Wosia wa baba - John Pombe Magufuli

Wosia wa baba - John Pombe Magufuli

Tutamkumbuka kwa mengi sana aliyotutendea Hayati JPM

Biashara ya dawa za kulevya ilishamiri sana nchini, alipoingia Jpm biashara ikakomeshwa haswa.

Wimbi la ujambazi na uvamizi wa vituo vya polisi na kupora silaha aliukomesha mara moja ikiwemo hata ugaidi wa kule Kibiti

Reports za CAG enzi hizo ilikuwa kila mwaka lazima ioneshe Serikali inavyopoteza mapato kwa kulipa watumishi hewa, alipoingia JPM alishughulika na hilo ipasavyo

Ameanzisha mifumo ya ukusanyaji kodi kwa kupitia ulipaji wa control number ambayo imeimarisha sana namna nzuri ya kukusanya na kudhibiti uvujaji wa mapato.

Alijitoa muhanga kudhibiti utoroshaji wa madini yetu, ambapo makampuni yalikuwa yakitorosha na hvyo Serikali kukosa kodi

Sekta ya miundombinu imeimarika sana ktk awamu yake, tumeshuhudia ujenzi wa barabara kiwango cha lami mitaani na barabara kuu za kuonganisha mikoa, Wilaya na vijiji

Sekta ya Afya nako tumeshuhudia ujenzi wa vituo vingi vya afya na kuimarisha usambazaji wa madawa na vifaa tiba

Enzi zile za miaka nyuma tulishuhudia mpaka Twiga wakitoroshwa kwenye ndege, tembo wakiuawa, ikafikia hatua mpaka ujio wa Rais wa China nchini ukiingia kwenye kashfa ya kuondoka na pembe za ndovu.
Ila alipoingia jembe Magufuli haya yote yalibaki historia

Pamoja na madhaifu yake machache lakini kiukweli MAGUFULI amepiga kazi, ameonesha ujasiri wa hali ya juu ktk kushughulikia changamoto ambazo tuliona ni ndoto kutatuliwa, ameonesha nia na uzalendo wa kupambania kulinda rasilimali za nchi ili ziifaidishe nchi

RIP JPM
Report ya CAG masikini 1.5trl ikamng'oa Assad jaman, daah
 
Dialo amesema huyu alikuwa kichaa,sasa kichaa anatoaga wosia?
... hujamtendea haki Mh. Diallo; mpe heshima yake anayostahili.

Former Minister, MP, Tycoon and CCM Regional Chairman Hon. Dr. Anthony Diallo (PhD).

Mtu wa namna hii tuna sababu gani ya kutomuamini ukizingatia kauli yake ile hakuitoa kisiasa wala hakuitoa ili kujipendekeza afanyiwe upendeleo au fadhila yoyote ile! He was so sincere kwa kauli ile maarufu ya "Mirembe".
 
Kuna watu wanaamini kabisa kuwa Tanzania ni masikini huku wazungu wanachukua utajiri hapa hapa nchini.

R.I.P JPM
Kuna mawakala wao humu humu nchini, na ndo hao wanaojaribu kumchafua hayati kwa kuwa aliwabana kila eneo.

Tatizo tayari sie tulioaminishwa ni maskini hatuwezi mpaka wao watake, tumeisha amka usingizini.
 
Dialo mwenyewe ndio kichaa 😂😂
Duh!! Siamini Kada kwa Kada wakizodoana

Dr. Anthony Mwandu Diallo..........CEO Sahara Media

Dr. John Pombe Joseph Magufuli....Former URT president (2015-March 2021)

Mtu aliye hai tena kwa dharau na chuki za bayana anamtukana na kumsema vibaya mtu ambaye hana pumzi ya kusikia, kuona, kuhisi, kuonja, kugusa na kufikiri.

Hicho chama cha mapinduzi bila shaka kina watu waliokosa maadili na sio waaminifu.

Shujaa yeyote humkemea mhusika wakati akingali hai, haogopi kupoteza uhai wala kudhurika yeye alikuwa wapi kama sio uoga wa uharifu angeshughulikiwa zaidi?
 
