DOKEZO Wenye Hospitali binafsi wakataa kuwahudumia wateja wa NHIF kutokana na vifurushi vipya

DOKEZO Wenye Hospitali binafsi wakataa kuwahudumia wateja wa NHIF kutokana na vifurushi vipya

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Aisee,
Mambo.haya yangekuwa yanawagusa na wao moja kwa moja wangeyafanyia kazi kwa haraka sana...... cha kufurahisha, wote wanaojadili haya, hawatumii NHIF, wao wanatumia Private na Premium packages.. so wakati hawa wanaweka mgomo sisi tunaendelea kudhoofishwa na maradhi.
 
Wewe unafikiri atakayeathirika ni nani,labda nikwambie athari itakayotokea wenye hospitali ndiyo wataathirika zaidi maana wengi wao kilichowasukuma kufungua hizo hospitali ni tamaa ya kupata utajiri wa haraka haraka kupitia NHIF japo wenyewe wanajifanya lengo lao ni kutoa huduma kwa wananchi na kwamba fedha sio kipaumbele chao lakini si kweli na kama wana jeuri wagome angalau kwa miezi sita tu kama hawajafunga hivyo vihospitali uchwara vya mchongo,haiwezekani huduma inayolipiwa kwenye hospitali za umma wao walipishe mara nne zaidi wakati hivyo vihospitali vyenyewe vingi havina maajabu.
Hawa watu ni wezi na inaonekana na wewe ni mmoja wao sasa safari hii muhesabu maumivu chaguo ni lenu ama mtoe huduma kwa bei halisi au mfunge hivyo vihospitali vyenu na kelele hizi zinapigwa sana na vile vihospitali vya uchochoroni siamini kwenye ujinga huu utawakuta hindu mandal,aghakhan au regency wao wanashurutishwa tu na huenda hata kutishiwa na hayo majizi.
Wewe utakuwa Chawa
 
Kwa hiyo sisi Waafrika tunaweza nini sasa, hata haya mambo ya bima tunashindwa kutengeneza sera na utaratibu unaokubalika kwa wadau wote, We cant solve our own problems and challenges.Mara kuna bima kwa wote, mara NHIF inakataliwa n.k.
Kwenye vitu physical kama miundo mbinu tumeshindwa na haya mambo ya policy tu, soft issues tunashindwa, shame on us
 
Nawaunga Mkono Mia fill 100..
Huwezi kuboresha kitita na ukaacha Kuboresha maslahi ya Watoa Huduma pamoja na Bidhaa husika na Baada ya kuambiwa bado unashupaza shingo..

Amoxyline iliyokuwa inalipwa kwa Bima miaka 10 iliyopita sh 80 kwa kidonge still bado baada ya miaka 10 bei ni hiyo.hiyo..Bila kuangalia Soko la Bidhaa la sasa unapanga bei bila huruma ya watu wenye Hospitali ambao wao hawaletewi dawa na MSD..
as one among the interested personel nasema wako sahihi na hatutapokea Mtu mwenye Bima Yoyote. Mpaka pale serikali itakapo thamini Mfumuko wa bei na maslahi ya pande mbili
Wasiokuwa na akili kichwani hawawezi kukuelewa na watakutafsiri wewe ni mkatili kumbe ukweli ni kwamba hawa watu walishafeli kitambo, hakuna Jambo lolote lile wanaloliweza.
 
Wewe unafikiri atakayeathirika ni nani,labda nikwambie athari itakayotokea wenye hospitali ndiyo wataathirika zaidi maana wengi wao kilichowasukuma kufungua hizo hospitali ni tamaa ya kupata utajiri wa haraka haraka kupitia NHIF japo wenyewe wanajifanya lengo lao ni kutoa huduma kwa wananchi na kwamba fedha sio kipaumbele chao lakini si kweli na kama wana jeuri wagome angalau kwa miezi sita tu kama hawajafunga hivyo vihospitali uchwara vya mchongo,haiwezekani huduma inayolipiwa kwenye hospitali za umma wao walipishe mara nne zaidi wakati hivyo vihospitali vyenyewe vingi havina maajabu.
Hawa watu ni wezi na inaonekana na wewe ni mmoja wao sasa safari hii muhesabu maumivu chaguo ni lenu ama mtoe huduma kwa bei halisi au mfunge hivyo vihospitali vyenu na kelele hizi zinapigwa sana na vile vihospitali vya uchochoroni siamini kwenye ujinga huu utawakuta hindu mandal,aghakhan au regency wao wanashurutishwa tu na huenda hata kutishiwa na hayo majizi.
Mungu akusamehe bure, hili siyo kosa lako, hapa ndio malengo ya CCM yametimia kuzalisha idadi ya raia wajinga na wapumbavu Kwa wingi kama wewe.
 
Kwa kweli tuombe Mungu atusaidie hawa Private hospitals na NHIF wafikie muafaka

Wagonjwa wenye Bima ya Afya ya NHIF wanataabika sana

Mungu wa Mbinguni utusaidie!
Unaona CCM mlivyokosa akili kichwani? Swala la utashi wa binadamu mnamuingiza Mungu? Mungu anahusika Vipi hapo na ujinga wenu na roho mbaya zenu?

