WW1, WW2 na kinachoendelea sasa Middle east vilipangwa mwaka 1871 kama barua hii ni kweli

WW1, WW2 na kinachoendelea sasa Middle east vilipangwa mwaka 1871 kama barua hii ni kweli

Mkuu umeshindwa hata kuangalia hiyo video hapo juu?
Binafsi hiyo video nimeipitia japo sio deep sana. Nitaipitia baadae kwa utulivu nikiegemea kwenye kuichambua zaidi .
Kwa ufupi Video kama Hiyo IPO YA KISWAHILI. Jamaa mmoja kama Sio wa BUKOBA (SIo mkandara Lufufu lakini) basi UGANDA ameitafsiri katika CDs zinazouzwa mitaani na wafuasi wa mrengo huu wa maarifa na niliiona nadhani 2010 mambo yake mengi ni ya kufikirika sana na inahitaji imani sio proof kuyaamini. Nitaipitia pia lkn kwa umakini kisha na mimi nitatoa maoni yangu mkuu. Na niliipata jamaa alianza introduction za vitisho kuwa watu waliotoa siri wengi walikufa ect Kazungumzia mambo ya Geneva kucontrol watu dunia nzima na mabenk, NSA secret underground High tech stations operated by ALLIENS na hao Extra terrestrial Beings uwepo wa vitu vingi ambavyo na wewe umevisema lkn kwa akili niliokuwa nayo sikuhitaji kutafakari sana kujua kama ulikuwa ni mchanganyiko wa FACTS, ASSUMPTIONS and LIE. Nitapitia na hii
 
Mkuu,hawa UFOs siyo hadithi....

Unamfahamu mtu mmoja anaitwa Phil Scheneider?



Jamaa aliuawa mwaka 1996,ukiangalia utajua alikuwa nani na nini kilimfanya auawe...

Walifanya majaribio zaidi ya 13 ya kumuua wakashindwa lakini walikuja kufanikiwa baadaye,angalia hiyo documentary mkuu.....

Mkuu nimemuangalia jamaa yako na inaonekana sio wewe tu watu wengi saana wanaamini anachokisema.
1: je unaamini maneno anayosema yanaukweli beyond doughts?
2:na wewe umeiangalia kwa kujiridhisha uko tayari tujadili ukweli au uongo uliomo?
Karibu
 
Kitu chakutusaidia hapa nikurud kwenye vitabu vyetu ambavo ni zabur ya daud taurat ya musa injili ya yesu na qur,an ya muhamad nimesema ya kwasababu hao ndo vitabu vilipitia kwao kutoka kwamung..kwann ninyi wanadam mnakua wajinga kias hiki ninyi kizaz cha nyoka mnaotafuta ishara kupitia kwa takataka plato sijui nakina wapumbavu gan,mnashindwa kuwasoma hao manabii walioletwa na mungu bakusoma kwaumakin walitumwa nn badala yake mnaleta habar za kina plato nakina nan sijui.ewe mola wang nijaalie mm nikujue ww kupitia wale uliowatuma kwan dunia navilivyomo ww ndio mjuz navo kuliko yeyote kwan ww ndio muumbaj wavitu hivo aaamin
 
Na mwenyez mung anasema mkiitilafiana kwakila jambo rudin kwenye vitabu vya mwenyezemung kwan yy anasema hatujaacha chochote katikavile mnavohitilafiana.hata hiv dunia ilivo tayar yy alishatabir kwann kutatokea haya.kwamfano yy aliweka amr kwamwanadam usifanye hiv nahiv kutatokea hivi nahivi akasema mwanamume kwamwanamume wasioane akatukumbusha nasodoma na gomora ss ndo kwanza wazungu wanatuambia tusipo ooana sisi kwass bas hatutapewa msaada tutakufa kwanjaa mpaka hapa tunataka plato gan aje atupe hadith za alfulela ulela
 
Hayo ni maandalizi ya serikali moja ya dunia, na dini moja ya dunia, sarafu moja, na kutokana na ishara zinazoonekana muda si mrefu hawa jamaa wataiteka dunia na kuiweka chini ya himaya yao.Shetani yupo kazini kuhakikisha anapata wafuasi wa kutosha kuelekea upotevuni.
 
Mkuu nimemuangalia jamaa yako na inaonekana sio wewe tu watu wengi saana wanaamini anachokisema.
1: je unaamini maneno anayosema yanaukweli beyond doughts?
2:na wewe umeiangalia kwa kujiridhisha uko tayari tujadili ukweli au uongo uliomo?
Karibu
Mkuu kwanza nikupe hongera kwa kutumia muda wako kuangalia video hii,hongera sana.....

Pili,Unapaswa mkuu uelewe kwamba sileti video tu uone kwasababu naleta bali naleta video kwasababu maalum na kutoka kwa watu maalum....

Ili chochote alichosema mtu kichukuliwe kwa uzingativu wa hali ya juu kuna mambo unapaswa uyajue kabla ya kuzingatia chochote ambacho mtu atasema....

