Wizi wa mapato ya Serikali katika Bandari ya Dar es Salaam ndiyo sababu kubwa ya DP World kukabidhiwa

Wizi wa mapato ya Serikali katika Bandari ya Dar es Salaam ndiyo sababu kubwa ya DP World kukabidhiwa

Kumekuwa na malalamiko makubwa sana kwa bandari ya Dar es Salaam kukabidhiwa kwa DP World, lakini sababu kubwa zaidi ni wizi wa mapato ya Serikali uliokithiri pamoja na dhuluma kubwa kwa wateja wanaoagiza mizigo bandarini.

Mizigo inayopita bandarini ni mingi sana lakini Serikali imekuwa haipati mapato sahihi ya bandari hiyo kwani fedha hizo zimekuwa zikidhulumiwa tangu kipindi cha Mwl Nyerere na hata alipokuja Dr Magufuli wizi huu ulimkera sana na kujaribu kuchukua hatua ambazo hazikuzaa matunda.

Watanzania tujitoe boliti kwenye macho yetu ndipo tumnyooshee kidole raisi Samia Suluhu Hassan pamoja na Serikali kwa uamuzi waliochukua.

Watanzania tujiulize je tumekuwa tukipeleka mapato sahihi serikalini kama tulivyopaswa kufanya? Je hatukuwa tukidhulumu wateja wanaoagiza mizigo kupitia bandari hiyo? Lengo la Serikali kuleta wawekezaji DP World ni kupata mapato makubwa kwasababu ya uendeshaji wao mzuri wa bandari usiokuwa na hujuma.

Kama kusingekuwa na wizi na ubadhilifu unaofanyika bandarini basi Serikali isingewakumbuka wawekezaji wa nje ya nchi.

Watanzania tujifunze kuacha hujuma kupitia uamuzi huu wa DP World kwenye mali za Serikali kwasababu kadiri itakavyozidi kukosa mapato sahihi ndipo itazidi kualika wawekezaji kutoka nje ya nchi yetu ili wasimamie kwa haki.

Reference:

Kiuhalisia jpm ilikuwa bahati mbaya kuzaliwa afrika. Alitakiwa azaliwe China,Russia,Cuba,USA and Europe ,hii mbegu haikutakiwa kuwepo kwenye nchi ambazo watu wanatanguliza matumbo yao kuliko maslahi ya nchi kwanza. Jamaa Ni kichwa kwa kweli nadhani hata wazungu walikuwa wanamkubali Kiana yaani ndani kwa ndani. Ila ngoja wamekuja wajanja maboni town, wasio malimbukeni ,not cowboys,ngoja tumalizane do wedi,tunakuja brt later sgr Mana waafrika hawezi kujisimamia wao wenyewe alijaribu gadafi naye Ni mwarabu ,tomasi Sankara aliuwa. Afrika Kuna kalaana sio bure am sure.
Acha tukomae kuongeza nguvu za kiume,kusimamia kucha,kula kimasihara,tubeti,Simba na yanga,later cdm vs ccm.

Hii demokrasia hakikuwepo huko ulaya walipokuwa na Hali Kama hii yetu,yaaani mababu yalitumika kuzinyanyua nchi zao. Someni history,unaleta mdomo kwenye kazi ,fanya kazi.

Ngoja kwanza tumesaini hapa mktaba wa software ya kufuatilia umeme kukatika na kampuni ya kihindi kwa 69bn ,huku huko kijijini watt wanasoma wanakaa chini na bado mnaleta siasa.

Naomba mno mifupa iozee ulaya ila sio afrika.

Wale blacks USA wameshajua kuwa kwao Ni huku Ila hakuna anayejaribu kurudi yaani Bora wabaguliwe kule kule wamechomwa Moto Ila hawarudi


Afrika tunaweza ngono, starehe full stop
 
Serikali inateseka sana mpaka inachukua huu uamuzi lengo ipate mapato makubwa lakini kila inapofumua utendaji wa pale bandarini basi wanakuja wafanyakazi wengine wenye tabia hiyo ya ubadhilifu.

Imani yetu kwa mali za uma imepotea kabisa, Serikali inatuogopa
Sasa Kama Serekali yenyewe inashindwa kuwadhibiti wezi, wengine wanachomeka hadi over invoice za Malipo ya Ndege lakini bado wanaachwa unategemea wizi utaisha kwenye Mali za Umma!!??
 
ANAANDIKA BABA ASKOFU BAGONZA (PhD)

BANDARI: Tumefikaje? Tutatokaje?