Swala la SGR hili kila mtu ameona . ... Ujenzi umeanza na JPM. Hilo nalo mnataka kupindisha?
Kikwete alikwisha kamilisha mipango yote ya ujenzi wa sgr. Kama ingefuatwa leo hii tungekuwa tungekuwa tumeanza kuitumia. Mwendazake akaachana na hiyo mipango na kuja na yakwakwe. Kwa mwenendo huu,ujenzi utachukua miaka mingi sana kukamiliaka.

Kusema ukweli,mwendazake kwenye mipango ya uchumi alikuwa mweupe kabisa. Ameturudisha nyuma sana kiuchumi.
 
Duh!! Siamini Kada kwa Kada wakizodoana

Dr. Anthony Mwandu Diallo..........CEO Sahara Media

Dr. John Pombe Joseph Magufuli....Former URT president (2015-March 2021)

Mtu aliye hai tena kwa dharau na chuki za bayana anamtukana na kumsema vibaya mtu ambaye hana pumzi ya kusikia, kuona, kuhisi, kuonja, kugusa na kufikiri.

Hicho chama cha mapinduzi bila shaka kina watu waliokosa maadili na sio waaminifu.

Shujaa yeyote humkemea mhusika wakati akingali hai, haogopi kupoteza uhai wala kudhurika yeye alikuwa wapi kama sio uoga wa uharifu angeshughulikiwa zaidi?
We taga unasumbuliwa na chuki kwa matajiri kama alivyokuwa baba yako mwendazake. Ujambazi wa Magufuli kila mpenda haki anaujua...wote tumeshuhudia kwa macho yetu..tumesikia kwa masikio yetu.
 
Dialo kamaliza kila kitu!
Tulidanganywa sana... Wanyonge gani wanaishi kwenye nchi Tajiri?
Kama nchi ilikuwa tajiri mbona alikuwa akiandamana na mikoba yenye mamilioni ya mahela kuhonga honga??
 
We taga unasumbuliwa na chuki kwa matajiri kama alivyokuwa baba yako mwendazake. Ujambazi wa Magufuli kila mpenda haki anaujua...wote tumeshuhudia kwa macho yetu..tumesikia kwa masikio yetu.
Wewe ndiye jambazi la kutupwa unamtetea asiye na chembe ya uadilifu.
 
Dialo amesema huyu alikuwa kichaa,sasa kichaa anatoaga wosia?
Kichaa gani anaweza kushusha nondo za hivyo?
Kama unataka kujua kichaa anaongeaje na anaongea nini basi msikilize huyu hapa:
 
Badala ya kujikomba sana kwa SSH tetea kwa nguvu Legasi ya mwendazake ambayo kila siku inapopolewa.
Utanyooka wewe. Subiri Rais wa kwanza mwenye jinsia ya kike akuonyeshe vile kazi inaendelea
Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan
 
Marehemu mwenyewe alikuwa anajitambua kuwa na tatizo la ukichaa, wewe utapingaje?

"Wewe Mpina nimekuteua kwenye nafasi hii maana weweni kichaa mwenzangu" - marehemu Magufuli.

The thing about smart people is that they seem like crazy people to dumb people.
 
Duh!! Siamini Kada kwa Kada wakizodoana

Dr. Anthony Mwandu Diallo..........CEO Sahara Media

Dr. John Pombe Joseph Magufuli....Former URT president (2015-March 2021)

Mtu aliye hai tena kwa dharau na chuki za bayana anamtukana na kumsema vibaya mtu ambaye hana pumzi ya kusikia, kuona, kuhisi, kuonja, kugusa na kufikiri.

Hicho chama cha mapinduzi bila shaka kina watu waliokosa maadili na sio waaminifu.

Shujaa yeyote humkemea mhusika wakati akingali hai, haogopi kupoteza uhai wala kudhurika yeye alikuwa wapi kama sio uoga wa uharifu angeshughulikiwa zaidi?

Maadili

 
Back
Top Bottom