Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Watu wa ushauri wa bure tupo, hilo tatizo tumeliona, tumelinote na tumeshauri kwenye HII kitu!Samia si tatizo letu.
Samia ni dalili tu ya tatizo letu.
Na kila tunavyo focus kwenye dalili ya tatizo na kuacha kuangalia tatizo lenyewe, tunazidisha tatizo.
Anamcha Mungu gani?Tofauti na yule, huyu mcha Mungu
Huyu mama amejichanganya kutaka kuiga style za Magu. Naona washauri wamemuambia ili apate madaraka kwa ulaini aanze kuteka, kupoteza na hata kuua. Sasa ameukalia.Na. M. M. Mwanakijiji
Rais Samia alitaka kupendwa. Rais Samia alitaka kukubalika. Rais Samia alitaka kuoenakana yeye siyo kama yule. Baada ya kuapishwa kufuatia maombolezo ya kifo cha Bw. Yule mara moja watu walianza kusema sasa "wanashusha pumzi". Wapo watu walisherehekea na wakajua kuwa sasa angalau wanaweza kuhema. Hali ya kuwa roho juu kisa bwana yule asiyelala na mwenye kukesha na mafaili hadi chumbani ikashuka. Watu wakaanza kutembea na kuchekeana bila kuogopana.
Upinzani ulishukuru zaidi kwana Bw. Yule aliwabana kweli kweli. Lakini upinzani dhidi yake ulikuwa wazi kabisa na kamili; mgogoro wake na upinzani na dhana ya demokrasia watu waliijua kabla hajaingia madarakani. Hakuwahi kuwa na ahadi za kidemokrasia hata kama aliziimba kidogo. Watu walijua kuwa yeye alichotaka ni "kazi" watu wakakutane kwenye kampeni. Hakutaka kuendekeza siasa za kushindana; walipojaribu kujitutumua vyombo vya dola vya nchi hii vikaingia kumfanya Bw. Yule atawale bila kuzingwazingwa.
Wale wajomba zetu walipojaribu kusema hakuwapepesea macho; na aliwaonesha kweli yeye hawajali kivile pale alipokataa kabisa kwenda kubeba tenga lake kulipeleka huko waliko kuwaomba. Kama aliwaomba aliwataka wao waje kwake ndio awaombe. Tena waje na matenga yao kwanza! Alikataa sana ile hali ya "kujidhalilisha". Sasa Rais Samia alipoingia madarakani siyo tu alitaka kupendwa na watendaji serikali ambao walikuwa roho juu hata kwenda Dubai ilikuwa Mbinde bali alitaka kupendwa na wajomba zetu huko nchi za Magharibi. Rais Samia katika kupendwa huko akaamua kujitenga kimaono na kiutendaji na Bw. Yule.
Bw. Yule alikuwa anafokafoka; mama hakasema yeye hafoki. Huku kijijini Mama akaanza kujulikana kwa "Mama Nahaya Mkayaangilie". Mama hakutaka watu waondoke wamenuna; alijua kuwabembeleza na hata akiwatimua kazi hakutaka wajue ni yeye amechukizwa. Mama akakwepa kabisa kutimua watendaji wabovu papo kwa papo japo anafanya hivyo kimya kimya. Niliandika mahali kuwa Rais Samia ni Simba Mwendapole.
Sasa haya ya juzi ndio yamefunua kuwa jani halitui mbali ya mti na kuwa atapikaye hutapika mbele yake. Mama alijaribu kuwapendeza wapinzani, amejaribu kuwatetea watu wabovu na kwa namna alibariki ulaji wa "urefu wa kamba zao" kumbe wajanja wakala na kamba zenyewe! Mama ambaye alisifiwa kuwa yeye hafokei watu juzi kwenye sherehe za Miaka 60 ya Jeshi la Polisi Mama akajikuta amegeuka kama Bw. Yule.
Yaani, kama hotuba ile ingetolewa kwa sauti ya Bw. Yule kuna watu wangebeba mashada ya maua na kumwambia mama kumbe umerudi! Sasa alivyojitenga vyote vile, na juhudi zote za 4R zimekuwa sasa ni juhudi za 4K - Kugeukana, Kukimbizana, Kutoleana Macho na Kupigana Mikwara! Alijaribu kujitenga na habari za Bw. Yule; lakini sasa karudi tena karudi na naona na tenga analipiga mkwara. Tunakoelekea jina la Bw. Yule litaanza kuimbwa mbele zake kama alama za kumuunga mkono.