Mfano leo,likitokea jambo linalohusu masuala ya nchi ya usalama wa ndani ni lazima ili tuamini yapo na yanatokea ni lazima tusikie kutoka kwa waziri wa wizara husika na siyo kwa mtu yoyote tu.Tunamsikiliza waziri kwasababu ya wadhifa wake na siyo kwasababu nyingine yoyote ile.....

Ugonjwa unapodaiwa kuwepo mahali,daktari mkuu wa eneo husika huulizwa kama ni kweli au sivyo na atakachokisema mtu huyu atasikilizwa kwasababu ya wadhifa wake na siyo sababu nyingine yoyote ile....

Nikija kwenye suala hili,je unafahamu huyu Phil Schneider alikuwa na wadhifa upi?

Ukijua hili kwanza ndiyo utaona kama unachotaka tujadili kina mashiko au hakina maana naona kama unadhani huyu jamaa alikuwa ni mtu tu aliyeibuka na kuanza kusema aliyotaka kusema bila kuzingatia alikuwa ni nani kwa maana ya wadhifa wake.....
 
Binafsi hiyo video nimeipitia japo sio deep sana. Nitaipitia baadae kwa utulivu nikiegemea kwenye kuichambua zaidi .
Kwa ufupi Video kama Hiyo IPO YA KISWAHILI. Jamaa mmoja kama Sio wa BUKOBA (SIo mkandara Lufufu lakini) basi UGANDA ameitafsiri katika CDs zinazouzwa mitaani na wafuasi wa mrengo huu wa maarifa na niliiona nadhani 2010 mambo yake mengi ni ya kufikirika sana na inahitaji imani sio proof kuyaamini. Nitaipitia pia lkn kwa umakini kisha na mimi nitatoa maoni yangu mkuu. Na niliipata jamaa alianza introduction za vitisho kuwa watu waliotoa siri wengi walikufa ect Kazungumzia mambo ya Geneva kucontrol watu dunia nzima na mabenk, NSA secret underground High tech stations operated by ALLIENS na hao Extra terrestrial Beings uwepo wa vitu vingi ambavyo na wewe umevisema lkn kwa akili niliokuwa nayo sikuhitaji kutafakari sana kujua kama ulikuwa ni mchanganyiko wa FACTS, ASSUMPTIONS and LIE. Nitapitia na hii
Mkuu unaleta ishu za akina mkandala kwenye mambo serious kama haya kweli?

Inawezekana walishaiona na kuifasiri hii lakini hao achana nao hapa....

Pia,sijui unasema humo kuna uongo kutokana na ulivyoona hizo tafsiri au ni nini,lakini nikushauri tu kwamba unapotaka kujifunza mambo mapya unapaswa kuondoa ulichojifunza kwanza na ukiweke pembeni kisha ubongo wako ubaki wazi kupokea kipya kisha baada ya hapo pima bila kupendelea upande wowote kati ya unayojua na haya mapya....

Kabla hujaamini chochote kutoka kwa yoyote anza kwanza kumfuatilia msemaji ni nani na ukishamjua ndipo uanze aidha kuamini au kutilia mashaka anachosema....

Rais mstaafu wa nchi fulani akisema kuwa kwenye ikulu ya nchi hiyo huwa wanafanya kafara ya binadamu hutaweza kubeza maneno yake kwasababu ya wadhifa aliokuwa nao hata kama anayosema hayafikiriki.....
 
Mkuu, ulivyotoa quote ya enoch wa kweli (kwa maelezo yako) naona MSEZA MKULU katoroka.

Sina utafiti wowote ila haya mambo mi naona kama ni njama flani tu kutoa watu kwenye reli flani, ama kuwajengea hofu ili wakimbilie ukombozi flani ama ni namna ya kuandaa mpango flani wa wajanjawajanja ambao waliwahi kuerevuka na wana lengo lao wengi hatulijui.

Vyovyote vile, napata shida sana kuamini kwamba kwa miaka yoooote hii kuna kitu kinafichwa. Kwa uwezo wa binadamu tungeshang'amua.
Mkuu,najua unasema "kwa uwezo alionao binadamu tungeshang'amua" ukiamini kabisa kuwa binadamu ana uwezo fulani mkubwa sana,hii ni kweli lakini siyo kama unavyoambiwa....

Kinachosababisha tudanganywe kuhusu uwezo wa binadamu ni ili tuone kwamba sisi tuna uwezo wa kutosha kuhimili kila kitu hivyo kwanza tulidanganywa kwenye vitabu vya dini na pili hakuna Mungu au hakuna haja ya kumtegemea Mungu.....

Kuna uwezo ambao binadamu anao na ni mkubwa sana lakini siyo kama tunavyoambiwa,Binadamu alipewa ujizi wa mengi na malaika waasi ambao walimpa ujuzi wa mambo hayo kwasababu hii ya kumfanya aone hakuna sababu ya kuwa karibu na Mungu.Lakini pia binadamu huyu huyu hakuumbwa kuhimili kujua siri hizi ambazo leo anazijua,kwa kuliona hili shuhudia namna tunavyouana kama mbuzi.....

