WW1, WW2 na kinachoendelea sasa Middle east vilipangwa mwaka 1871 kama barua hii ni kweli

Sina shida na cheo wala elimu yake. Baada ya hilo sema kitu au jibu maswali ili na mimi nasema vitu
Vizuri...

Baada bya kujibu hili nieleze ni kwanini unadhani amedanganya wakati anaonekana kuwa na wadhifa ambao unamfanya anachoongea kiwe na uzito mkubwa sana....
 
Good.....
 
Mkuu aliyesema kuwa Shetani ni mkuu wa ULIMWENGU siyo mimi ni Yesu mwenyewe,labda uniambie kuwa unatilia mashaka maneno ya Yesu....

Ukubwa wa Ulimwengu huu hata uwe mkubwa namna ipi hauwezi kuzuia Shetani kuwa mkuu wake,huo ukubwa unakupa tatizo kwasababu unafikiria kimwili zaidi siyo kiroho.Kiroho hakuna cha ukubwa wala nini,kama unahitaji kwenda mahali penye umbali wa miaka maelfu kwa spidi ya mwanga ukiwa kwenye physical body ni chuni ya sekunde moja tena zaidi ya hapo ukiwa kwenye spiritual body....

Sijui ni wapi umepata ushahidi wa kwamba huko kwenye ulimwengu kuna viumbe wengine let alone kukubali ukuu wa Shetani.Nitafurahi ukinishirikisha jambo hili kwa ushahidi mkuu....
 
Mkuu mbona hapa panazungumzia mambo ya kawaida kabisa?

Pamoja na hayo,hata kama ujuzi huu utakuwa ni wa ajabu,Mungu aliutoa kwa watu maalum tu kama unavyosoma hapo na siyo kwa kila mtu vinginevyo hakukuwa na sababu ya Musa kusema hayo...

Kikubwa zaidi,unadhani mwanadamu kabla hajanguka dhambini aliumbwa kwaajili ya mambo haya?
Mkuu haya mawazo ya kusema ningesema hivi au vile ni yako wewe siyo yangu,kama unahitaji mawazo yangu utaniuliza...

Kuhusu hao kutengeneza silaha za ajabu,hap panajieleza wazi kwamba ni kwa namna ipi walipata uwezo huo.Hapo juu nimeeleza hili....
b)WANADAMU WAMEUMBWA NA UWEZO MKUBWA SANA AMBAO UNATOSHA KUWAHALALISHA KUWA NYUMA YA MAENDELEO HAYA YA DUNIA NA SIO HAO VIUMBE UNAOWATETEA. KAMA WANAUWEZO ZAIDI YENU NI KWA FAIDA YAO NA HUKO WATOKAKO ILA HAWAKO NYUMA YA MAMBO YANAYOENDELEA DUNIANI.
Hapana, tena HAPANA kubwa....

Nijibu,mwanadamu kabla hajakosea alikuwa ameumbwa kuja kufanya haya unayoyasema hapa?
Mkuu kwanza aliyeitaja Misri wa kwanza kwenye mjadala huu ni wewe ukijibu post yangu ya kwanza kwenye mjadala huu,hili usilikane kabisa.....

Post yako hii hapachini

Pili,naomba uniwekee huo mstari ambao Mungu alimpa somo Nebukadneza kabla sijasema lolote kuhusu jambo unalosema alilifanya....
Hili una elimu ndogo sana kulihusu....

Watu unaowaamini wanakueleza kwamba dunia sasa iko kwenye maendeleo makubwa kuliko wakati mwingine wowote ule,kitu ambacho binafsi sikubaliani nacho.Tunaelezwa kwenye biblia kwamba Adamu aliishi miaka 900,kwa akili ya kawaida tu,huyu binadamu wa kwanza na wewe na mimi na wengine wote walioko humu duniani leo ni nani alikuwa na uwezo mkubwa wa kimwili na kiakili?

1;Kama ni wewe na mimi,eleza ni kwanini leo tunaishi muda mfupi zaidi...
2;Kama ni Adamu,huoni kwamba uwezekano wa watu wa kale kuwa na uwezo mkubwa wa akili ni mkubwa kuliko leo?

