Oops !! Hili Bhalaa Kubwa Sana SanaUnajuwa nazo Mahakama zetu chini ya Jaji Mkuu Prof Ibrahim Juma ziko CORRUPT.
Naamini ni nguvu ya fedha ndiyo imetembea hadi kufikia maamuzi hayo.
Mahakama palikuwa ni mahali pa haki enzi za Nyerere hadi Mkapa kwa kiasi kikubwa. Wakati wa JK kidogo tu ziliyumba.
Lakini alipokuja Mwendazake Mahakama ziligeuka kuwa "kangaroo courts"
Ngoja tutulie tusikie nini kitajiri
Mamlaka ya Rais kwenye Ardhi yakoje!?It's not true.
The Correct Provision is:
"All land in Tanzania is a public land and vested to the President as the Trustee on behalf of all citizens."
Kwa hiyo, SIYO KWELI kwamba ardhi yote ya Tanzania ni Mali ya Rais au Mali ya Serikali.
Ardhi ya Tanzania ni Mali ya Raia wote wa nchi hii ( Mali ya imma), Rais ni kama Mdhamini tu kwa niaba ya Wananchi wote.
Chini ya waziri kuna kamishina wa Ardhi ambaye kwa niaba ya Rais ana uwezo wa kutengua upangaji wa mtu.
Kwa ivo kushinda kwako kesi mahakamani hakuzuii Waziri mwenye dhamana ya Ardhi kumpangisha mtu mwingine kwenye Ardhi unayoitumia.
Mahakama haizuii mamlaka ya waziri kupangisha (allocate) Ardhi yoyote ile toka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
Kwanza Kwa kesi hii Waziri hajaingilia maamuzi ya Mahakama.Kunapokuwa Kuna Hukumu ya Mahakama, Mamlaka ya Waziri wa Ardhi au Kamishina wa Ardhi yanakoma katika kupangisha au kugawa au kumilikisha Ardhi hiyo kwa mtu mwingine yoyote tofauti na yule aliyeshinda Kesi (Decree Holder), unless kuwe na Makubaliano maalumu Kati ya Decree Holder na Watu hao wengine.
Endapo kama Waziri huyo hajasitisha zoezi la utekelezaji wa hukumu ya Mahakama (yaani hajasitisha ubomoaji wa Nyumba za Judgement Debtors wote) au Kama amekata Rufaa kupinga hukumu hiyo, basi atakuwa hajaingilia Maamuzi ya Mahakama. Lakini endapo kama ametoa maagizo kwamba zoezi la ubomoaji wa Nyumba za Judgment Debtors lisitishwe kwanza, basi atakuwa ameingilia Maamuzi ya Mahakama.Kwanza Kwa kesi hii Waziri hajaingilia maamuzi ya Mahakama.
Nadhani kasitisha Kwa muda. Siyo maamuzi ya mahakama bali jinsi ya utekelezaji wa maamuzi hayo ya mahakama.Endapo kama Waziri huyo hajasitisha zoezi la utekelezaji wa hukumu ya Mahakama (yaani kusitisha ubomoaji wa Nyumba za Judgement Debtors wote) au Kama amekata Rufaa kupinga hukumu hiyo, basi atakuwa hajaingilia Maamuzi ya Mahakama. Lakini endapo kama ametoa maagizo kwamba zoezi la ubomoaji wa Nyumba za Judgment Debtors lisitishwe kwanza, basi atakuwa ameingilia Maamuzi ya Mahakama.
Hata kusitisha kwa muda kwa utekelezaji wa hukumu ya Mahakama, Waziri huyo anapaswa aende kufungua Maombi/Kesi ndogo Mahakamani (Stay Execution) ili kuzuia utekelezaji wa hukumu hiyo. Kutoa maagizo yoyote Yale ya kusitisha kwa muda utekelezaji wa hiyo Hukumu ya Mahakama bila ya kufungua Kesi ndogo au bila ya kukata rufaa, inahesabika ni kuingilia Maamuzi ya MahakamaNadhani kasitisha Kwa muda. Siyo maamuzi ya mahakama bali jinsi ya utekelezaji wa maamuzi hayo ya mahakama.
HUJUI SHERIAKatiba inasema ardhi ni mali ya serikali, mwananchi ni mpangaji tu, waziri ndiye mwenye dhamana ya ardhi, hapo unaonaje? Ahakikishe kuwa hapakuwa na hata chembe ya rushwa.