Ukweli mkubwa zaidi ni kwamba binadamu tunazidi kuwa dhaifu kadiri ziku zinavyosonga mbele na ukweli huu hatuabiwi na matokeo yake tunaelezwa kinyume chake....

Adamu aliishi miaka 900,wewe leo ukifikisha miaka 50 umeshaanza kuisha.Sasa jiulize,kati ya Adamu na wewe aliyekuwa na ubongo imara wa kufanya mambo ni nani? Kama kweli sasa tuna maendeleo kuliko kale....

Kama Adamu alikuwa bora zaidi kwa kuangalia ushahidi huo basi tunadanganywa,swali la msingi,Je,ni kwanini tunadanganywa?
Na hata kama kinafichwa hakihusiani na shetani na Mungu maana hata hiyo stori ya Adam na Hawa mi huwa inanipa shida sana kuiamini. Haya ni mawazo yangu.
Sawa ni mawazo yako,lakini kwakuwa umeyaweka hapa tutayajadili na kuyajibu....

Ungesema sababu ya kuona suala la Adamu kuwa siyo kweli ingekuwa vyema zaidi....

Kwanini unadhani tuliyofichwa hayahusiani na Mungu na Shetani?Usichokijua ni kwamba kila kitu kinachokuzunguka kinahusiana na mambo hayo na hakuna hata kimoja kilichopo kisichohusiana na mambo hayo au hao wawili....

Iko vita kubwa sana inaendelea ndugu yangu na usipojua hili utapotea mazima....
Kuna jambo umeongelea juu ya waisraeli ama wayahudi kuwa wabantu. Tafadhali fafanua na kama una vyanzo credible nidadavulie.
Mkuu hili ni mada tofauti kabisa na tutajitahidi siku moja tuje tulijadili....
 
Mkuu kwanza nikupe hongera kwa kutumia muda wako kuangalia video hii,hongera sana.....

Pili,Unapaswa mkuu uelewe kwamba sileti video tu uone kwasababu naleta bali naleta video kwasababu maalum na kutoka kwa watu maalum....

Ili chochote alichosema mtu kichukuliwe kwa uzingativu wa hali ya juu kuna mambo unapaswa uyajue kabla ya kuzingatia chochote ambacho mtu atasema....

Mfano leo,likitokea jambo linalohusu masuala ya nchi ya usalama wa ndani ni lazima ili tuamini yapo na yanatokea ni lazima tusikie kutoka kwa waziri wa wizara husika na siyo kwa mtu yoyote tu.Tunamsikiliza waziri kwasababu ya wadhifa wake na siyo kwasababu nyingine yoyote ile.....

Ugonjwa unapodaiwa kuwepo mahali,daktari mkuu wa eneo husika huulizwa kama ni kweli au sivyo na atakachokisema mtu huyu atasikilizwa kwasababu ya wadhifa wake na siyo sababu nyingine yoyote ile....

Nikija kwenye suala hili,je unafahamu huyu Phil Schneider alikuwa na wadhifa upi?

Ukijua hili kwanza ndiyo utaona kama unachotaka tujadili kina mashiko au hakina maana naona kama unadhani huyu jamaa alikuwa ni mtu tu aliyeibuka na kuanza kusema aliyotaka kusema bila kuzingatia alikuwa ni nani kwa maana ya wadhifa wake.....
Sasa naomba unajibu chief. Kuhusu huyu jamaa yeye anadai alikuwa ni Geologist and engineer na alifanya kazi kwenye us high security level 3. Katika yeye anachoita black project s. Au D. U. M.B PRODUCT yaani Deep underground Military Bases. Yeye akiwa na kikosi cha Delta force na kikosi cha NATO watu 66 huko new Mexico wakijenga underground base Dulce base walivamiwa na Grey creature ambao ni UFo. Akapona yeye na wenzake wawili huku yeye akiua UFo wawili kwa bastora yake.
Ndio maana nakuuliza Yale maswali mawilli unijibu kwanza. Nimemfuatilia kuliko unavyodhani mkuu hadi baba na mama yake walikuwa nane. Kifo chake hakuna ushahidi wowote kama kanyongwa au kajinyonga au kauwawa au hajauwawa. Hiyo kazi waliifanya 1979 kakaa kimya hadi 1995 ndio kafunguka 1996 kadedi. Naona unakwepa kumuelezea sana basi mimi nitamfunguka kila kitu ili watu waone kama story zake zinamashiko au ni deception auze vitabu vyake. Pia sijapenda alivyokuwa anajibu watu maswali husikilizi anawaingilia. Ukimuangalia Mara ya kwanza unaweza kumuamini lkn ukianalyse na kumuhoji anaacha maswali mengi kuliko majibu.
 
Mkuu,najua unasema "kwa uwezo alionao binadamu tungeshang'amua" ukiamini kabisa kuwa binadamu ana uwezo fulani mkubwa sana,hii ni kweli lakini siyo kama unavyoambiwa....

