Wito wangu kwa DGIS na Taasisi yako: Msipomtumia Tundu Lissu kupata Katiba Mpya na Bora sasa, mtajuta milele.

Wito wangu kwa DGIS na Taasisi yako: Msipomtumia Tundu Lissu kupata Katiba Mpya na Bora sasa, mtajuta milele.

Niseme tu, this guy is gifted. Tumshukuru sana Mungu kwa kutupa huyu mtu wakati huu. Tumshukuru Mungu kwa sababu hakuruhusu mtu huyu afe mwaka 2017 kwa sababu alijua kuna wakati tutamuhitaji.
Kuhusu Ubora wa TL sina ubishi kabisa.
 
Wito wangu kwenu. Mtumieni Tundu Lissu sasa, na hakikisheni anatumika vizuri kutupatia Katiba Mpya iliyo bora inayojenga mifumo imara itakayohakikisha Taifa hili kuwa imara hata miaka 500 ijayo.
100% perfect
 
Kwa speed anayokwenda nayo Mama Mashuguli, hii nchi inaelekea kubaya hasa.
 
Mngejua Rais wa nchi hii ana nguvu kias gani mngetulia tu.

Na nchi hii hakuna taasisi wala mtu binafsi anaweza fanya kitu ambacho yeye hajaridhia.
 
Tunajua sana. Na ndo mana tunashauri marekebisho ya Katiba ili kuiponya nchi na majanga yatakayoikumba huko mbeleni.
Mkuu unadhani DGIS anaweza fanya kitu kinyume na kiapo chake?

TL kuna makosa ya kimkakati alifanya yatamgharimu sana, saana...

Pengine hakudhamiria ila ameshayafanya..., pengine alidhani ni ngumu kupata nafasi aliyo nayo ila ameipata...

Hata zile siasa kali zilizompa umaarufu muda si mrefu zinaenda kukosa audance...

Unfortunate but true.
 
Naunga mkono hoja!!.🤝🙏🙏
 
Ki ukweli, mimi ni mwana CCM, lakini Lissu ana uwezo na uzalendo mkubwa sana.
Nashauri DGIS afanye haraka kufanya mpango ili tunusuru Taifa letu pendwa.
Mungu Ibarki Tanzania.
 
Atumiwe mara ngapi?

Unadhani uamuzi wa kuchukua fomu kumchaklenge mkt aliutoa ndotoni?
 
Tapeli la kisiasa .Hana karma ya uongozi CHADEMA imekufa
images (1).jpeg
 
Lissu sio lazima awe Rais sasa lakini Lissu ni chaguo sahihi na ana uwezo wa kusukuma agenda ya mabadiliko ndani ya chama cha CHADEMA na Taifa hili. Lissu sasa tunamtegemea kuweka msingi mzuri na uongozi katika vuguvugu la kuanza kupiagania uhuru wa Tanganyika upya. Lissu anatakiwa aanzie pale alipokosea Nyerere ili nchi ipone na kuweza kuendelea kama nchi zingine.

Tundu Lissu ni mwanaharakati lakini mwanasheria mzuri na kwa maoni yangu angefaa zaidi kwenye mambo ya sheria,mambo ya utawala na ufuatiliaji. Kumpa urais, kuna hatari ya kumfunga mdomo kama ilivyo kwa Mwambukusi hivi sasa.

Vyama vya upinzani vitafute mtu yeyote mwenye uwezo na nia ya kulitumikia taifa hili akiwa na umri mdogo wa miaka 35-45 ndio agombee Urais. Kwa hakika ikifanyika hivyo nitatoka kwenda kupiga kura.... Otherwise: No reform, No election!!.
 
Back
Top Bottom