WWF waponda na kupinga mradi wa umeme wa Stiegler’s Gorge

WWF waponda na kupinga mradi wa umeme wa Stiegler’s Gorge

Paskali umepiga lager kabla kuandika haya au? unaikana Environmental impact assessment hujui faida yake? Kuna maendeleo yoyote Nchi inaweza kuyapata bila athari za kimazingira kutokea? Taratibu ushabiki gani huu!
Wewe kibaraka wa imperialists mwache pascal mayala to hell with you
 
Mnajidanganya nyie, wamarekani licha ya kutokuwa na wanyama wengi kama sisi lakini karibia kila jimbo wana ZOO na wanyama ni hawa hawa
Kuna kitu nikiandika kuhusu hizo Zoo hakuna MTU ataenda na itakuwa kashfa kubwa mno ya kimataifa ambayo yaweza sababisha collapse ya hiyo biashara ya zoo.Naomba niheshimu wamiliki wa zoo ila niombe WWF na Whoever that leave us alone .Hiyo WWF Nina ya kwao mazito please leave us alone msituchokonoe please
 
Sikubaliani na WWF wala serikari katika kuangalia mahitaji ya umeme na maslahi mapana ya taifa.

Nishati ndio nguzo ya stability kwenye kujenga uchumi na maendeleo ya jamii nchi yoyote makini katika sera muhimu za taifa energy security ndio top of the agenda hiyo ainaga mjadala ata serikari zinapobadilika.

Matiafa yote yaliyopiga hatua kubwa za maendeleo ukipekuwa utakuta wanazalisha kutumia the most pollutant source ambayo ni makaa ya mawe kati ya 60%-80% ya total energy output. To put into perspective USA and UK respectively 70% ya chanzo cha umeme wao ni makaa ya mawe one US household uses 10 times of their counterparts moreover the Washington subway system alone uses enough energy to power the whole city of Geneva.

Na hao watu wala hawana mpango wa kuachana na hivyo vyanzo hivi karibuni ndio kwanza Trump kajitoa kwenye Paris agreement, wachina ndio uwaambi lolote kwenye makaa ya mawe na UK badala ya kupunguza ndio wanaongeza kimya kimya. Kwanini makaa ya mawe ni cheap source to run, more reliable than any other source (an important factor in stability of supply) katika mataifa yaliyoweka kipaumbele uchumi wao and over the long term it the best investment in terms of value for money.

Nimejaribu kutafuta energy security policy yetu online sijaona something which came close to it is "POWER SYSTEM MASTER PLAN 2012 UPDATE" ambayo inazungumzia pretty much aspects za energy policy za Tanzania mpaka 2036 humo ndani utaona kuna prediction za population growth za sehmu mbali mbali na technical aspects za energy policy ambazo kwakweli zinaridhisha na makaa ya mawe yamepewa sehemu kubwa ya uzalishaji kufikia capacity planned.

Leo hii watu walioandaa huo mkakati kama Eliakim C. Maswi, James Andilile, Eng. Innocent Luoga and na timu yao ya ufundi kutoka TANESCO sidhani kama wanaimpact tena japo kwenye ushauri wa policy yao. Inaonekana waliokuja wamekuja na agenda nyingine na mkakati mwingine.

Tayari tunazalisha umeme wa maporoko Pangani na Mtera na tumeshaona sio reliable source ni kwasababu hizi hizi ndio maana nchi zilizoendelea awaupi kipaumbele China Yangtze river unaweza ufananisha na Nile tu kwa ukubwa na wanamito mitatu kama hiyo umeme wamaporoko kama reliable kwanini wasiongeze na wana means and resources au USA wana great river ngapi ya kufanya miradi ya umeme wa maji.

Sisi waafrika ni watu wenye matatizo sana kutaka kukimbia ata kutembea vizuri atujaweza Stiegler's Gorge' ni bad investment na sio kitu tunachoitaji kwa sasa, what we need are more reliable sources na vyanzo vyake tunavyo vya kutosha. Alieturoga kesha kufa
 
Wazungu hawapendi tuendelee wanatafuta kila sababu, faida ya kujenga mradi huo ni kubwa kuliko hiyo urithi wa dunia kwann watupangie???
 
