo Mahakama zetu chini ya Jaji Mkuu Prof Ibrahim Juma ziko CORRUPT.

Naamini ni nguvu ya fedha ndiyo imetembea hadi kufikia maamuzi hayo.

Mahakama palikuwa ni mahali pa haki enzi za Nyerere hadi Mkapa kwa kiasi kikubwa. Wakati wa JK kidogo tu ziliyumba.

Lakini alipokuja Mwendazake Mahakama ziligeuka kuwa "kangaroo courts"

Ngoja tutulie tusikie nini kitajiri
Oops !! Hili Bhalaa Kubwa Sana Sana
 
It's not true.

The Correct Provision is:

"All land in Tanzania is a public land and vested to the President as the Trustee on behalf of all citizens."

Kwa hiyo, SIYO KWELI kwamba ardhi yote ya Tanzania ni Mali ya Rais au Mali ya Serikali.
Ardhi ya Tanzania ni Mali ya Raia wote wa nchi hii ( Mali ya imma), Rais ni kama Mdhamini tu kwa niaba ya Wananchi wote.
Mamlaka ya Rais kwenye Ardhi yakoje!?
 
Chini ya waziri kuna kamishina wa Ardhi ambaye kwa niaba ya Rais ana uwezo wa kutengua upangaji wa mtu.

Kwa ivo kushinda kwako kesi mahakamani hakuzuii Waziri mwenye dhamana ya Ardhi kumpangisha mtu mwingine kwenye Ardhi unayoitumia.

Mahakama haizuii mamlaka ya waziri kupangisha (allocate) Ardhi yoyote ile toka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.


Kunapokuwa Kuna Hukumu ya Mahakama, Mamlaka ya Waziri wa Ardhi au Kamishina wa Ardhi yanakoma katika kupangisha au kugawa au kumilikisha Ardhi hiyo kwa mtu mwingine yoyote tofauti na yule aliyeshinda Kesi (Decree Holder), unless kuwe na Makubaliano maalumu Kati ya Decree Holder na Watu hao wengine.
 
Kunapokuwa Kuna Hukumu ya Mahakama, Mamlaka ya Waziri wa Ardhi au Kamishina wa Ardhi yanakoma katika kupangisha au kugawa au kumilikisha Ardhi hiyo kwa mtu mwingine yoyote tofauti na yule aliyeshinda Kesi (Decree Holder), unless kuwe na Makubaliano maalumu Kati ya Decree Holder na Watu hao wengine.
Kwanza Kwa kesi hii Waziri hajaingilia maamuzi ya Mahakama.

Pili kisheria mahakama ilikuwa inajadili nani ni mpangaji halali wa Ardhi yenye utata na mahakama haikujadili kama Waziri anayo mamlaka ya kufanya "Reallocation" kwenye Ardhi yenye utata au lah!!??
 
Kwanza Kwa kesi hii Waziri hajaingilia maamuzi ya Mahakama.
Endapo kama Waziri huyo hajasitisha zoezi la utekelezaji wa hukumu ya Mahakama (yaani hajasitisha ubomoaji wa Nyumba za Judgement Debtors wote) au Kama amekata Rufaa kupinga hukumu hiyo, basi atakuwa hajaingilia Maamuzi ya Mahakama. Lakini endapo kama ametoa maagizo kwamba zoezi la ubomoaji wa Nyumba za Judgment Debtors lisitishwe kwanza, basi atakuwa ameingilia Maamuzi ya Mahakama.
 
Endapo kama Waziri huyo hajasitisha zoezi la utekelezaji wa hukumu ya Mahakama (yaani kusitisha ubomoaji wa Nyumba za Judgement Debtors wote) au Kama amekata Rufaa kupinga hukumu hiyo, basi atakuwa hajaingilia Maamuzi ya Mahakama. Lakini endapo kama ametoa maagizo kwamba zoezi la ubomoaji wa Nyumba za Judgment Debtors lisitishwe kwanza, basi atakuwa ameingilia Maamuzi ya Mahakama.
Nadhani kasitisha Kwa muda. Siyo maamuzi ya mahakama bali jinsi ya utekelezaji wa maamuzi hayo ya mahakama.
 