Kinachosababisha tudanganywe kuhusu uwezo wa binadamu ni ili tuone kwamba sisi tuna uwezo wa kutosha kuhimili kila kitu hivyo kwanza tulidanganywa kwenye vitabu vya dini na pili hakuna Mungu au hakuna haja ya kumtegemea Mungu.....

Kuna uwezo ambao binadamu anao na ni mkubwa sana lakini siyo kama tunavyoambiwa,Binadamu alipewa ujizi wa mengi na malaika waasi ambao walimpa ujuzi wa mambo hayo kwasababu hii ya kumfanya aone hakuna sababu ya kuwa karibu na Mungu.Lakini pia binadamu huyu huyu hakuumbwa kuhimili kujua siri hizi ambazo leo anazijua,kwa kuliona hili shuhudia namna tunavyouana kama mbuzi.....

Ukweli mkubwa zaidi ni kwamba binadamu tunazidi kuwa dhaifu kadiri ziku zinavyosonga mbele na ukweli huu hatuabiwi na matokeo yake tunaelezwa kinyume chake....

Adamu aliishi miaka 900,wewe leo ukifikisha miaka 50 umeshaanza kuisha.Sasa jiulize,kati ya Adamu na wewe aliyekuwa na ubongo imara wa kufanya mambo ni nani? Kama kweli sasa tuna maendeleo kuliko kale....

Kama Adamu alikuwa bora zaidi kwa kuangalia ushahidi huo basi tunadanganywa,swali la msingi,Je,ni kwanini tunadanganywa?

Sawa ni mawazo yako,lakini kwakuwa umeyaweka hapa tutayajadili na kuyajibu....

Ungesema sababu ya kuona suala la Adamu kuwa siyo kweli ingekuwa vyema zaidi....

Kwanini unadhani tuliyofichwa hayahusiani na Mungu na Shetani?Usichokijua ni kwamba kila kitu kinachokuzunguka kinahusiana na mambo hayo na hakuna hata kimoja kilichopo kisichohusiana na mambo hayo au hao wawili....

Iko vita kubwa sana inaendelea ndugu yangu na usipojua hili utapotea mazima....

Mkuu hili ni mada tofauti kabisa na tutajitahidi siku moja tuje tulijadili....
LA waisrael kuwa wabantu au watu weusi limewahi kujadiliwa lkn kwa mtazamo wa bibilia ukweli huo unatia mashaka. Ila ukweli Kuna uwezekano wakawepo watu weusi hybrid ndani ya waisrael.
Mfano Musa alitoa mtoto wa yethro. Utajua hawakuwa weusi maana milliam na ndugu yake walimcheka mke wa Musa kwa sababu yeye alikuwa mweusi Mungu akawalaani wanapata ukoma.

Pili malkia wa sheba alipokuja Jerusalem miaka hiyo ya nyuma Kuna uwezekano aither yeye au watoto wake wakike Walikuwa miongoni mwa wake na michepuko 1000 wa Sulaiman hivyo kunauwezekano Sulaiman alizaa watoto weusi ambao wakaongezeka na kuwa wengi. Huu Ni ushahidi based on Bible ila Kuna story nyingi nje ya bibilia.
 
Ulichandika sasa Hakishabihiani na Ulichandika mwanzo Page 2 kuhusu Lucifer/shetani labda kama mko wawili t
Kwa UFUPI SHETANI anaabudiwa kama LUCIFER leo kwenye Masonic lodges. na Wao wanamwita yesu ni Adonai. na Wanaamini Lucifer alionewa kwa fitna zilizosababishwa na Adonai. Sasa unapotaka Kuleta ujanjaujanja wa kumkwepesha Lucifer asiwe Shetani maana yake unaanza kunipa mashaka yawezekana hivyo vitabu vya pembeni vinavyokupa hizo tafsiri ni product za unazotakiwa kuziangalia upya valid source yake.
LUCIFER
Lucifer (/ˈluːsɪfər/;[1][2][3] loo-sif-ər) is the King James Version and Vulgate translation rendering of the Hebrew word הֵילֵל in Isaiah 14:12. This word, transliterated Hêlêl[4] or Heylel (pron. as HAY-lale),[5] occurs once in the Hebrew Bible[4] and according to the KJV-based Strong's Concordance means "shining one, light-bearer".[5] The Septuagint renders הֵילֵל in Greek as ἑωσφόρος[6][7][8][9][10] (heōsphoros),[11][12][13] a name, literally "bringer of dawn", for the morning star.[14] The word Lucifer is taken from the Latin Vulgate,[15] which translates הֵילֵל as lucifer,[16][17] meaning "the morning star, the planet Venus", or, as an adjective, "light-bringing".[18]

PIA UKUMBUKE KAMA SIKO SAHIHI NIKOSOE AGANO LA KALE HALIKUANDIKWA KILATINI BALI KIEBRANIA na KIGIGIRIKI ni Agano Jipya.



