binti kiziwi
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 11,201
- 28,642
Wanasheria wa JF mmeingia mitini, njooni huku mjadili mambo ya kisheria na mwakilishi wa wizara juu sisi tunaamini ninyi mnafahamu vingi kuliko sisi tusio wana sheria.
Swali kwa Wizara: Ni lini wizara itashirikiana na Social workers kutoa elimu kwa umma juu ya haki za raia wa Tanzania? sababu ni ukweli ulio wazi kuwa raia wengi wa Tanzania hawafahamu haki zao, hata wakionewa hawafahamu wafuate mchakato gani ili kupata haki zao, mimi nashauri zifanyike kampeni (advocacy) juu ya elimu kwa raia kuhusiana na haki zao za msingi kama binadamu na kama raia wa nchi hii.
Swali namba mbili: Wizara inamchukuliaje mfungwa wa Tanzania aliyeko gerezani? Ninyi mnaona wafungwa wanatendewa haki huko gerezani? Hali ya magereza yetu ikoje kuweza kumu-accomodate mfungwa ambaye anatambulika kuwa na haki kama binadamu wengine? Je, Magereza yetu yameundwa ili yarekebishe tabia au yanachochea kuharibu tabia ya wale wanaopelekwa kule? Kisheria nini kinafanyika ili wafungwa wahakikishiwe wanakingwa katika mwamvuli wa haki za binadamu. Ahsante.
Swali kwa Wizara: Ni lini wizara itashirikiana na Social workers kutoa elimu kwa umma juu ya haki za raia wa Tanzania? sababu ni ukweli ulio wazi kuwa raia wengi wa Tanzania hawafahamu haki zao, hata wakionewa hawafahamu wafuate mchakato gani ili kupata haki zao, mimi nashauri zifanyike kampeni (advocacy) juu ya elimu kwa raia kuhusiana na haki zao za msingi kama binadamu na kama raia wa nchi hii.
Swali namba mbili: Wizara inamchukuliaje mfungwa wa Tanzania aliyeko gerezani? Ninyi mnaona wafungwa wanatendewa haki huko gerezani? Hali ya magereza yetu ikoje kuweza kumu-accomodate mfungwa ambaye anatambulika kuwa na haki kama binadamu wengine? Je, Magereza yetu yameundwa ili yarekebishe tabia au yanachochea kuharibu tabia ya wale wanaopelekwa kule? Kisheria nini kinafanyika ili wafungwa wahakikishiwe wanakingwa katika mwamvuli wa haki za binadamu. Ahsante.