Uchaguzi 2020 World Bank yapitisha Mkopo wa Zaidi ya Trillion 1 Uliopingwa na Wanasiasa pamoja na Wanaharakati

Uchaguzi 2020 World Bank yapitisha Mkopo wa Zaidi ya Trillion 1 Uliopingwa na Wanasiasa pamoja na Wanaharakati

Ukiwa tegemezi au Omba Omba huwezi kuwa muweka masharti. Na huna jeuri ya kukataa msaada kwa vile wewe Tanzania bado ni nchi maskini.
Ww acha hizo, Tz ni donor country, siyo maskini, ofcourse ww huwezi elewa sasa ila baadae kama Mungu atakujalia maisha utaelewa in near future! Tunaweza kuukataa kama tulivyoikataa misaada mingi mingine...soma historia rafiki uelewe!
 
Tuache unaa inabidi tuwashukuru wapinzani kwa kiasi chake kwa kuwapigania ndugu zetu watoto wetu ili waendelee na masomo. Unajua kwa akili za kawaida huweziona umuhimu wa mtoto wa kike mwenye ujauzito kuendelea na shule ila nimuhimu sana. Kama ni kodi tunalipa wote bila kubaguliwa kwanini inapofikia kwenye matumizi yanayofanyika kutoka na kodi zetu tuanze kubaguana? Hiyo haikubaliki hata kidogo ndo maana hata wazungu huwa wanatucheka sn kwa ujinga wetu. Ulishawahi kufikiri kwanini mtu anajua mwanae anamtindio wa ubongo yaani tunasemaa zezeta lkn bado atapelekwa shule akasome . Lkn kwa mtu ambaye ana uwezo mzuri lkn kutoka na nature ya maumbile yao na mpango wa Mungu anaujauzito akose shule hii haiingii akilini. Naishukuru pia serikali kwa kubadili msimamo wake na kuwasupport hawa watoto wakike.

DUMU KUBWA
 
Hero , wewe mwenyewe ni zao la mwanamke aliyepata mimba akiwa shule, shika adabu yako. Mama yako aangekatizwa kuendelea kusoma na wewe usingesoma
😂😂😂😂😂😂😂😂😂! Hapana, mie sio zao ya mimba dropout! Bado nasimamia palepale, tukiruhusu wazazi waendelee kusoma elimu rasmi ni sawa na kuwaambia mabinti zetu sasa ni ruhusa ngono nzembe, msisubiri kumaliza shule! Ninauhakika zaidi ya nusu watakuwa na mimba na kuwa wazazi wanafunzi!
 
Tuache unaa inabidi tuwashukuru wapinzani kwa kiasi chake kwa kuwapigania ndugu zetu watoto wetu ili waendelee na masomo. Unajua kwa akili za kawaida huweziona umuhimu wa mtoto wa kike mwenye ujauzito kuendelea na shule ila nimuhimu sana. Kama ni kodi tunalipa wote bila kubaguliwa kwanini inapofikia kwenye matumizi yanayofanyika kutoka na kodi zetu tuanze kubaguana? Hiyo haikubaliki hata kidogo ndo maana hata wazungu huwa wanatucheka sn kwa ujinga wetu. Ulishawahi kufikiri kwanini mtu anajua mwanae anamtindio wa ubongo yaani tunasemaa zezeta lkn bado atapelekwa shule akasome . Lkn kwa mtu ambaye ana uwezo mzuri lkn kutoka na nature ya maumbile yao na mpango wa Mungu anaujauzito akose shule hii haiingii akilini. Naishukuru pia serikali kwa kubadili msimamo wake na kuwasupport hawa watoto wakike.

DUMU KUBWA
Zaidi ya kupigia debe la kuwataka watoto wetu wa kike kuzalia mashuleni, na kupigia debe mimba za utotoni bila kujali madhara ya kiafya ya uzazi kwa watoto hawa kuna nini cha ziada? Hebu nieleweshe ndugu!
 