MAELEZO YAKO YA AWALI;

Kama ujuavyo ni kwamba Lucifer alikuwa ni malaika kule mbinguni na alianzisha harakati za kudai "haki" kutoka kwa Mungu.Yeye kwa tafsiri yake aliona hakuna haki hivyo alianzisha kampeni ambayo ilipelekea kufanikiwa kuwadanganya robo ya malaika wa mbinguni ambapo inakadiriwa ni malaika zaidi ya 300.......

Harakati hizi za Shetani zilisababisha kutokea kwa mvurugano huko mbinguni na kulazimika Shetani kuondolewa huko na kutupwa hapa duniani ambapo nako alidhamiria kuendeleza kampeni ya "kukomboa" viumbe wengine kutoka kwenye "udikteta" wa Mungu.Shetani hakuwa akikubaliana na Mungu namna ambayo aliamua kuwahudumia viumbe wote pamoja na kanuni zote alizoweka hivyo akaamua kuanzisha movement yake ambayo mwanzo alidhani angeweza kushinda....

Ukweli ni kwamba alishindwa,baada ya kushindwa na kujua kuwa hataweza kutimiza malengo yake aliamua kuendeleza harakati zile kwenye viumbe wengine lakini akitaka kumtumia kiumbe mmoja maalum...

Aliamua kumtumia kiumbe ambaye Mungu alimuumba kwa unadhifu na kwa malengo maalum kutimiza malengo yake.Malengo ya Shetani ni kutaka kuzuia malengo ya Mungu kutimia kwa kiumbe huyu na kwa kufanya hivyo atakuwa ametimiza angalau lengo moja ambalo ni kuvuruga mipango ya Mungu kwa kiumbe huyu aliyempenda kabisa.....

Kiumbe huyu ni binadamu.Shetani anajua kabisa kuwa kiumbe huyu ndiye kiumbe pekee ambaye Mungu alimpenda na kuchagua yeye [Mungu] kuwa sehemu yake,hivyo akaamua kufanya harakati zote ili amdhalilishe Mungu kupitia kiumbe huyu....

Aliamua kuanzisha harakati nyingi sana ili aweze kutimiza lengo lake hili.Harakati ya kwanza kabisa ni tukio la pale Eden ambapo alimtumia mwanamke kumuangusha mwanadamu huyu na alifanikiwa.Tool kubwa sana anayotumia Shetani ni uongo maana akisema ukweli hataweza kufanikiwa kabisa....

Baada ya kufanikiwa kwenye tukio hili Shetani aliamua au niseme alipanga kuvuruga kabisa uumbaji wa Mungu kwa kiumbe huyu,kwakuwa Mungu alimfukuza Shetani kule mbunguni na huyo huyo Mungu akaamua kuwa sehemu ya kuimbe ambaye Shetani anamuona kama dhaifu,aliamua na yeye kutengeneza harakati za yeye naye kuingia ndani ya binadamu na kuwa sehemu yake....


PAGE 2
Dah!!

Mkuu sijataka kumuondoa Shetani kuwa Lucifer hata mara moja isipokuwa kwenye maelezo yangu hayo nimesema kwamba "kuna story zingine ambazo zinadai kuwa hao ni tofauti" lakini siyo kwamba mimi ndiyo ninasema wako tofauti.Mkuu nakuomba sana unaposoma maandijko yangu na ukaona kama najipinga uliza kwanza ili nikujibu kwa namna nijuavyo...

Mfano hapa ungeniuliza "Mkuu mbona unaonekana kama unataka kumuondoa Lucifer kuwa Shetani"? na ningekupa jibu lakini siyo kunituhumu moja kwa moja....

Inaonekana aina yangu ya uandishi inakupa shida kunielewa wakati mwingine nitajaribu kubadili ili twende sanjari....
 
Mkuu,kila mara umekuwa uking'ang'ania tu kuwa kitabu cha Enoch kinapingana na Biblia huku ukileta nukuu potofu na zisizokuwepo za kitabu hicho.Naomba uelewe kwamba sijakurupuka kabisa kwenye jambo hili,kitabu cha Enock kipo sanjari Biblia na hakikinzani nayo.....

Jamii za kale ziliamini vitabu vingi sana hilo lisikupe shida kabisa mkuu.....
Kupunguza mpishano huu, nikupe assignment ya kunitafutia copy unayoiamini wewe kuwa ni valid copy ya hicho kitabu ili soft copy nipm kama ni hard copy snapshot unitumie page kadhaa maana nje ya hiyo Jude quotation na vitu vichache yaliyobaki yote ni apocalyptic stories which are inversely proportional to the bible ndio maana wenzako waliombali kwenye kukiresearch wanasema it's uninspired book and does not have chance to be equated with inspired books of the Bible. Utakapo fanya hivyo ndio tutaendelea mjadala huo vizuri maana nikasema vyangu vinaonekana ni uongo.
 
Dah!!