Kama ni kweli kuwa Adamu alikuwa na uwezo mkubwa zaidi ni kwanini tunadanganywa kuwa tuna maendeleo wakati huu kuliko wakati mwingine wowote?
 
Vizuri...

Baada bya kujibu hili nieleze ni kwanini unadhani amedanganya wakati anaonekana kuwa na wadhifa ambao unamfanya anachoongea kiwe na uzito mkubwa sana....
Nitakuletea hapa maelezo yake yote kwa kina kutoka kwenye video zote mbili sio hii moja tu. Then tutaanza kuangalia uhalali au uharamu wa kimoja baada ya kingine. Point tuliyofika ni ya muhimu mno katika mijadala huu maana nimegundua hapa ndipo tunapishana wewe unaenda mashariki na mimi magharibi wote tukawa na ajenda Sawa NWO.
Kwa kukuongezea tu huyu sio wa kwanza kuzungumza alichokisema ndio ma wengine wakaenda mbali kabisa hadi mwaka 193o ambapo jamaa anaitwa H. G Wells aliitunga novel THE WAR OF THE WORLD s na siku ilipokuwa broadcasted live mfano nchini Ecuador 1949 watu walikimbilia makanisani kuhofia kuuliwa na hao UFOs taharuki hii iligharimu maisha ya zaidi ya watu 6 hadi 20 na hicho kituo cha radio kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali. Concept za kwenye hicho kitabu ndio nyingi huyu mdau alikuwa akijipa uhusika kuwa alipigana na aliens pia eti 1954 us gov event walisighn mkataba na aliens ili washirikiane kujenga hizo dumb sijui walikuwa wanaongea lugha gani. Kwa kukuongezea tu vyote hivyo ni conspiracy zisizo na ushahidi wa kutotiliwa Shaka.

Pia nilitaka nikusaidie Phil Schneider sio reliable source ya hizi conspiracy za UFOs. Bali ni Senetor Barry Goldwater, Lord Hill Norton mkuu kitengo flani British loyal army, Brigedia General Urther Axon.Director wa kwanza wa CIA Roscoe Hillenkoeter, waziri wa ulinzi wa Canada Paul Helyer hawa ndio watu walikaa wakawasikiliza hoja zao za UFOs na hadi kesho hawajawahi kuonyesha au kutoa ushahidi usio na Shaka. Huyu jamaa yako alikuwa anatembea na jiwe eti material yake anadai hayapo kwenye periodic table ya kibinadamu hence ni product ya ufo space craft s Bila hata kumpa mtu yoyote athibitishe anachokisema. Vyote anavyosema shahidi ni huyohuyo mtoa taarifa.

Hizi zilikuwa dondoo za awali ujue huyo jamaa sio wa kwanza na taarifa zake sio mpya. Na Mara ya kwanza taarifa hizi kusomwa kwenye media nchi mbalimbali kabla hata huyu jamaa hajazaliwa ziliteta taaruki. Nitaendelea kuona analink vipi na mada hapo juu ya vita ila kwa kuhusisha na hao viumbe wako
 
Kwa kuwa ni muumini wa bibilia basi unafnya mjadala kuwa raini zaidi.
Soma Daniel 12:4
But thou, O Daniel, shut up the words, and seal the book, even to the time of the end: many shall run to and fro, and knowledge shall be increased.

MUNGU anamwambia Daniel akifunge kitabu chake maana sio cha wakati huo hayo mambo ni ya wakati wa siku za mwisho. Na akasisitiza siku za mwisho watu wataenda huku na kule na MAARIFA YATAONGEZEKA. Huu Ni unabii wa siku zetu. Adam alikuwa hapandi ndege, Goliath hakutumia AK 47,
Kimsingi ninaamini kwa unabii na utabiri huu leo maarifa ni makubwa kuliko wakat wa nyuma na Mungu anasupport hilo chief. Umri kupungua ni madhara ya Muda mrefu ya dhambi.
So usiwape credit hao ufo Bali ni sisi sisi tu.
 