Jamani wengine kusoma document ya
@WorldBank
changamoto, ni hivi: 96% ya fedha itatolewa tu pale Benki itakaporidhika na matokeo yatakayoidhinishwa na Agent anayejitegemea na Serikali ikiwa imetumia pesa zake zenyewe sawa na kiasi kinachoombwa Malipo yanaanza 2021 #ArudiShule
1585737687760.png
 
Hivi unaongea ukiwa unaifahamu Tz au unasikiaaika tu kuhusu Tz! Ni utamaduni wa kitz mtoto akipaxhikwa mimba anatimuliwa shule na antafita njia mbadala za elimu ya watu wazima!
FYI, huwa siandiki mambo kwa hisia kama mfanyavyo wengine especially watetezi wa mfumo! Kwamba ni "utamaduni wa Kitanzania" maana yake nini?! Taifa haliendeshwi kwa tamaduni bali kwa misingi iliyojiwekea!!

Tafuta online, au nenda pale Wizara ya Elimu waombe document titled:
Girls.png

Huo ni muongozo wa serikali kupitia Wizara ya Elimu ambao ulitolewa April 2009. Section 2.3 ya muongozo inatoa maelekezo kwa wazazi/walezi kwamba:-
  • Shall be counseled and guided by the school leadership on the pregnancy of the school girl;
  • Shall show empathy and accept to take care of the pregnant girl;
  • Shall be guided and counseled by the school leadership concerning maternal health of the pregnant schoolgirl;
  • Shall be informed and required to fulfill re-admittance requirements;
  • Shall be required to update the school leadership on the health condition during pregnancy and after birth; and
  • Shall be involved in deciding on which mode of education (Formal or informal) and school the pregnant girl would like to continue with, after giving birth.
Aidha, section 2.6 ya Muongozo unatoa maelekezo kwa serikali kwamba:-
  • Shall educate and sensitize the society/community on the importance of readmitting impregnated school girls;
  • Shall educate and sensitize the society/community on the process of readmitting impregnated school girls; and
  • Shall empower school leadership on the issue of readmission of pregnant school girls; and
  • Shall task the ward social welfare officers to monitor the health welfare of the impregnated school girls.
Huo ndio MWONGOZO halali ambao Magufuli anaukanyaga! Sasa wewe niwekee hapa huo utamaduni unaosema kwamba watoto wa kike wakipata ujauzito, ni marufu kuendelea na elimu rasmi kwa shule za serikali!!!
Maana hatakuwa tena kwenye kundi la watoto bali wazazi! Huu utamaduni kwa kiasi kikubwa umesaidia kuwatisha wototo wa kike kuogopa kushiriki ngono za kizembe!
Kwanini uwatishe badala ya kuweka mikakati inayoeleweka kuhakikisha hakuna ujauzito?! Hivi unaweza kunieleza hapa serikali ina mkakati upi kuhakikisha watoto hawafanyi ngono za mapema au angalau hizo ngono salama?

Btw, kama kuwatisha mbona mimba bado zipo pale pale hata siku hizi ambapo watoto wanaanza shule mapema sana?
Haiingii akilini, mtu mwenye akili timamu aje kutaka wazazi nao waruhuaiwe kusoma na watoto wakati kuna elimu ya watu wazima!
Unamaanisha Wizara ya Elimu hawana akili timamu, au?!

Ukweli ni kwamba, kama nilivyowahi kusema kwenye post moja wapo hapa jamvini, Mh. JPM ni mkurupukaji, na wala hafahamu misingi ya serikali mwenyewe!!

Hapa JPM alikuwa kama wewe tu kwa kuamini "kutimua shule wanaopata ujauzito ni utamaduni wetu" bila kufahamu mwaka 2009 serikali kupitia wizara ilitengeneza utaratibu wa kuhakikisha watoto wanopata ujauzito hawafukuzwi, bali wanakuwa suspended na kurudi tena shuleni unless kama ataamu mwenyewe kuendelea kwenye mfumo usio rasmi ambao Magufuli na wafuasi wake wanadhani ndo sheria inavyosema!
Hoja ya huyo ziro wako huyo haikuwa na mashiko hata kidogo ndio maana wameidharau hata hao watoa mkopo!
Hoja ya Zitto kivipi?! Kwani Zitto anafanya kazi Wizara ya Elimu au alihusika kwenye kuandaa huo muongozo?

