Wizara ya Katiba na Sheria Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na ushauri

Wizara ya Katiba na Sheria Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na ushauri

Sheria ya mafao kwa mtu aliyeachishwa kazi ni sheria inayobagua..
Swali zuri.

Sheria hii ilizingatia kwamba aliye na taaluma anayo nafasi kubwa ya kuajiriwa tena kutokana na taaluma yake, hivyo bado akawa anaendelea kujazia akiba yake hadi atakapostaafu, tofauti na asiye na taaluma.

Hizi asilimia 33 ni za kumpa unafuu wa kujikimu wakati akifuatilia kazi nyingine.

Asante.
 
Taarifa ndio hiyo sasa, mahakama za mwanzo wakishirikiana na watendaji wa kata na vijiji wanatesa watu kisa hawana fedha za kuchangia ujenzi wa madarasa,wazazi wetu wameanza kuiona nchi hii ni chungu kweli kama alivyotabiri mgombea mmoja hivi wakati wa uchaguzi 2020.
Chaajabu,mzee wa miaka 70 bado mnakurupushana nae achangie maendeleo!!!

Asante kwa taarifa. Tutafuatilia suala hili kwa undani.

Kimsingi, Mahakama zote zinatakiwa kusimamia sheria, endapo itabainika kuna watumishi na watendaji wanatenda kinyume na sheria watachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa sheria.
 
Tumeshuhudia watendaji wa serikali wakitoa adhabu za viboko kwa watu waliowaona ni wakosaji(mwenye mamlaka ya kusema mtu amekosea ni mahakama tu)...
Hili jambo lilishatolewa ufafanuzi na serikali.

Hakuna sheria inayoruhusu watendaji wa serikali kutoa adabu ya viboko kwa mtu yeyote. Aliyefanyiwa hivyo, ana haki ya kwenda kufungua kesi dhidi ya viongozi hao.

Sisi kama wizara tunatoa wito kwa viongozi na watumishi wote wa umma, kufuata sheria katika utekelezaji wa majukumu yao.
 
Hili jambo lilishatolewa ufafanuzi na serikali.

Hakuna sheria inayoruhusu watendaji wa serikali kutoa adabu ya viboko kwa mtu yeyote. Aliyefanyiwa hivyo, ana haki ya kwenda kufungua kesi dhidi ya viongozi hao.

Sisi kama wizara tunatoa wito kwa viongozi na watumishi wote wa umma, kufuata sheria katika utekelezaji wa majukumu yao.
Kwanini bado nyie kama wizara hamu wachukuliii hatua zangu kisheria.?.wanao endelea na utamaduni huuu
 
Ni kwanini hadi leo swala la dhamana kwenye makosa ya dhamana imebaki kua ni hisani kutoka kwa polisi/hakimu?

Kwanini hadi leo hii watumishi wa uma (wana siasa),wakuu wa wilaya, mikoa wanaendelea kupiga watu bakora japo ni kinyume na katiba na sheria, na wizara mpo mpooo tuu kama haya wahusu vile?

Nasubiri majibu
 
Ni maoni mazuri. Hata hivyo, sheria inampa nafasi ya kufungua kesi ya madai ili kulipwa fidia. Ni haki yake kisheria na atapatiwa stahiki zake akifuata utaratibu huo.
Samahani naomba kuongezea nyama hapo kidogo hivi hapo unakuwa unamshitaki nani hasa aliyekukamata au jamhuri?
 
Ni kwanini hadi leo swala la dhamana kwenye makosa ya dhamana imebaki kua ni hisani kutoka kwa polisi/hakimu?...
Ndugu Mwanadome, asante kwa maswali mazuri.

Unaweza kufafanua zaidi swali lako kuhusu dhamana kuwa hisani?

Kuhusu watumishi wa umma kutoa adhabu ambazo zipo kinyume na sheria na maadili ya utumishi wa umma, tumeshafafanua katika majibu yetu yaliyopita.

Asante.
 
Ndugu Mwanadome, asante kwa maswali mazuri.

Unaweza kufafanua zaidi swali lako kuhusu dhamana kuwa hisani?

Kuhusu watumishi wa umma kutoa adhabu ambazo zipo kinyume na sheria na maadili ya utumishi wa umma, tumeshafafanua katika majibu yetu yaliyopita.