Jamaa unapenda umwagaji wa damu za watu,wafuasi wa magufuli mlipandikizwa roho chafu kabisa kabisa ,laana ya Mungu iwe juu yenu,,Na. M. M. Mwanakijiji
Rais Samia alitaka kupendwa. Rais Samia alitaka kukubalika. Rais Samia alitaka kuoenakana yeye siyo kama yule. Baada ya kuapishwa kufuatia maombolezo ya kifo cha Bw. Yule mara moja watu walianza kusema sasa "wanashusha pumzi". Wapo watu walisherehekea na wakajua kuwa sasa angalau wanaweza kuhema. Hali ya kuwa roho juu kisa bwana yule asiyelala na mwenye kukesha na mafaili hadi chumbani ikashuka. Watu wakaanza kutembea na kuchekeana bila kuogopana.
Upinzani ulishukuru zaidi kwana Bw. Yule aliwabana kweli kweli. Lakini upinzani dhidi yake ulikuwa wazi kabisa na kamili; mgogoro wake na upinzani na dhana ya demokrasia watu waliijua kabla hajaingia madarakani. Hakuwahi kuwa na ahadi za kidemokrasia hata kama aliziimba kidogo. Watu walijua kuwa yeye alichotaka ni "kazi" watu wakakutane kwenye kampeni. Hakutaka kuendekeza siasa za kushindana; walipojaribu kujitutumua vyombo vya dola vya nchi hii vikaingia kumfanya Bw. Yule atawale bila kuzingwazingwa.
Wale wajomba zetu walipojaribu kusema hakuwapepesea macho; na aliwaonesha kweli yeye hawajali kivile pale alipokataa kabisa kwenda kubeba tenga lake kulipeleka huko waliko kuwaomba. Kama aliwaomba aliwataka wao waje kwake ndio awaombe. Tena waje na matenga yao kwanza! Alikataa sana ile hali ya "kujidhalilisha". Sasa Rais Samia alipoingia madarakani siyo tu alitaka kupendwa na watendaji serikali ambao walikuwa roho juu hata kwenda Dubai ilikuwa Mbinde bali alitaka kupendwa na wajomba zetu huko nchi za Magharibi. Rais Samia katika kupendwa huko akaamua kujitenga kimaono na kiutendaji na Bw. Yule.
Bw. Yule alikuwa anafokafoka; mama hakasema yeye hafoki. Huku kijijini Mama akaanza kujulikana kwa "Mama Nahaya Mkayaangilie". Mama hakutaka watu waondoke wamenuna; alijua kuwabembeleza na hata akiwatimua kazi hakutaka wajue ni yeye amechukizwa. Mama akakwepa kabisa kutimua watendaji wabovu papo kwa papo japo anafanya hivyo kimya kimya. Niliandika mahali kuwa Rais Samia ni Simba Mwendapole.
Sasa haya ya juzi ndio yamefunua kuwa jani halitui mbali ya mti na kuwa atapikaye hutapika mbele yake. Mama alijaribu kuwapendeza wapinzani, amejaribu kuwatetea watu wabovu na kwa namna alibariki ulaji wa "urefu wa kamba zao" kumbe wajanja wakala na kamba zenyewe! Mama ambaye alisifiwa kuwa yeye hafokei watu juzi kwenye sherehe za Miaka 60 ya Jeshi la Polisi Mama akajikuta amegeuka kama Bw. Yule.
Yaani, kama hotuba ile ingetolewa kwa sauti ya Bw. Yule kuna watu wangebeba mashada ya maua na kumwambia mama kumbe umerudi! Sasa alivyojitenga vyote vile, na juhudi zote za 4R zimekuwa sasa ni juhudi za 4K - Kugeukana, Kukimbizana, Kutoleana Macho na Kupigana Mikwara! Alijaribu kujitenga na habari za Bw. Yule; lakini sasa karudi tena karudi na naona na tenga analipiga mkwara. Tunakoelekea jina la Bw. Yule litaanza kuimbwa mbele zake kama alama za kumuunga mkono.
