Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Lloyd Austin aionya Iran kuwa ikithubutu kujibu shambulizi la Israeli huo ndiyo utakuwa mwisho wake!

Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Lloyd Austin aionya Iran kuwa ikithubutu kujibu shambulizi la Israeli huo ndiyo utakuwa mwisho wake!

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Wadau hamjamboni nyote?

Wakati mvutano unaendelea huko Mashariki ya Kati kufuatia mashambulizi ya kisasi ya Israel dhidi ya Iran, Marekani imeionya Tehran dhidi ya mipango yoyote wa kulipiza kisasi.

Pentagon imesema kuwa mashambulizi ya Israel ya Jumamosi yanakusudiwa kumaliza uhasama kati ya mataifa hayo mawili.

"Iran haipaswi kufanya kosa la kujibu mashambulizi ya Israel, mashambulizi ambayo yanapaswa kuwa mwisho wa mtafaruku huu," alisema Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin.

Rais wa Marekani Joe Biden alisema anatumaini kuwa mashambulizi hayo dhidi ya Iran yatakuwa mwisho wa mzunguko wa muda mrefu wa kuongezeka kwa mivutano. “Natumaini huu ndio mwisho,” aliwaambia waandishi wa habari Jumamosi.

Wakati huo huo, Iran ilionekana kupuuza shambulizi hilo, ikisema kuwa ina majukumu katika kulinda amani na usalama wa kanda hiyo.

Iran US.png
Source: India Today
 
Wadau hamjamboni nyote?

Jisomeeni


US defense chief: Iran ‘should not make the mistake of responding to Israel’s strikes’

By Reuters

“Iran should not make the mistake of responding to Israel’s strikes, which should mark the end of this exchange,” Austin says in a statement.
Bado mnasema Israel ndo Taifa Lenye Nguvu...
Anakupiga Mtu halafu onyo anatoa Mwingine Ole wako umrudishie 🤣🤣..
Ina maana anajua Ukimrudishia Watu watajua kuwa hana Nguvu 🤣🤣 kama anavyosifiwa
 
Bado mnasema Israel ndo Taifa Lenye Nguvu...
Anakupiga Mtu halafu onyo anatoa Mwingine Ole wako umrudishie 🤣🤣..
Ina maana anajua Ukimrudishia Watu watajua kuwa hana Nguvu 🤣🤣 kama anavyosifiwa
Isaya 60:9-10
[9]Hakika yake visiwa vitaningojea,
Na merikebu za Tarshishi kwanza,
Ili kuleta wana wako kutoka mbali,
Na fedha yao na dhahabu yao pamoja nao,
Kwa ajili ya jina la BWANA, Mungu wako,
Kwa ajili yake Mtakatifu wa Israeli,
Kwa kuwa amekutukuza wewe.
[10]Na wageni watajenga kuta zako,
Na wafalme wao watakuhudumu;
Maana katika ghadhabu yangu nalikupiga,
Lakini katika upendeleo wangu nimekurehemu.

Hao USA wanajipendekeza kama Neno la Mungu linavyosema
 
Back
Top Bottom