Mjadala wa “kuuzwa”, “Kubinafsishwa”, “Kukodishwa” au vyovyote ilivyofanywa, umeonyesha nyufa za hatari katika nyumba yetu TANZANIA. Nitaje kadhaa:

1. Rushwa

Rushwa bandarini ndiyo imesababisha bandari ifanywe inachofanyiwa. Wakiishapeana rushwa, serikali inakosa mapato, mizigo inachelewa, inapotea, na bandari limekuwa pango la majizi.
Swali ni je, kila penye rushwa tuuze? Tubinafsishe? Tukabidhi sekta binafsi? Je rushwa ikishika kichwani na moyoni? Tujadili ufa huu bila jazba. Rushwa itavuruga wawekezaji wapya.

2. Umoja na Utaifa

Mjadala umeonyesha, wanaodai wanaujenga/kuutetea umoja na utaifa, ndio wanaubomoa. Wanaoonekana kuubomoa, ndio wanaujenga. Bandari imeujeruhi umoja na utaifa wetu. Hii ina gharama mbeleni. Tumejuana, tuishi kwa tahadhari.

3. Udini na Siasa Zetu

Viongozi wetu wana dini zao. Sitamani kuchagua kiongozi asiye na dini. Tatizo tunalo viongozi wa dini. Tunawakosoa viongozi wa dini ileee na kupongeza wa dini zetu. Au tunanyamaza mpaka tupigwe sindano ya kupongeza badala ya kushauri. Inapendeza kumkosoa na kumshauri kiongozi wa dini yako japo haizuiwi kumkosoa wa dini isiyo yako.

4. Ujuzi wa Sheria na Uchumi.

AJABU: Wanasheria walioongea tukaelewa ni wachache sana. Walio wengi ujanja wao unaishia Kisutu.
Wanauchumi wetu ujanja wao unaishia Kariakoo. Mkataba huu hawauelewi na wakiuelewa hawatuelezi tukaelewa. Huu ni ufa wa hatari.

5. Bunge

Hili lingebinafsishwa kabla ya bandari. Walichoongea bungeni sicho wanachoongea mitaani na kwenye baa. Wanamdanganya rais kuwa wanamuunga mkono wakati wamebeba mishale ya kumwangamiza. Mjadala wa Bandari umefanywa mgumu na bunge letu.

6. Serikali

Mjadala na tabia za watu vimeonyesha serikali hii si ya rais Samia hata kama kaiteua yeye. Hii ni mchanganyiko wa serikali zilizopita. Ina utii uliogawanyika - kiapo kimoja Chamwino na vingine huko makaburini, Msufini, na Butiama. Serikali bila “Uwajibikaji wa pamoja” ni sawa na genge la wasela. Ufa huu unadai tuanze upya.

7. Rushwa part 2.

Katika Mjadala wa Bandari tumesikia malalamiko ya rushwa za aina tatu: Wanaonufaika na uzembe wa bandari wakikazana kukwamisha mkataba; DP World wakikazana mkataba upite; na wanaoitwa wazalendo wasio wa taka DP World wala wazembe wa bandari LAKINI bila kutoa suluhisho. Ufa huu ni mgumu kuushughulikia bila kuchelewesha mkataba na kusikilizana kwanza.

8. Rais Wetu

Rais SSH ni wetu sote. Ni muhimu kama taifa kumkinga na mipasuko inayotokana na mjadala huu. Kuna maisha baada ya mjadala wa bandari. Yeye analo jukumu la kutuongoza sote na makundi yote mpaka tuvuke. Subira itatufundisha kuliko haraka. Ufa huu unazibwa kwa kusikiliza na kuchukua hatua.

9. Miafaka yetu

Mjadala huu umejeruhi miafaka yetu na kufukua baadhi ya makaburi. Baadhi ya makaburi tumekuta marehemu hawajaoza.
Katiba, maridhiano, Muungano, maelewano ya kidini, uhuru wa maoni na mamlaka ya wananchi bila bunge ni mambo muhimu sana katika kuziba nyufa zilizojitokeza.

10. Upinzani wetu

Mjadala unaonyesha aina mpya ya upinzani. Ndani ya chama tawala na serikali kuna upinzani mkali dhidi ya suala la bandari. Hii ni afya kwa nchi lakini hatari kwa utawala. Vyombo vyetu vijifunze kutotumia nguvu kupambana na maoni. Bora upinzani wa hadharani kuliko wa moyoni.