Ipigwe marufuku kabisa viongozi kutibiwa nje ya nchi ndio watajuwa thamani ya huduma za afya.
 
Aiseee mbona kimeumana. Sasa hapo ni either cash au ndio kama ni mwanachama wa nssf utumie bima yake. Wao wanatumia bima za strategies huko nyie wenye nhif mpambane na hali zenu.
 
Muone huyu,
Usiwe mjinga kama mke wa Ayubu.
Waraka upon wazi kwamba wanaokataa kutoa huduma ni Umoja wa hospitali binafsi, mashirika ya dini na bakwata.
We waja na hoja ya vihospotali vya vichochoroni, kana kwamba kichochoroni pana nafasi ya kuweka hospitali.
Tatizo ni hivyo vihospitali binafsi hao wengine wanalazimishwa tu na huenda wanatishiwa kama watakubaliana na NHIF.
 
Aiseee mbona kimeumana. Sasa hapo ni either cash au ndio kama ni mwanachama wa nssf utumie bima yake. Wao wanatumia bima za strategies huko nyie wenye nhif mpambane na hali zenu.
Kuna taasisi walishaonaga hawa NHIF ni wapuuzi, rafiki yangu mke wake ni banker insurance yao wanatumia hiyo Strategies, sasa hivi ni mgonjwa kalazwa Agha khan huduma za viwango vya London.

Hilo liNHIF Agha Khan alipokelewi, labda kwenye vile viextention vya Agha khan polyclinic.
 
Kuna taasisi walishaonaga hawa NHIF ni wapuuzi, rafiki yangu mke wake ni banker insurance yao wanatumia hiyo Strategies, sasa hivi ni mgonjwa kalazwa Agha khan huduma za viwango vya London.

Hilo liNHIF Agha Khan alipokelewi, labda kwenye vile viextention vya Agha khan polyclinic.
Strategies ni bonge la bima. Halafu nhif nao wana bima tofauti. Wanayo bima ya viwango hiyo unatibiwa hata aghakhan ila kina najali sijui wezesha hizo zinakua na limits kuna magonjwa hutibiwi.
 
Umoja wa Watoa Huduma Sekta ya Binafsi APHTA, Mashirika ya Dini (CSSC), na Bakwata wanapenda kutaarifu umma kuwa mazungumzo yaliyokuwa yakifanyika baina ya umoja huo na Wizara ya Afya. Kamati ya Waziri na NHIF yameshindwa kupata muafaka katika suala zima la kitita cha bei mpya zilizopendekezwa na Wizara kupitia kamati iliyoundwa na Waziri.

Kwa kuwa Wizara pamoja na NHIF wameamua kudharau maagizo yaliyotolewa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ya namna bora ya kumaliza suala hilo na kuamua kutangaza kitita hicho bila maridhiano, basi umma unatangaziwa kuwa vituo binafsi vya huduma za afya vitashindwa kutoa huduma hizo kwa wanachama wa Mfuko huo kuanzia tarehe 1 mwezi Machi 2024.

Ili kuepuka usumbufu, wanachama wa NHIF wanaombwa kuwasiliana na Mfuko wapi wataweza kupata huduma hizo.

Suala la hili limekuja baada ya Wizara ya Afya kutoa barua ya kuendelea na vifurushi vyao kwenye barua iliyoandikwa 27/02/2024.

Barua ilisema "Hivyo, Mfuko unapenda kukufahamisha kuwa utatumia Kitita cha Mafao cha Mwaka 2023 kuanzia tarehe 01.03.2024. Vilevile, unafamishwa kuwa, orodha ya huduma na bei katika Kitita hicho zinapatikana katika ofisi zote za Mfuko, tovuti ya Mfuko na kupitia mfumo wa Service Porta/. Aidha, Mfuko utaendelea kupokea maoni, ushauri na mapendekezo mbalimbali yenye lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma bora za matibabu kwa wanufaika wake na kuendelea kuishauri Serikali ipasavyo."
View attachment 2918961
View attachment 2918951
Bima za Mchongo
 
Nadhani tungeangalia Kwanza Manufaa ya ya Maboresho haya kabla ya kuingia kwenye lawama na Migogoro.
Em kuwa serious basi..
Manufaa ya maboresho gani wakati unaambiwa kadi za NHIF hazitapokelewa hospitali zote za binafsi kuanzia kesho
(1 March, 2024)?!!
 
Mbona kuna hospitali nyingi tu za binafsi hasa za Wahindi huwa hazipokei wagonjwa wenye Bima za afya za NHiF tangu zamani?
Nahisi Wahindi walishaweka wizara husika mfukoni mwao
Hao wanaokataa na wafanye kama hao wahindi sijui kelele za nini kwanza kila hospital inaingia mkataba kivyake na NHIF kwahiyo anayetaka kufanya kazi na NHIF afanye anayekataa akatae.
 
Back
Top Bottom