Nadhani kasitisha Kwa muda. Siyo maamuzi ya mahakama bali jinsi ya utekelezaji wa maamuzi hayo ya mahakama.
Hata kusitisha kwa muda kwa utekelezaji wa hukumu ya Mahakama, Waziri huyo anapaswa aende kufungua Maombi/Kesi ndogo Mahakamani (Stay Execution) ili kuzuia utekelezaji wa hukumu hiyo. Kutoa maagizo yoyote Yale ya kusitisha kwa muda utekelezaji wa hiyo Hukumu ya Mahakama bila ya kufungua Kesi ndogo au bila ya kukata rufaa, inahesabika ni kuingilia Maamuzi ya Mahakama
 
Watu tunaweza Ku comment kirahisi sana kwa kuwa hatuko kwenye position ya hao watu 100 ambao familia zao zitakosa makazi. Siamini kama hao watu kila mtu alijijia tu akajenga. Ni lazima waliuziwa. May be na matapeli kama ni kweli kiwanja cha huyo alieshinda kesi.
Kibinadamu tu, unawezaje kumbomolea mwenzio nyumba iliyomgharimu mamilioni tena usikute ya mkopo kisa ardhi mali yako. Nafikiri ni vyema serikali ingekaa na pande zote ili waone kila upande unanufaikaje.

Kiukweli Mimi sina hiyo nyumba ila nafeel maumivu wanayopitia hawa watu. Dunia tunapita. Imenikumbusha kipindi watu wanabomolewa kwa kuvamia eneo la yule mama mchungaji, aisee kuna baba anatoka job anakuta vyombo na familia wako nje, nyumba ishaanguka, alianguka na kupoteza fahamu, kuja kuzinduka ni machozi. Mwanaume kulia si jambo dogo. Leo hii mama mchungaji yuko ndani ya ardhi, ardhi na vilivyoko juu yake kaviacha. Kweli ilikuwa ni mali yake, ila asingepungukiwa kuwaachia wale maskini kisehemu tu katika eneo kubwa alilonalo, mbaya zaidi wao walitapeliwa na walikuwa tayari kumlipa vile viwanja.
Na chanzo cha yote haya ni ccm kupitia viongozi wao wa serikali za mitaa!! Kwa imeshakuwa kama sheria kuwa kila ardhi isyopimwa ikiuzwa lazima wapate chao!! Likitokea la kutokea wanakimbia!! Hapo mala nyingi ni busara zaidi ndio hutumika, watu wana miaka 15,hapo na kuna nyumba zaidi ya mia, muda wote huo mlikuwa wapi walipokuwa wakijenga??
 
Baada ya Mdau kuelezea kuhusu mchakato wa kubomoa nyumba zaidi ya 100 zilizopo Mapinga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani, Serikali imechukua hatua ya kusitisha mchakato huo, malalamiko ya awali soma hapa ~ Nyumba zaidi ya 400 za Mapinga (Bagamoyo) kuwekewa X ili zivunjwe kuna harufu yenye shaka, Waziri Silaa fuatilia kinachoendelea

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa ameingilia kati mgogoro wa ardhi uliozua taharuki katika eneo la Mapinga wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani kati ya wananchi zaidi ya 100 na mtu mmoja ambaye aliyejulikana kwa majina ya Sevestine Mtunga ambaye anadai kumiliki eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 12 baada ya Mahakama kuwataka wananchi hao kuondoka eneo hilo.

Waziri Silaa ameelekeza zoezi hilo lisimame kwanza na kumuomba mwakilishi wa Sevestin Mtunga ampe muda ili Serikali iweze kulifanyia kazi swala hilo na kuondoa taharuki kwa wananchi kama maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kumwelekeza mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bi Halima Okash kukutana na pande zote kuanzia Jumanne 18 Juni 2024.
Ekari 12 nyumba 400!
 
Hata kusitisha kwa muda kwa utekelezaji wa hukumu ya Mahakama, Waziri huyo anapaswa aende kufungua Maombi/Kesi ndogo Mahakamani (Stay Execution) ili kuzuia utekelezaji wa hukumu hiyo. Kutoa maagizo yoyote Yale ya kusitisha kwa muda utekelezaji wa hiyo Hukumu ya Mahakama bila ya kufungua Kesi ndogo au bila ya kukata rufaa, inahesabika ni kuingilia Maamuzi ya Mahakama
Nakuelewa.
 
kama maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kumwelekeza mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bi Halima Okash kukutana na pande zote kuanzia Jumanne 18 Juni 2024.
HATUTAKI HISANI ya maagizo ya Rais. Tunataka sheria na mifumo ifanye kazi.

Ukikubali unusurike kwa maagizo ya Rais itabidi ukubali siku akitumia nguvu hiyo hiyo kuamuru muondoke auze eneo kwa Mwarabu.

Rais Joseph Biden wa Marekani angeweza kujifungia ndani miezi sita wala wasijue, na himaya bado ikasimama kwa sababu nchi ile inaendeshwa kwa sheria na mifumo. Na kamwe haingilii migogoro ya ardhi.

Kwanza hawana migogoro ya ardhi, nchi ishapimwa. Na bahari yao pia ishapimwa, kila bonde na mwamba na barafu baharini, na the deepest point ndani ya Atlantic Ocean, wanajua ilipo. Sisi tumeshindwa kupima nchi kavu. Pimbi wakubwa.
 
Back
Top Bottom