Asante.
Kwamba kosa lina dhaminika kisheria lakini polisi/mahakama hawatoi dhamana.

Tena bila sababu yoyote.
 
Kwanini sheria imekuwa kichaka cha kuumiza watu?

Mfano: Mtu anashitakiwa kwa uhujumu uchumi anakaa ndani miaka 4 kila siku upelelezi haujakamilika, kwanini msisubiri upelelezi ukamilike ndiyo akamatwe?

Mnaumiza watu sana na ni uonevu wa hovyo kabisa kuwahi kutokea.
 
Kwamba kosa lina dhaminika kisheria lakini polisi/mahakama hawatoi dhamana.

Tena bila sababu yoyote.

Kama kosa linadhaminika kisheria, basi huo ni utovu wa nidhamu wa baadhi ya watumishi na sio utaratibu wa kimahakama/kipolisi.

Unaweza kuripoti kwa ngazi husika ili hatua zichukuliwe kwa watumishi hao.

Asante.
 
Lingine muhimu ni hili, kwanini watuhumumiwa wanakaa mahabusu ya polisi bila kupelekwa mahakamani kwa muda mrefu zaidi ya ulio wekwa kisheria?

Hamuoni haya mambo yana igharimu nchi na kuvunja haki za raia na mnatengeneza mfumo sugu wa rushwa?
 
Kama kosa linadhaminika kisheria, basi huo ni utovu wa nidhamu wa baadhi ya watumishi na sio utaratibu wa kimahakama/kipolisi.

Unaweza kuripoti kwa ngazi husika ili hatua zichukuliwe kwa watumishi hao.

Asante.
Sasa nyie kama wizara mnayajua haya mpooo kimyaaa, mnafanya jitihada gani kukomesha haya? Kama wizara mnashindwa kulisimamia hili mimi mwananchi wa huku kaliua ndani ndani nawezaje katika hili?

Mfano: Kutoka wilayani kaliua ukiwa unaelekea mpanda,hadi unafika ugala umbali wa kilomita miamoja kuna kituo kimoja tuu cha polisi pale lumbe kilomita 60 kutoka kaliua mjini. Kwa mazingira haya huyu mwananchi anayefanyiwa hila na polisi wa huko una tegemea aripoti wapi?
 
Hii sheria ya Wizara ya Ardhi kutaka kila kiwanja kisome namba ya Nida ya mhusika mnaizunguziaje?

Hamuoni kama kuna wananchi watapoteza haki zao as asilimia kubwa ya wa-tz hawana Nida?

Inakuwaje kwa watu wa vijijini wasio na hati?
 
Hongereni sana kwa hatua hii nzuri, ombi langu tu pamoja na hongera hizo ni kwamba muutendee haki uzi huu, kwa kujibu maswali yote, kuyafanyia kazi yale ambayo inabidi muyafanyie kazi, na pia kwa KUTOA MREJESHO kuhusu yale ambayo mmeyafanyia kazi kutoka kwenye uzi huu (mnaweza kuwa na utaratibu, kwa mfano kila baada ya mwezi mmoja mnatoa mrejesho ya yale ambayo mmeyafanyia kazi kutoka uzi huu, na yamefikia wapi)-Hii ni muhimu sana, maana kusema tu kwamba, "tutalifanyia kazi" halafu imeishia hapo, inaweza isiwe inatusaidia sana sisi wananchi na wala nyie wenyewe.

Swali langu:
Mkoani Mbeya, wilaya ya Mbeya Mjini, kata ya Mwakibete, mtaa wa Shewa viongozi wa mtaa wamekua wakilazimisha wananchi wa mtaa huu kuchangia "kwa lazima" michango ya ujenzi wa shule. Hii imekua kero kubwa kiasi cha kufikia viongozi hawa kutishia wananchi ambao wameshindwa kuchangia mchango huo kuwa watawafunga.

Hii imekua ni kero kubwa sana, kwani wananchi wanakua harrased sana, na viongozi wanasisitiza kuwa ni MCHANGO WA LAZIMA KWA KILA MWANA-MTAA.