Na chanzo cha yote haya ni ccm kupitia viongozi wao wa serikali za mitaa!! Kwa imeshakuwa kama sheria kuwa kila ardhi isyopimwa ikiuzwa lazima wapate chao!! Likitokea la kutokea wanakimbia!! Hapo mala nyingi ni busara zaidi ndio hutumika, watu wana miaka 15,hapo na kuna nyumba zaidi ya mia, muda wote huo mlikuwa wapi walipokuwa wakijenga??Watu tunaweza Ku comment kirahisi sana kwa kuwa hatuko kwenye position ya hao watu 100 ambao familia zao zitakosa makazi. Siamini kama hao watu kila mtu alijijia tu akajenga. Ni lazima waliuziwa. May be na matapeli kama ni kweli kiwanja cha huyo alieshinda kesi.
Kibinadamu tu, unawezaje kumbomolea mwenzio nyumba iliyomgharimu mamilioni tena usikute ya mkopo kisa ardhi mali yako. Nafikiri ni vyema serikali ingekaa na pande zote ili waone kila upande unanufaikaje.
Kiukweli Mimi sina hiyo nyumba ila nafeel maumivu wanayopitia hawa watu. Dunia tunapita. Imenikumbusha kipindi watu wanabomolewa kwa kuvamia eneo la yule mama mchungaji, aisee kuna baba anatoka job anakuta vyombo na familia wako nje, nyumba ishaanguka, alianguka na kupoteza fahamu, kuja kuzinduka ni machozi. Mwanaume kulia si jambo dogo. Leo hii mama mchungaji yuko ndani ya ardhi, ardhi na vilivyoko juu yake kaviacha. Kweli ilikuwa ni mali yake, ila asingepungukiwa kuwaachia wale maskini kisehemu tu katika eneo kubwa alilonalo, mbaya zaidi wao walitapeliwa na walikuwa tayari kumlipa vile viwanja.
Umeeleza vizuri kabisa. Haya na Mahakama ni nini?Katiba inasema ardhi ni mali ya serikali, mwananchi ni mpangaji tu, waziri ndiye mwenye dhamana ya ardhi, hapo unaonaje? Ahakikishe kuwa hapakuwa na hata chembe ya rushwa.
Huyu waziri ni kimeo, atatumbuliwa tuKisheria hii imekaaje? Watu wamevamia, wamepelekwa mahakamani na wameshindwa, waziri anakuja kusitisha how?
Kisheria hii imekaaje? Watu wamevamia, wamepelekwa mahakamani na wameshindwa, waziri anakuja kusitisha how?
Acheni uchochezi...Kwahiyo waziri amezuia amri ya mahakama?
Ekari 12 nyumba 400!Baada ya Mdau kuelezea kuhusu mchakato wa kubomoa nyumba zaidi ya 100 zilizopo Mapinga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani, Serikali imechukua hatua ya kusitisha mchakato huo, malalamiko ya awali soma hapa ~ Nyumba zaidi ya 400 za Mapinga (Bagamoyo) kuwekewa X ili zivunjwe kuna harufu yenye shaka, Waziri Silaa fuatilia kinachoendelea
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa ameingilia kati mgogoro wa ardhi uliozua taharuki katika eneo la Mapinga wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani kati ya wananchi zaidi ya 100 na mtu mmoja ambaye aliyejulikana kwa majina ya Sevestine Mtunga ambaye anadai kumiliki eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 12 baada ya Mahakama kuwataka wananchi hao kuondoka eneo hilo.
Waziri Silaa ameelekeza zoezi hilo lisimame kwanza na kumuomba mwakilishi wa Sevestin Mtunga ampe muda ili Serikali iweze kulifanyia kazi swala hilo na kuondoa taharuki kwa wananchi kama maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kumwelekeza mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bi Halima Okash kukutana na pande zote kuanzia Jumanne 18 Juni 2024.
Nakuelewa.Hata kusitisha kwa muda kwa utekelezaji wa hukumu ya Mahakama, Waziri huyo anapaswa aende kufungua Maombi/Kesi ndogo Mahakamani (Stay Execution) ili kuzuia utekelezaji wa hukumu hiyo. Kutoa maagizo yoyote Yale ya kusitisha kwa muda utekelezaji wa hiyo Hukumu ya Mahakama bila ya kufungua Kesi ndogo au bila ya kukata rufaa, inahesabika ni kuingilia Maamuzi ya Mahakama
HATUTAKI HISANI ya maagizo ya Rais. Tunataka sheria na mifumo ifanye kazi.kama maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kumwelekeza mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bi Halima Okash kukutana na pande zote kuanzia Jumanne 18 Juni 2024.
Kwa mahakama zipi? Bongo ??.Kwahiyo waziri amezuia amri ya mahakama?