Black Sniper
JF-Expert Member
- Dec 10, 2013
- 32,406
- 55,148
Hili limeanza limeanza baada huyu waziri wa afya wa sasa kuwa katibu mkuu tamisemi akishughulikia afya.Bila kulipa hiyo hela, daktari angekatwa mshahara au posho yake, kinachoendelea kwenye vituo vya afya kuhusu ukusanyaji wa mapato, audits za fedha, dawa na huduma kimewafanya watumishi waone hakuna haja tena ya kuheshimu utu na kuwa na huruma wala busara maana ukifanya hivyo unaitwa mwizi wa dawa au fedha za umma, taratibu za kupata msamaha wa matibabu kwa mtu asiye na uwezo zimekuwa ngumu mno sawa na kusema tu misamaha hakuna maana mpaka unakamilisha kupata msamaha kama ni mgonjwa sana ndugu yako atakuwa mbele za haki, mtumishi akijaribu kupindisha taratibu akatoa msamaha haraka ataitwa mwizi na atalipa mwenyewe fedha hizo. Roho mbaya ya watumishi wa afya inayosemwa siyo ya kuzaliwa nayo, imetengenezwa na mfumo wenye negative attitude na watumishi wa afya nchini, hivyo system hiyohiyo inao uwezo wa kuiondoa kwa kubadili attitude hiyo, ni lini jambo zuri lililofanywa na watumishi wa afya limeongelewa? Wao hufanya mabaya kila siku? Ukiyatukana Maji kwenye glass yakikukwama usilalamike, hii ni nature, ndivyo ilivyo, inakupa unachotia. Kusema haya sio kwamba naunga mkono tendo baya alilofanya huyo ndugu au matendo mengine maovu, hapana, najaribu kuonesha wapi tulipojikwaa badala ya kulaumu tulikoangukia.
Wizara ya Afya imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa hii inayozunguka mitandaoni kuwa, mtaalamu wa Afya katika kituo ambacho bado hakijatambuliwa amemshona mgonjwa jeraha kisha akalifumua kwa madai kuwa mgonjwa huyo hakuweza kulipia gharama. Ikiwa hili limetokea nchini Tanzania, basi ni ukiukwaji mkubwa wa huduma za kitabibu. Hivyo, wizara inaomba wenye taarifa za wapi huku au kituo gani wawasilishe mara moja kwa namba ya huduma kea mteja 199 ya wizara ya afya au watume ujumbe mfupi kwenye namba ya waziri wa Afya ya 0734124191.
View attachment 1923425
Wizara ya Afya imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa hii inayozunguka mitandaoni kuwa, mtaalamu wa Afya katika kituo ambacho bado hakijatambuliwa amemshona mgonjwa jeraha kisha akalifumua kwa madai kuwa mgonjwa huyo hakuweza kulipia gharama. Ikiwa hili limetokea nchini Tanzania, basi ni ukiukwaji mkubwa wa huduma za kitabibu. Hivyo, wizara inaomba wenye taarifa za wapi huku au kituo gani wawasilishe mara moja kwa namba ya huduma kea mteja 199 ya wizara ya afya au watume ujumbe mfupi kwenye namba ya waziri wa Afya ya 0734124191.
View attachment 1923425
Hospitali ya Marangu ni ya Kanisa hawawezi kufanya huo upuuziItakuwa Marangu hiyo!
Kwani huyo kapasuliwa kimakosaUpumbavu wa enzi za JK wa watu kupasuliwa vichwa badala ya miguu umeanza kurudi tena,
Mahakamani atashinda kesiHuyu bwege afukuzwe hicho kibarua aje kitaa atatia akili
Tatizo hatutaki kuambiana ukweli kwamba shetani ni mtu ila vita siyo kimwili nikupambana naye kwa nguvu za kiroho.Tanzania hii imezaliwa tena siyo ile yetu
Muache mihemkoNimemsikiliza huyo kiongozi kaongea kwa utu na busara sana kwamba huyo mama kupata hio ajali ni dharura,je kuna mtu huwa anajiandaa na ajali au dharura?
Hivi huyo daktari unawezaje kufanya unyama kama huu?
Na alivyo na roho Chafu,Huyu hata akipewa dili la kuiba vitovu vya watoto hapo kituoni anafanya huyu