Nimeona kuwa watu wengine kadhaa kutoka mikoa mingine kwenye uzi huu huu wakilalamika pia kuhusu suala hili, na nimeona pia response yenu kuwa hamna taarifa juu ya hili. Ushauri wangu ni kwamba kwa sababu hili suala lipo, na wananchi wamelilalamikia sana, je kwa nini wizara isichukue hatua ya kulifanyia uchunguzi kidogo, kisha kutoa tamko kulaani vitisho hivyo na kutamka wazi kuwa hilo suala ni kinyume cha sheria? Hii itasaidia sana kuwakinga wananchi na uonevu unaoendelea huku mitaani na vijijini kuhusiana na hili la michango ya lazima ya shule?

Ahsante sana.

Wizara Katiba Na Sheria
 
Hongereni sana kwa hatua hii nzuri, ombi langu tu pamoja na hongera hizo ni kwamba muutendee haki uzi huu, kwa kujibu maswali yote, kuyafanyia kazi yale ambayo inabidi muyafanyie kazi, na pia kwa KUTOA MREJESHO kuhusu yale ambayo mmeyafanyia kazi kutoka kwenye uzi huu (mnaweza kuwa na utaratibu, kwa mfano kila baada ya mwezi mmoja mnatoa mrejesho ya yale ambayo mmeyafanyia kazi kutoka uzi huu, na yamefikia wapi)-Hii ni muhimu sana, maana kusema tu kwamba, "tutalifanyia kazi" halafu imeishia hapo, inaweza isiwe inatusaidia sana sisi wananchi na wala nyie wenyewe.

Swali langu:
Mkoani Mbeya, wilaya ya Mbeya Mjini, kata ya Mwakibete, mtaa wa Shewa viongozi wa mtaa wamekua wakilazimisha wananchi wa mtaa huu kuchangia "kwa lazima" michango ya ujenzi wa shule. Hii imekua kero kubwa kiasi cha kufikia viongozi hawa kutishia wananchi ambao wameshindwa kuchangia mchango huo kuwa watawafunga.

Hii imekua ni kero kubwa sana, kwani wananchi wanakua harrased sana, na viongozi wanasisitiza kuwa ni MCHANGO WA LAZIMA KWA KILA MWANA-MTAA.

Nimeona kuwa watu wengine kadhaa kutoka mikoa mingine kwenye uzi huu huu wakilalamika pia kuhusu suala hili, na nimeona pia response yenu kuwa hamna taarifa juu ya hili. Ushauri wangu ni kwamba kwa sababu hili suala lipo, na wananchi wamelilalamikia sana, je kwa nini wizara isichukue hatua ya kulifanyia uchunguzi kidogo, kisha kutoa tamko kulaani vitisho hivyo na kutamka wazi kuwa hilo suala ni kinyume cha sheria? Hii itasaidia sana kuwakinga wananchi na uonevu unaoendelea huku mitaani na vijijini kuhusiana na hili la michango ya lazima ya shule?

Ahsante sana.
Wizara Katiba Na Sheria

Ndugu Dr. Wansegamila,

Asante kwa pongezi na ushauri mzuri. Tumeupokea kwa mikono miwili.

Kuhusu malalamiko ya michango ya lazima katika maeneo mbalimbali, wizara itafuatilia kwa kina na kutoa mrejesho.

Kwa kawaida, michango ya shughuli za maendeleo huwa ni ya hiyari na wananchi wanapaswa kuhamasishwa na kushawishiwa kushiriki, sio kulazimishwa.

Asante.
 
Hii sheria ya Wizara ya Ardhi kutaka kila kiwanja kisome namba ya Nida ya mhusika mnaizunguziaje?

Hamuoni kama kuna wananchi watapoteza haki zao as asilimia kubwa ya wa-tz hawana Nida?

Inakuwaje kwa watu wa vijijini wasio na hati?

Sheria hiyo ina nia njema ya kuweka utambuzi ili kuondoa kero sugu ya migogoro ya ardhi.

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ipo mbioni kukamilisha utoaji vitambulisho kwa wananchi wote ambao walishasajiliwa.

Aidha, tunataraji kutakuwa na utaratibu maalum wa dharura utakaotumika kuwatambua wamiliki wa ardhi ambao bado hawajapata hati za ardhi zao.

NB: Suala hili lipo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Wao watakuwa na majibu ya kina na uhakika zaidi.

Asante.
 
Back
Top Bottom