Waziri wa Elimu kataza wanafunzi kulazimishwa kwenda na madaftari yote shule

Waziri wa Elimu kataza wanafunzi kulazimishwa kwenda na madaftari yote shule

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Huwezi kuelewa mzigo wanaobebeshwa wanafunzi wa shule za kutwa mpaka pale utakapojaribu kuubeba mfuko wa madaftari wanaobeba wakienda shuleni. Kitendo cha watoto kulazimishwa kwenda na Vitabu vya kiada na Madaftari ya Masomo yote shuleni kila siku kinawaletea wanafunzi hao matatizo kwenye uti wa mgongo.

Hivi kila shule si ina ratiba ya Masomo. Kwa nini watoto wabebeshwe mzigo wa madaftari na vitabu kwa masomo yasiyohusika kwa siku hiyo.

Kama Ratiba inaonesha kutakuwa na masomo manne ni kwa nini mtoto asibebe madaftari ya masomo hayo tu?

Miaka ijayo jamii itaingia gharama ya kutibu watu wazima chungu nzima watakaokuwa wanaumwa uti wa mgongo, chanzo kikiwa ni uzembe tu wa walimu kulazimisha watoto kubeba mzigo wa madaftari na vitabu bila ya sababu.
 
Elimu ya siku hizi imekua ya hovyo.... mambo yasiyo na mantiki ni mengi
1. Hilo ulilosema, watoto kubeba madaftari kama makuli

2. Watoto kulazimishwa kukaa boarding umri mdogo.

3. Kufutwa kwa masomo ya stadi za kazi na michezo.

Tunazalisha watoto wajinga, wakati ulimwengu huu wa fujo na teknolojia, malezi inabidi yatiliwe mkazo na ubunifu mwingi kuliko sisi vijana wa early 90s tulivyolelewa
 
Nadhani tuliowengi humu tumesoma St.Kayumba na tunafahamu kuwa walimu ni nadra sana kufuata ratiba ya darasa mathalani unakuta mwalimu wa somo la siku husika hajafika shule hivyo itampasa mwalimu/walimu waliopo waje kuwafundisha darasani ili mradi tu isipite siku bila kufundishwa angalau somo lolote lile.

My take kwa wizara wangetengeneza LOCKER kama wenzetu Ulaya na kila mwanafunzi angekuwa na locker yake itakayoweza kuwa maalamu kwakuhifadhi vitabu na vitu vingine vya mwanafunzi.
 
Tatizo kubwa ni watu kuzaa bila uzazi wa mpango hivyo kushindwa kuwahudumia ipasavyo watoto wao.
Elimu ya siku hizi imekua ya hovyo.... mambo yasiyo na mantiki ni mengi
1. Hilo ulilosema, watoto kubeba madaftari kama makuli
2. Watoto kulazimishwa kukaa boarding umri mdogo
3. Kufutwa kwa masomo ya stadi za kazi na michezo.....

Tunazalisha watoto wajinga, wakati ulimwengu huu wa fujo na teknolojia, malezi inabidi yatiliwe mkazo na ubunifu mwingi kuliko sisi vijana wa early 90s tulivyolelewa
 
Umetoa suluhisho sahihi kabisa, wakati mwingine madaftari yananyeeshwa na mvua watoto wakiwa njian, ila kuna shule bado hata madawati ya kukalia ni tatizo, locker inaweza kuwa anasa.
Nadhani tuliowengi humu tumesoma St.Kayumba na tunafahamu kuwa walimu ni nadra sana kufuata ratiba ya darasa mathalani unakuta mwalimu wa somo la siku husika hajafika shule hivyo itampasa mwalimu/walimu waliopo waje kuwafundisha darasani ili mradi tu isipite siku bila kufundishwa angalau somo lolote lile.
My take kwa wizara wangetengeneza LOCKER kama wenzetu Ulaya na kila mwanafunzi angekuwa na locker yake itakayoweza kuwa maalamu kwakuhifadhi vitabu na vitu vingine vya mwanafunzi.
 
