Wizara kuweka gharama za kulipia nguzo 1,2,3 = Tsh 27000/= linaleta kero kubwa, TANESCO hawana uwezo wa kufidia punguzo hilo

Wizara kuweka gharama za kulipia nguzo 1,2,3 = Tsh 27000/= linaleta kero kubwa, TANESCO hawana uwezo wa kufidia punguzo hilo

Sawa, sekta binafsi waruhusiwe sasa.

Tatizo lilipo hapa sio kulipia, tatizo ni watu wanalipia umeme halafu wanasubiri mwaka mzima kuunganishwa huo umeme.Urasimu wa aina hiyo hauwezi kutokea kama kampuni binafsi ingekuwa inasambaza umeme.
Inategemea na speed ya yako na unavyo wapush....ukishalipia kabla ya siku 30 wanakuja
Kukuingizia umeme,
Sema tatizo ndy hapo kwenye uzito

Ova
 
Iundwe tume ya nishati au tanesco iwe chini ya ofisi ya Rais
Sikubaliani na wewe ktk hili tu. Kwani suluhisho haliwezi kupatikana pasipo kuunda kikundi cha walaji (tume)?

Tanesco haina hela halafu tuunde tume itakayotumia hela ambazo hazipo. Tunaongeza tatizo.
Quote Reply
 
Wizara ya Nishati umeshindwa kutatua kero za kuunga umeme kwa wananchi na badala yake imezidisha ugumu wa kupata huduma ya umeme hasa kwa wateja Wanahitaji nguzo 1,2,3,4,5,6,7,8,9, Hadi kumi.

Wizara ilitoa sharti gumu kwa TANESCO inayojiendesha kihasara kupunguza gharama za umeme wa nguzo na kufanya zote ziwe 27,000/= yaani mtu atalipia nguzo moja 27000 badala ya 177000/= nguzo mbili atalipia 27000/= badala ya 385000 na hata mtu akitaka nguzo 10 atalipia 27000/=
Maelekezo hayo ni hatua nzuri kwa machoni kwa wengi lakini kiukweli watu Wana zaidi ya mwaka mmoja hawajaungiwa umeme na wamelipia nguzo 27000. Kiuhalisia TANESCO hawana bajeti ya kulipia hizo nguzo, hivyo wananchi wengi kukosa umeme.

Ukitaka kulipia gharama halisi tanesco hawataki wanaogopa kufukuzwa kazi lakini hapo hapo mteja hapati huduma.

TANESCO wanadai walilazimishwa na serikali kuwalipisha watu 27000, Ila wao hawakuridhia, hivyo kwao ni sawa wananchi kuendelea kukosa umeme. Naamini serikali itatatua shida hii na kuacha kuitwika tanesco mizigo na lawama

Umetoa dukuduku lako, japo linajibika kirahisi sana kwa kujibu maswali yafuatayo...;

1. Huduma ya kusambaza nishati ya umeme ni jukumu la nani?

JIBU: Obviously, ni la serikali na TANESCO ni wakala wa serikali tu ktk kutoa huduma hiyo..

2. Ni nani katoa agizo la kila mwananchi mwenye kuhitaji kuunganishwa na huduma ya nishati ya umeme alipie Tshs. 27,000 bila kujali anahitaji nguzo 1,2,3,4 nk au la?

JIBU: Mtoa huduma ambaye ni SERIKALI na kumtaka wakala wake atii na kufuata maelekezo hayo...

3. Kama haya mambo yako hivyo, shida ya TANESCO na msingi wa malalamiko yao ni nini hasa?

JIBU: Kwa maoni yangu, msingi wa malalamiko ya TANESCO uko ktk hoja hizi:

å MOSI, TANESCO kupitia watumishi wake walikuwa wananufaika na gharama hizi kwa njia moja au nyingine. Biashara yao hii ya faida kubwa kwao binafsi imekuwa "shaken", sasa wanalia na kutafuta sympathy kwa umma tuone kuwa serikali inakurupuka ktk kutoa muelekeo wa utendaji kazi wa TANESCO...

