KERO Waziri wa Elimu, tunaomba msaada wako. Shule binafsi bweni hawataki tuone watoto

KERO Waziri wa Elimu, tunaomba msaada wako. Shule binafsi bweni hawataki tuone watoto

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Waziri aingilie kati vipi wakati umeshasema ni shule binafsi? Kila shule ina utaratibu wake, unadhani wakiruhusu hivyo kila mzazi kumtembelea mtoto wake anavyo jisikia kutakuwa na shule tena hapo? Na vipi kuhusu yule mtoto ambaye hato tembelewa huoni kwamba atakuwa anajisikia unyonge? Kama kuna tatizo hasa wasiliana na uongozi watakujuza maendeleo ya mtoto wako, ila ukiona umeshindwa huo utaratibu unaweza kumhamisha mtoto wako bila kusumbua watu wengine.
Umemaliza utata, kikao kifungwe.

Siku moja nilikwenda kumtembelea mwanangu na kuhudhuria mkutano wa mwaka wa wazazi. Baada ya mkutano kuna kama masaa mawili hivi, mzazi unakaa na mwanao kula nae na kupiga story. Nilipomaliza kupiga story na mwanangu, ile naagana nae, akaniambia tazama baba jirani yetu hajafika, mwanae yule pale analia. Kweli nageuka kumtazama mtoto ameshindwa hadi kula kwa kuwa hakuna mzazi /mlezi aliyemtembelea.

Nilipiga simuvaongee na mamake, akamwambia sikuwa na nauli. Aliniomba nimwachia japo hela ya sabuni. Nilifanya hivyo na mtoto akapata angalau ahueni.

Tuchukulie kila mwezi wazazi watembelee watoto wao. Kwa wazazi wasio na uwezo wa kutosha kumudu nauli, itakuwaje kisaikolojia kwa watoto wao?

Halafu mawazo haya ni ya kishamba sana. Hivi miaka ile unatoka Mtwara unapangiwa sekondari Mwanza, tulikuwa tunatembelewa na wazazi? Januari hadi Juni no mzazi wala rafiki na kama huna nauli ya kuendea kwenu unabaki shule hadi Desemba. Shule zilijua hilo na zilitoa nafasi kwa wasio na nauli unajiandikisha kubaki shuleni.

Kwa sasa tunadekeza sana watoto kiasi cha kutaka umfuate kila alipo kila mara. Ni sehemu ya kuharibu watoto.
 
Salaam na heshima kwako Mh Waziri Elimu Prof Mkenda.

Awali ya yote nawapa pongezi sana kwa jitihada zenu kuboresha elimu tangu msingi hadi sekondari..hongera sana awamu hii pongezi kwa Mama Samia.

Wazazi tuna malalamiko hasa kwa shule binafsi za bweni shulw msingi na sekondari....kwa nini hawataki na wamefuta utaratibu kutembelea watoto mwisho mwezi ? Kwa kitu gani wanachosoma iwe hakuna ruhusa kuona watoto kujua afya zao na maendeleo yao ?

Naomba Mh Waziri ingilia kati suala hili tumeongea na shule binafsi bila mafanikio naona kila shule wanajiamulia tu, ni haki ya wazazi kuwaona watoto wao mwisho mwezi hata masaa machache.

Asante nakutakia kazi njema
MZAZI
Na Maelimu yao ya kukaririsha mtoto....unakuta mtoto ana Div 1 ila kilaza wa mwisho hana anachojua
 
Waziri aingilie kati vipi wakati umeshasema ni shule binafsi? Kila shule ina utaratibu wake, unadhani wakiruhusu hivyo kila mzazi kumtembelea mtoto wake anavyo jisikia kutakuwa na shule tena hapo? Na vipi kuhusu yule mtoto ambaye hato tembelewa huoni kwamba atakuwa anajisikia unyonge? Kama kuna tatizo hasa wasiliana na uongozi watakujuza maendeleo ya mtoto wako, ila ukiona umeshindwa huo utaratibu unaweza kumhamisha mtoto wako bila kusumbua watu wengine.
Mkuu wa hiyo shule. 😂😂
 
Aliekuambia upeleke watoto wako huko nani!!?

Elimu ni Bure na fate za watoto kielimu zinafanana kwanini uwapeleke huko!!?
 
Hii sio tatizo la shule 1 mkuu
Mleta mada ameshindwa kututajia jina la shule inayohusika. Lakini hata hivyo bado nasisitiza Utaratibu uliokubalika uzingatiwe. Nakuomba usome post #95 japokuwa ni ndefu kidogo-vumilia mpendwa.
 
Maana ya kumpeleka bweni ni nini? Kama unataka kumwona mara kwa mara bora akae day tu!
Siku hizi hata wa day hulazimishwa kukaa bweni Kwa madai ya kujiandaa na mtihani na ni shule karibu zote za binafsi
 
Dawa ni kupeleka watoto wenu shule za Kayumba .

Acheni kujistress .

Acheni kuwa stress watoto wenu.

Haya Sasa twende Kazi. Kimbia haraka Sana nenda kachukue watoto wako warudishe Kayumba.

Utakuja kunishukuru mno
Fuoni na Temeke sekondari
 
Duuu wanajali watt wapate wani ,kwani wani ni kitu gani, tuanze kuwa cheki ma to since 90s wako wapi, A's zimeshapitwa na wakati Ile claiming capacity, Kuna jamaa walipata wani Tena ya 7 later ya 3 advance, mtu y
 
Back
Top Bottom