TANZIA Waziri wa TAMISEMI Mohammedi Mchengerwa Amefiwa na Baba Yake Mzazi Akiwa Ibadani Makka Na Atazikwa hukohuko Makka

Lete mahala palipoeleza ama vifungu vya sheria kutoka sijui Makka, Saudi Arabia ama wapi vikesema mtu akifia Makka anazikwa Makka.
 
Kule ukienda mgonjwa lazima ukate moto...
Sio lazima.
Kwani kule hakuna wagonjwa ?! Siku yako ya kufa kama imefika Allaah haangalii upo wapi na unafanya nini! Siku ya kufa ikifika lazima ufe.
Siku ya kufa ikifika ukiwa bar unapiga safari lager na mishikaki ya kitimoto utakufa na pia siku ya kufa ikifika ukiwa msikitini umemsujudia mola wako pia utakufa!.
 
Lete mahala palipoeleza ama vifungu vya sheria kutoka sijui Makka, Saudi Arabia ama wapi vikesema mtu akifia Makka anazikwa Makka.
Kabla ya kusoma hivyo vifungu vya sheria bwana KITIMOTO ambaye najua wewe siyo muislamu na hujui machimbuko
( مصادر ) ya sheria za kiislamu ni mangapi, ni kwamba Mzee Mchengerwa siyo muislamu wa kwanza kufia katika mji wa makka akiwa kwenye ibada.
Mwaka 2016 palitokea tukio la watu kuanguka na kukanyagwa hadi kufa katika ibada ya HIJA na hapa Tanzania familia kadhaa zilipoteza ndugu zao katika tukio hilo waliokuwa katika ibada ya hijja.
Sasa naomba uniambie mtu mmoja tu unayemjua aliyewahi kufia Makka halafu maiti yake ikasafirishwa kuzikwa huku Tanzania.
 
Hii Dua ni Kwa wale wanaofia Makkah au marhum Wote?
Ni kwa Marhum waislamu wote!.
Zingatia waislamu wote!
Dua hii katika swala ya jeneza ( Swala ya kumswalia maiti katika vitabu vya dini ya kiislamu huitwa swala ya jeneza صلاة الجنازة) husomwa baad ya takbira ya tatu ( swala ya jeneza huwa na takbira nne )
 
Maswali gani hayo unamuuliza chawa, yeye alipoona habari imemtaja Mchengerwa moja kwa moja msiba ukawa wake na si ajabu alilia kabisa bila hata kumjua hata kwa picha marehemu.

Chawa huyu, ukiitaja ccm anabubujikwa na mchozi
Acha dharau 😄😄
 
Umeulizwa??machoko mna shida sana
 
Inna lillah wainna ilayhi raajiun
 
Poleni.
Huko siyo kwa kwenda kiholele, usipokaa sawasawa hurudi
Watu wengi bali mamilioni ya waislamu kila mwaka wanaenda Makka wakafanya ibada na kurudi salama kabisa kwenye nchi zao.
Hata hapa Tanzania maelfu ya waislamu walishaenda hijja na kurudi.
Kule kwetu mkoani Kagera mtu akienda Makka akirudi ukitaka kutaja jina lake lazima uanze Al haji au Haji fulani au kama ni mwanamke Hajati Fulani.
Sasa ma Al haji na Mahajati waliopo mkoani Kagera peke yake ni wengi sana.
Kilichomtokea Mzee Mchengerwa hutokea mara mojamoja sana na idadi ya watu waliofia Makka wakiwa kwenye ibada ni ndogo sana ukilinganisha na wale waliokwenda na kurudi salama.
 
Labda shetani naye katika kujitetea alirusha jiwe kwa huyo marehemu
 
Wasipelelezane wao kwa wao wala wasisengenyane wao kwa wao kwahiyo inamaana wakina nani wasengenywe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…