Ubaya uko wapi kuwa na hizo dini sarafu na serikali moja?
 
Nipe link nikajionee humo majadiliano yalivyokua maana nimehamasika na hiyo stori
 
Neno yawezekana ulitendee haki mkuu. Lkn pia hata hao viumbe unaowahusudu ni conspiracy tu hakuna ushahidi usiotiliwa Shaka juu yao. Hiyo ni assumption yangu. Pili kuhusu kiroho na distance havina uhusiano shetani angeweza kufikia dunia kwa microseconds lkn kama angekataliwa angekataliwa isingeleta tofauti. Nilikuwa nakupa physical overview of universes. Kwa hiyo kwa assumptions yangu Huko kwenye product za kazi ya Mungu ikitokea aliumba viumbe zaidi na kuwawekea makazi hata shetani akienda kwa nanosecond with supersonic speed na wakamkataa haileti tofauti. Hata kama tukiexpand concept ya Ulimwengu huu kuwa sio dunia kama inavyotafsiriwa kwa English versions tuassume Mungu kaumba malimwengu Mengi ikiwemo huu ambao kadunia ketu ni member anaweza kuumba mingine Mingi tu ambayo wakamkataa Shetani hata kama akafika kwa supersonic speed.

Kuhusu Uwezo wa kiroho wa Shetani kufikia sehemu Kubwa najua ndio maana Luka 10:18 yesu alimuona Shetani akianguka kama umeme. Nadhani unajua speed ya light japo bado ni ndogo kiroho.
 
Naona Adamu na Hawa ni ya kutunga maana baada ya Kaini kuwekwa alama alioa nani? Na anawekwa alama ili 'mataifa' kila mtu ajue alichotenda.

Walitoka wapi hao watu wengine?
 
...

Adamu aliishi miaka 900,wewe leo ukifikisha miaka 50 umeshaanza kuisha.Sasa jiulize,kati ya Adamu na wewe aliyekuwa na ubongo imara wa kufanya mambo ni nani? Kama kweli sasa tuna maendeleo kuliko kale
...

Kuishi muda mrefu sio kipimo cha ubongo imara. Na hapo ni kama ni kweli alikuepo huyo Adamu.

Na kama alikuwepo, wewe unasema tunayoyafanya leo haikua lengo la kuwekwa pale Edeni. Basi hata Adamu haiwezekani alikua na uwezo zaidi ya watu wa leo kwa muktadha huo.
 

Mkuu mi naona kauli kama hizo ni kutisha tu watu. Haiwezekani kila kinachofanyika iwe ni mahusiano na kiroho. Nashawishika kuungana na MSEZA MKULU kuwa kuna namna au kundi linajaribu kuhofisha watu kwa malengo flani.

Lakini pia hoja ya watu wenye damu ya kishetani mi naona nayo ni ngumu sana kumeza.

Same na ambavyo pia siamini stori za Mseza za vita vya kwanza na pili. Pale Tunisia tu kijana alijichoma moto kisa ugumu wa maisha na kikanuka Arabuni kote. Kuuwawa mtu akasababisha vita vya dunia inawezekana kabisa. Ishu ni tension imefikia kiwango cha kulipuka?

Tunachojifunza ni kuwa binadamu anaweza kuchochea au kuchochewa kwa kitu kidogo sana na kuleta catastrophe. Mfano mdogo angalia siasa zetu. Rais kaamua kutoa pesa za serikali kwenye benki binafsi na sasa nchi nzima wanalia hali ngumu.

Destruction ya mwanadamu imo mikononi mwake. Uokozi wake umo pia mikononi mwake kwa kuamua kufuata ya Mungu. Again ni mawazo yangu.
 
Kosa ulilolifanya kwenye post yako ya kwanza bado unaendelea kulifanya....

Unasema hukubaliani na jambo fulani bila kusema sababu zinazokufanya usikubali,hili linafanya hoja zako kuelea tu hewani na unaonekana unakataa jambo bila sababu na hili ni kosa kubwa kwa mtu anaye reason....

Kupinga ni rahisi sana lakini kupinga kwa hoja ni ngumu sana....
 
