Wizara ya Afya yamtafuta mtaalamu aliyefumua jeraha la mgonjwa baada ya kushindwa kulipa hela

Wizara ya Afya yamtafuta mtaalamu aliyefumua jeraha la mgonjwa baada ya kushindwa kulipa hela

Kilichonishangaza zaidi ni huyo mgonjwa kuachwa kajilaza chini na huku wakubwa wanamjadili utafikiri kama ni ng’ombe na sio binadamu

Najua wengi hawalioni hili kwa sababu wamezoeshwa udhalilishaji
Yaani badala ya huyo anaejinasibu zaidi ya mara 10 kuwa wao ndio wakubwa
Ameshindwa kutumia busara na kusema aondolewe hapo na awekwe hata sehemu safi
Au mimi ndio mkorofi
 
Ndio muone ccm walipotufikisha kutwa kujigamba tumerejesha nidhamu kwa watumishi hyo nidhamu ndo Hadi kukosa utu? Ccm mtayalipa haya yote ikiwemo ugaidi was Jada wenu Hamza.
 
Bila kulipa hiyo hela, daktari angekatwa mshahara au posho yake, kinachoendelea kwenye vituo vya afya kuhusu ukusanyaji wa mapato, audits za fedha, dawa na huduma kimewafanya watumishi waone hakuna haja tena ya kuheshimu utu na kuwa na huruma wala busara maana ukifanya hivyo unaitwa mwizi wa dawa au fedha za umma, taratibu za kupata msamaha wa matibabu kwa mtu asiye na uwezo zimekuwa ngumu mno sawa na kusema tu misamaha hakuna maana mpaka unakamilisha kupata msamaha kama ni mgonjwa sana ndugu yako atakuwa mbele za haki, mtumishi akijaribu kupindisha taratibu akatoa msamaha haraka ataitwa mwizi na atalipa mwenyewe fedha hizo. Roho mbaya ya watumishi wa afya inayosemwa siyo ya kuzaliwa nayo, imetengenezwa na mfumo wenye negative attitude na watumishi wa afya nchini, hivyo system hiyohiyo inao uwezo wa kuiondoa kwa kubadili attitude hiyo, ni lini jambo zuri lililofanywa na watumishi wa afya limeongelewa? Wao hufanya mabaya kila siku? Ukiyatukana Maji kwenye glass yakikukwama usilalamike, hii ni nature, ndivyo ilivyo, inakupa unachotia. Kusema haya sio kwamba naunga mkono tendo baya alilofanya huyo ndugu au matendo mengine maovu, hapana, najaribu kuonesha wapi tulipojikwaa badala ya kulaumu tulikoangukia.
Hili limeanza limeanza baada huyu waziri wa afya wa sasa kuwa katibu mkuu tamisemi akishughulikia afya.
 
Wizara ya Afya imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa hii inayozunguka mitandaoni kuwa, mtaalamu wa Afya katika kituo ambacho bado hakijatambuliwa amemshona mgonjwa jeraha kisha akalifumua kwa madai kuwa mgonjwa huyo hakuweza kulipia gharama. Ikiwa hili limetokea nchini Tanzania, basi ni ukiukwaji mkubwa wa huduma za kitabibu. Hivyo, wizara inaomba wenye taarifa za wapi huku au kituo gani wawasilishe mara moja kwa namba ya huduma kea mteja 199 ya wizara ya afya au watume ujumbe mfupi kwenye namba ya waziri wa Afya ya 0734124191.

View attachment 1923425

IMG-20210904-WA0077.jpg
 
Wizara ya Afya imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa hii inayozunguka mitandaoni kuwa, mtaalamu wa Afya katika kituo ambacho bado hakijatambuliwa amemshona mgonjwa jeraha kisha akalifumua kwa madai kuwa mgonjwa huyo hakuweza kulipia gharama. Ikiwa hili limetokea nchini Tanzania, basi ni ukiukwaji mkubwa wa huduma za kitabibu. Hivyo, wizara inaomba wenye taarifa za wapi huku au kituo gani wawasilishe mara moja kwa namba ya huduma kea mteja 199 ya wizara ya afya au watume ujumbe mfupi kwenye namba ya waziri wa Afya ya 0734124191.

View attachment 1923425

AMEKIUKA MIIKO YA UDAKTARI Tukio hili lilitokea Mwezi Julai, 2021 na mtumishi aliyekiuka miiko ya Udaktari anaitwa Jackson Meli ni Clinical Officer wa Kituo cha Afya Kerenge Tarafa ya Magoma, Halmashauri ya Wilaya ya korogwe Mkoani Tanga. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ameshachukua hatua kwa kumsimamisha kazi na amempa Hati ya Mashtaka na pia ameshafikishwa kwenye Baraza la Taaluma ili achukuliwe hatua stahiki kwa kwenda Kinyume na Miiko ya Taaluma ya Udakrari. Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Ofisi ya Rais - TAMISEMI 04.09.2022
 
SubhanAllah, daa hata kiofu kidogo kabis hakikua ndani mwake?
 
Tozo na kukaa na maiti watu hawana hela kuna tofauti gani wanatafuta video wakati wenyewe ni video tosha...
 
Watanzania na frustrations ni sawa na uji na mgonjwa..

Maisha yamekuwa magumu sana chini ya CCM..
 
hio wizara ya Afya kama wangekuwa wanawalipa hao watumishi vizuri yasingetokea hayo, lazima ijitathmini....kuna mambo ya kipuuzi mengi yana go unreported..
 
Aise kumbe ni korogwe tu hapo kwa watani zangu, wapare nyie ndo maana mnanunua uchawi kumbe roho zenu ni mbaya hivyo, aibu
 
Watu ni wengi ila binadamu ni wachache, aliyefanya huo unyama ana cheti cha kuchonga, hakusomea hiyo fani. Angejua maadili hangefanya hivyo. Namlaani kwa nguvu zote.
 
Nimemsikiliza huyo kiongozi kaongea kwa utu na busara sana kwamba huyo mama kupata hio ajali ni dharura,je kuna mtu huwa anajiandaa na ajali au dharura?

Hivi huyo daktari unawezaje kufanya unyama kama huu?

Na alivyo na roho Chafu,Huyu hata akipewa dili la kuiba vitovu vya watoto hapo kituoni anafanya huyu
Muache mihemko

Msikilize na madai ya muhusika


Asipolipa mgonjwa muhudumu atalipia yeye
Mbona majeneza mnanunua? Yani mtu akuhudumie halafu ghalama azilipe yeye?
 
Back
Top Bottom