Nawashukuru wooote wanaochangia kwa hoja na kutuelimisha tulio wajinga wa sheria, uchumi, mikataba ya kimataifa na katiba yetu.
 
Kiuhalisia jpm ilikuwa bahati mbaya kuzaliwa afrika. Alitakiwa azaliwe China,Russia,Cuba,USA and Europe ,hii mbegu haikutakiwa kuwepo kwenye nchi ambazo watu wanatanguliza matumbo yao kuliko maslahi ya nchi kwanza. Jamaa Ni kichwa kwa kweli nadhani hata wazungu walikuwa wanamkubali Kiana yaani ndani kwa ndani. Ila ngoja wamekuja wajanja maboni town, wasio malimbukeni ,not cowboys,ngoja tumalizane do wedi,tunakuja brt later sgr Mana waafrika hawezi kujisimamia wao wenyewe alijaribu gadafi naye Ni mwarabu ,tomasi Sankara aliuwa. Afrika Kuna kalaana sio bure am sure.
Acha tukomae kuongeza nguvu za kiume,kusimamia kucha,kula kimasihara,tubeti,Simba na yanga,later cdm vs ccm.

Hii demokrasia hakikuwepo huko ulaya walipokuwa na Hali Kama hii yetu,yaaani mababu yalitumika kuzinyanyua nchi zao. Someni history,unaleta mdomo kwenye kazi ,fanya kazi.

Ngoja kwanza tumesaini hapa mktaba wa software ya kufuatilia umeme kukatika na kampuni ya kihindi kwa 69bn ,huku huko kijijini watt wanasoma wanakaa chini na bado mnaleta siasa.

Naomba mno mifupa iozee ulaya ila sio afrika.

Wale blacks USA wameshajua kuwa kwao Ni huku Ila hakuna anayejaribu kurudi yaani Bora wabaguliwe kule kule wamechomwa Moto Ila hawarudi


Afrika tunaweza ngono, starehe full stop
Kama ni mtihani basi chukua alama 💯 Excellent
 
Sasa Kama Serekali yenyewe inashindwa kuwadhibiti wezi, wengine wanachomeka hadi over invoice za Malipo ya Ndege lakini bado wanaachwa unategemea wizi utaisha kwenye Mali za Umma!!??
Ndio maana wameamua kukabidhi wageni sisi tumeshindikana
 
Wizi upo kila mahala nchi hii kuanzia Serikali, chamani nk, kwahiyo chama na serikali navyo vibinafsishwe?.
 
ANAANDIKA BABA ASKOFU BAGONZA (PhD)

BANDARI: Tumefikaje? Tutatokaje?

Mjadala wa “kuuzwa”, “Kubinafsishwa”, “Kukodishwa” au vyovyote ilivyofanywa, umeonyesha nyufa za hatari katika nyumba yetu TANZANIA. Nitaje kadhaa:

1. Rushwa

Rushwa bandarini ndiyo imesababisha bandari ifanywe inachofanyiwa. Wakiishapeana rushwa, serikali inakosa mapato, mizigo inachelewa, inapotea, na bandari limekuwa pango la majizi.
Swali ni je, kila penye rushwa tuuze? Tubinafsishe? Tukabidhi sekta binafsi? Je rushwa ikishika kichwani na moyoni? Tujadili ufa huu bila jazba. Rushwa itavuruga wawekezaji wapya.

2. Umoja na Utaifa

Mjadala umeonyesha, wanaodai wanaujenga/kuutetea umoja na utaifa, ndio wanaubomoa. Wanaoonekana kuubomoa, ndio wanaujenga. Bandari imeujeruhi umoja na utaifa wetu. Hii ina gharama mbeleni. Tumejuana, tuishi kwa tahadhari.

3. Udini na Siasa Zetu

Viongozi wetu wana dini zao. Sitamani kuchagua kiongozi asiye na dini. Tatizo tunalo viongozi wa dini. Tunawakosoa viongozi wa dini ileee na kupongeza wa dini zetu. Au tunanyamaza mpaka tupigwe sindano ya kupongeza badala ya kushauri. Inapendeza kumkosoa na kumshauri kiongozi wa dini yako japo haizuiwi kumkosoa wa dini isiyo yako.

4. Ujuzi wa Sheria na Uchumi.

AJABU: Wanasheria walioongea tukaelewa ni wachache sana. Walio wengi ujanja wao unaishia Kisutu.
Wanauchumi wetu ujanja wao unaishia Kariakoo. Mkataba huu hawauelewi na wakiuelewa hawatuelezi tukaelewa. Huu ni ufa wa hatari.