Swali kubwa linabaki kuwa hili;

Kwamba, serikali ambayo ndiyo mtoa huduma ya nishati hii kwa wananchi wake inawezaje kutoa maagizo ya kujichanganya na kujipinga yenyewe..?

å PILI, kama nilivyosema kuwa kuwa TANESCO ni shirika la umma (serikali) lenye jukumu la kutoa huduma ya nishati ya umeme kwa wananchi wote. Kwa 100% linaitegemea serikali kujiendesha ili litoe huduma hii. Hoja ya fidia ya gharama ya nguzo inatoka wapi? Kwani mwenye TANESCO hakujua kuwa kwa kushusha gharama ya uunganishaji umeme kutahitajika fedha zaidi kwa TANESCO..??

Kama tatizo ni "UHABA WA NGUZO" ndiyo unawapelekea mshindwe kutoa huduma hii kwa wananchi kwa gharama ya Tshs. 27,000 kwa kila mteja, kwanini TANESCO isitoe taarifa kwa mwenye fedha na shirika ambayo ni serikali yenyewe ili iongeze/ifidie bajeti hii kama kweli mnachokilalamikia ni cha kweli..?

Kama TANESCO mmeshaiambia serikali juu kufidia gharama hizi ambazo kabla zilikuwa zinalipwa/zinabebwa na mteja na imekataa (kitu ambacho mimi siamini), basi leteni kama hoja ili tuijadili kupitia platforms mbalimbali...

Kumbukeni sauti ya umma (wananchi) ndizo zenye nguvu kuliko serikali maana serikali tumeiweka sisi wananchi...!!
 
Jamani tanesco hatuwaelewi kama wanadanya biashara au ni huduma ya kijamii? Ukilipia 27000 kufungiwa umeme utasubili sana mpaka unachoka,tunaomba serikali iweje ushindani kwenye umeme,kama ilivyo kwenye kampeni za simu na vingamuzi.
 
Hilo shirika Ni mzigo tu...nawaza tu ...ingependeza LIKABINAFSISHWA...maana hakuna namna Sasa!!!ah!
Hebu jaribu kumbinafsisha mkeo kwanza ndo ujue madhara ya kubinafsisha... watu msio na shukrani. Ukisikia kuandika unaandika chochote tu. Acha uvivu wa kufikiri na mawazo mgando.
 
Jamani tanesco hatuwaelewi kama wanadanya biashara au ni huduma ya kijamii? Ukilipia 27000 kufungiwa umeme utasubili sana mpaka unachoka,tunaomba serikali iweje ushindani kwenye umeme,kama ilivyo kwenye kampeni za simu na vingamuzi.
Hiyo27000 REA iko vijijini mzee
Gharama ya maeneo ya mijini inategemea na umbali kutokea kwako mpk kwenye nguzo
Ndomana surveyor akija a nakupigia hesabu
Gharama ukatayolipa

Ova
 
Hebu jaribu kumbinafsisha mkeo kwanza ndo ujue madhara ya kubinafsisha... watu msio na shukrani. Ukisikia kuandika unaandika chochote tu. Acha uvivu wa kufikiri na mawazo mgando.
Wabongo wanataka waingiziwe umeme bure

Ova
 
Wizara ya Nishati umeshindwa kutatua kero za kuunga umeme kwa wananchi na badala yake imezidisha ugumu wa kupata huduma ya umeme hasa kwa wateja Wanahitaji nguzo 1,2,3,4,5,6,7,8,9, Hadi kumi.

Wizara ilitoa sharti gumu kwa TANESCO inayojiendesha kihasara kupunguza gharama za umeme wa nguzo na kufanya zote ziwe 27,000/= yaani mtu atalipia nguzo moja 27000 badala ya 177000/= nguzo mbili atalipia 27000/= badala ya 385000 na hata mtu akitaka nguzo 10 atalipia 27000/=
Maelekezo hayo ni hatua nzuri kwa machoni kwa wengi lakini kiukweli watu Wana zaidi ya mwaka mmoja hawajaungiwa umeme na wamelipia nguzo 27000. Kiuhalisia TANESCO hawana bajeti ya kulipia hizo nguzo, hivyo wananchi wengi kukosa umeme.