Yeah!....ya kushughulikia wapinzani pekeeAnakuambia serikali ina intelligence kali sasa mbona wasiojulikana mpaka bado awajulikani .au intelligence anayozungumzia kuichunguza chadema tu
Mtu mweusi huwa hapewi uhuru hata siku mojaNi ngumu kumwepuka bwana yule. Njia aliyoichagua amegundua haimfikishi salama.
Any way ngumu sana kuaapply "demokrasia" kwa mtu mweusi halafu utegemee matokeo chanya. Njia ya bwana yule ndiyo demokrasia sahihi kwa mwafrika hii ya mzungu ni sahihi kwao
Tena yule alikuwa mwamba kweli sembuse huyu.Mama mbona wasiwasi wake tu?
Alikuwa nayo nafasi ya kusimama katika haki na akaungwa mkono na walio wengi.
Nchimbi mbona anaongea lugha nzuri na anaeleweka?Kwani angeongea kama Nchimbi shida ilikuwa wapi?
Asingekubaliana na teka teka nani angekuwa na taabu naye?
Tatizo lake kulewa madaraka akisikia katiba mpya anaona urais wake 2025 unakuja kwenda na maji.
Laiti angejikita kwenye kujenga legacy yake kuliko 2025 mbona alikuwa na yote ya kupata?
Alipo sasa na ajiangalie asije akaanguka.
Kwani yaliisha je na yule mwamba aliyeambiwa mgombea shuruti awe mwanamke?
Tena anatakiwa azidishe maradufuJamaa unapenda umwagaji wa damu za watu,wafuasi wa magufuli mlipandikizwa roho chafu kabisa kabisa ,laana ya Mungu iwe juu yenu,,
Mi binafsi namkubari Samia, kinachotokea sasa Samia amechoka na kashfa zenu na dharau za kutaka sijui afanye kama alivyokuwa anafanya jiwe, amehamua sasa kuongoza kwa staili ile
Sijakusoma!Kwa hiyo sasa umejifunza jina jipya na mama umewaachia kina Lukasi wahangaike naye?
Yule alionekana kanisani kabisa zaidi ya mara moja. Alikuwa karibu sana na kanisa we lini ushamuona huyu msikitiniš¤£Tofauti na yule, huyu mcha Mungu
Demokrasia ya mtu mweusi ni kumswaga nakubaliana na hilo ila je, dhamira ni safi? Unamswaga mtu ukilenga ku achieve nini?Ni ngumu kumwepuka bwana yule. Njia aliyoichagua amegundua haimfikishi salama.
Any way ngumu sana kuaapply "demokrasia" kwa mtu mweusi halafu utegemee matokeo chanya. Njia ya bwana yule ndiyo demokrasia sahihi kwa mwafrika hii ya mzungu ni sahihi kwao
Tatizo lenyewe ni lipi sasa. Taifa lenyewe linategemea 1 man show kusinamia kila kitu badala ya katiba.Samia si tatizo letu.
Samia ni dalili tu ya tatizo letu.
Na kila tunavyo focus kwenye dalili ya tatizo na kuacha kuangalia tatizo lenyewe, tunazidisha tatizo.
Kaka mkubwa usipotee sana michango yako bado inahitajika hapa jukwaani,mmemuacha brother Mayala peke yakeNa. M. M. Mwanakijiji
Rais Samia alitaka kupendwa. Rais Samia alitaka kukubalika. Rais Samia alitaka kuoenakana yeye siyo kama yule. Baada ya kuapishwa kufuatia maombolezo ya kifo cha Bw. Yule mara moja watu walianza kusema sasa "wanashusha pumzi". Wapo watu walisherehekea na wakajua kuwa sasa angalau wanaweza kuhema. Hali ya kuwa roho juu kisa bwana yule asiyelala na mwenye kukesha na mafaili hadi chumbani ikashuka. Watu wakaanza kutembea na kuchekeana bila kuogopana.
Upinzani ulishukuru zaidi kwana Bw. Yule aliwabana kweli kweli. Lakini upinzani dhidi yake ulikuwa wazi kabisa na kamili; mgogoro wake na upinzani na dhana ya demokrasia watu waliijua kabla hajaingia madarakani. Hakuwahi kuwa na ahadi za kidemokrasia hata kama aliziimba kidogo. Watu walijua kuwa yeye alichotaka ni "kazi" watu wakakutane kwenye kampeni. Hakutaka kuendekeza siasa za kushindana; walipojaribu kujitutumua vyombo vya dola vya nchi hii vikaingia kumfanya Bw. Yule atawale bila kuzingwazingwa.