Mkuu sijataka kumuondoa Shetani kuwa Lucifer hata mara moja isipokuwa kwenye maelezo yangu hayo nimesema kwamba "kuna story zingine ambazo zinadai kuwa hao ni tofauti" lakini siyo kwamba mimi ndiyo ninasema wako tofauti.Mkuu nakuomba sana unaposoma maandijko yangu na ukaona kama najipinga uliza kwanza ili nikujibu kwa namna nijuavyo...

Mfano hapa ungeniuliza "Mkuu mbona unaonekana kama unataka kumuondoa Lucifer kuwa Shetani"? na ningekupa jibu lakini siyo kunituhumu moja kwa moja....

Inaonekana aina yangu ya uandishi inakupa shida kunielewa wakati mwingine nitajaribu kubadili ili twende sanjari....
Hapo tuko sanjari. Nilitaka kuweka takwimu Sawa.
 
Sasa naomba unajibu chief. Kuhusu huyu jamaa yeye anadai alikuwa ni Geologist and engineer na alifanya kazi kwenye us high security level 3. Katika yeye anachoita black project s. Au D. U. M.B PRODUCT yaani Deep underground Military Bases. Yeye akiwa na kikosi cha Delta force na kikosi cha NATO watu 66 huko new Mexico wakijenga underground base Dulce base walivamiwa na Grey creature ambao ni UFo. Akapona yeye na wenzake wawili huku yeye akiua UFo wawili kwa bastora yake.
Ndio maana nakuuliza Yale maswali mawilli unijibu kwanza. Nimemfuatilia kuliko unavyodhani mkuu hadi baba na mama yake walikuwa nane. Kifo chake hakuna ushahidi wowote kama kanyongwa au kajinyonga au kauwawa au hajauwawa. Hiyo kazi waliifanya 1979 kakaa kimya hadi 1995 ndio kafunguka 1996 kadedi. Naona unakwepa kumuelezea sana basi mimi nitamfunguka kila kitu ili watu waone kama story zake zinamashiko au ni deception auze vitabu vyake. Pia sijapenda alivyokuwa anajibu watu maswali husikilizi anawaingilia. Ukimuangalia Mara ya kwanza unaweza kumuamini lkn ukianalyse na kumuhoji anaacha maswali mengi kuliko majibu.
Lengo langu na kukuhoji niliyokuhoji nilikuwa nataka ujue kwanza ni mtu gani unataka kuanza kumtuhumu tu kuwa anadanganya....

Unachotakiwa kabla ya kuanza mjadala huu ukubali huo wadhifa wake kama ni kweli alikuwa nao au alidanganya na utaje ni kwanini unadhani alidanganya....

Kama hautakubaliana na wadhifa wake mjadala wa kumhusu huyu jamaa unajifia wenyewe maana kikubwa ambacho kilifanya nizingatie alichokisema ni wadhifa wake kwanza kisha alichokisema kinafuata baadaye....

Pia,unachotakiwa kujua ni kwamba,watu wa namna hii ambao waujua ukweli fulani kisha wakaja kuusema na kukutana na watu ambao wanaona wanayoyasema hayafikiriki wanakuwa wanapata vitu kama hasira hivi na mihemko kwasababu wanakuwa wanajiuliza "huyu anakataa nini wakati mimi nimeshiriki kabisa kufabnya haya"? Maswali kama haya yanapelekea jazba au kumkatisha mtu swali ambalo linaonekana kama siyo la msingi....

Yote haya yanatokea kwasababu watu hawa wanakuwa hawako trained kwenye mijadala ya namna hii kitu kinachopelekea wao kuonekana kama wanalazimisha mambo.Haya ni mambo unapaswa uyazingatie.Pia siyo kila mtu ni mzuri kwenye kujieleza au kukielezea anachokijua kwa Flow inayotakiwa maana hii nayo ni elimu,hivyo unapoona hatoi maelezo yaliyonyooka unapaswa ujikimbilie kwenye hitimisho kwasababu hilo hitimisho ndilo unalolitaka...

Baada ya kusema hayo naomba uniambie kama unakubaliana na wadhifa wake kwanza kabla hatujajadili kingine kumhusu huyu ndugu ili tupate basic ya mjadala huu....

Ahsante....
 
Kupunguza mpishano huu, nikupe assignment ya kunitafutia copy unayoiamini wewe kuwa ni valid copy ya hicho kitabu ili soft copy nipm kama ni hard copy snapshot unitumie page kadhaa maana nje ya hiyo Jude quotation na vitu vichache yaliyobaki yote ni apocalyptic stories which are inversely proportional to the bible ndio maana wenzako waliombali kwenye kukiresearch wanasema it's uninspired book and does not have chance to be equated with inspired books of the Bible. Utakapo fanya hivyo ndio tutaendelea mjadala huo vizuri maana nikasema vyangu vinaonekana ni uongo.
Nukuu ya Yuda inakuwaje siyo valid mkuu?

Hapa nashindwa kukuelewa kabisa,naomba unifafanulie hili....
 