Tatizo kubwa ni watu kuzaa bila uzazi wa mpango hivyo kushindwa kuwahudumia ipasavyo watoto wao.
Wala sio uzazi wa mpango..... shule tu zimejiwekea visera ambavyo havina msingi, it's even worse kama unakaa eneo ambalo shule za karibu ndo hizo mtoto wa la nne lazima boarding...... binafsi nna watoto watatu wemefatana kama nyanya lakini hakuna mwanangu ataiona boarding mpaka aende chuo for as long as nipo hai

Mama yao sijasoma boarding na shule ufaulu wangu uliridhisha level zote za elimu
 
Huwezi kuelewa mzigo wanaobebeshwa wanafunzi wa shule za kutwa mpaka pale utakapojaribu kuubeba mfuko wa madaftari wanaobeba wakienda shuleni. Kitendo cha watoto kulazimishwa kwenda na Vitabu vya kiada na Madaftari ya Masomo yote shuleni kila siku kinawaletea wanafunzi hao matatizo kwenye uti wa mgongo.

Hivi kila shule si ina ratiba ya Masomo. Kwa nini watoto wabebeshwe mzigo wa madaftari na vitabu kwa masomo yasiyohusika kwa siku hiyo. Kama Ratiba inaonesha kutakuwa na masomo manne ni kwa nini mtoto asibebe madaftari ya masomo hayo tu?

Miaka ijayo jamii itaingia gharama ya kutibu wato wazima chungu nzima watakaokuwa wanaumwa uti wa mgongo, chanzo kikiwa ni uzembe tu wa walimu kulazimisha watoto kubeba mzigo wa madaftari na vitabu bila ya sababu.

Aiseee Mkuu
Naomba niwatag wote
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan,Naomba uwape maelekezo watoto wanapata Shida Kubwa Mnoo ya Migongo,

Waziri Mkuu.. Majaliwa Kassim Majaliwa,

Hili Binafsi Nimeisha Kisema Sanaaa,Tena Mnooo Lakini Wenye Shule hawasikii wala Kufuata…Ukiwabana sana Watakuonyesha Ratiba ya Masomo ya kila Siku,…Kumbe wanawaambia watoto waje na Madaftari yote kwasababu hawafuati ratiba,Anaweza Ingia Mwl yeyote pale Mwl mwingine anapokuwa Hayupo!

Hili Hawawezi Sikia Kamwe!

Nadhani Kwenye Uzi wako ungewatag Tamisemi,Waziri wa Elimu Hata Waziri Mkuu Kwa Msisitizo na Maelekezo!
Hakyanani Mtu Mzima wa Miaka 30-40 Ule Mzigo anaobeba Mtoto Under 10yrs Hufikishi Hata 1km[emoji1787]
 
Umetoa suluhisho sahihi kabisa, wakati mwingine madaftari yananyeeshwa na mvua watoto wakiwa njian, ila kuna shule bado hata madawati ya kukalia ni tatizo, locker inaweza kuwa anasa.

Naonba Nikuulize Swali…Na Akiwa nyumbani hasomi? Sababu vitabu na Madaftari ameweka Shuleni kwenye Locker[emoji2368]
Pili Huu Mzigo Anapotoka Tuu Shule anabeba Na Anapoenda Shule mgongo Itauma sana Baadae
 
Mmh!

Na hilo nalo hadi waziri atoe tamko?

Hii nchi imeoza kuanzia wananchi hadi viongozi...
 
Mmh!

Na hilo nalo hadi waziri atoe tamko?

Hii nchi imeoza kuanzia wananchi hadi viongozi...
Unawezaje kulifanya jambo kama hili liwe na matokeo chanya kitaifa bila ya Waziri wa Elimu kulitolea agizo??

Mbona wakati ule ulikuwa hushangai Rais wa nchi kuzungumzia migogoro ya Ardhi na ndoa za watu?
 
Nadhani tuliowengi humu tumesoma St.Kayumba na tunafahamu kuwa walimu ni nadra sana kufuata ratiba ya darasa mathalani unakuta mwalimu wa somo la siku husika hajafika shule hivyo itampasa mwalimu/walimu waliopo waje kuwafundisha darasani ili mradi tu isipite siku bila kufundishwa angalau somo lolote lile.
My take kwa wizara wangetengeneza LOCKER kama wenzetu Ulaya na kila mwanafunzi angekuwa na locker yake itakayoweza kuwa maalamu kwakuhifadhi vitabu na vitu vingine vya mwanafunzi.
Comments nyingi zimelaumu ila wewe umetoa na njia moja wapo ya namna ya kurekebisha.
 
Back
Top Bottom