Ukitaka kulipia gharama halisi tanesco hawataki wanaogopa kufukuzwa kazi lakini hapo hapo mteja hapati huduma.

TANESCO wanadai walilazimishwa na serikali kuwalipisha watu 27000, Ila wao hawakuridhia, hivyo kwao ni sawa wananchi kuendelea kukosa umeme. Naamini serikali itatatua shida hii na kuacha kuitwika tanesco mizigo na lawama
Mawazo mfu kabisa haya! Hujui kuwa kuanzia mitambo hadi kwenye mita ni mali ya tanesco. Yaani unapendekeza tuibiwe zaidi! Mbona nguzo ikioza au kuangushwa na upepo hawakudai ulipie ili waweke nguzo mpya?

Kama hawana mtaji waombe serikalini, mbona tuko uchumi wa kati!
 
Ukinunua LUKU kuna percent unakatwa kwa ajili ya REA, pia kuna hela zinatolewa na wafadhili kwa ajili ya REA.

Au wewe unahisi hela za umeme wa REA anatoa nani?
Sasa kama hivyo ndivyo, huoni hata hiyo 27,000/= ni dhuluma kwa mwananchi kutoa?

Tuambiwe mwisho wa kuichangia REA ni lini? Lazima kuwe na mwanzo mpaka mwisho, lini wanadhani adhma yao ya kusambaza umeme vijiji vyote itakuwa imetimia/kamilika? Je, watafuta hiyo tozo baada ya kukamilisha hilo?
 
Wizara ya Nishati umeshindwa kutatua kero za kuunga umeme kwa wananchi na badala yake imezidisha ugumu wa kupata huduma ya umeme hasa kwa wateja Wanahitaji nguzo 1,2,3,4,5,6,7,8,9, Hadi kumi.

Wizara ilitoa sharti gumu kwa TANESCO inayojiendesha kihasara kupunguza gharama za umeme wa nguzo na kufanya zote ziwe 27,000/= yaani mtu atalipia nguzo moja 27000 badala ya 177000/= nguzo mbili atalipia 27000/= badala ya 385000 na hata mtu akitaka nguzo 10 atalipia 27000/=
Maelekezo hayo ni hatua nzuri kwa machoni kwa wengi lakini kiukweli watu Wana zaidi ya mwaka mmoja hawajaungiwa umeme na wamelipia nguzo 27000. Kiuhalisia TANESCO hawana bajeti ya kulipia hizo nguzo, hivyo wananchi wengi kukosa umeme.

Ukitaka kulipia gharama halisi tanesco hawataki wanaogopa kufukuzwa kazi lakini hapo hapo mteja hapati huduma.

TANESCO wanadai walilazimishwa na serikali kuwalipisha watu 27000, Ila wao hawakuridhia, hivyo kwao ni sawa wananchi kuendelea kukosa umeme. Naamini serikali itatatua shida hii na kuacha kuitwika tanesco mizigo na lawama
Hizo nguzo ni uwekezaji kwa TANESCO wasibebeshe wateja mzigo kwani wanapopata wateja wengine na kuwaunga kwenye nguzo zilizolipiwa na wateja huwa wanawapa gawio? Je faida waliyopata enzi zile wanauza nguzo kwa wateja ilienda wapi?
 
Ushauri serikali ijikite kuzalisha umeme kwenye mabwawa, umeme wa jua, umeme wa upepo , umeme wa gesi iuzie kampuni binafsi na hizo binafsi zisambaze umeme kwa wateja kwa masharti kwamba eneo moja linaweza kuhudumiwa na kampuni zaidi ya Tatu , itapelekea kuwa na ushindani wa kutoa huduma .
Hizo kampuni binafsi haziwezi kuzalisha umeme wake?
 
Back
Top Bottom