Kuna kitu nikiandika kuhusu hizo Zoo hakuna MTU ataenda na itakuwa kashfa kubwa mno ya kimataifa ambayo yaweza sababisha collapse ya hiyo biashara ya zoo.Naomba niheshimu wamiliki wa zoo ila niombe WWF na Whoever that leave us alone .Hiyo WWF Nina ya kwao mazito please leave us alone msituchokonoe please
Hahaha uandike wewe watu wasiende kwenye zoo?! Andika labda utasaidia serikali yako ijitambue. Wanyama tunawauza wenyewe halafu tunahamasishana kukuza utalii.Wachina wanamiliki panda wote walioko marekani hata wanaizaliwa huko. Sisi tunauza jumla jumla halafu tunalialia ohoo shitholes.
Hahaha andika mkuu waache kwenda huko zoo waje Tanzania tuingize pesa. Andika labda tutapata patent ya wanyama wetu. Waambie na huo ukweli wao hao WWF.
 
Haturudi nyuma...energy for development through industrialization
Very pathetic,apart from having resources required for industrialisation,key factor is human resource,something tht we as a country we dont have,Singapore didnt have much resources but they devoloped their human resources..same applies for japan..so before you start throwin stones think about that....
 
Tunahitaji umeme.
WWF au UN wakafuge wanyama na ecology systems pale Washington DC au Brussels.

Mbona, Trump kajiondoa kwenye mkataba wa Climate Change Summit uliofanyikia Paris!?

Waache upoyoyo.
No choice, tutajenga bwawa!
 
Tanzania ni ya watanzania.

Ni upuuzi mtu kukaa Washington alafu atupangie watanzania namna ya kutumia rasilimali zetu!

Hawa jamaa hawatutakii mema. This is imperialism at its best.

Yani wanaguswa zaidi na nyumbu wa Sealous kuliko watanzania mamilioni ambao wanaishi gizani?

Ni upumbavu zaidi kuwasupport hawa jamaa!

Trump anasema "America first", na sisi tunasema Tanzanians first!
Amazon kuna power Dam 250 na hawa WWF hawakuzuiya ije kuwa hii yetu?
 
Very pathetic,apart from having resources required for industrialisation,key factor is human resource,something tht we as a country we dont have,Singapore didnt have much resources but they devoloped their human resources..same applies for japan..so before you start throwin stones think about that....
Learn to use kind words, it will help you to be listened tentatively by your prospective audiences. By the way, be specific, what do you mean by these words" human resources" in relation to our country strategic plan toward industrialization!?
 
WWF to hell... We need electricity kwa haraka sana kwa ajili ya viwanda na treni ya umeme..!! WWF wafie mbali..!!
 
Mkuu unajua jamaa hawa ni vigeugeu. Hydro ni renewable energy, gas siyo renewable. na mara zote wanashabikia renewable energy. Pale TANESCO upande wa solar energy wamekuwa wakipiga hela ndefu sana kwa kisingizio cha cheaper energy, ingawa mimi naelewa ni kupoteza pesa zetu na kutafuta mbinu za kuiba kupitia makandarasi binafsi.

Kama alternative ya hydro ingekuwa ni nuclear ningesema twende nuclear lakini huwezi kuacha hydro over gas. South Africa hawakuwahi kuwa na hydro. energy source yao ilikuwa nuclear na wanapanua reactor zao beyond anyone sasa hivi, lakini wamekwisha anza hydro kwenye Limpopo. Iache gesi iwepo lakini tusiache hydro. Hiyo faida ya pili ya gesi kutumika majumbani, kwa TZ bado. Hiyo ni methane ambayo ni flamable kuliko propane na butane tunazotumia kwenye mitungi. Kwa hali ya maendeleo tulipo ni hatari kuingiza methane majumbani na wataalamu wanaelewa hilo na itachukuwa miaka mingi. Nyumba zetu hizi na mazingira yake hayafai.

Angalia ripoti inavyogusagusa vipengele vingi kutaka kuhalisha maamuzi yao. Wanagusa hata Climate change bila kusema climate change inasema nini juu ya East africa. Ukisoma ripoti za IPCC utagundua jamaa hawa ni watunzi wa hadithi tu! Bahati mbaya tunao watu humu JF ambao nahisi wanajifunza kujenga hoja na ikifikia ushabiki, hoja wanaacha na kuanza CCM vs CHADEMA. Ndo maana nimewahi kuomba rais atimue mbio tu maana baadhi ya wanaoomba kusikilizwa hawana la kusikilizwa!

Honestly naona umetoa maelezo mazuri lakini sijaona kama umetoa maelezo nikaridhika kutokana na mahitaji yangu. Yaani ni kama nimetaka kujua habari za Tanga, lakini ukaniletea habari za Morogoro kwa ufasaha. Anyway ngoja niridhike na maelezo yako, lakini bado hujakidhi haja yangu kama nilivyotarajia.
 