LA waisrael kuwa wabantu au watu weusi limewahi kujadiliwa lkn kwa mtazamo wa bibilia ukweli huo unatia mashaka. Ila ukweli Kuna uwezekano wakawepo watu weusi hybrid ndani ya waisrael.
Mfano Musa alitoa mtoto wa yethro. Utajua hawakuwa weusi maana milliam na ndugu yake walimcheka mke wa Musa kwa sababu yeye alikuwa mweusi Mungu akawalaani wanapata ukoma.

Pili malkia wa sheba alipokuja Jerusalem miaka hiyo ya nyuma Kuna uwezekano aither yeye au watoto wake wakike Walikuwa miongoni mwa wake na michepuko 1000 wa Sulaiman hivyo kunauwezekano Sulaiman alizaa watoto weusi ambao wakaongezeka na kuwa wengi. Huu Ni ushahidi based on Bible ila Kuna story nyingi nje ya bibilia.
Umekuwa ukisema tu jambo fulani kibiblia linatia mashaka lakini tukija kwenye hiyo biblia mara zote imekula kwako kwenye mjadala huu,sijaona mtazamo wako hata mmoja ambao umekuja kuwa sahihi kwenye mjadala huu.Kwasababu hiyo hata jambo hili nalitilia mashaka kwa asilimia nyingi tu.....

Si hivyo tu,bali hata kwenye Biblia yenyewe kuna ushahidi pia kuwa Suleiman alikuwa mweusi,Yesu alikuwa mweusi n.k...

Kuhusu Wabantu kuwa ni Waisraeli hili nalo kuna maeneo kwenye Biblia linaonesha hivyo....

Mkuu,hili halihusiano moja kwa moja na mada yako,lakini pia ni kweli nimeshajadili jambo hili hapa lakini kwenye mada hizo hukuwepo,nilijadiliana na watu wengine na mkuu Wickama atakuwa anakumbuka sana jambo hili vizuri sana maana hadi Biblia tuliijadili kule na pia ulikuwepo ushahidi kuonesha hawa wanaoitwa Waisraeli leo siyo wenyewe.....

Sijaona sababu ya kulijadili hili sasa kwakuwa linahitaji maandalizi,tumalize hili la mada yako kisha tutajadili siku nyingine suala hili....
 
Lengo langu na kukuhoji niliyokuhoji nilikuwa nataka ujue kwanza ni mtu gani unataka kuanza kumtuhumu tu kuwa anadanganya....

Unachotakiwa kabla ya kuanza mjadala huu ukubali huo wadhifa wake kama ni kweli alikuwa nao au alidanganya na utaje ni kwanini unadhani alidanganya....

Kama hautakubaliana na wadhifa wake mjadala wa kumhusu huyu jamaa unajifia wenyewe maana kikubwa ambacho kilifanya nizingatie alichokisema ni wadhifa wake kwanza kisha alichokisema kinafuata baadaye....

Pia,unachotakiwa kujua ni kwamba,watu wa namna hii ambao waujua ukweli fulani kisha wakaja kuusema na kukutana na watu ambao wanaona wanayoyasema hayafikiriki wanakuwa wanapata vitu kama hasira hivi na mihemko kwasababu wanakuwa wanajiuliza "huyu anakataa nini wakati mimi nimeshiriki kabisa kufabnya haya"? Maswali kama haya yanapelekea jazba au kumkatisha mtu swali ambalo linaonekana kama siyo la msingi....

Yote haya yanatokea kwasababu watu hawa wanakuwa hawako trained kwenye mijadala ya namna hii kitu kinachopelekea wao kuonekana kama wanalazimisha mambo.Haya ni mambo unapaswa uyazingatie.Pia siyo kila mtu ni mzuri kwenye kujieleza au kukielezea anachokijua kwa Flow inayotakiwa maana hii nayo ni elimu,hivyo unapoona hatoi maelezo yaliyonyooka unapaswa ujikimbilie kwenye hitimisho kwasababu hilo hitimisho ndilo unalolitaka...

Baada ya kusema hayo naomba uniambie kama unakubaliana na wadhifa wake kwanza kabla hatujajadili kingine kumhusu huyu ndugu ili tupate basic ya mjadala huu....

Ahsante....
Sina shida na cheo wala elimu yake. Baada ya hilo sema kitu au jibu maswali ili na mimi nasema vitu
 
Nakubaliana na wewe kuhusu kutojadili hili humu. Kuhusu inconsistencies ya maelezo yangu kutoka kwenye bibilia ni sehemu moja tu au mbili nilichangananya wala isikupe shida nitakuwa nakupa mistari kabisa. Mimi sio padri wala pastor Bali Bible lover and believer ninapokosea nakubali na tunasonga sioni mantiki ya kutumia hilo kama utetezi wako. Tuendelee na mada
Umekuwa ukisema tu jambo fulani kibiblia linatia mashaka lakini tukija kwenye hiyo biblia mara zote imekula kwako kwenye mjadala huu,sijaona mtazamo wako hata mmoja ambao umekuja kuwa sahihi kwenye mjadala huu.Kwasababu hiyo hata jambo hili nalitilia mashaka kwa asilimia nyingi tu.....