Wale wajomba zetu walipojaribu kusema hakuwapepesea macho; na aliwaonesha kweli yeye hawajali kivile pale alipokataa kabisa kwenda kubeba tenga lake kulipeleka huko waliko kuwaomba. Kama aliwaomba aliwataka wao waje kwake ndio awaombe. Tena waje na matenga yao kwanza! Alikataa sana ile hali ya "kujidhalilisha". Sasa Rais Samia alipoingia madarakani siyo tu alitaka kupendwa na watendaji serikali ambao walikuwa roho juu hata kwenda Dubai ilikuwa Mbinde bali alitaka kupendwa na wajomba zetu huko nchi za Magharibi. Rais Samia katika kupendwa huko akaamua kujitenga kimaono na kiutendaji na Bw. Yule.
Bw. Yule alikuwa anafokafoka; mama hakasema yeye hafoki. Huku kijijini Mama akaanza kujulikana kwa "Mama Nahaya Mkayaangilie". Mama hakutaka watu waondoke wamenuna; alijua kuwabembeleza na hata akiwatimua kazi hakutaka wajue ni yeye amechukizwa. Mama akakwepa kabisa kutimua watendaji wabovu papo kwa papo japo anafanya hivyo kimya kimya. Niliandika mahali kuwa Rais Samia ni Simba Mwendapole.
Sasa haya ya juzi ndio yamefunua kuwa jani halitui mbali ya mti na kuwa atapikaye hutapika mbele yake. Mama alijaribu kuwapendeza wapinzani, amejaribu kuwatetea watu wabovu na kwa namna alibariki ulaji wa "urefu wa kamba zao" kumbe wajanja wakala na kamba zenyewe! Mama ambaye alisifiwa kuwa yeye hafokei watu juzi kwenye sherehe za Miaka 60 ya Jeshi la Polisi Mama akajikuta amegeuka kama Bw. Yule.
Yaani, kama hotuba ile ingetolewa kwa sauti ya Bw. Yule kuna watu wangebeba mashada ya maua na kumwambia mama kumbe umerudi! Sasa alivyojitenga vyote vile, na juhudi zote za 4R zimekuwa sasa ni juhudi za 4K - Kugeukana, Kukimbizana, Kutoleana Macho na Kupigana Mikwara! Alijaribu kujitenga na habari za Bw. Yule; lakini sasa karudi tena karudi na naona na tenga analipiga mkwara. Tunakoelekea jina la Bw. Yule litaanza kuimbwa mbele zake kama alama za kumuunga mkono.
Ni wale wale....harafu unalinganisha hizo hit hole countries na china?Nilikuwa wa kwanza kusema Mama arudishe siasa za kuwashughulikia Wapinzani bila kuingiza mambo hayo kwenye uchumi.
Mifano Iko Mingi sana kuanzia Uganda,Rwanda,Egypt,China nk.
Bwana wako yule alikuwa haelewi yeye akaleta chuki zake Hadi kwenye Uchumi,Hali ikawa mbaya wawekezaji wakakimbia, account zikaanza kufungwa ,watu kubambikiwa Kodi Kwa sababu pesa imepungua na Biashara kukaba kiasi kwamba vilio vya vyuma kukaza vilitamalaki.
Rais awashughulikie Wanasiasa uchwara na vibaraka wote ila silete siasa za ujamaa hapa.
Mwisho kama unaembeba habebeki unategemea uendelee kumbeba? Una mdamp tuu unasonga mbele mwenyewe.
Tunapenda shortcuts.Tatizo lenyewe ni lipi sasa. Taifa lenyewe linategemea 1 man show kusinamia kila kitu badala ya katiba.
Ktk uislam mwanamke anatakiwa aswali nyumbani ni aula zaidi kuliko kuswali msikitiniYule alionekana kanisani kabisa zaidi ya mara moja. Alikuwa karibu sana na kanisa we lini ushamuona huyu msikitiniš¤£
Mcha Mungu!Tofauti na yule, huyu mcha Mungu
Kufunika kichwa sio uchamungu, anaficha mvi tu. Uchamungu ni vitendo zaidiTofauti na yule, huyu mcha Mungu