5. Bunge

Hili lingebinafsishwa kabla ya bandari. Walichoongea bungeni sicho wanachoongea mitaani na kwenye baa. Wanamdanganya rais kuwa wanamuunga mkono wakati wamebeba mishale ya kumwangamiza. Mjadala wa Bandari umefanywa mgumu na bunge letu.

6. Serikali

Mjadala na tabia za watu vimeonyesha serikali hii si ya rais Samia hata kama kaiteua yeye. Hii ni mchanganyiko wa serikali zilizopita. Ina utii uliogawanyika - kiapo kimoja Chamwino na vingine huko makaburini, Msufini, na Butiama. Serikali bila “Uwajibikaji wa pamoja” ni sawa na genge la wasela. Ufa huu unadai tuanze upya.

7. Rushwa part 2.

Katika Mjadala wa Bandari tumesikia malalamiko ya rushwa za aina tatu: Wanaonufaika na uzembe wa bandari wakikazana kukwamisha mkataba; DP World wakikazana mkataba upite; na wanaoitwa wazalendo wasio wa taka DP World wala wazembe wa bandari LAKINI bila kutoa suluhisho. Ufa huu ni mgumu kuushughulikia bila kuchelewesha mkataba na kusikilizana kwanza.

8. Rais Wetu

Rais SSH ni wetu sote. Ni muhimu kama taifa kumkinga na mipasuko inayotokana na mjadala huu. Kuna maisha baada ya mjadala wa bandari. Yeye analo jukumu la kutuongoza sote na makundi yote mpaka tuvuke. Subira itatufundisha kuliko haraka. Ufa huu unazibwa kwa kusikiliza na kuchukua hatua.

9. Miafaka yetu

Mjadala huu umejeruhi miafaka yetu na kufukua baadhi ya makaburi. Baadhi ya makaburi tumekuta marehemu hawajaoza.
Katiba, maridhiano, Muungano, maelewano ya kidini, uhuru wa maoni na mamlaka ya wananchi bila bunge ni mambo muhimu sana katika kuziba nyufa zilizojitokeza.

10. Upinzani wetu

Mjadala unaonyesha aina mpya ya upinzani. Ndani ya chama tawala na serikali kuna upinzani mkali dhidi ya suala la bandari. Hii ni afya kwa nchi lakini hatari kwa utawala. Vyombo vyetu vijifunze kutotumia nguvu kupambana na maoni. Bora upinzani wa hadharani kuliko wa moyoni.

Nawashukuru wooote wanaochangia kwa hoja na kutuelimisha tulio wajinga wa sheria, uchumi, mikataba ya kimataifa na katiba yetu.
Rushwa ikishatawala njia pekee ni kukabizi wawekezaji sisi sote tuwe wateja na sio wasimamizi
 
KWahiyo bora waibe waarabu sio waTZ???
Hoja ya mtu mwenye roho ya kwanini hii
Acheni tuibiane ndani kwa ndani
Wale hawana ujinga wetu ndugu yangu
 
Sawa, Kwa hiyo tutegemee wafanyakazi Bandarini kukosa kazi, kwani wamesema asilimia 60 na ushee itakuwa ni wageni ambao wanategemea kuondolewa ushuru, tozo, sijui na vimbwanga gani ili waweze kufanya kazi kwa "Ufanisi" tunashindwa nini kuwafanyia wafanyakazi wetu....yaani kuwapatia motisha hizo hizo tunazokwenda kutunga sheria kwa ajili ya DP?

Serikali imesema mapato Asilimia karibia ya 40 yanatoka bandarini, tuliambiwa, Royal tour itaongeza mapato, tumesherehekea TRA kuongeza mapato, tumesherehekea Ugawiaji wa "gawio" za mashirika tena tumaambiwa hazina shuruti, tumeambiwa baada ya mikopo iliyokopwa kuwa itasaidia serikali kuboresha maeneo ya kuongezea vipato vya serikali... sasa hizi haraka za nini? Kwanini tusisubiri matunda ya uwekezaji wa kodi za Wananchi?
Je tunaweza mtenganisha mswahili na upigaji ili tuendelee?
 
Hilo ni jibu rahisi sana.

Wizi maana yake ni kushindwa kwa management ya bandari kuisimamia bandari, na kushindwa pia kwa serikali kuisimamia bandari.
 
Back
Top Bottom