Si hivyo tu,bali hata kwenye Biblia yenyewe kuna ushahidi pia kuwa Suleiman alikuwa mweusi,Yesu alikuwa mweusi n.k...

Kuhusu Wabantu kuwa ni Waisraeli hili nalo kuna maeneo kwenye Biblia linaonesha hivyo....

Mkuu,hili halihusiano moja kwa moja na mada yako,lakini pia ni kweli nimeshajadili jambo hili hapa lakini kwenye mada hizo hukuwepo,nilijadiliana na watu wengine na mkuu Wickama atakuwa anakumbuka sana jambo hili vizuri sana maana hadi Biblia tuliijadili kule na pia ulikuwepo ushahidi kuonesha hawa wanaoitwa Waisraeli leo siyo wenyewe.....

Sijaona sababu ya kulijadili hili sasa kwakuwa linahitaji maandalizi,tumalize hili la mada yako kisha tutajadili siku nyingine suala hili....
 
Nimekuambia unatumia kigezo gani kuamini Yuda kaquote Enoch,

Ni kwasababu Yuda mwenyewe amesema na siyo mimi mkuu....
na unatumia kigezo gani kupinga kuwa kuna uwezekano ni kitabu ni mpango wa watu kuchomekea haya ya kwenye bibilia ili Kukipa authentication kwa wafuasi wa bibilia ili wapenyeze mafundisho ambayo wewe unayaamini na kuyasimamamia.

Mkuu,in my poit of view ni kwamba,Biblia ni sahihi na haina aina yoyote ya uchafu au kuchafuliwa,kwangu ni tool ya ku verify aina yoyote ya maandiko nje ya Biblia kuwa ni sahihi,kama umefikia hatua ya kuanza hadi kutilia mashaka maandiko ya kwenye Biblia kwasababu tu yanaonekana kukipa uhalali kitabu ambacho wewe unakikataa hili ni tatizo lako mkuu....

Kwangu mimi,as long as Yuda ameandika aliyoandika kutoka kwenye kitabu cha Enoch,kwangu mimi ni sahihi na kweli...
Kwa nini Uamini kwamba Yuda amequote kitabu hicho wakati mwenyewe unasema kuna DISTORTED/CONTAMINATED COPIES YA HICHO KITABU?
Kwanza,kama nilivyokueleza hapo juu ni kwamba Yuda mwenyewe amesema....

Pili,kuwepo kwa vitabu fake hakuondoi uwepo wa kitabu halisi na kinyume chake kunathibitisha uwepo wa halisi,huwezi kuwa na kopi bila kuwa na halisi....
Unatumia Ushahidi gani kuamini ENOCH aliandika kitabu wakati ambao population ya dunia ilikuwa centralized sehemu moja bado na Kama Ni mtu wa saba kutoka adamu inamaanisha hadi anakuwa mtu mzima watu walikwa ni kama Familia au kijiji. Utamuandikia nani hicho kitabu.
Hii inaonekana hujasoma kitabu hiki na pia unanishangaza kidogo kwenye maelezo yako haya....

Kwanini nasema unaonekana hujakisoma?
Nasema hivyo kwasababu kitabu cha Enoch kwa sehemu kubwa ni kitabu cha kinabii,kama ujuavyo mtu anapotoa unabii huwa hazungumzii wakati uliopo bali wakati ujao,hivyo,kama Enoch aliandika kitabu hiki basi hakuandika kwaajili ya watu wake au wakati wake bali wakati ujao,sasa unanishangaza kuuliza kuwa alimwandikia nani wakati hakuandika kwaajili ya watu wa wakati wake au wakati wake....

Unanishangaza kwenye maelezo yako kwasababu,sijui ni kwanini unaona hawezi kuandika kitabu hiki,kwanini hasa unadhani hivi?
Kama ni Hivyo Kwa Nini Mungu asingewaacha wakina ADAM,EVE, METHUSELA,NUHU,RUTU,ABRAHAMU,ISAKA,YAKOBO,na wengine wengi akiwemo ENOCH (Hajaandika hicho kitabu) Wasiandike habari zao kama wakina DAUDI, Sulemani,Yohana, Isaya, YEremia,MAthao au PAULO na kumwacha Musa pekee aandike habari za Mwanzo hadi kuwepo kwake?
Jibu ni rahisi sana,hao wote hawakuandika kwasababu hawakupewa unabii wa siku za mwisho,usiniulize kwanini hawakupewa maana sijui ni kwanini na jibu la swali hili analo Mungu mwenyewe....

Wote walioandika hawakuandika mambo yao yanayowahusu wao bali waliandika mambo ya Mungu na maagizo ya Mungu hivyo unanishangaza unapohoji "kwanini hawakuandika mambo yao" utadhani Enoch aliandika mambo yake.....
 
Back
Top Bottom