Btw, Wakopeshaji gani waliodharau hoja ya Zitto?! Hivi umesoma maelezo ya WB au unaongea tu?!

Kipengele kimoja cha taarifa ya World Bank kinasema:-
Of the 60,000 students who drop out of secondary school every year in Tanzania, 5,500 leave due to pregnancy. While there is no government policy that states that students who become pregnant must be expelled from public schools, most pregnant girls do drop out.
Hiyo ndo kauli ya WB ambayo inaakisi sehemu ya mwongozo wa serikali nilioweka hapo juu!

Kwa maana nyingine, suala la wanafunzi kutimuliwa sio la kisera bali ni la JPM na watu wake!!!

Sehemu nyingine ya taarifa hiyo ya WB inasema:-
through discussions during project preparation, the government has reconfirmed its commitment that all children who take Form 4 or Form 6 examinations, regardless of which education institution they have attended, will have the opportunity to continue their education in the public school or college system.
Sasa wewe habari kwamba WB wamempuuza Zitto umezitoa wapi?!

Na labda nikujuze lingine! WB hawatatoa fungu lote kwa pamoja bali watatoa kwa awamu baada ya kuhakikisha serikali inatekeleza masharti waliyopewa, including kuwaacha watoto wajawazito kuendelea na shule kama mwongozo wa wizara unavyosema:-
Of the project funds, 96 percent (US$480 million) are subject to (a) achievement of agreed results verified by an Independent Verification Agent subject to the World Bank’s approval; and (b) submission of evidence that the government has already spent an equivalent amount on eligible expenditures in the secondary education sector. Assuming that these conditions are met each year, the disbursement schedule, is as follows:
  • FY 2021 - US$72.47 million
  • FY 2022 - US$101.10 million
  • FY 2023 - US$114.73 million
  • FY 2024 - US$98.52 million
  • FY 2025 - US$85.37 million
  • FY 2026 - US$27.81 million
Na sio tu kwamba serikali watakuwa wanasema "tumetekeleza kwa kiwango fulani bali hadi pale Independent Verification Agent atakapothibitisha!!!
Kuhusu TL, hayo unayosema sijui umeyatoa wapi!? Tumesikia wenyewe kwa masikio yetu mara nyingi sana hata kabla blankoo hazijamjeruhi, akiwatetea mabeberu na hata kuwapatia habari na taarifa muhimu za namna ya kuikomoa serikali na nchi yetu! Ww umetumwa na nani kwa kuandika gazeti lililosheni uzushi huu! Hata sasa TL ndio kaamua kuonyeza rangi zake za asili kwa yale anayopakazia nxhi yetu kwa jamaa zake mabeberu!
Eti mmesikia wenyewe, achana na hao wengine; niambie wewe ulimsikia wapi kama sio unatumia nukuu za propaganda za Lumumba!!

Ambacho alisema Tundu Lissu, ni hiki hapa chini:-



Hiyo video ni ya dakika 3:43 lakini MATAGA kwa kujua Wa-TZ hamna utamaduni wa kutafuta ukweli, waka wanaongelea maeleo ya dakika 2 za mwanzo na wakawaficha zaidi ya dakika 1 unusu nyingine zilizobaki!

Sasa pamoja na kunitolea povu kwamba eti nimetumwa kuandika uzushi, kwa mwenye akili timamu hapa atajua ni nani aliyetumwa kuleta uzushi kati yangu na wewe! Yote niliyosema hapo kabla nimekuwekea ushahidi, weka hapa ushahidi wa maelezo yako!!!
 
Xaf
ZITTO KABWE AUMBUKA.

Kampeni yake chafu dhidi ya Tanzania yakwama.
_
Benki ya Dunia yaidhinisha Mabilioni ya fedha za kusaidia Elimu alizotaka Tanzania inyimwe.