Watulie, Magufuli amesema EIA itafanyika baada ya ujenzi, Yani ni sawa na kumtia mimba msichana halafu baada ya kujifungua unamwambia mkapime kama mna ngoma. 🙄.

All in all wafunge midomo yao hii ni ardhi yetu na tunauwezo wa kuifanyia tunachotaka tunasema ni "Sovereignty of the state"
Hahaaa. Huo mfano wa mimba ni BALAAAAA...
 
Learn to use kind words, it will help you to be listened tentatively by your prospective audiences. By the way, be specific, what do you mean by these words" human resources" in relation to our country strategic plan toward industrialization!?
Hahahah....kind words....industrialisation requires not only natural resources but also attitude of the people who controlls the natural resources....your attitude and the likes of you hinders flourishing of industrialisation....
 
Mnajidanganya nyie, wamarekani licha ya kutokuwa na wanyama wengi kama sisi lakini karibia kila jimbo wana ZOO na wanyama ni hawa hawa wetu tunaojivunia, Tembo, Twiga, Nyani, Chui, na wengine wengi. Wamewatunza vizuri na kuwazalisha, sisi tunazo mbuga za asili na wanyama wa asili sio ZOO. Hao WWF wanatusaidia sisi na wanyama wetu, ushauri wao kwetu ni wa kitaalam sisi tuna leta siasa na ujuaji.
Watalii wengi kutoka huko marekani waliisha waona Twiga, Tembo,Chui na wengine huko huko marekani, hukuk wetu, Tanzania, Kenya, Afrika kusini Namibia wakija wanataka kuwaona wanyama hao kwenye natural habitat zao, na hicho ndicho hao WWF wanakitetea, eti sisi tunawasikiliza wanasiasa wasiofahamu chochote kuhusu ecologia na maisha ya wanyama wetu lakini wanahamasisha UTALII waingize pesa.
Ohoo viwanda, hata hawafahamu wanataka viwanda gani vya kutengeneza nini, kwa teknologia ipi na ya nani kutoka wapi?!
Siasa zenu ziishie bungeni acheni wataalamu wawaambie ukweli.

Tunazo mbuga za kutosha sana ikiwepo Ruaha ambayo ni first or second largest national park in Africa. Eneo litakalomegwa kutoka Selous ni dogo sana kulinganisha na litakalokuwa covered na Dam. Wanyama hasa tembo hawatadhurika.
Mwaka 1993 China walianza ujenzi wa bwawa la umeme (Three Gorges Dam) kwa ajili ya kuzalisha umeme MW 22,500 mradi ambao ulibuniwa mwaka 1919. Wakati wa ujenzi mamia ya watu walifariki, watu zaidi ya milioni 1.3 walihamishwa (sisi tunalalamikia wanyama). China bado wanazalisha umeme wa Nuklia pamoja na makaa ya mawe. China wameendeleza viwanda na kuuza bidhaa zao kwa bei nafuu kutokana na kuwa na umeme mwingi na wanaendelea kujenga Dams nyingine. Tunahitaji umeme wa bei nafuu unaozalishwa kwa maji. Hao WWF wapotelee kwa mbali.
 
Kuna kitu kiko nyuma hapa.. Kwamba walifikiri tunataka kufanya Mradi mkubwa kama huo huku hatukujipanga na athari zake ikiwemo hiyo ikolojia?
Hawa WWF wanatakiwa kupotezewa tu kama China wanavyofanya. Mradi uendelee hiyo ikolojia wanailinda Africa tu? Hao ulaya na marekani wakati wanafanya industrialization walifanya mangapi zaidi ya hili letu? MazaFanta.
 
Pamoja na Magufuli kuanzisha mradi wa Stegler, sijasikia kusimama ujenzi wa mitambo ya umeme utakao zalishwa kwa gesi. Nadhani miradi hiyo bado ipo, ndio maana miradi ya Kinyerezi I na Kinyerezi II inaendelea.

Umeme wa Maji utakuwa wa bei rahisi kulinganisha na gesi, vyote vikiwa pamoja gharama za uzalishaji viwandani zitapungua hivyo kuongeza kasi ya uwekezaji katika viwanda.
 
Hebu fikiria tutakaposema kwa kuwa tunayo Uranium ya kutosha na tunataka kujenga mtambo wa Nuklia kupata umeme watakavyo react. Mambo ya Iran yatahamia kwetu.
 
Back
Top Bottom