Wizara kuweka gharama za kulipia nguzo 1,2,3 = Tsh 27000/= linaleta kero kubwa, TANESCO hawana uwezo wa kufidia punguzo hilo

Acha uongo wako wewe!

Umeme wa 27,000 ni wa REA ambao gharama zake zinabebwa na selikali!

Sehemu ambayo hukuna mradi wa REA ukitaka umeme na nguzo laki 5 inakuhusu.
Tunacholipia ni service line cost
Hiyo haikwepeki,lazima ulipe
Sasa sijui watu wanataka waunganishiwe bure

Ova
 
Mama aione hii!

Viongozi wetu badala ya kufanya kazi kisayansi wanafanya kazi kisiasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tanesco wana toa huduma ya kibiashara, wana takiwa wapeleke huduma kwenye makazi. Watu walipie huduma ya umeme na sio miundo mbinu. Nchi nyingi ndivyo wanavyo fanya.
Maana wewe ukilipia nguzo kumi, akitokea jirani yako ana taka umeme kwenye hizo nguzo, tanesco haimlipixi, na wewe hupewi fidia, bali tanesco husema miundo mbinu ni yao na sio wewe ulie lipia.
 
Acha uongo wako wewe!

Umeme wa 27,000 ni wa REA ambao gharama zake zinabebwa na selikali!

Sehemu ambayo hukuna mradi wa REA ukitaka umeme na nguzo laki 5 inakuhusu.
Wamepunguza bei ya service lines zote, ni sh 27,000
 
Acha uongo wako wewe!

Umeme wa 27,000 ni wa REA ambao gharama zake zinabebwa na selikali!

Sehemu ambayo hukuna mradi wa REA ukitaka umeme na nguzo laki 5 inakuhusu.
Hujui kitu , kakojoe ukalale
 
Mnaosema huduma iwe bure hamjui jinsi ilivyongumu kupata umeme tanesco kwa hiyo 27000/=, ni Bora ulipie million 1 upate umeme ndani ya mwezi kuliko kulipia 27000 uupate baada ya miaka miwili,

Mkuu umeongea ukweli kabsa, tanesco kila kitu ni rushwa tu. Watu wanakaaa miaka zaidi ya mitatu na wameshalipia kila kitu na huduma hapati.
 
Kwanini useme gharama ya kulipia nguzo? Kwani TANESCO wanauza nguzo?
Nadhani hapa unatakiwa useme gharama ya kuweka umeme labda mita hadi 70 au mpaka 120. Umbali wa mita 70 ndio utakuwa na nguzo 1 itahitajika ili ku support kwakuwa span moja si zaidi ya mita 50.
Ukiwa na umbali wa mita 120 hapo maana yake span ni 2 na nguzo zitakazohitajika ni 2.
Hiyo huduma ya kuvuta umeme (Service Line) haizidi mita 120. Ikizidi huo unakuwa ni mradi.
Kwahiyo mleta mada uelewe kwamba TANESCO hawauzi nguzo mbali wanatoa huduma ya umeme kulingana na umbali. Kama wanauza nguzo basi leta na gharama za mita, waya, bolts, vikorokoro vingine, wafanyakazi na usafiri.
Nadhani umeelewa.
 
Hapo sawa sasa watu wakilipishwa gharama ya service line hadi kuwekea luku etc wanaona kero
Naona wadau wanataka demo

Ova
 
Hii ya 27,000 ni nzuri sana ila wamefanya haraka kuliingiza kwa sasa,wajiandae vizuri then waliingize ili kuona ufanisi wake.Wanachotakiwa walifanye hili zoezi kwa phase wakishakaa vizuri ndio lisambae nchi zima,kwasasa ibakie kwa REA tu kama ilivyokuwa awali...
 