Saa chache zilizopita Benki ya Dunia kupitia Bodi ya Wakurugenzi Watendaji ya Chama cha Maendeleo ya Kimataifa (IDA) imefanya maamuzi ya kihistoria ya kuruhusu mkopo wa Dola za Marekani Milioni 500 utolewe kwa Tanzania kwa ajili ya kusaidia kuboresha elimu ya Sekondari baada ya mjadala mrefu uliochukua miezi zaidi ya mitatu.

Uamuzi wa Benki ya Dunia umezima kampeni ya kidhalimu iliyofanywa na Mwanasiasa mpuuzi Zitto Kabwe aliyeandika barua kwenda benki hiyo akitumia nembo za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutaka Tanzania inyimwe mkopo huo bila kujali athari zake kwa wananchi hasa wanyonge na maskini.

Zitto Kabwe akishirikiana na mabeberu wanaomfadhili alifanya uharamia kwa kuchochea uongo kuwa Tanzania inakandamiza wanafunzi wa kike kwa kuwanyima fursa ya kuendelea na masomo baada ya kupata ujauzito ilihali anajua kuwa sio kweli na kuna utaratibu ulio wazi wa watoto hao kupata elimu kupitia programu mbalimbali za Elimu ya Watu Wazima, Mpango wa Elimu kwa walioikosa na vyuo mbalimbali.

Hili ni pigo jingine baya sana kwa Zitto Kabwe na washirika wake ambao wamekuwa wakiichonganisha na kuichafua Serikali ya Tanzania na Mashirika ya Kitamaifa kwa kutafuta umaarufu wa kisiasa bila kujali athari ambazo wananchi wanazipata kutokana na kuinanga Tanzania ama kukwamisha miradi mikubwa na washirika wa maendeleo.

Katika safari ndefu ya mjadala ambao ulianza tangu Januari mwaka huu wa 2020, Benki ya Dunia imepiga chini msimamo wa mabeberu waliotaka Tanzania inyimwe fedha hizo baada ya kuingizwa mkenge na Zitto Kabwe.

Watu wengi wanaweza kujiuliza kwa nini Zitto Kabwe na wafadhili wake walikuwa wanashupalia Tanzania inyimwe fedha hizo? Ukweli ni kwamba Zitto na wadhalimu wenzake hawakuzuia fedha hizo kwa sababu ya kupigania wanafunzi wa kike wanaopata ujauzito wakiwa shule kama wanavyodai, bali walishupalia Tanzania isipewe fedha hizo baada ya msimamo wa Serikali ya Awamu ya Tano kukataa kukopeshwa fedha ambazo zingeingizwa nchi kupitia mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO) na miradi ambayo haina matokeo kwa wananchi ili baadaye zitumike kwa maslahi ya siasa za upinzani na sio wananchi.

Kwenye hili, Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Jemedali Rais Dk. John Pombe Joseph Magufuli inastahili pongezi za dhati kwa msimamo thabiti usiyoyumba na ushindi mkubwa dhidi ya kibaraka Zitto Kabwe na washirika wake ambao wamekuwa wakipiga tripu kwenda mabeberu hao kufanya kampeni ya kuiangamiza Tanzania eti wakitaka kuiondoa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani.

Kongole Rais Magufuli, hongera Watanzania wote kwa ushindi huu mkubwa. Zitto Kabwe na washirika wake washindwe na walegee.

Sasa Tanzania itapata Dola za Marekani Milioni 500 sawa na zaidi ya shilingi Trilioni 1 na Bilioni 135 kwa ajili ya kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopata elimu ya Sekondari, kuboresha mazingira ya elimu kwa wasichana na kuinua ubora wa elimu kwa wasichana na wavulana.

Mkopo huu ni wa gharama nafuu na sio fedha za bure. Watanzania watazilipa, lakini sasa watalipa fedha ambazo zinakopwa na kuelekezwa kuwasaidia mamilioni ya Watoto wa Tanzania na sio kwenda kwenye NGO na miradi ya kupitisha fedha zinazokwenda kwa wachumia tumbo akina Zitto Kabwe na washirika wake.