Nilijua swali kama hili litakuja tu....

Lakini,body ability inahusiana na mambpo mengi sana,ukifikiria afya ya mwili inahusiana na afya ya ubongo pia,hili halipingiki kabisa....
 
Naona Adamu na Hawa ni ya kutunga maana baada ya Kaini kuwekwa alama alioa nani? Na anawekwa alama ili 'mataifa' kila mtu ajue alichotenda.

Walitoka wapi hao watu wengine?
Swali dogo sana hili na hii siyo mada yake....

Tuache kuharibu mada hii na hili tutajadili kwenye mada nyingine.Lakini unapaswa kujua mambo mengi kabla hujauliza swali kama hili....

Unapaswa kujua kwamba huyo Kain aliishi miaka mingapi pia unapaswa kujua kwamba alipata ndugu wengine kutoka kwa wazazi wake vile vile.....

Mwishowe utauliza Musa alijuaje mambo ya uumbaji wakati hakuwepo wakati wa uumbaji....
 
Haya maelezo yako yote yanakosa maana mkuu nukta moja tu Yesu aliposema kwamba Shetani ndiyo Mungu wa dunia hii...

Sioni haja ya kujadili kama Shetani ni mkuu wa ulimwengu kwasababu Yesu ameshasema....

Una ushahidi wa hao viumbe wa kwenye sayari zingine mkuu?
 
Mkuu,maandiko yamesema maarifa yataongezea bila kusema hayo maarifa ni yapi na yatatoka wapi na nani atahusika kuyaleta,hayajasema binadamu atakuwa na maarifa mengi na hata yangesema hivyo bado kulikuwa na uwezekano wa kuyapata mahali hayo maarifa.....

Adam anaweza kuwa hajatumia AK47 lakini kutumia silaha hiyo siyo kipimo cha maendeleo makubwa kihivyo....

Ninajua sana kwamba kipindi hiki Shetani na washirika wake watatumia silaha zao za mwisho kabisa katika kupambana na kile kinachoendelea katika upande wa watu wa Mungu na hapa ndiyo sababu Mungu akasema maarifa yataongezeka maana watu watapewa maarifa mengi sana na hawa viumbe....

Kwa kuliona hili,kwenye D.U.M.B's kuna treni zenye uwezo wa kukimbia kwa speed ya sauti na hili halijulikani na wengi....

Mkuu,labda nikuulize,hivi unadhani binadamu ameshindwa kudhibitiwa na silaha zilizopo hadi watengeneze silaha nzito kama lile bomu la Russia linaloitwa "Satan II" ambalo bomu moja tu linaweza kuiangamiza Ufaransa yote na mabomu kama hayo 50 yanaweza kuiangamiza Marekani yote?

Kwa namna unavyo reason,unaona kabisa silaha hizi ni kwaajili ya binadamu kweli?

Jeshi la Marekani lina chopper zaidi ya 50,000.Chopper hizi ni za kisasa kabisa zenye uwezo wa kupita umbali wa futi 3000 juu na wakaweza kuona kila binadamu aliyeko ndani ya nyumba yako,wanajiandaa kupambana na binadamu?

Again,bado kabisa mkuu unapaswa kujua kinachoendelea chini ya miguu yetu ambako kuna mengi sana na yanayoendeshwa na viumbe ambao siyo binadamu kabisa....

Kuna tukio moja lilitokea kule Afghanistan ambapo giant mmoja aliuawa baada ya kuua na kuangamiza battalion moja ya jeshi la Marekani akiwa peke yake.Giant huyu alikutwa kwenye cave moja huko Afghanistan. Baada ya kuuawa,pailot aliyeusafirisha mwili wake alisema kwamba giant yule alikuwa na urefu wa futi 10 hadi 12 na alikuwa na kilo zaidi ya 400....

Hiyo ni mwaka 2005 mkuu...

Mambo haya yanapatikana kutoka kwa watu ambao wamefanya mahojiano na pailoti yule ambaye aliamua kutoa siri hii baada ya kuona kazi ya mtafiti mmoja ambaye aliamua kumpa siri hiyo.Jina la mtafiti huyo nimelisahau nadhani nikilikumbuka nitakuambia maana documentary ya jambo hili iliharibika....
 