Nijuavyo ni kuwa bado shirika linatoa huduma kama inavyotakiwa mfano sehemu ikiwa potential kwa TANESCO huwa wanapeleka mradi na hii ndio kawaida, hapo mteja hatalipia nguzo bali ile gharama ya kuunganishwa tu. Tatizo kwa sasa maeneo yenye sifa hizi ni machache hivyo haionekani sana japo miradi ipo.Sasa maeneo mengi yamefikiwa kinachofanyika yaani demand kubwa ni hitaji la mtu mmoja mmoja kuomba kuunganishwa sasa hapo ndio utaratibu ukawekwa wa kuangalia umbali kutoka kwa mteja hadi nguzo ilipo.Hii ndio inaonekana inaleta malalamiko yote hayo
 
Unataka kutuambia kuwa mpaka leo Tanesco haina mtaji? Hivi hujui kwamba mteja anapohitaji huduma kwenu mnapaswa kumletea huduma alafu umchaji gharama za huduma? Thamani ya shilingi 177,000/= hailingani na gharama atakazolipa mteja kwa Tanesco kipindi chote cha maisha na uwepo wa dunia. Tanesco imewahi kuuza nguzo shilingi milioni moja laki mbili lakini hapajawahi kuwa na huduma nzuri zaidi ubabaishaji tu.
Kwa kuwa wewe uko kwenye tarrif ya Tanesco ya kupewa umeme bure mpaka utakapostaafu basi unaona sawa tu. Unaniuzia nguzo leo, kesho jirani anakuja kuomba umeme naye anachajiwa nguzo na nguzo inayotumika ni ile ya kwangu, akija wa tatu na nne wote unawaunganisha hapo kwangu.
Endeleeni kupiga siasa mitandaoni na mwisho wa siku umeme mtatuletea tu
 
Hapo sawa sasa watu wakilipishwa gharama ya service line hadi kuwekea luku etc wanaona kero
Naona wadau wanataka demo

Ova
Demo sio mbaya.
Ila tatizo uelewa wa watu. Hivi huduma ya maji imakaaje. Jinsi unavyokuwa mbali si ndivyo gharama za bomba zinaongezeka.
 

Nguzo si zao kwani nikihama nahama nazo na wengine pia wanaungwa hapo hapo.
 
Hakuna gharama za kulipia nguzo. Ukilipia nguzo maana yake upewe nguzo tu na usipate umeme. Sema gharama za kuwekewa umeme ndani ya mita 70 mpaka 120.
 
Serikali iko sawa mteja kuchangia 27000 Kwanza ingepaswa kupewa Bure kwani kwa kumuwekea umeme tayari watakua wameweka kidaka uchumi kwa mda mrefu na hiyo nguzo ni Mali ya tanesco wanamamlaka nayo kumfungia yeyote kumlazimisha mteja kuinunua wakati hatakua na umiliki nayo ni kumuibia sawa kabisa serikali Tena use bure
 
Hujui kitu , kakojoe ukalale
Wewe ni mjinga na inaonekana bado unakaa kwa wazazi wako!

Umeme wa REA ndio unatoa 27,000 lakini lazima mradi ukukute ndio unatoa hiyo 27,
Mradi ukipita itakulazimu kulipa gharama za kawaida.

Ukitaka kufungiwa umeme kama huhitaji nguzo unalipa 325,000
Kama unahitaji na nguzo itabidi uongeze hela ifike laki 5

Haya leta wewe sasa mchanganuo wa gharama za tanesco
 
Demo sio mbaya.
Ila tatizo uelewa wa watu. Hivi huduma ya maji imakaaje. Jinsi unavyokuwa mbali si ndivyo gharama za bomba zinaongezeka.
Ndiyo,unavyokuwa mbali ndy gharama inaongezeka

Ova
 
Watu uelewa kidogo shida

Ova
 
Tanesco haizalishi nguzo na yenyewe inanunua gharama ya nguzo ni kubwa sana hiyo bei mnayoona ni very fair
 
Tena mteja kulipa 27,000 bado ni nyingi kwa sababu atawalipa umeme wenu maisha yake yote. Ilitakiwa umeme ufungwe bure
Hata hiyo 27,000/- bado ni wizi kwa sababu huwezi niuzia kitu halafu bado kibaki kuwa mali yako, TANESCO hapa muangalie upya mifumo yenu vinginevyo nguzo iwe ni huduma ya bure igharamiwe na tanesco wenyewe.
 
Tanesco haizalishi nguzo na yenyewe inanunua gharama ya nguzo ni kubwa sana hiyo bei mnayoona ni very fair
Nguzo Tanesco inauza ghari sana na zinatoka mufundi tu hapo kumbuka kuna miaka nguzo ilifika hadi laki saba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…