Tunaamini Serikali ya Tanzania itatoa mchanganuo wa fedha hizi zinakwenda wapi na zitawanufaishaje Wanzania.

Kila la kheri Watanzania na pole sana Zitto Kabwe kwa kuangukia pua katika mchazo huu mchafu. Tambua kuwa Mwenyezi Mungu husimama na wenye haki na katika hili amesimama na Watanzania wenye haki na Rais wao mpendwa Dk. John Pombe Joseph Magufuli.

Taarifa hii haina uhusiano na siku ya Wajinga Duniani. Ni ukweli mtupu na inapatikana katika tovuti mbalimbali za Kimataifa. Waweza kuisoma hapa kwenye tovuti ya Benki ya Dunia yenyewe

New Financing to Make Secondary Education Safer, Better, and More Accessible for Tanzanian Girls and Boys

Mwl. Damas Masele MPJ
Mkufunzi Mstaafu.
31 Machi, 2020.

Sent using Jamii Forums mobile app
Xana rais wetu Na Mungu akuongoze katika uongoz wako
 
Aliyeaibika hapa ni nani ?! Yule aliyeapa kule simiyu kwamba hawezi kusomesha wazazi, au huyu aliyepigania wakubaliwe kuendelea na masomo baada ya kuzaa ??!!. .



Odhis *
Lakini msimamo wa serikali si upo pale pale? Ukipata mimba altenative program ni veta au kajifunze kijiweni charahani. Kwa mantiki hii aliyeabika ni yule aliyaekurupuka kupinga pesa za mkopo zisitolewe.
 
Yes, very serious! Ruhusu waendelee na shule rasmi wakiwa wazazi uone kama idadi hiyo kama haitakuwa ya wasiobeba mimba na kinyume chake ndio watakaokuwa wazazi waliopo shule rasmi! Sijui kama unaweza kuelewa kwa hii statement; ila kwa bahati mbaya sina muda kwa sasa!
Tatizo lako unaongea tu hisia zako bila uhalisia!Uganda na Kenya hawawazuii watoto kirudi shule wanaopata ujauzito na kujifungua,lakini rate ya wanaopata mimba Tanzania inaizidi ya Kenya na Uganda!Unafikiri kwanini?Kwa mazingira hayo hoja yako ni mfu!
 
Msaada Wa Masharti.duh yaleyale yaliyopigiwa kelele ndo tumekubali
 
Upuuzi mtupu! Eti mzazi asome darasa hilohilo na mtoto! Haitawezekana abadani Tz! Wao walete hizo hela, after all ni mkopo tu! Mambo ya nyumbani na namna tunavyoendesha jamii yetu watuachie wenyewe! Otherwise waurudishe mkopo wao!
Ndio tushanywea hivyo!Kenya na Uganda hawawazuii watoto kurudi shule wanapojifungua,hakuna ushahidi wowote wa madhara wanayoleta kuchanganyika na wenzao wa umri wao!Zinabaki tu hisia za Jiwe!Team ya CCM ilikaa na kuandaa sera na ilani za CCM 2015,moja ya mambo waliyoahidi ni pamoja na hilo la watoto watakapata ujauzito watapewa fursa ya kurydi shule katika mfumo rasmi kumalizia masomo yao!Hata Mama Samia Suluhu wakati mmoja akihutubia alizungumza hayo kabla ya siku chache baadae JPM kuja na msimamo wake!So suala hilo la kuondoa kabisa watoto wa aina hiyo kwenye mfumo rasmi ni mawazo ya JPM na si CCM!Hapa ndio tunaona madhara ya Rais wa nchi kuwa kichwa ngumu na kutoshaurika au kusikiliza wengine!
 
Kwa utaratibu huu mfano nchi ingekuwa inapigana vita ya Kagera leo makada wa vyama vya siasa bado wangekuwa wanatafuta matukio ya kufanyia cheap politics; tunasiasa za kishamba kweli.
 
Back
Top Bottom