Hahahahahaaaaaaaaaaaaaa.......

Mkuu unanifurahisha sana aisee.Nani kasema kuwa Phil Schneider ni mtu wa kwanza kuzungumzia haya mambo? Masuala ya UFOs yapo since B.C huko halafu nije niseme mtu aliyekuja kusema kwenye miaka ya 1990's ndiye wa kwanza?

Hivi hao akina Senetor Barry Goldwater, Lord Hill Norton mkuu kitengo flani British loyal army, Brigedia General Urther Axon.Director ni reliable source namna ipi aisee?

Nilikupa hiyo video kwasababu nilitaka usikilize kutoka kwa mtu ambaye ana wadhifa ambao hutaweza kutilia mashaka kirahisi rahisi tu anachokisema kama unavyotilia mashaka ninayosema mimi hapa kwakuwa hata hunifahamu....

Masuala ya UFOs sijui unataka uyasikie kutoka kwenye vyanzo vipi unavyoviamini.Ungeelewa msingi wa hoja zangu ni kwamba tunadanganywa juu ya uwepo wa hawa viumbe na wenye mamlaka makuu kabisa duniani kwaajili ya faida zao binafsi na kwasababu wao wanahusiana kwa namna moja au nyingine na hawa viumbe wala usingekuwa unataka vyanzo kutoka kwa watu ambao ndiyo wanatudanganya kama unamaanisha vyombo vya habari vikubwa vukubwa kusema au wataalam wenye noble prize waseme....

Unataja watu ambao ni wahusika wa serikali,unarudi kule kule.Kama hujui ni kwamba kuna web nyingi sana za hawa hawa wanaotudanganya ambao wanatoa fake info kupoteza watu.Wale ambao waliasi na baadaye kuuawa ndiyo hutoa ushuhuda unaoshikika....

Unaposema ushahidi usio na shaka kutoka kwa Phil Schneider unakuwa na maana ipi? Yaani kwa mfano hilo "jiwe" ulitaka awape watu wakahakikishe asemacho au ulitaka afanye nini? Hivi unajua ni nini alichokuwa anamaanisha huyu mtu? Unajua ni aina ipi ya maisha alikuwa anaishu huyu jamaa? Unajua ni madhara yapi ambayo aliyapata akiwa kazini akijihusisha na haya masuala?

Hoja zako ni nyepesi sana kwa wale ambao tunajua ni namna gani haya mambo yanaendeshwa lakini kwa watu ambao hawajui wanaweza kuona zina mashiko.Ni ngumu sana kuthibitisha kitu ambacho kwanza ni kinyume cha sheria kuwa nacho halafu ni ngumu kumpa mtu yoyote tu aka verify ili aamini.Mazingira haya ni magumu sana.Mtu alikuwa hadi anahama nyumba tano kwa usiku mmoja ili aendelee kuwa hai unakuja kusema tu hapa "hataki kutoa nafasi kwa wengine kuthibitisha asemacho" utadhani ni mtu tu ana gari halali halafu anasema linakimbia kuliko yote kisha ukahoji sababu ya yeye kutompa mtu mwingine aendeshe kuthibitisha....

Unayohoji yangekuwa ya maana sana kama ingekuwa ni kitu halali tu tunakijadili hapa ambapo tungeweza kwenda kwenye maabara zozote za kisayansi tukathibitisha....

Bado,huwezi kupata majibu ya maswali yako kirahisi hivyo kwa kuangalia video moja....

Eti tuje tujadili ukweli na uongo kwenye maelezo yake.Utatumia nini kusema hiki ni uongo au hiki ni ukweli? Hisia au nini hasa? Una hilo "jiwe" lake ili ukalipime uone ni uongo aliyokuwa akiyasema kulihusu?

Unafurahisha sana aisee...
 
kama basis ya haya unayotoa unayaassociate na maelezo ya yule jamaa yako. Basi utakuwa na tatizo kubwa sana.
nitaeleza baadae kdg
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…